Wanavyuo, kwanini huwa mnaona noma kutaja majumbani kwenu?

Wanavyuo, kwanini huwa mnaona noma kutaja majumbani kwenu?

Good morning....
Enzi hizo naanza chuo nlikua nashangaa kila mwana chuo anasema kwao dar, mtu anaongea lafudhi yani kisukuma cha ndani kabisa huko mwamashimba ila ukimuuliza kwao anasema dar tena anajitahidi na kumix kidogo lafudhi ya dar mi naiita kuvunja nazi..... Hiyo mixer ya kisukuma plus kuvunja nazi sasa mweh!!!

Juzi nlikutana na masista duu wa chuo, tunafamiana wakawa wananiaga wanaenda likizo, wa kwanza nikamuuliza home wapi, akajibu naenda dar af kesho kutwa narudi, nikamuuliza kwanini unarudi soon akasema narudi afu ndo naenda home Arusha. Dar kunani huko nami nije? Mtu anaona noma kusema arusha kisa dar?

Wa pili sasa lol nae nikamtel safari njema home wapi, akajibu napita dar kwanza nisipoenda itakua lawama, Ha ha nkauliza tena so home wapi nkaona sura yake imenyong'onyea, imejaa wasiwasi, kwa sauti ya chini akajibu nikitoka dar naenda kigoma kwa mama nilijizuia tu kucheka ila kweli ilinichekesha sana.

Jamani dar kuna nini huko? Wahenga walisema mkataa kwao mtumwa. Wasomi tabia mbaya hiyo kwani ukisema kwenu mwamashimba kuna ubaya gani?
wanavyuo nawatakia likizo njema, BILA SHAKA WOTE MPO NDANI YA SHABIBY KWENDA DAR HAKUNA ALIEPANDA SARATOGA YA KIGOMA LOL
Kuna lilojificha hapo?Dar kifursa, kimaendeleo,vyuo vingi pia vipo dar nk, dar imepiga hatua ukilinganisha na mikoa mingine,pamekuwa sehemu ya watu kupakimbilia na kuonekana ukiishi dar wewe ni mjanja,ni vyema sana serikali ingepanua wigo wa uwekezaji katika mikoa mingine, offisi za wizara mbalimbaili sisogezwe kwenye mikoa mbalimbali respectively na shughuli za wizara husika,na pia watumie system za decentralised sio centralised kwamba activities nyingi katika taasisi za serikali eg G. P. S. A ambapo depot zipo mikoani zifanyike huko huko mikoani kupunguza ulimbukeni wa kila kitu kifanyike dar.kwa hizi factors zitaondoa hiyo fallacy kwa kila mtu kujinadi anatokea dar na kupenda makwao,
 
Kuna lilojificha hapo?Dar kifursa, kimaendeleo,vyuo vingi pia vipo dar nk, dar imepiga hatua ukilinganisha na mikoa mingine,pamekuwa sehemu ya watu kupakimbilia na kuonekana ukiishi dar wewe ni mjanja,ni vyema sana serikali ingepanua wigo wa uwekezaji katika mikoa mingine, offisi za wizara mbalimbaili sisogezwe kwenye mikoa mbalimbali respectively na shughuli za wizara husika,na pia watumie system za decentralised sio centralised kwamba activities nyingi katika taasisi za serikali eg G. P. S. A ambapo depot zipo mikoani zifanyike huko huko mikoani kupunguza ulimbukeni wa kila kitu kifanyike dar.kwa hizi factors zitaondoa hiyo fallacy kwa kila mtu kujinadi anatokea dar na kupenda makwao,
But sio sababu ya mtu kupakana kwao
 
Mweh somo, sasa tusipoenda daslamu itakuwaje? Inamaana hatujawahi kuishi Tanzania jamani.
 
Taratibu jamani ambao hatujafika dar kawaida yetu kujionyesha tunakufahamu huko dar hatakama tunatokea mbeya, alafu hii ishu sio wanachuo tu hadi kwa baadhi ya watu wazima na nchi za jirani zetu mfano mzuri kama wiki mbili zilizopita nilienda hapa kwa wabwezi(malawi) nilikutana na majanki wakaniuliza natokea Tz mkoa gani nikawaambia mi jirani yao hapa karibu. Basi kila wakati wananiulizia ishu za dar ambako mie mwenyewe sijawahi fika, wabwezi wanakukubali sana dar na kwa matajiri wao lazima kwanza uwe umefika johnnesberg halafu dar wewe ndio tajiri mjanja
 
Wengi wanakuwa hawajawahi kufika dar wakiwa chuoni ndio wanapata uwezo wa kutembelea jiji
 
Mi huwa nacheka sana mtu ana lafudhi ya kihaya/kichagga bado atakwambia kwao dar na kazaliwa dar.....dah,hatari sana.
 
mimi nawaambiaga kwetu kigoma ila wanakuona mshamba balaa,

unakuta mtu anakwambia na anajisifia mm kwetu hapa hapa nimezaliwa hapa hapa, nikitzama maisha yake na yangu levo sawa sasa najiuliza MZIMA KWELI HUYU.KIJANA
 
Back
Top Bottom