Jamaa ananisimulia Kilichotokeaβ¦
βNimepiga mchongo mmoja nikapata kama laki,mida ya saa Moja kasoro nikasema ngoja nitokee pande hizi nipoze koo kwa bia hata 3 kisha nirudi home nikapumzike
Nimefika hapa napiga zangu lite ,mara mtoto mkali huyo akavuta kiti akajoin na Mimi,nikasema fresh ni moja ya kampani.
Mrembo: Hello,mambo mkaka?
Jamaa: poa,niaje mrembo?
Mrembo : poa sana,naweza kujoin na wewe hapa,au una mtu?
Jamaa:Hapana,unaweza tu kujoin sister,usijali.
Mrembo:Asante.
Tukapiga stori mbili tatu,waiter akafika kumaikiliza mrembo.
Mrembo akaniangalia,macho yake ni ka yalikuwa yananiuliza βvipi niagize?β
Mimi nikaona siyo kesi,nikamwambia waiter βmsikilizeβ.
Demu akaagiza Heineken. Kimoyomoyo nikaguna nikasema βyani Mimi makunywa lite ya buku jero alafu huyu demu from nowhere anaibugia bia ya elfu 5!!? Fresh siyo kesi!! Akaagiza bia mbili.
Wakati nimefika bar nilikuwa na elfu 40 mfukoni na elfu 60 kwenye simu,jumla laki Moja.
Piga bia,piga bia,kuja kustuka elfu 40 imekata,alafu bill imeelemea upande wa demu,ameshatumia kama elfu 30. waiter Kila akirudi na tripu demu ana Heineken mbili,manake elfu kumi inakata kwa tripu moja. Wakati yeye anakunywa bia za uchumi wa kati mim ninakunywa lite zangu za bei ya kimasikini.
Wakati ananisimulia alipofika hiki kipengere nilicheka sana.
Akaniuliza βkwa hiyo unanicheka au siyo? Unaniona bogus Fulani hivi?
Nikamjibu βmwanangu,Hela yenyewe laki Moja alafu unaenda bar kutumia,tena na mrembo pembeni ulitegemea nini? Wacha mademu wakupukutishe vihela vyako hadi uchakae ubakie kama moja.
We si kenge,hutaki kunisikiliza mwanao nikikushauri inshu za kupunguza kulewa?β
Akanijibu βsawa MWAMPOSA,ila subiri kwanza nimalize stori ndiyo uje na mahubiri yakoβ.
Akaendelea..
Ikafika hatua nikaanza kulipa bill kwa βlipa nambaβ mana kwa wallet hela imeshaisha.
Nikasema huu ujinga gani nafanya? Mbona natumia Hela na mtu asiyenihusu kabisa,alafu malaya? Ngoja nimcheki mwanangu Satoh Hiroshi atokee pande hizi aje kunipa kampani.
Ndiyo nikakucheki utokee tujoin kucheki game pia.
Sasa wakati tutaendelea na kupata vinywaji,demu alikuwa bize sana na simu,hata stori na Mimi alikata kabisa.
Ghafla akaniambia βkaka, samahani Nina dharula nasepa zangu. Asante kwa bia.β
Kwanza nikamwangalia kwa jicho Fulani la hasira. Nikamuuliza βdada unasamaje?β
Yani kirahisi tu unaniambia Asante alafu unasepa? Unanichukulia kama BOYA flani hivi naelea kwenye maji huku mawimbi yananipelekesha yanakotaka,si ndiyo? Yani umetumia Hela zangu alafu kirahisi tu unaniaga na kuishia zako utoke na mwanaume mwingine huko? Mimi ninachojua ni kwamba tukitoka hapa tunaenda kwangu au tunaenda kule Miki nataka na siyo wewe kuniacha hapa kirahisi hivyo.
Mrembo: We mkaka vipi kwani? Yani kutumia visenti vyako kidogo tu unatokwa na mipovu alafu unataka uondoke na mimi? Unadhani Kila mtu Malaya eeh?
Hili jibu ndiyo litatibua kabisa mashetani yaliyolala kichwani.
Tukajibizana na kutukanana sana,hadi bar yote ikawa kimya imehamia kwenye vita yangu na demu.
Kuna mabaunsa wakaja pale kuamua ugomvi,lakini Kuna baunsa mmoja mstaarabu akatuuliza sababu ni nini ya huo ugomvi,nikatiririka Kila kitu.
Watu wote hasa wanaume wenzangu wakaniunga mkono na kusema Mimi Nina haki au vinginevyo demu anilipe gharama zangu zote,maana yeye ndiye kanifuata Mimi kwa hiyo hadi mwisho alitakiwa awe chini ya himaya yangu. kwa ustaarabu wangu ndiyo nilitakiwa nimruhusu aende au nitoke nae,na siyo alivyonifanyia. Kwanza alikuwa anakunywa bia kwa kunikomoa,haikuwa mstaarabu.
Mimi naagiza bia ya buku na mia nane,yeye anaagiza bia ya buku Tano asee!!
Ugomvi ulivyokuwa mkali,wakatutoa nje,maana tulikuwa tumekaa karibu na sehemu ya kuingilia,si unajua sipendi kukaa ndani ndani napenda kutulia maeneo ambayo nitakuwa naona matukio yote,hasa karibu na geti la kuingilia ili nifaidi kuona watoto wakali!? Tukacheka!!
Ugomvi ulipohamia nje,ndiyo wewe(akimaanisha Mimi)ukaja ukanikuta nimemtia roba ya mbao yule Mwanamkeβ
Ndipo nilipofika na kukuta ugomvi mkubwa.
Yule mdada alipoona amelemewa kwa point na Kila mtu amemgeuka pale,ikabidi amwambie jamaangu amwachie ili amrudishie gharama zake zote za bia alizokunywa.
Binti: Siwezi kuondoka na wewe nimekuambia,ni heri nikurudishie Hela zako zote. Naomba uniachie.
Akatoa mkoba akamkabidhi jamaa elfu 50 kwa hasira. Mabausa wakasema hapo mmemalizana fair play kabisa.Ila jamaangu aliyaoga matusi balaa. Dada anatukana yule wanawake wa keko wakasome!!
Baada ya lile tukio hata sikuingia Tena ndani,yule bibie alipomlipa mshikaji hela yake tukageuza home.
Njiani wakati tunasepa akaniambia βunajua nini Satoh, kwenye haya maisha usijifanye mjinga Kila mahali. Yule bibie anajiuza,na inaonekana kabisa nilikuwa Kuna uwezekano mkubwa wa kusepa nae,ila inavyoonyesha Kuna mwamba alifika dau kubwa kwenye simu yake. Ndiyo akataka kunifanya Mimi kiazi Anywe bia alafu asepe tu kirahisi.
Zikapita siku kadhaa,siku Moja Tena tukatoka pale bar na mwanangu, wakati tumechill tupo bize na mpira,Kuna bibie mmoja mrembo akajoin meza yetu.
Kuna baunsa akapita mitaa ya meza yetu akamuona mshikaji aka mkumbuka maana jamaa alishakuwa maarufu kwa lile tukio la ile siku. Akamwambia yule bibie aliyeungana nasi pale mezani βLatifa,naomba ukimaliza kutumia Hela za hao jamaa wakisema usepe nao,uende. Usituletee balaa kama mwenzio Linahβ.
Sote wanne kwa pamoja tukacheka sana, jamaangu akajibu Siku hizi ameokoka,hawezi kuleta fujo tena!!