Wanawake ni wazuri wakiwa kazini

Wanawake ni wazuri wakiwa kazini

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
4,290
Reaction score
2,468
Habari za Jumapili.

Nikiwa nimetulia ndani jioni namuona mamsap akirudi toka kwenye mishe. Pia alipitia saluni. Katengeneza nywele zake vizuri anavutia kumtazama

Sasa ujinga ni kuwa kufika tu kachukua kilemba kafungia nywele humo kazibania vizuri hata isionekane hata moja! Hapo tayari kuanza mishe za nyumbani. Ule mvuto aliokuja nao ukatoweka.

Ikifika asubuhi anajikwatua tena na kuziachia vizuri tayari kwenda kazini. Huko anakutana na wenzake. Mabosi, vijana, wababa, wapita njia, n.k. Wote kwa nyakati tofauti wanavutiwa nae kwa muonekano ambao alipokuwa nyumbani aliuficha.

Jioni inafika tena anafika nyumbani na kujitupia tambara lake kichwani. Tena anaweza kutafuta na nguo nguo huko akajitupia kisha akaendelea na mishe za nyumbani.

Kwa hali hii hamasa itakuwepo? Hakika yatabakia mazoea tu.


 
Nchi Kavu naomba umfikishie wife huu ujumbe kama ulivyo. Inawezekana anadhani akipendeza huwa huoni au huvutiwi

Mapenzi ili yawe matamu na kudumu hayataki mazoea... yanataka kufanyiwa kazi kila muda na pande zote mbili

Umeniamsha usingizini sasa ngoja na mimi niondokane na mazoea nianze kujipodoa hata jioni😃😃😃
 
Niliwahi kumchana rafiki yangu KE aliyewahi kuwa office mate. Huyu dada tulikuwa ni marafiki wakubwa sana hadi ndugu zake wote na wazazi wake walinifahamu na kuniheshimu kama ambavyo mimi niliwaheshimu. Nikaacha kazi pale naye akawa ameacha lakini urafiki wetu haukufa. Akasikia nimetoka zangu bush niko MUJINI hivyo akanialika kwa lunch. Mumewe tunafahamiana sana na tunaheshimiana sana tu.

Basi nikafika pale nikamkuta na mama yake mzazi tukapiga story kisha msosi ukawekwa mezani tukajichana. Baada ya kula nikaaga na yule dada kunishindikiza. Basi ile tuko wawili nikaanza “umepatwa na kitu gani mbona umejiachia hivi?” “Kwanini nyumbani kwako unakuwa nyuku nyuku kama house girl?” “Wewe ni mtu unayejipenda sana lakini kwako umevaaa kisempele kimechoka sana Nywele zako nzuri umezifunga na kilemba kilichochoka sana” “Hivi unadhani mumeo akirudi kutoka kazini akikukuta hivi atakuwa na hamu hata ya kukugusa?” “Si bora tu awe na mchepuko wake anayevutia na havai visempele kama wewe na kuficha uzuri wale?”

Akainamisha kichwa kama dakika tano hivi. Ule ukimya nikajua nimeshapoteza rafiki yangu wa miaka mingi.

Akasema ahsante sana nashukuru sana. Tumegombana sana na hubby kuhusu issue hii kuliko issue nyingine yeyote ile. Naona kuna kila sababu ya kujirekebisha.
Ukweli ni kwamba KE wengi waliokuwa kwenye ndoa wanajisahau sana kuhusu kupendeza na kuwa maridadi wanapokuwa majumbani mwao na hii husababisha ME wengi kwenye ndoa kuanza kuangaza angaza huku na kule kutafuta warembo.
 
Nchi Kavu naomba umfikishie wife huu ujumbe kama ulivyo. Inawezekana anadhani akipendeza huwa huoni au huvutiwi

Mapenzi ili yawe matamu na kudumu hayataki mazoea... yanataka kufanyiwa kazi kila muda na pande zote mbili

Umeniamsha usingizini sasa ngoja na mimi niondokane na mazoea nianze kujipodoa hata jioni😃😃😃
Asante mama D kama nimekugusa. Huu ujumbe nitamfikishia hakika
 
Niliwahi kumchana rafiki yangu KE aliyewahi kuwa office mate. Huyu dada tulikuwa ni marafiki wakubwa sana hadi ndugu zake wote na wazazi wake walinifahamu na kuniheshimu kama ambavyo mimi niliwaheshimu. Nikaacha kazi pale naye akawa ameacha lakini urafiki wetu haukufa. Akasikia nimetoka zangu bush niko MUJINI hivyo akanialika kwa lunch. Mumewe tunafahamiana sana na tunaheshimiana sana tu.
Basi nikafika pale nikamkuta na mama yake mzazi tukapiga story kisha msosi ukawekwa mezani tukajichana. Baada ya kula nikaaga na yule dada kunishindikiza. Basi ile tuko wawili nikaanza “umepatwa na kitu gani mbona umejiachia hivi?” “Kwanini nyumbani kwako unakuwa nyuku nyuku kama house girl?” “Wewe ni mtu unayejipenda sana lakini kwako umevaaa kisempele kimechoka sana Nywele zako nzuri umezifunga na kilemba kilichochoka sana” “Hivi unadhani mumeo akirudi kutoka kazini akikukuta hivi atakuwa na hamu hata ya kukugusa?” “Si bora tu awe na mchepuko wake anayevutia na havai visempele kama wewe na kuficha uzuri wale?”
Akainamisha kichwa kama dakika tano hivi. Ule ukimya nikajua nimeshapoteza rafiki yangu wa miaka mingi.
Akasema ahsante sana nashukuru sana. Tumegombana sana na hubby kuhusu issue hii kuliko issue nyingine yeyote ile. Naona kuna kila sababu ya kujirekebisha.
Ukweli ni kwamba KE wengi waliokuwa kwenye ndoa wanajisahau sana kuhusu kupendeza na kuwa maridadi wanapokuwa majumbani mwao na hii husababisha ME wengi kwenye ndoa kuanza kuangaza angaza huku na kule kutafuta warembo.
Asante BAK kwa ushuhuda huu. Tena bahati mbaya huwa hawawasikilizi wenzi wao. Atabadilika kwa kuambiwa na mtu wa pembeni, kama ulivyofanya
 
Back
Top Bottom