Wanawake tupunguze mdomo, tunawaponza waume zetu wenyewe

Wanawake tupunguze mdomo, tunawaponza waume zetu wenyewe

Judithkaunda

Member
Joined
Aug 21, 2022
Posts
90
Reaction score
231
Ni kweli wanawake tunapenda kuongea tena ni jadi yetu, lakini tujitahidi kuchuja maneno tusisahau hata Bibilia imeandika, "Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake, lakini mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe".

Leo ntaongelea wenzangu na mie mama wa nyumbani.

Dada unajijua huingizi kipato kinachoweza kumudu mahitaji ya familia yako na hata kama unabiashara yako lakini asilimia 80 mume anahudumia familia. Embu tusijisahau rafiki zangu, huenda ni kweli kuna namna mwanaume anakosea au hajatoa pesa kwa wakati imepelekea na wewe ukapata changamoto fulani hapo nyumbani, ndugu yangu ndiyo unune siku nzima jamani?

Mumeo katoka kazini kachoka hujui hata amepitia mangapi huko kazini, karudi nyumbani akitegemea kupumzika, kuliwazwa wewe ndio umenuna hapo, ukiulizwa kelele zinaanza.

Dada mwenye tabia hii chunguza vizuri, wewe ndiyo sababu ya mumeo kuwa mlevi kupindukia. Wewe ndiyo sababu anachelewa kurudi au harudi kabisa. Wewe ndiyo unawapa nafasi kubwa michepuko.

Halafu utasikia mdada anaongea kwa ujasiri, huyu mwanaume hana shukrani amekosa nini kwangu jamani?

Wanawake tusijisahau, mume anahitaji heshima.
 
Ni kweli wanawake tunapenda kuongea Tena ni jadi yetu lakini tujitahidi kuchuja maneno tusisahau hata bible imeandika..
Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake, lakini mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

Leo ntaongelea wenzangu na mie wa mama wa nyumbani.

Dada unajijua huingizi kipato kinachoweza kumudu mahitaji ya familia yako na hata kama unabiashara yako lakini asilimia 80 mume anahudumia familia embu tusijisahau rafiki zangu, huenda ni kweli Kuna namna mwanaume anakosea au hajatoa pesa kwa wakati imepelekea na ww ukapata changamoto fulani hapo nyumbani ndugu yangu ndio unune siku nzima jamani.

Mumeo katoka kazini kachoka hujui hata amepitia mangapi huko kazini karudi nyumbani akitegemea kupumzika, kuliwazwa wewe ndio umenuna hapo ukiulizwa kelele zinaanza.

Dada mwenye tabia hii chunguza vizuri wewe ndio sababu ya mumeo kuwa mlevi kupindukia.
Wewe ndio sababu anachelewa kurudi au harudi kabisa.
Wewe ndio unawapa nafasi kubwa michepuko.

Alafu utasikia mdada anaongea kwa ujasiri huyu mwanaume Hana shukrani amekosa Nini kwangu jamani..

Wanawake tusijisahau Mume anahitaji heshima.
Watakuponda na kusema umewasaliti wanawake wenzio
 
Ongeza ka sauti wamamama walioko huku nyuma et hawakusikii kile wasema!
.
IMG_20200825_072749.jpg
 
Itakuwa mmewe/mpenzi hajui Kuna vyemaaa ndo maana kidomo kimeendelea kuwakuwa Hadi ndani ya mahusianoo/ familia
 
Back
Top Bottom