Wanawake wa JF mbona hamjibu Private messages?

Wanawake wa JF mbona hamjibu Private messages?

Hii ndio nzuri sasa mtu anakusalimia swali linalofuata uko wapi? Yaani ndani ya siku moja anataka kujua unaishi wapi, una miaka mingapi, unafanya kazi gani, una watoto wangapi. Watu wa namna hii hata nikiwajibu huwa wanajibiwa lolote linalokuja kichwani muda huo

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna mmoja aliniPM picha ya mdada....ikabidi nimuulize hiyo picha ni ya nani?akaninijibu eti ni mimi huyo kwenye picha

Nikabaki hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!JF ina vichaa
 
Hizi za Kwenda moja kwa moja Kwenye mada sio nzuri Sana.
Unakuta mtu anakupm kaandika"kwa Jina la mapenzi karibu moyoni"
Hiyo Ni text yake ya kwanza juu kabisa.

Ni vema mtu anapokupm akaanza na salamu na kukujulia Hali kwanza.
Hii inatoa nafasi ya kujua Khali ya mtu anayewasiliana Naye,mf kujua Kama Ni mzima,mgonjwa, Kuna shida anapitia au Yuko bize .

Kuanza tu kujieleza moja kwa moja kwa mtu,unaweza jieleza kumbe Ana Shida au anaumwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama tumewahi kuwasiliana kabla ndio naweza nikakwambia ukweli kuhusu hali yangu.
Lakini secretary Pompeo anipm Mambo? Nianze kutiririka kwamba "mabaya, nimeamka najisikia vibaya sijui mgongo sijui kichwa" hapana, hata yeye akiwa anaandika "mambo" anategemea tuu jibu litakuwa ni poa.

Halafu Anne mbona mimi ukini pm unanyooka kwenye mada lakini hapa unanigeuka.
 
Kimtu kinakuja kabisa kinakusalimia vizuri kabisa,
Unaweka mapozi pembeni unakijibu halafu kinakuchunia.! Ni kama kilikuwa kinakupima tu kama utamjibu ama la..!!
Hahahaaaa. Lol.

Mdogo wangu mi tukio langu ni la kinyume kabisa. Yaani kuna mtu nilimkosea jukwaani mwenzangu si nikasema nikamtake radhi kwa PM. Weeee sikumbukagi hata kama alinijibu aiseee.

Mana nilikaa baada ya wiki nikaifuta ile PM na kuignore future msgs mana nilikuwa namuona anaandika majukwaani. Daaah.

Sijui ndio alinisamehe au bado mana hata sigongani naye siku hizi. Itokee tu japo nikigongana na comments zake kama ameandika vyenye kunifaa nampaga likes. 😅😅😅
tukileta pozi mnatusema, tukiwa wastaarabu tukajibu mnaanza kutu take for granted.! Na tutawachunia mpaka mkome.!
Hahahahaaa!! Lol.

Mleta uzi asome ulichoandika hapo huenda akaelewa nini umemaanisha mdogo wangu.
 
Back
Top Bottom