Wanawake wa JF mnanipa raha

Kwani Jf ni sehemu ya matangazo ya maisha ya mtu binafsi?wenye maisha mazuri siku zote hawajitangazi bali yanaonekana yenyewe...
Kusema mme wangu siku hizi analewa anashindwa hata kudrive ni kutangaza maisha?


Halafu mbona mambo ya kawaida haya au mtu kutaja vitu na sehemu za level ambazo mwingine hawezi kuzifika ndiko kusema wanajisifia.

Kusema mimi ni muuza mkaa na gemge na mwingine kusema mimi namiliki kampuni kubwa ....huyu wa kampuni kisa hafanani na wa mkaa kusema tu anajisifia????

Kai kai kai....
 
Kula hotelini beach fulani ya kifahari ndiyo maisha safi?

Hujaona watu wanakula hotelini beach fulani ya kifahari lakini wana madeni mpaka kwenye kope za macho?
 
Kwa hiyo nyie mlitaka mtu akiandika stori aanze mpenzi wangu anayekaa kwenye nyumba kuukuu....

Kama mtu mpenzi wake anapunch gear kwanini asiandike? Au kama anaishi pazuri kwanini asiseme...
[emoji113]
 
Mimi andika vyovyote cha msingi kiwe kinafurahisha hata ukiandika ukweli sikujui na sikujui uongo mtamu bwana uonagi @ gudume anavyosepa na kijiji
 
Stori inataka ushauri juu ya mpenzi mlevi ila taandikwa hivi

Jamani naomba ushauri ,tukitokea vacation zanzibar mimi na mpenzi wangu ghafla ameanza tabia ya ulevi yaani jana kanywa chupa 3 za hennessy hata gari akashindwa kuendesha ......
Umesahau kutaja aina ya gari mkuu [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kweli kabisa... Anaish tandare, anauza vitumbua asubuhi, anapata hela ya vocha anakuja na story za ajabu humu... Nilienda kempisiky na boy fulan.. Braaa....braaaa...braaa
Be natural bana people tunaelewa vizur tu
Umejuaje kama anachoongea sio kweli?
 
Kila mtu apambane na hali yake
Alafu mbona hata wanaume wapo hivyo humu?kila mwanaume ana gari humu,anadrive[emoji23][emoji23][emoji23]

Endelea kupata raha mkuu,maisha yenyewe ndio haya haya
 
Kwa hiyo nyie mlitaka mtu akiandika stori aanze mpenzi wangu anayekaa kwenye nyumba kuukuu....

Kama mtu mpenzi wake anapunch gear kwanini asiandike? Au kama anaishi pazuri kwanini asiseme...
Sweetheart
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…