Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
..Binafsi sijakuelewaToday is what is calling 3D (x, y, z),in additions of time & space together making a 5D.
eg. Discovering of micro chip devices.
mkuu hapo anaitwa roho ya Mungu, binadanu pia tuna roho lakini hatuna nafsi mbili. Roho ni nguvu. kwa binadamu roho yetu inatufanya tuishi na Mungu anaitumia roho yake kufanya kazi zake. hata kuna viumbe wa roho ikimaanisha wanaexist in energy form. usishangae nguvu za Mungu kuwa juu ya uso wa maji.Kaka hiyo Mwanzo 1: umeisoma mpaka wapi, umejaribu kuisoma yote? Au umesoma mstari mmoja tu?
Hiyo Mwanzo 1 ndio utatu mtakatifu unapojizihirisha wazi kabisa, Hiyo Mwanzo 1, inasema hivi " Hapo mwanzo MUNGU, aliziumba Mbingu na nchi, Hapa hakuna Mkristo hata mmoja anayebisha kuwa Mungu ndiye aliyeumba, swali linakuja hapa Aliumbaje hiyo Dunia,
Mwanzo 1:2 unasema ROHO YA MUNGU ikatua juu ya uso wa maji, hapo ni Dhairi Mungu anaanza kuzigawa Nafsi zake katika uumbaji, kwamba Mungu ndiye aliyeumba, lakini ROHO YAKE NDIYO ILIYOTUA JUU YA USO WA MAJI, hapo kuna Mungu na Roho lakini upo katika umoja japo inaonekana utofauti wa nafsi
Mwanzo 1:3 Mungu AKASEMA, iwe Nuru, Hapa Mungu anatoa NENO na kusema iwe Nuru,
Hivyo kwenye huu uumbaji tunaona MUNGU, ROHO YAKE na kisha NENO lake, MUNGU, ROHO YAKE NA NENO LAKE NI MUNGU MMOJA,
Ukija kwenye Yohana 1:1-4, inasema hivi Hapo mwanzo alikuwako NENO (mwanzo 1:3) na huyo NENO alikuwako kwa MUNGU na huyo NENO ALIKUWA MUNGU, mstari wa 14 (yohana 1:4), unasema na huyo NENO alifanyika Mwili, Akaaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa MWANA PEKEE atokaye kwa BABA amejaa Neema na Kweli
CC: Red Giant , mgen , Mango833 , mwana2015 , @G' taxi, Hb wa Ilala
Hiyo mimi huwa nina ipinga sana....nchi ya watu wengine na wameamua kuamini wanavyotaka wao. ...basi waache. .ikifikia hapo huwa nawapenda wachina. ..Kulikuwa na kundi la wasabato wenye siasa kali waliotaka kwenda Iran sijui liliishia wapi wakuu. Mwenye taarifa tafadhali
Dini ni survival tactics. ..Hapo mwanzo hakukuwa na dini bali kulikuwa na Muumba.Na ndio maana hakuna habari yoyote inayomuhusisha binadamu wa kwanza na dini.Dini ni matokeo ya mihangaiko ya binadamu katika kutaka kujua kila kinachomzunguka na yale asiyoyaona.But suala la kuwepo kwa Muumba haliepukiki cuz hata kama hapo mwanzo hakukuwa na dini kila kitu kilikuwa kipo kwenye mpangilio maalumu mfano sayari,maumbo ya viumbe,mfumo mzima wa jua nk.Mtazamo wangu juu ya hili ni huo..
Waafrika tulikuwa na dini zipi?Inabidi tusome vizuri historia ya dini. Tuzifahamu vizuri hizi ambazo sasa tunaaminishwa kuwa ni dini bora kwakuwa tu zimeletwa na wazungu na waarabu tukadharau dini ambazo ni za asili ya babu zetu ambao baadaye wakawa watumwa kwa hawa hawa ambao leo tunasutana juu ya dini zao tukibishana juu ya namna ambayo wanatumia kuabudu. Kwa msimamo wangu hakuna dini ya wapagani na kwangu mimi hakuna mpagani ila wapo watu ambao tunaamini katika njia tofauti. Kuitwa Juma ama Hamisi badala ya rutashobya au kokutona siyo kusema sasa wewe umeondokana na kile kinachoitwa upagani. Na ama kuitwa Joseph au Justine badala ya malimi ama masanja sio kusema sasa umeondokana na kile kinachoitwa upagani. Kwangu mimi dini ni kile unachokiamini na kujenga misingi ya imani juu yake. Mungu ni mmoja hakuna mungu wa israel na uarabuni na ama wa afrika ni mmoja. Utatu mtakatifu katika Roman Catholic hujumuishwa katika kile kinachoitwa fumbo la imani ni fumbo hili la imani ndilo ambalo lilizaa hicho ambacho kinachoitwa the holly trinity. Na fumbo hili huadhimishwa katika kila misa. Ndio maana hata tukiiangalia dini ya kiislam kuna segments the same as ukristo kama kweli ndizo zilizo dini za kweli kwanini kusingekuwa tu ukristo ulio mmoja na ama uislam ambao uko unified kuliko hizi segments na manabii kibao. Niungane na dhana ambayo member mmoja amesema kwamba dini hizi tunazozizungumzia sasa na kusutana wamebeba mambo mengi sana ambayo wafrika kabla ya ukoloni waliyafanya katika kutimiza ibada zao kwa mungu wao aliyejuu.
Siyo kweli kwamba waliabudu utatu mtakatifu, au labda wewe una define vipi utakatifu ndugu?? Naweza sema waliabudu utatu wa kishetanikwanini watu wameendeleza hii ibada ya kipagani?
![]()
Brahmma, vishnu na Siva wahindi.
![]()
![]()