The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 747
- 2,112
Kamishina wa Polisi Jamii (CP), Fausitine Shilogile amewaelekeza wakuu wa upelelezi katika mikoa (RCO) pamoja na madawati ya jinsia kuhakikisha wanafuatialia kwa ukaribu kesi za ukatili wa kijinsia na unayanyasaji wa watoto ili wanapopeleka jalada kwa Mwanasheria wa Serikali liwe na ushahidi unaojitosheleza.
Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo yaliyoandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Nchini (THRDC) kwa kushirikiana na Shirika la CSEMA kwa kuwahusisha maafisa wa kutoka kwenye baadhi ya vyombo vya dola akiwemo maafisa wa Jeshi la Polisi pamoja na Mawakili kutokea ofisi ya mashtaka Nchini, amesema kesi za ukatili wa kijinsia na unayanyasaji kwa watoto zimekuwa zikiachwa kwa maafisa wanaoshughulika na masuala ya madawati ya jinsia.
"Nawaelekeza Wakuu wa upelelezi wa Mikoa mlioko hapa pamoja na madawati haya (madawati ya jinsia) kuhakikisha mnafuatilia kwa ukaribu kesi hizo (kesi za ukatili wa kijinsia) kuna atendensi kesi hizi tumekuwa tukiwaachia watu wa madawati lakini hizi ni kesi ambazo ni 'sireas' lazima tuzisimamie na tuzitekeleze sisi wenyewe ili tunapo ili tunapochukua 'file' au jalada kulipeleka kwa mwanasheria wa Serikali liwe limekamilika na na liwe limeshiba na ushahidi wote" amesema Kamishina wa Polisi Jamii (CP), Fausitine Shilogile
CP Fausitine Shilogile ameongeza kuwa "Haipendezi wala haifurashi kesi inafika mahakamani inafutwa na mara nyingi mimi uwa nasema kuwa kufaulu kwa kesi ndio kufaulu kwako mpelelezi kesi inapofutwa ina maana kwamba haujafanya kitu ambacho kilitakiwa kifanyike kwahiyo tuhakikishe RCO tunasimamia kwa ukaribu sana kesi hizi na zitoe matokeo chanya"
Aidha, amesema kuwa hali ya ukatili wa kijinsia na unayanyasaji kwa watoto bado sio ya kuridhisha akitoa takwimu za mwaka 2021 na 2020, amesema kupungua kwa kiwango cha matukio hayo ni kutokana na jihudi ambazo zimekuwa zikiendelea kufanyika.
"Takwimu za makosa ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji wa watoto bado si za kuridhisha katika miaka ya hivi karibuni kwani katika kipindi cha Januari Disemba, 2021 Jumla ya matukio 11,499 yaliripotiwa ukilinganisha na matukio 15,870 yaliyoripotiwa kipindi kama hicho mwaka 2020 hii inaonyesha kuwa juhudi zinafanyika za kupambana na matukio haya hadi kupelekea matukio kupunguza", amesema Kamishina wa Polisi Jamii (CP), Fausitine Shilogile
Pia CP Fausitine Shilogile ametoa wito kwa Taasisi na watu binafsi kuwa vita hiyo ya sio ya Jeshi la Polisi pekee bali amehasa kuwepo kwa ushirikiano kutoa elimu na mafunzo kama kama walivyofanya waandaaji wa mafunzo hao ili wananchi wawe na uelewa wa kutosha waweze kutoa taarifa kwenye vyombo vya sheria na ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Kwa upande waandaaji wa mafunzo hayo Mratibu wa THRDC, Wakili Onesmo Olengurumwa amesema kuwa dhumuni la kuandaa mafunzo hayo yanayofanyika kwa siku mbili kuazia leo Augosti 17, 2022 katika ukumbi wa Golden Tulip Hotel Jijini Dar es Salaam, yakiwahusisha maafisa kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Tanga, ni kukumbushana kuhusu misingi ya haki za binadamu na kujadili changamoto zilizopo hususani za ukatili wa kijinsia pamoja na ukatili wa watoto ili kushauriana namna bora ya kuzitatua.
Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo yaliyoandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Nchini (THRDC) kwa kushirikiana na Shirika la CSEMA kwa kuwahusisha maafisa wa kutoka kwenye baadhi ya vyombo vya dola akiwemo maafisa wa Jeshi la Polisi pamoja na Mawakili kutokea ofisi ya mashtaka Nchini, amesema kesi za ukatili wa kijinsia na unayanyasaji kwa watoto zimekuwa zikiachwa kwa maafisa wanaoshughulika na masuala ya madawati ya jinsia.
"Nawaelekeza Wakuu wa upelelezi wa Mikoa mlioko hapa pamoja na madawati haya (madawati ya jinsia) kuhakikisha mnafuatilia kwa ukaribu kesi hizo (kesi za ukatili wa kijinsia) kuna atendensi kesi hizi tumekuwa tukiwaachia watu wa madawati lakini hizi ni kesi ambazo ni 'sireas' lazima tuzisimamie na tuzitekeleze sisi wenyewe ili tunapo ili tunapochukua 'file' au jalada kulipeleka kwa mwanasheria wa Serikali liwe limekamilika na na liwe limeshiba na ushahidi wote" amesema Kamishina wa Polisi Jamii (CP), Fausitine Shilogile
CP Fausitine Shilogile ameongeza kuwa "Haipendezi wala haifurashi kesi inafika mahakamani inafutwa na mara nyingi mimi uwa nasema kuwa kufaulu kwa kesi ndio kufaulu kwako mpelelezi kesi inapofutwa ina maana kwamba haujafanya kitu ambacho kilitakiwa kifanyike kwahiyo tuhakikishe RCO tunasimamia kwa ukaribu sana kesi hizi na zitoe matokeo chanya"
Aidha, amesema kuwa hali ya ukatili wa kijinsia na unayanyasaji kwa watoto bado sio ya kuridhisha akitoa takwimu za mwaka 2021 na 2020, amesema kupungua kwa kiwango cha matukio hayo ni kutokana na jihudi ambazo zimekuwa zikiendelea kufanyika.
"Takwimu za makosa ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji wa watoto bado si za kuridhisha katika miaka ya hivi karibuni kwani katika kipindi cha Januari Disemba, 2021 Jumla ya matukio 11,499 yaliripotiwa ukilinganisha na matukio 15,870 yaliyoripotiwa kipindi kama hicho mwaka 2020 hii inaonyesha kuwa juhudi zinafanyika za kupambana na matukio haya hadi kupelekea matukio kupunguza", amesema Kamishina wa Polisi Jamii (CP), Fausitine Shilogile
Pia CP Fausitine Shilogile ametoa wito kwa Taasisi na watu binafsi kuwa vita hiyo ya sio ya Jeshi la Polisi pekee bali amehasa kuwepo kwa ushirikiano kutoa elimu na mafunzo kama kama walivyofanya waandaaji wa mafunzo hao ili wananchi wawe na uelewa wa kutosha waweze kutoa taarifa kwenye vyombo vya sheria na ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Kwa upande waandaaji wa mafunzo hayo Mratibu wa THRDC, Wakili Onesmo Olengurumwa amesema kuwa dhumuni la kuandaa mafunzo hayo yanayofanyika kwa siku mbili kuazia leo Augosti 17, 2022 katika ukumbi wa Golden Tulip Hotel Jijini Dar es Salaam, yakiwahusisha maafisa kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Tanga, ni kukumbushana kuhusu misingi ya haki za binadamu na kujadili changamoto zilizopo hususani za ukatili wa kijinsia pamoja na ukatili wa watoto ili kushauriana namna bora ya kuzitatua.