Wapendwa naona kama mwisho wangu umekaribia

Wapendwa naona kama mwisho wangu umekaribia

Status
Not open for further replies.
Usiache kumuomba Mungu kipindi hiki.Wakati mwingine huwa naamini Mungu anaamua kukupitisha tu kwenye tanuru la moto ili uuone ukuu wake na uwe mwanadamu bora.
 
Ushimen
Mshana Jr
Grahams
OKW BOBAN SUNZU na wengine njoeni msaidien hata ushauri mwanaume mwenzenu
Nimechelewa kuona tag yako Mjukuu...

Hata hivyo nitajitahidi kusoma comments zote za wadau ili nione alichoshauriwa nami nitaongezea ikibidi.

Kwakuwa JF ni pool, nina amini anaweza kushikwa Mkono akapata ajira ya udereva ama ajira za viwandani as nimeona amesoma mechanical engineering Kwa ngazi ya diploma.

Wito wangu, kama Kuna mtu mwenye nafasi ya ajira kwenye hayo maeneo mawili tajwa hapo juu vyema tumsaidie mtoa mada(Wanasema mpe nduguyo ajira badala ya kumpa mkate Kila Siku).

Wakati huu ambao atakuwa anashughulikiwa suala la ajira yake, iwapo itawezekana tumsaidieni japo kiasi kidogo cha fedha ili aweze kununua chakula ili apate kuishi na mtoto wake na Mama yake Mzazi ambao wote ni Wategemezi wake kwasasa
 
Naona uwepo wa tatizo ambalo halijafumbuliwa kwa mujibu wa maelezo yako.Mauzauza nyumbani bila shaka ndiyo chanzo cha anguko lako.Maombi yako kama yanatosha basi huenda ulizembea.Lakini kiukweli wahitaji mtaalam alitazame tatizo kwa kina ili lidhibitiwe kwani hata biashara kwa sasa zaweza kutosaidia.Kilichopandikizwa kwako hakijatolewa na hivyo adui anayekutafuna unaishi naye.
 
Habari za wakati huu,

Sijui wapi pa kuanzia Ila tangia mwaka 2018 niliamua kuacha kazi na kuanza maisha ya kujiajiri.

Kazi niliacha baada ya kuona biashara zangu zingine ndogo ndogo zinalipa Ila changamoto ilikuwa ni kukosa usimamizi nzuri.

Pia sababu nyingine ilikuwa kutoelewana na supervisor wangu kutokana na roho ya kijicho kuona maendeleo niliyokuwa nayo hayaendani na mshahara ninaopata.ingawaje sikuwahi kuwa na loss yoyote au kujibizana naye Ila alichokuwa anafanya kunipiga Vita ya chinichini.kwanza mmiliki wa kampuni alikuwa ni mwenyeji wa Kanda ya ziwa hivyo kufanya asilimia kubwa ya wafanyakazi kuwa watu wa Kanda ya ziwa.

Pili kwenye vitengo vyote waliweka watu wa Kanda ya ziwa. Mimi peke yangu ndio nilikuwa mtu wa kaskazini.hii ilipelekea supervisor wangu kutengeneza na kueneza sumu ya chuki kwa urahisi kuwa watu wa kaskazini ni wezi .turudi kwenye mada

Baada ya kuacha kazi mambo yalinyooka kuliko mwanzoni.niliwaza muda wote nilikuwa wapi kwanini sikuingia mapema kwenye biashara.Ndani ya miaka mitatu nilifanikiwa kupata sehemu ya kujihifadhi na kausafiri kutokana na wakati mwingine Mishe zangu zilikuwa za udalali.

Mwishoni wa mwaka 2022 mambo yalianza kwenda mrama baada ya kuhamia kwenye kibanda changu.Mama yangu mzazi alikuwa akiumwa kifundo Cha mguu na pilingili mbili za mgongo zilikatika pia na sukari ilikuwa ikimsumbua.Hivyo ilibidi aje dar as salaam kwa ajili ya tiba

Tulipambana naye kwa wakorea pale mbezi kwa msuguri ikashindikana tukahamia mhimbili huko nako hakukuwa na nafuu ya kudumu.wakati huo nilikuwa na mtoto mdogo ambaye alikuwa Hali chakula Wala usiku halali.Lakini changamoto haikushia hapo kwenye maisha ya nyumbani.usiku kulikuwa hakuna kulala Mara watu wanagonga mlango wengine wanafagia nje .ukichungulia nje huoni mtu yoyote .hili nilimaliza kwa njia maombi

Changamoto hizi hazikuishia nyumbani tu Bali hata sehemu zangu za kutafuta ridhki.nilikuwa na ofisi mbili moja ya uwakala nyingine ya duka la vinywaji vya jumla na rejareja.Pesa nyingine nilikuwa nazungushia kwenye udalali.

Siku isiyokuwa na jina naenda kufunga hesabu kwenye ofisi ya uwakala mambo hayakuwa mazuri.Wakala hakuwa na cash yoyote wa float.pesa iliyokuwepo ilikuwa ni kamisheni jumla yake Kama laki tatu na machenchi.kuulizia pesa nyingine nikaambiwa iko kwa wakala mwenzake.basi pale tukagawana faida nikaondoka.kufupisha stori Yule wakala alikuja akasema pesa ametapeliwa hivyo atanilipa mdogo mdogo.

Wakati huo nimeshauza gari la kutembelea ili ninunue guta.kumbe guta limeuzwa Mara mbili na Mimi ndiye mtu wa pili .kufupisha guta sikupata niliishia kulipwa mdogo mdogo.

Duka la vinywaji Mambo hayakuwa mazuri nilichezea vitasa Sana kwa TRA kutokana na mambo ya risiti .mbaya zaidi madeni yalikuwa mengi kwenye mabar na mapub .kuna meneja alifukuzwa kazi ,Kuna miliki alishindwa kulipa Kodi ya mwaka mzima Kama mwenye nyumba anavyotaka.

Kifupi ndani ya mwezi wa 11 mwaka 2022 maji yalifika shingoni ikabidi niende nyumbani Kilimanjaro kupumzisha akili.huku nikiwa siamini ni nini kilichonitokea.hatimaye Kodi ya duka iliisha duka nikarudisha kwa mwenye nalo.nikauza vitu vyote vya dukani pia asilimia kubwa niliuzia members wa if.

Tokea hapo maisha yakawa ni kuunga unga mjini kwa kutumia uzoefu .Naishi kwa kulipwa madeni na kuongeza madeni mapya .nikajaribu kutafuta kazi mtaani na humu jf Lakini sikufanikiwa mpaka Sasa bado mambo yamekuwa magumu.

Kusudi la kuandika haya yote wakuu kwa Sasa nimekosa rafiki au hata mtu wa karibu wa kuzungumza naye magumu ninayopitia.mke amerudi kwao amechoka kukaa na mtu anayeishi maisha ya kubahatisha .Nimeamini wakati wa magumu hata wapendwa wako wa karibu wanajitenga na wewe

Wakuu najiona kama nafika mwisho na siku zangu zinahesabika kwa sababu nimebaki na mama yangu na mtoto wangu mdogo.wote wananitazama Mimi Lakini kiukweli jaribu limekuwa kubwa kuliko uwezo wangu.madukani madeni yamefika mwisho.

Wakati mwingine huwa napiga saidia fundi ikipatikana maisha yanaenda japo nakuwa slow kutokana sio mzoefu na hizo Kazi.Pia Nina diploma ya mechanical engineering na leseni class d ,e na c1,c2 na c3 Ila leseni kwa Sasa leseni ni ya kurenew

Napatikana kibaha kwa Mathias wakuu .mwenye ajira yoyote ya halali naomba anishike mkono
Nawaambiaga vijana nyie kuleni bata ila hapa duniani kila mmoja anamda atasota tu,ukiona maisha yamekunyookea sana juwa kuna siku utanyooshwa,ishi na watu vinzuri ili siku ukipitia kwenye msota wawe hata wawili wa kukishika mkono
 
Pole sana mkuu kwa changamoto yako, kaza moyo utavuka. Kama umeoa na wife anaendelea kukuheshimu ni jambo jema. Niliwahi kuanguka pia, tena vibaya sana. Kibaya zaidi hata mke wangu hakuniheshimu hadi aliondoka tena kwa influence ya wazazi wake.

Ila nashukuru nilirudi kwenye njia baada ya kupata kazi yenye mkataba mzuri sana Bwawa la umeme Rufiji. Kuanzia hapo, mambo yakawa poa, nikamaliza mkataba na kuanza kupata deals na kampuni tofauti hadi za mbali na nyumbani. Kwa hiyo amini na uendelee kupambana mkuu. Utashinda
Kasema mke wake kakimbia
 
Nimechelewa kuona tag yako Mjukuu...

Hata hivyo nitajitahidi kusoma comments zote za wadau ili nione alichoshauriwa nami nitaongezea ikibidi.

Kwakuwa JF ni pool, nina amini anaweza kushikwa Mkono akapata ajira ya udereva ama ajira za viwandani as nimeona amesoma mechanical engineering Kwa ngazi ya diploma.

Wito wangu, kama Kuna mtu mwenye nafasi ya ajira kwenye hayo maeneo mawili tajwa hapo juu vyema tumsaidie mtoa mada(Wanasema mpe nduguyo ajira badala ya kumpa mkate Kila Siku).

Wakati huu ambao atakuwa anashughulikiwa suala la ajira yake, iwapo itawezekana tumsaidieni japo kiasi kidogo cha fedha ili aweze kununua chakula ili apate kuishi na mtoto wake na Mama yake Mzazi ambao wote ni Wategemezi wake kwasasa
Nimepata wazo Kuna kiwanda kinaitwa Keds kipo picha ya ndege wanalipa kidogo nafuu na inalipwa Kwa wiki
 
Kwanza naona milango inafunguka, mke kukukimbia ni mlango mmoja huo umefunguka. Niliwahi kupitia hali kama yako na mke akaondoka. Kuondoka mke mambo yakarudi mdogo mdogo sasa anatamani awe mchepuko.
Bila mke nakuhakikishia utatoboa huu mwaka 2025, amini Mungu.
Daaah, alikpata ujasiri gani wa kuondoka mkuu?
 
Pole mkuu kwa changamoto za maisha, nina Imani siku si nyingi utajipata tu changamoto tumeumbiwa sisi sote wanadamu.
 
Ku renew driving license ni gharama kiasi gani kinatakiwa?

Pole sana. Lakini kadri mapambano yanavyozidi kuwa makali, ndivyo ushindi unavyokaribia.

Ondoa kabisa mawazo kwamba mwisho wako umekaribia, "awazavyo mtu nafsini mwake, ndivyo alivyo..."

Zichukulie hizi changamoto zote kama ngazi na darasa la kukuvusha hapa ulipo kwenda hatua nyingine.

Ianze Kwa kujiweka nadhifu, ujikae kinyonge hata kama unapitia wakati mgumu kiasi Gani, zingatia kwamba ni hali ya muda tu na itapita.
 
Pole sana mkuu kwa changamoto yako, kaza moyo utavuka. Kama umeoa na wife anaendelea kukuheshimu ni jambo jema. Niliwahi kuanguka pia, tena vibaya sana. Kibaya zaidi hata mke wangu hakuniheshimu hadi aliondoka tena kwa influence ya wazazi wake.

Ila nashukuru nilirudi kwenye njia baada ya kupata kazi yenye mkataba mzuri sana Bwawa la umeme Rufiji. Kuanzia hapo, mambo yakawa poa, nikamaliza mkataba na kuanza kupata deals na kampuni tofauti hadi za mbali na nyumbani. Kwa hiyo amini na uendelee kupambana mkuu. Utashinda
Mkeo ulimrudisha?
 
Pole Sana mkuu kwa magumu unayopitia.
Mungu akufanyie wepesi uinuke tena
 
Ukiwa unafanya biashara za magendo au dilidili kama zako hizo hutoi risiti na blaablaa jitahidi sana uwe umejiwekea EXIT plan maana hizo biashara huwa hazina lifespan ya kueleweka.

Kama mama yako ameshindwa kutibika arudi alipokuwa mwanzo, uza nyumba hela utakayopata tumia kama mtaji na nyingine ya kujikimu. Au kama unaviwanja uzaa upate pa kuanzia.Hakikisha kabla hujauza unabusiness plan ya kueleweka🤝

Jikaze,hao unaita marafiki wamekupa somo la msingi sana katika maisha. Usije kutegemea mtu yoyote hapa duniani.Ndomaana wengine wakifanikiwa pesa zao wanakula wenyewe maana uliteseka mwenyewe ni haki yako.

Wanasema ACHA KAZI UONE ILIVYOKAZI KUPATA KAZI!!!

Huwa siamini sana kwenye hizi biashara( UCHUUZI) zetu za kibongo za kuiganaigana.Ni bora ukazifanya kama part time tu.Ila kufanya kama ndio tegemeo lazima uwe na channel nyingi sana maana muda wowote umaskini unakuita.

1.unacheti cha MECHANICS- kwanini usiende gereji ukatumie ujizi wako japo mwanzo mgumu ila kama shule ipo ni swala ma muda tu.

2.Unaleseni ya kubeba abiria; kwanini usijitumbukize kwenye kazi ya udereva daladala???

#Jitafakari,chukua hatua!
#kataa ndoa,ndoa ni utapeli!!!
 
Habari za wakati huu,

Sijui wapi pa kuanzia Ila tangia mwaka 2018 niliamua kuacha kazi na kuanza maisha ya kujiajiri.

Kazi niliacha baada ya kuona biashara zangu zingine ndogo ndogo zinalipa Ila changamoto ilikuwa ni kukosa usimamizi nzuri.

Pia sababu nyingine ilikuwa kutoelewana na supervisor wangu kutokana na roho ya kijicho kuona maendeleo niliyokuwa nayo hayaendani na mshahara ninaopata.ingawaje sikuwahi kuwa na loss yoyote au kujibizana naye Ila alichokuwa anafanya kunipiga Vita ya chinichini.kwanza mmiliki wa kampuni alikuwa ni mwenyeji wa Kanda ya ziwa hivyo kufanya asilimia kubwa ya wafanyakazi kuwa watu wa Kanda ya ziwa.

Pili kwenye vitengo vyote waliweka watu wa Kanda ya ziwa. Mimi peke yangu ndio nilikuwa mtu wa kaskazini.hii ilipelekea supervisor wangu kutengeneza na kueneza sumu ya chuki kwa urahisi kuwa watu wa kaskazini ni wezi .turudi kwenye mada

Baada ya kuacha kazi mambo yalinyooka kuliko mwanzoni.niliwaza muda wote nilikuwa wapi kwanini sikuingia mapema kwenye biashara.Ndani ya miaka mitatu nilifanikiwa kupata sehemu ya kujihifadhi na kausafiri kutokana na wakati mwingine Mishe zangu zilikuwa za udalali.

Mwishoni wa mwaka 2022 mambo yalianza kwenda mrama baada ya kuhamia kwenye kibanda changu.Mama yangu mzazi alikuwa akiumwa kifundo Cha mguu na pilingili mbili za mgongo zilikatika pia na sukari ilikuwa ikimsumbua.Hivyo ilibidi aje dar as salaam kwa ajili ya tiba

Tulipambana naye kwa wakorea pale mbezi kwa msuguri ikashindikana tukahamia mhimbili huko nako hakukuwa na nafuu ya kudumu.wakati huo nilikuwa na mtoto mdogo ambaye alikuwa Hali chakula Wala usiku halali.Lakini changamoto haikushia hapo kwenye maisha ya nyumbani.usiku kulikuwa hakuna kulala Mara watu wanagonga mlango wengine wanafagia nje .ukichungulia nje huoni mtu yoyote .hili nilimaliza kwa njia maombi

Changamoto hizi hazikuishia nyumbani tu Bali hata sehemu zangu za kutafuta ridhki.nilikuwa na ofisi mbili moja ya uwakala nyingine ya duka la vinywaji vya jumla na rejareja.Pesa nyingine nilikuwa nazungushia kwenye udalali.

Siku isiyokuwa na jina naenda kufunga hesabu kwenye ofisi ya uwakala mambo hayakuwa mazuri.Wakala hakuwa na cash yoyote wa float.pesa iliyokuwepo ilikuwa ni kamisheni jumla yake Kama laki tatu na machenchi.kuulizia pesa nyingine nikaambiwa iko kwa wakala mwenzake.basi pale tukagawana faida nikaondoka.kufupisha stori Yule wakala alikuja akasema pesa ametapeliwa hivyo atanilipa mdogo mdogo.

Wakati huo nimeshauza gari la kutembelea ili ninunue guta.kumbe guta limeuzwa Mara mbili na Mimi ndiye mtu wa pili .kufupisha guta sikupata niliishia kulipwa mdogo mdogo.

Duka la vinywaji Mambo hayakuwa mazuri nilichezea vitasa Sana kwa TRA kutokana na mambo ya risiti .mbaya zaidi madeni yalikuwa mengi kwenye mabar na mapub .kuna meneja alifukuzwa kazi ,Kuna miliki alishindwa kulipa Kodi ya mwaka mzima Kama mwenye nyumba anavyotaka.

Kifupi ndani ya mwezi wa 11 mwaka 2022 maji yalifika shingoni ikabidi niende nyumbani Kilimanjaro kupumzisha akili.huku nikiwa siamini ni nini kilichonitokea.hatimaye Kodi ya duka iliisha duka nikarudisha kwa mwenye nalo.nikauza vitu vyote vya dukani pia asilimia kubwa niliuzia members wa if.

Tokea hapo maisha yakawa ni kuunga unga mjini kwa kutumia uzoefu .Naishi kwa kulipwa madeni na kuongeza madeni mapya .nikajaribu kutafuta kazi mtaani na humu jf Lakini sikufanikiwa mpaka Sasa bado mambo yamekuwa magumu.

Kusudi la kuandika haya yote wakuu kwa Sasa nimekosa rafiki au hata mtu wa karibu wa kuzungumza naye magumu ninayopitia.mke amerudi kwao amechoka kukaa na mtu anayeishi maisha ya kubahatisha .Nimeamini wakati wa magumu hata wapendwa wako wa karibu wanajitenga na wewe

Wakuu najiona kama nafika mwisho na siku zangu zinahesabika kwa sababu nimebaki na mama yangu na mtoto wangu mdogo.wote wananitazama Mimi Lakini kiukweli jaribu limekuwa kubwa kuliko uwezo wangu.madukani madeni yamefika mwisho.

Wakati mwingine huwa napiga saidia fundi ikipatikana maisha yanaenda japo nakuwa slow kutokana sio mzoefu na hizo Kazi.Pia Nina diploma ya mechanical engineering na leseni class d ,e na c1,c2 na c3 Ila leseni kwa Sasa leseni ni ya kurenew

Napatikana kibaha kwa Mathias wakuu .mwenye ajira yoyote ya halali naomba anishike mkono
Pole sana mkuu kwa changamoto unazopitia.

Ila mkuu kuanzia Sasa usisahau kutoa zaka / sadaka kwa Imani yako, kutoka kwenye kila senti unayoipata.......usipuuze hili nakuhakikishia milango yako itafunguka tena.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Sasa mali na utajiri zitakaporudi(Maana ni suala la muda) usisahau waliosimama na wewe wakati huu na walio kukimbia watakapoanza kurudi na visababu kedekede na tumachozi, usiusahau usaliti wao. Pole sana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom