Wapenzi walioanzia Chuoni ndoa zao zinadumu sana

Wapenzi walioanzia Chuoni ndoa zao zinadumu sana

Tangu nizaliwe mpka Leo hii nimekuwa mtu mzima sijawahi kuona wala kusikia eti kuna wanachuo wameoana ambao uhusiano ulianzia Chuo

Kwa kifupi tuu hizo ni ndoto za alinachaaaa
Wapo wengi mbn mifamo ipo mingi, simple eg. kigwangala na mkewe walkutana chuo na etcs
 
Ukipata nafasi oa/olewa na mpenzi wako ambaye mpo wote chuo sababu mnajuana uhalisia.

Tafiti isiyo rasmi inaonesha waliooana na wapenzi wao wa chuo ndoa zinadumu sana.

Na Ndoa nyingi za wapenzi walioanzia chuo zilidumu sana.
Mimi na mke wangu ni classmate chuo kimoja hapa bongo. Mwaka wa 10 tangu tuoane mwaka wa 14 tangu tuanze kuweka mipango ya pamoja. [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Hata mitaani siyo chuoni tu wanandoa waliokaa kwenye uchumba zaidi ya miaka minne ndoa zao hudumu sana kutokana na muda mrefu kusomana na kujua jinsi ya kuset mambo yanapoenda mrama tofauti na ndoa za siku hizi uchumba miezi sita miezi tisa ndoa mwaka ½ wanakutana mahakamani kugawana vyeti vya ndoa sijui wenyewe wanaita talaka.
 
Ukipata nafasi oa/olewa na mpenzi wako ambaye mpo wote chuo sababu mnajuana uhalisia.

Tafiti isiyo rasmi inaonesha waliooana na wapenzi wao wa chuo ndoa zinadumu sana.

Na Ndoa nyingi za wapenzi walioanzia chuo zilidumu sana.
Ke sisi tulioanzia sekondari?
 
Tangu nizaliwe mpka Leo hii nimekuwa mtu mzima sijawahi kuona wala kusikia eti kuna wanachuo wameoana ambao uhusiano ulianzia Chuo

Kwa kifupi tuu hizo ni ndoto za alinachaaaa
Wapo wengi wanaoana tembea uone.
 
Inategemea kuna wengine walikuwa kwenye mahusiano miaka kumi kabla ya ndoa, baada ya kufunga ndoa tu walidumu kwa miaka miwili ndoa ikavunjika.
 
Absolutely true
Nimeishuhudia ndoa yenye furaha kwa wazazi wangu toka nikiwa mtoto mpaka Leo Nina 20's
 
Hata mi ni shahidi, nafahamu kama 8 hivi ziko imara kabisa
 
Ni ngumu kwa wanachuo kuoana au kudumu kwenye ndoa kwa furaha muda mrefu akiwa wataoana. Sababu haswaa ni hizi.

1. Watu wenye kufanana kiumri, elimu na fani ni vigumu kufikiria kuoana au kufurahia maisha ya ndoa kwa muda mrefu. Wanachuo wanaangukia kwenye hilo kundi.

2. Tabia na maisha ya chuoni yako kimpito sana, yanakosa uhalisia wa kudumu (Fake life). Hata mahusiano yanayoanzia chuoni yanabebwa na mazingira ya chuo, wahusika wakimaliza chuo wanakuwa watu tofauti.

3. Chuo kinawaweka watu pamoja kijamii (hivyo watu wanajenga mahusiano kirahisi sana wakiwa chuoni), baada ya kumaliza chuo karibu kila mtu anasepa zake mbali kuanza maisha mapya au kurejea maisha yake ya awali kabla ya chuo (Na hii huvunja mahusiano).

4. Maisha ya chuo yanatoa uhuru mpana kwa mwanafunzi, kuanzia muda, pesa, tabia, mavazi, malazi, shughuli na tabia. Hili huwafanya vijana kutengeneza mahusiano ya rejareja kirahisi mnoo. Baada ya kumaliza chuo, kijana hurejea upya kwenye jamii yake na uhuru huo hupotea ghafla (jamii nyingi zinaupinga huo uhuru wa kijana), na hapo hapo kuua mahusiano ya rejareja ya kijana aliyoyaanzisha akiwa chuoni.
 
Ni ngumu kwa wanachuo kuoana au kudumu kwenye ndoa kwa furaha muda mrefu akiwa wataoana. Sababu haswaa ni hizi.

1. Watu wenye kufanana kiumri, elimu na fani ni vigumu kufikiria kuoana au kufurahia maisha ya ndoa kwa muda mrefu. Wanachuo wanaangukia kwenye
Points. Hongera
 
Ni ngumu kwa wanachuo kuoana au kudumu kwenye ndoa kwa furaha muda mrefu akiwa wataoana. Sababu haswaa ni hizi.

1. Watu wenye kufanana kiumri, elimu na fani ni vigumu kufikiria kuoana au kufurahia maisha ya ndoa kwa muda mrefu. Wanachuo wanaangukia kwenye
N ngum sanaaaa[emoji41]
 
Mnapata mda wa kufahamiana na kujuana mkiwa chuoni. Huo mda ndio unaofanya mdumu katika ndoa
 
Back
Top Bottom