Waraka uliowaondoa Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo CHADEMA huu hapa

Waraka uliowaondoa Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo CHADEMA huu hapa

Ila wakuu Mwita ni bonge la 'snitch', namkumbuka tangu Azania, jamaa ni msaliti mbaya!

Jamaa anatamaa mno halafu hana msimamo imara wa kusimamia anachokiamini. Ndio maana hata CCM walimnunua kirahisi!
 
Mbona waraka wenyewe ni wa kawaida sana hauna jambo la kuhatarisha maslahi ya chama. Ni uoga wa viongozi tu.
 
Chadema imeshakufa, thats all. Kwenye uchaguzi kunakuwa na kambi, kwann chadema ni dhambi kuwa na kambi na ni dhambi kutofautiana kimawazo na mtizamo?

Kama kambi ndio kufa CCM kimeishazikwa. Kuna kambi ya Lowassa itateswa na kambi ya Sumaye. Kosa la Lowassa kuwanunua wapiga kura za wagombea wa CC ili mama Nagu ashinde. Siri zote zitakuwa nje nje. Uko wa Kikwete mawazo yote yametuama Lindi. Sana sana ni Membe ikishindikana walau Migiro. Lkn mkuu pia anapresha ya Zanzibar ambako kuna Salim na Bilal. Koo zilizoko Mbeya zinaweka kambi kwa Mwakyembe na Mwandosya. koo za ziwa zina Wassira na Maghufuli. kuna uko wa Makamba, ukoo wa wangoni na Nchimbi, ukoo wa wanyamwezi na Sitta. hata Pinda anaangalia upepo kama Tibaijuka. kila uko unamtafutiatmwenzie anguko potelea mbali anguko la chama.
 
Dr. Kitila Mkumbo katumia elimu yake vibaya. Citation and referencing ya Obama is quite irrelevant, invalid and unreliable.



Matumizi mabaya ya madaraka yanayoweza kuhusishwa na ufisadi. Taasisi yetu inayo kamati ya tenda ambayo iko chini ya kamati ya makatibu na wakurugenzi. Lakini uzoefu unaonyesha kwamba kamati hii haifanyi kazi imezimwa kimya kimya na wajumbe wote wa kamati ya tenda kwa kuwa ni wachumia tumbo wanaojigonga kwa wakuu, wamekubali kuzimwa. Leo ikidaiwa kamati hiyo ilete nyaraka za mchakato wa manunuzi ya magari, pikipiki, vifaa vya kueneza taasisi, set ya televisheni iliyofungwa ofisini kwa mtendaji mkuu, hawana. Manunuzi haya yote yote yanafanywa na wakuu hasa hasa mkuu wa taasisi bila utaratibu wowote jambo ambalo ni hatari na linarahisisha matendo ya kifisadi. Bila aibu, mkuu wa taasisi ndio amekuwa mnunuzi wa vifaa vyote vya chama nje ya nchi kwa bei anayoijua mwenyewe na ambaye haihojiwi popote. Huu ni mfano wa wazi wa mgongano wa kimaslahi jambo ambalo ni hatari kwa kiongozi mkubwa wa taasisi kama yetu inayojitambulisha katika kupinga vitendo vya ufisadi na uvunjifu wa maadili ya uongozi kwa ujumla -Kitila Mkumbo
 
Upo katika huu uzi kwa msukumo wa "dini" ya Zitto Kabwe..... bhaaasi!

NANI TUMUUNGE MKONO KUCHUKUA NAFASI YA MKUU:
Baada ya utangulizi huo unaoonyesha kinagaubaga kwamba tunahitaji mabadiliko, hatua iliyofuata ilikuwa ni kuangalia nani anaweza kuleta mabadiliko tunayohitaji. Ni vema ikazingatiwa kwamba mtu ambaye tungemuunga mkono lazima awe ni mtu mwenye uwezo mkubwa kuliko tunayetaka kumtoa. Awe ana qualities za kiuongozi na zaidi sana awe na uwezo wa kupambana na mkuu aliyeko. Tukileta mtu asiyefahamika sana kwenye mifumo ya taasisi yetu hata kama angekuwa mzuri kiasi gani hatachagulika na mkuu aliyeko atarudi kwa urahisi na kuendelea kuididimiza taasisi.

Katika kuchunguza ndani ya taasisi tuliridhika kwamba mtendaji mkuu msaidizi ana sifa zote tulizozitaja hapo juu ingawa kila mwanadamu ana udhaifu wake. Ni dhahiri pia kwamba udhaifu wa mtendaji mkuu msaidizi unarekebika kuliko wa mkuu aliyepo. Kwa ujumla mtendaji mkuu:

Ni kiongozi anayeweza kuongoza taasisi bila kujenga makundi akijali zaidi kazi ya taasisi kuliko maslahi binafsi.
Ameonyesha kwa vitendo kwamba hana maslahi binafsi kwa kuwa tumeshuhudia akifanya kazi nyingi za taasisi bila kudai malipo kwa njia ya posho ama vinginevyo.

Anaheshimika na viongozi wa ndani na nje ya taasisi jambo ambalo ni la muhimu sana kwa ustawi wa taasisi na kwa yeye kuwa mkuu wa taasisi tunatarajia wakubwa wengi sana kutoka nje ya taasisi yetu kuiamini na hata kujiunga nasi katika kuhakikisha tunafanikisha lengo la taasisi.

Ni msomi wa kiwango cha juu na mwenye uwezo mkubwa katika kuchanganua mambo ya kiuchumi, kisiasa, kijamii, kimichezo, nk jambo ambalo ni muhimu sana kwa kuwa ni hatari kuwa na kiongozi asiye na ujuzi wa kutosha kwenye masuala kama hayo.
Ndani ya taasisi anakubalika kwa makundi yote ya vijana, wazee na akina mama.

Uongozi wa sasa wa taasisi yetu umefanya tuonekana kwamba taasisi yetu ipo kwa ajili ya kuvuruga amani ya nchi. Yote hii ni kwa sababu tumekuwa hatuna mbinu mpya za mapambano zinabadilikabadilika zaidi ya maandamano ya kila mara. Kwa kuzingatia utamaduni wa watanzania wa kupenda amani, kuna haja ya kufuta hii taswira na njia rahisi ni kubadilisha uongozi wa taasisi haraka iwezekanavyo.

Uelewa wake wa mambo ya kiuchumi ni muhimu sana kwa taasisi kwa sasa. Tunahitaji kuja na vyanzo vipya vya mapato ikiwa tunahitaji kufanikiwa. Mkuu aliyepo si kwamba ameishiwa bali hana mbinu za maana za kuiimarisha taasisi kimapato kwa ajili ya malengo yake ya mbele.

Exposure kubwa na kukubalika katika siasa za kimataifa. Tunahitaji kiongozi ambaye anazifahamu siasa za kimataifa na anayeweza kuungwa mkono na viongozi wengi wa kimataifa. Ni hatari kutegemea utaweza kufanikisha malengo kama ya taasisi yetu bila mpango kabambe wa kuungwa mkono na jumuia ya kimataifa. Mpaka hivi sasa hakuna mpango wowote wala hata mchakato wa maana kuwa connected na jumuia ya kimataifa. Kiongozi wetu mkuu wa sasa yupo ‘too local’ na hana mawasiliano yeyote ya maana na viongozi wengine katika kanda na kimataifa. Ndio maana mkuu huyo na mtendaji wake mkuu wamekuwa hawaonekani katika matukio makubwa ya kimataifa. Hata katika kutoa maoni katika mambo makubwa ya kitaifa na kimataifa viongozi hawa hawapo. Kwa kifupi kwa sababu ya aina ya viongozi tulio nao, nafasi ya taasisi yetu katika nyanja za kimataifa haipo!

Aina na staili ya uongozi wa sasa wa taasisi yetu ni kina kwamba nchi hii haipo hadi taasisi yetu itakapochukua dola. Yaani tunafanya mambo kama kwamba tutaanza upya kabisa tukichukua dola. Ni kwa sababu tumegombana na kila mtu katika utawala wan chi, vikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama. Ukweli ni kwamba tutavihitaji vyombo hivi kabla na baada ya kuingia madarakani na ni ndoto kudhani kwamba tutakabidhiwa nchi kwa kugombana na kila mtu. Ni kwa sababu ya mtazamo kama huu ndio maana wakuu wetu wa sasa hawaonekani kabisa katika shughuli za kitaifa kama vile sherehe za uhuru wan chi, n.k.

Uwezo wa kuwaunganisha wasomi wa kada mbalimbali, wafanyabiashara wakubwa, watumishi wa umma na sekta binafsi, nk katika kupata muunganiko wa mawazo na kutoka na sera murua zinazogusa kila sekta. Hili la kuwashirikisha litaenda sambamba na kutoa elimu kwa wote waelewe na watuunge mkono. Tunasema hivi kwa kuwa watu wa kada mbalimbali hawajaelewa sera zetu juu ya mambo yanayowahusu mfano wafanyabiashara wakubwa, wawekezaji, wakulima, watumishi, wanafunzi,nk na hivyo hawajawa tayari kutuunga mkono. Kile kinachofanywa wakati wa uchaguzi kwa njia ya ilani ya uchaguzi na elimu kutolewa kwa njia ya kampeni majukwaani hakitoshi. Tunahitaji watu wajue tumeunda think tank kwa ajili hiyo na baadaye wajue nini kimetokana na think tank hiyo ili wajadili na kutoa maoni na hatimaye tutoke na kitu kinachokubalikwa na wananchi wote. Na tuna imani hilo tunayempendekeza ana uwezo nalo.

Kubwa zaidi ni kwamba alishaiangalia taasisi yetu na kuona mambo yanayohitaji mabadiliko na kujiangalia yeye na kuridhika kwamba ataweza kuleta mabadiliko tunayoyahitaji na ndipo mwaka 2009 aliamua kujitosa kuutafuta ukuu wa taasisi yetu kabla ya kuombwa kumwachia aliyepo. -MM3
 
we si uwe busy na chama chako ...mbona unawashwa sana na mambo yasiyokuhusu

Hayanihusu? pata ujumbe mdogo kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM:


"Mtakwenda mtarudi mimi ndio Rais wenu hakuna mwingine mtakae mkimbilia"

Dr. Jakaya Khalfan Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM.
 
Huwezi kuona kitu ambacho hutaki kukiona. Ukianzisha kikundi chako ndani ya Chama kama siyo kukigawa maana yake nini. Usituambie kuwa demokrasia unayoielewa wewe ndiyo maana ya demokrasia.

Mpinzani wetu hana historia nzuri ya utendaji uliotukuka ndani na nje ya chombo cha uwakilishi. Hakuonyesha utendaji wowote wa pekee alipokuwepo kwenye chombo mwaka 2000 -2005 na hata alipopewa uongozi wa upande wetu ndani ya chombo tokea 2010 hadi leo 2013 hajafanya lolote la kutukuka ndani ya chombo hicho.

Mpinzani wetu hana uwezo mkubwa wa uelewa wa mambo mbalimbali ya uchumi, jamii, utamaduni, michezo, nk. Si tuelimu yake ya darasani ni ya magumashi bali pia vipaji na akili ya kuzaliwa havijaonekana katika maisha yake.

Uzalendowampinzani wetu unatia shaka akiwa hajaonyesha lolote la maana katika kulitetea taifa letu kimataifa. Ingawa ameshapata nafasi lukuki ya kwenda nje ya nchi lakini mara zote akifika huko ni kuiponda tu nchi yake. Ingawa anayo majukwaa ya kufanya hivyo akiwa ameshakuwa mwakilishi mara mbili kwenye chombo chetu lakini hatujawahi kumsikia akiibua kashfa mahsusi ya ufisadi na kuisimamia zaidi ya yeye mwenyewe wakati fulani fulani kutuhumiwa kwa ufisadi mfano pale alipokopa kwenye shirika la umma na kugoma kulipa mkopo. -MM3
 
Hapa, si kuhodhi madaraka daima! Bali ni kutumia njia halali zilizowekwa na taasisi husika katika kushughulikia suala husika. Kinyume cha hapo ni usaliti au kujaribu kuigawa taasisi husika. Sina hakika (labda wana CDM wanielimishe) kama akina Mkumbo (Dr.) wameweka ushahidi katika waraka wao kuonesha kwamba wamejaribu kutumia njia zote za kikatiba katika kulifanikisha walilokuwa wanapigia chapuo katika waraka huo ambao kwa bahati mbaya waliukana haraka sana mara ulipovuja..

Mpinzani wetu ni mgumu sana katika kuchangamana na makundi yote ambapo vijana humwona kama si mwenzao kiumri na kifedha, wanawake humwona kama malaya anayependa kutumia miili yao kujistarehesha wakati wazee humwona kama mtu anayedhalilisha hata nafasi aliyopewa kwa kufanya uhuni waziwazi hata kuvunja ndoa si ya kwake tu bali hata za watu wengine.

Mpinzani wetu hana mahusiano mema na mazuri na viongozi wa ngazi za chini kutokana na dharau nyingi anazozionyesha pale anapokukutana na viongozi wa ngazi za chini akiwa katika kuijenga taasisi hii. Hutumia muda mwingi kuwaponda viongozi wenzake hata kufikia kutamka mara nyingi kwamba kama kiongozi hawezi kujigharamia nauli na malazi ya kutoka mahali fulani kwenda mahali fulani kwa siku kadhaa hafai kuwa kiongozi bila kujali kwamba kuna viongozi wetu wana moyo na taasisi hii na ndo wameifikisha hapa ilipo lakini hawana uwezo wa kifedha na hivyo kauli kama hizo za mkuu huyu huona kama anawadharau kwa kuwa yeye ni tajiri. Hii imemfanya kutopendwa na viongozi wengi wa ngazi ya chini hivi sasa na kutoa fursa ya pekee kwa tunayemtaka.
Mkuu aliyepo amekuwa na mkakati unaoitwa kuondoa watu wa zamani. Jambo hili linawaudhi sana viongozi wa ngazi za chini ambao wanaona kama baada ya kuifikisha taasisi mahali ilipo kwa sasa wanaonekana hawana maana tena. Wengi wamefikia kuapa kwamba kama mwendo ni wa kuwaondoa watu wa zamani basi na yeye ni wa zamani lazima aondoke.

Mpinzani wetu amejionyesha dhahiri kujipenda na kujijali nafsi bila kujali watu wa hali ya chini. Matukio mawili yanamwacha uchi katika hili pale alipolitangazia taifa kwamba wawakilishi wetu wote hawatachukua posho za vikao halafu yeye na wengine wote wanazichukua hadi leo na kumwacha mtendaji msaidizi peke yake. Na la pili linalofanana na hilo ni pale alipotangaza kutotumia gari la serikali ambalo ni la kifahari kisha akalirudia kimya kimya.-MM3
 
Mpinzani wetu ni mgumu sana katika kuchangamana na makundi yote ambapo vijana humwona kama si mwenzao kiumri na kifedha, wanawake humwona kama malaya anayependa kutumia miili yao kujistarehesha wakati wazee humwona kama mtu anayedhalilisha hata nafasi aliyopewa kwa kufanya uhuni waziwazi hata kuvunja ndoa si ya kwake tu bali hata za watu wengine.

Mpinzani wetu hana mahusiano mema na mazuri na viongozi wa ngazi za chini kutokana na dharau nyingi anazozionyesha pale anapokukutana na viongozi wa ngazi za chini akiwa katika kuijenga taasisi hii. Hutumia muda mwingi kuwaponda viongozi wenzake hata kufikia kutamka mara nyingi kwamba kama kiongozi hawezi kujigharamia nauli na malazi ya kutoka mahali fulani kwenda mahali fulani kwa siku kadhaa hafai kuwa kiongozi bila kujali kwamba kuna viongozi wetu wana moyo na taasisi hii na ndo wameifikisha hapa ilipo lakini hawana uwezo wa kifedha na hivyo kauli kama hizo za mkuu huyu huona kama anawadharau kwa kuwa yeye ni tajiri. Hii imemfanya kutopendwa na viongozi wengi wa ngazi ya chini hivi sasa na kutoa fursa ya pekee kwa tunayemtaka.
Mkuu aliyepo amekuwa na mkakati unaoitwa kuondoa watu wa zamani. Jambo hili linawaudhi sana viongozi wa ngazi za chini ambao wanaona kama baada ya kuifikisha taasisi mahali ilipo kwa sasa wanaonekana hawana maana tena. Wengi wamefikia kuapa kwamba kama mwendo ni wa kuwaondoa watu wa zamani basi na yeye ni wa zamani lazima aondoke.

Mpinzani wetu amejionyesha dhahiri kujipenda na kujijali nafsi bila kujali watu wa hali ya chini. Matukio mawili yanamwacha uchi katika hili pale alipolitangazia taifa kwamba wawakilishi wetu wote hawatachukua posho za vikao halafu yeye na wengine wote wanazichukua hadi leo na kumwacha mtendaji msaidizi peke yake. Na la pili linalofanana na hilo ni pale alipotangaza kutotumia gari la serikali ambalo ni la kifahari kisha akalirudia kimya kimya.-MM3

Sawa kabisa hizi ni hoja zinazotakiwa kufanyiwa kazi! Lakini si njia za kificho, kutumia njia za kificho ni woga wa demokrasia. Kwa nini huyo mpinzani wao (wenu) asikabiriwe katika vikao husika na ikishindikana (yaani kama vikao haviitishwi) aandikiwe barua au waraka wa wazi badala ya kuwa waraka wa siri. Na ikishindikana hapo wanachama na wapenzi/mashabiki wa chama waambiwe wazi wazi katika mikutano ha hadhara. Na ikifanyika hivi hakutakuwa na fitna bali atapima mwenyewe na kuchukua hatua.

Mbinu ilijaribu kutumika ya waraka wa siri si sahihi kabisa na ingefanikiwa amini nakwambia chama kilikuwa kinaelekea shimoni kwa maana watu wasio amini nafsi zao na kushindwa kukabiliana kasoro hadharani, hawafai hata kidogo wakitishwa na wenye nchi na dola, kutabaki chama hapo?
 
Kumbe CCM wavumilivu sana,yaliyotokea kama yangekuwa yametokea CDM nadhani hiki chama kisingekuwepo hadi sasa,hawa viongozi wanaowafukuza wenzao ndiyo wanaoua chama hawana jema na hiki chama zaidi ya maslahi yao wenyewe muda wao umefika lazima na wao waende
 
Sawa kabisa hizi ni hoja zinazotakiwa kufanyiwa kazi! Lakini si njia za kificho, kutumia njia za kificho ni woga wa demokrasia. Kwa nini huyo mpinzani wao (wenu) asikabiriwe katika vikao husika na ikishindikana (yaani kama vikao haviitishwi) aandikiwe barua au waraka wa wazi badala ya kuwa waraka wa siri. Na ikishindikana hapo wanachama na wapenzi/mashabiki wa chama waambiwe wazi wazi katika mikutano ha hadhara. Na ikifanyika hivi hakutakuwa na fitna bali atapima mwenyewe na kuchukua hatua.

Mbinu ilijaribu kutumika ya waraka wa siri si sahihi kabisa na ingefanikiwa amini nakwambia chama kilikuwa kinaelekea shimoni kwa maana watu wasio amini nafsi zao na kushindwa kukabiliana kasoro hadharani, hawafai hata kidogo wakitishwa na wenye nchi na dola, kutabaki chama hapo?

Subiri kidooogo, utapata jibu, niko bize nasoma nyaraka nilizotumiwa kwenye email. Kimbembe chaja.
 
Kamanda Mungi huwa sikupingi hata siku moja. Ni kweli kuwa kugombea ubunge ndani ya Chama ni jambo kingine ila nilimuhusisha Waitara na hili la kugombea ubunge na huu Usaliti wanaoufanya ndani ya chama kwa kuwa km kweli yeye ni Mwana chadema "Mwaminifu"na anaetarajia kuja kuwa mgombea wa ubunge kwa kupitia Cdm, ni Chadema ipi hiyo wakati wanakipasua?

Unajua Bwana Mungi, watu au Wasaliti hawa sio tu lengo lao ni kuwa viongozi wakuu wa CDM bali pia ni Kukiuwa ili kufanikisha malengo ya waliowatuma.
Sasa najiuliza ikiwa Cdm kitakufa huku wao wakitamani kuwa viongozi je wataongoza nini sasa!?

Ndio maana nimemtaja Waitara na kuhusika kwake ktk huo Mkakati wa MM2013 huku yeye akiwa ni M2! Na anaetaka kuwa Mbunge atakuwa mbunge kivipi huku kukiwa na Mkakati wa kuiuwa Chadema?
Kumbuka kwamba mlipa Zumari ndio Mchagua wimbo!

Mkuu sokoinei,
Nakubaliana na wewe kabisa, kwamba huyu jamaa ni njaa sana.
Kwa watu wanaokumbuka wakati yupo Chuo kikuu mlimani watakumbuka jamaa alivyokuwa makini kujenga hoja, lakini alikuwa mla rushwa mkubwa. The guy was very corrupt.
sokoinei,
Vyanzo vyangu vimethibitisha kwamba M2 ni Mzee Said Arfi. Labda kama M2 ni taasisi ndiyo sijui.
 
Last edited by a moderator:
Waraka huu ni wakinafiki kwa sababu kwanza hauna mtazamo wa kukijenga Chama bali ni kikundi kidogo kinachotafuta maslahi binafsi, pili kama kweli kakikundi haka kangekuwa na nia njema kangefikisha mapendekezo yake kwa njia ya uwazi na bila kumuogopa mtu yeyote na si kwa njia hii ya kificho, ambayo naweza kuitafsiri kama ni ishara ya woga au kuto kujiamini kwa kakikundi haka. Tatu kakikundi haka kapo kwa ajili ya aidha kukizalilisha chama kwa kuonyesha kuwa hakina wanachama wenye uwezo zaidi ya huyo wanayempigia debe au wana maslahi binafsi na mtu huyo. KAMA KWELI KAKIKUNDI HAKA KANA NIA NJEMA WANGESHAURI MAMBO YOTE HAYO KWA UWAZI, KUJIAMINI, BILA KUJIPENDEKEZA KWA MTU FULANI NA KWA KUFUATA NJIA SAHIHI. Hivyo basi nashawishika kuamini kuwa kakikundi haka sio tu kwamba kana nia ya kukidhoofisha chama,ila pia ni kawatu walafi wa madaraka, posho na malimbukeni wa madaraka wanaodhani uhai wa chama unawategemea wao tu. NASHAURI kwa wakati tulionao hekima itumike, tuvumiliane lakini tuangaliane kwa jicho la TATU hadi hapo tutakapopata muda mzuri wa kukosoana na ikibidi kusahihishana, kwani kwa kipindi hiki tulichonacho ni sawa na kuwapa faidi wenzetu wa upande wa pili wasiojuwa umuhimu wa kuwa na chama imara cha upinzani na kuuona kama ni uadui. CDM tuvumiliane, tuelimishane huku tukiwasoma wapinzani wetu ambao licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kifedha kutokana na ufisadi wanaoufanya bali pia wamejiwekea mizizi ya kutosha hadi ndani ya kambi yetu, tutatumika sana na tusipoangalia mwisho wetu utakuwa mbaya.
 
Very poor document, sasa mbona hii document inaongelea watu badala ya ideas. Mkumbo usipokuwa makini sasa Mwigulu atakuchezea.
 
Wachaga waliopo Chadema ni waaminifu sana. rekodi zangu zinaonyesha hakuna mchaga aliyewahi kufukuzwa Chadema.
 
Wakati Mh. Godbless Lema, Mbunge wa Arusha mjini aliporipotiwa na vyombo vingi vya habari kuwa alimrushia tofali mwenyekiti wa chadema mkoa wa Arusha aliyesimamishwa ndugu Mwigamba na kuamuru anyang'ang'we Laptop yake ili ichunguzwe, Mimi ni mmojawapo ambaye niliona kile kilikuwa kitendo cha uonevu sana. Ilifikia hadi ndugu yangu mwanasheria Nyaronyo Kicheere kutoa ule uchambuzi wake mahili ulio-classify aina ya makundi yaliyopo chadema, kundi la Lema akiliita ni la watu wa kutumia mabavu.

Lakini ukiangalia vizuri kile kitendo alichokifanya Lema ndicho kilicho-trigger a chain of events hatimaye chama kikapata ushahidi usio wa mashaka wa usaliti ndani ya chama. Tokea kwisha kwa uchaguzi wa mwaka 2010 kumekuwepo tuhuma za usaliti zikiwaandama watu kadhaa kinara wao akiwepo ni Zitto, lakini kwa kuwa mwanasiasa huyu anajua kusafisha traces/clue kwenye mambo haya palikuwa hakuna sehemu ya kumbana. Zitto ni mjanja kama walivyo wanasiasa wengine ambao huwa hawaachi trace za ushahidi katika uovu wao. Zitto mara nyingi amesikika kwenye vyombo vya habari akisema mwenye ushahidi wa tuhuma zake alete. anajua matendo anayoyafanya gizani ni ngumu mtu kutoa ushahidi ingawa ushahidi wa mazingira wa tuhuma zake nyingi ni mkubwa kuliko hata huo ushahidi anaouomba. Nafikiri ni sababu hii ya ushahidi wa mazingira kuwa mkubwa sana ndio iliyopelekea hata uongozi wa chama chake kumweka pembeni kwenye baadhi ya shuguli za chama jambo ambalo lipo dhahili shahili tokea siku nyingi.

Kama ilivyo katika sheria, "there is no perfect crime", katika uhalifu wowote ule lazima kutakuwa na clue zilizoachwa na perpertrators wake. Watu waki-dig dipper tu watazipata hizo clue. Cahedema isingeweza kuchimbua tuhuma za zito kwa undani kwa kuwa haina instrument za kuweza kufanya hivyo kama ilivyo serikali, lakini hata hivyo ilijitahidi kupata ushahidi mwingi sana wa mazingira ambapo zitto ame-appear mara nyingi akiwa at the centre of the saga. Mimi naomba kusema kuwa nimeona umuhimu wa kuwepo lile kundi la chadema mabavu linaloongozwa na Mhe. Lema kwa kuwa bila lile kundi si ajabu 2015 tungehujumiwa kuliko kawaida na ingetukatisha tamaa wapenda mabadiliko wengi sana.
 
Back
Top Bottom