Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sioni hoja hapaa
Hakuna sekeseke la udini kwenye nchi hii. Ila kuna kakikundi kanatumiwa ili kuleta chokochoko za kidini.
We bwana nahisi unatumia mihadarati.
Tatizo sio mpaka ulione ww, Zuwena ametajwa vipi kwenye huo wimbo?
Mimi ni miongoni mwa mamilioni ya watanzania ambao wana ji identify themselves kama mashabiki wako wakubwa. But kina kitu kimoja ambacho kwa maoni yangu ninaona hakipo sawa . Nacho ni kuhusu wmbo wako uitwao YAHAYA. Wimbo wako ni mzuri na unaelimisha jamii but kwa nini usingetumia jina tofauti na YAHAYA. Kwanini ninasema hivyo?
1. YAHAYA ni jina la kiislamu, na miongoni mwa majina ya kiislamu yenye maana kubwa kwa waislam.
2. Wewe ni mkristo wa madhehebu ya wasabato.
3. Hapa kwetu nchini Tanzania kuna vugu vugu la waislamu na wakristo. Waislamu wamekuwa makini sana kwa kila kitu kinacho fanywa na mtu yoyote yule mwenye jina la kikristo hususani pale maslahi ya dini ya kiislamu ama jina la kiislamu linapotajwa. Sihitaji kulizungumzia hili kwa kina kwa sababu naamini huwa unafuatilia taarifa mbalimbali za habari so am sure as hell unafahamu ni kitu gani kinaendelea kati ya wakristo na waislamu Tanzania wakati huu.
( KITU CHA MSINGI KUELEWA HAPA NI KWAMBA, KITU CHOCHOTE KILE KITAKACHO TAJWA NA MKRISTO DHIDI YA UISLAMU AMA MUISLAMU KWA NAMNA YOYOTE ILE KINAWEZA KUCHUKULIWA KAMA KASHFA DHIDI YA UISLAMU )
Hivyo basi wimbo wako wa YAHAYA ingawa una ujumbe mzuri, but unaweza kukuletea matatizo na waislamu wa Tanzania ambao wanaweza kuuchukulia kama kashfa dhidi yao. Maadui zako wanaweza kuitumia hiyo kama loop hole na ku dress beef lenu kulifanya lionekane kama beef kati yako waislamu.
MAPENDEKEZO: Nikiwa kama shabiki wako, ninakushauri ubadilishe haraka iwezekanavyo jina la wimbo YAHAYA na kutafuta jina lingine lolote lile. Katika kutafuta jina nakushauri utafute jina ambalo halihusiani na jina la dini yoyote kati ya ukristo na uislamu. Unaweza kutumia majina yanayo tumiwa na watu wa dini zote kama vile MAWAZO.
Ukibadilisha jina la wimbo wako, utajijengea heshima kubwa sana kwa mashabiki wako ambao ni waislamu na watachukulia hiyo kama heshima kwao.
Sina mengi ya kuongea zaidi ya hayo. Natumaini umenielewa.
NAKUTAKIA MAANDALIZI MEMA YA MAADHIMISHO YA MIAKA 13 YA LADYJAYDEE.
Mimi ni Muislaam lakini sioni tatizo hapo. Kama ameutukana Uislaam au amemtukana Mtume Yahya au Issa au Ibrahim, hapo tutakomaa nae, lakini kama anamsifia mpenzi wake aitwae Yahaya. Sioni tatizo, mwache ajifaraguwe.
Mkuu, naheshimu sana Mawazo yako!
Binafsi sioni kama kuna tatizo hapo, ingekua mbaya kama ni video halafu inaonesha mambo ambayo yanagusa imani moja kwa moja!...kwa mfano kuhusisha Holy Quran (Kitabu), Jeneza, Maziara, Msikitini nk.
Weka "Audio" tusikie mashahiri yake ili tusafiri pamoja katika mawazo yako!
hakika wewe ndio m-baguzi inaonekana hata kusalimia mtu lazima umjue ni wadini gani? Kwahio unataka jide kwa vile ni msabato aimbe nyimbo za kisabato kwa wasabato?
as practice muslim ni jukumu langu kuona tatizo..
naongelea nyimbo ya Mr. paul zuwena ...
majina si kigezo cha uislam
unalazmisha kilichopo kichwani mwako kiwe majibu,umesahau mtoto iddy,radhia n.k
[B said:Lazaro[/B] john;6560206]sasa unatangaza udini au? mbona ueleweki