Mzee Warioba amesema zipo shutuma kwamba Tanganyika ilijivua na kuvaa koti jipya la muungano ambalo hapana shaka Tanzania bara kuonekana kufaidi matunda ya muungano kuliko Wazanzibari hata kupelekea Tanzania kuonekana ndiyo ile Tanganyika iliyo kufa.
Hali hiyo ndiyo inayofanya ongezeko la kero za muungano.Kwa maneno yake Wazanzibari wanaona ni ujanja tu ulitumika kuinyang'anya mamlaka yake Zanzibar nakisha kuiua kabisa na labda ndiyo chanzo cha hali duni za maisha ya Wazanzibari.
Wangetamani wajiunge na umoja wa nchi kama OIC unaojumuisha nchi za kiislamu hatua ambayo ingebadili kipato chao lakini haiwezekani kwakuwa koti linavaliwa Bara kwa mgongo wa muungano.
amesema tume yake ime angalia options nyingi ili kuondosha Muonekano huo lakini imeshindwa kupata balikurejesha pendekezo la kwenye rasimu ya kwanza la serikali tatu.
Ame chukua muda mrefu hadi kuchosha kuelezea hilo naona baaba ya kuhisi ccm wasinge taka hata kusikia serikali tatu.Kwakweli ameonyesha kuwa Wazanzibari walikuw wanataka kitu kingine siyo serikali mbili tena kitu ambacho ni mwiba kwa ccm.
Na hadhani kama wangetaka serikali moja kwani hiyo ni kuimeza kabisa Zanzibar.amesema zaidi ya 60%ya Watanzania Bara walitaka tatu hali kadhalika huko Zanzibar.
Nakiasi kikubwa Zanzibar walitaka muungano wa mkataba.
Tupo katika takuli kubwa wa kuu hali ndiyo hiyo
Naunga mkono serikali tatu Na huo muungano sioni faida zake uvunjwe tu
Sasa hizo tatu ni za nini iwapo hakuna muungano?Naunga mkono serikali tatu Na huo muungano sioni faida zake uvunjwe tu
Naunga mkono serikali tatu Na huo muungano sioni faida zake uvunjwe tu
Japo naunga mkono serikali 3, lakini Zanzibar itageuka kuwa tawi la Al Qaeda
Umeishawahi kaa na wazanzibari mkaongea kuhusu muungano ukasikiliza maoni yao?
Tutakuwa viziri mjini hapa kwa ving'ora vya misafara ya maraisi wa 3.....sasa wakiwa watembezi kama huyu bado watakuwa wanagongana angani
Umeishawahi kaa na wazanzibari mkaongea kuhusu muungano ukasikiliza maoni yao?
mi nimewasikia wanataka madaraka kamili lakini angalau serikali tatu kuliko mbili au moja
tunazunguka sana ila suluhisho ni serikali moja na znz iwe mkoa rasmi au muungano uvunjwe tukutane EAC,kwa hali hii matatizo yatajirudia tena na znz wataendelea kulalamika wanataka mamlaka kamili
Marais 3!!!!!! what a nice chance to become a president one day
Ha ha ha ha ha aaa,Mkuu unanivunja mbavu hapa,mmoja tu tuliambiwa tutakula nyasi,sasa watutu Si tutaambiwa tujile wenyewe!
wewe ndo huoni faida yake lakini sisi chama chetu cha ccm ni muhim sana, wewe nahisi ni upinzani weweNaunga mkono serikali tatu Na huo muungano sioni faida zake uvunjwe tu
Naunga mkono serikali tatu Na huo muungano sioni faida zake uvunjwe tu
Huwezi kuwaridhisha wazanzibari ni watu wenye kupenda malumbano. Zenj kuunganika na nchi kubwa ya tanganyika, si lazima tanzania ionekane kama ndio iliyokua tanganyika? ndio maana waasisi wakaona lazima zanzibar iendelee kua na utambulisho wake kwa kua na serikali yake ambayo hakika ina strong autonomy. Mfumo wa serikali tatu hakika hauna maslahi kwa zanzibar ila unatimilisha hatua muhimi kwa wale wanzibari wenye nia ya kuvunja muungano.
Hizi hassle zote za nini?. Kwani nani amesema wananchi wanataka muungano?.
kwa mazingira yalivyo kwa sasa nchini, serikali tatu ni njia ya kuelekea katika uvunjifu wa Muungano wakati huo huo serikali mbili kwa sasa wala hazina hata mandate ya Watanzania wengi.
Kwa nini kama nchi mbili tunapita njia ndefu yenye gharama kubwa za kisiasa na kiuchumi wakati kuna njia fupi isiyo na gharama kubwa kama hizo!.
Kura ya maoni kuhusu kuwepo muungano au hapana ni mwarobaini kisiasa na bila hivyo, ni kuwalazimisha wananchi wakubali au kukataa serikali tatu huku wameziba options zingine za serikali moja, mbili, etc.
Itakuwaje wananchi au bunge likikataa hii Rasimu ya Katiba hasa kipengele cha aina ya serikali?.
Ndiyo maana tume ya Jaji Warioba inataka iendelee kuwepo hata wakati wa mchakato wa bunge la Katiba na kura ya maoni kwa sababu ulaji bado uko mezani kwa maana kuwa, wanafahamu kuna uwezekano mkubwa baadhi ya vipengele vya Rasimu ya Katiba (serikali tatu) vikakataliwa na wabunge wengi hasa ikichukuliwa kuwa sera ya CCM ni serikali mbili.
Tutaona na kusikia mengi!.