Warioba:Tanganyika ina shutumiwa kwa kuvaa koti la Muungano na kufanya Tanzania ndiyo Tanganyika

Warioba:Tanganyika ina shutumiwa kwa kuvaa koti la Muungano na kufanya Tanzania ndiyo Tanganyika

Huwezi kuwaridhisha wazanzibari ni watu wenye kupenda malumbano. Zenj kuunganika na nchi kubwa ya tanganyika, si lazima tanzania ionekane kama ndio iliyokua tanganyika? ndio maana waasisi wakaona lazima zanzibar iendelee kua na utambulisho wake kwa kua na serikali yake ambayo hakika ina strong autonomy. Mfumo wa serikali tatu hakika hauna maslahi kwa zanzibar ila unatimilisha hatua muhimi kwa wale wanzibari wenye nia ya kuvunja muungano.
 
Mzee Warioba amesema zipo shutuma kwamba Tanganyika ilijivua na kuvaa koti jipya la muungano ambalo hapana shaka Tanzania bara kuonekana kufaidi matunda ya muungano kuliko Wazanzibari hata kupelekea Tanzania kuonekana ndiyo ile Tanganyika iliyo kufa.

Hali hiyo ndiyo inayofanya ongezeko la kero za muungano.Kwa maneno yake Wazanzibari wanaona ni ujanja tu ulitumika kuinyang'anya mamlaka yake Zanzibar nakisha kuiua kabisa na labda ndiyo chanzo cha hali duni za maisha ya Wazanzibari.

Wangetamani wajiunge na umoja wa nchi kama OIC unaojumuisha nchi za kiislamu hatua ambayo ingebadili kipato chao lakini haiwezekani kwakuwa koti linavaliwa Bara kwa mgongo wa muungano.

amesema tume yake ime angalia options nyingi ili kuondosha Muonekano huo lakini imeshindwa kupata balikurejesha pendekezo la kwenye rasimu ya kwanza la serikali tatu.

Ame chukua muda mrefu hadi kuchosha kuelezea hilo naona baaba ya kuhisi ccm wasinge taka hata kusikia serikali tatu.Kwakweli ameonyesha kuwa Wazanzibari walikuw wanataka kitu kingine siyo serikali mbili tena kitu ambacho ni mwiba kwa ccm.

Na hadhani kama wangetaka serikali moja kwani hiyo ni kuimeza kabisa Zanzibar.amesema zaidi ya 60%ya Watanzania Bara walitaka tatu hali kadhalika huko Zanzibar.

Nakiasi kikubwa Zanzibar walitaka muungano wa mkataba.

Tupo katika takuli kubwa wa kuu hali ndiyo hiyo

Alilazimika kutowa vidonge vichungu ili ubishi ukome!
 
Tutakuwa viziri mjini hapa kwa ving'ora vya misafara ya maraisi wa 3.....sasa wakiwa watembezi kama huyu bado watakuwa wanagongana angani

Kwa vile makao sasa hayatakuwa pahala pamoja basi kutakuwa hakuna mgongano, Rais wa Zanzibar atakuwa hana haja ya kupiga ripoti kwa Bwamkubwa kule magogoni na Slaa atafanya maskani yake kwao Moshi!
 
Umeishawahi kaa na wazanzibari mkaongea kuhusu muungano ukasikiliza maoni yao?

Unataka kuniambia Watanganyika hawataki kuongozwa na kitu serikali? Wanapoilaumu na kuiponda serikali ni kwa vile serikali haina cha manufaa kwao, hali hiyo sawa na muungano huu kwa zanzibar na ndio maana wanataka kuwepo na mkataba.
 
Huu muungano hauna maslahi kwa Tanganyika ipigwe kura ya maoni ili uvunjiliwe mbali...na zanzibar haiwezi kuwa alqaeda cos ni ka nchi kadogo US atakatumia drones 3 tu kwishney....serikali tatu ni mzigo kwa walipa kodi kwa nchi masikini kama tanzania....muungano uvunjwe tu asap.
 
tunazunguka sana ila suluhisho ni serikali moja na znz iwe mkoa rasmi au muungano uvunjwe tukutane EAC,kwa hali hii matatizo yatajirudia tena na znz wataendelea kulalamika wanataka mamlaka kamili

Mambo huenda taratibu hakuna haja ya pupa!
 
Marais 3!!!!!! what a nice chance to become a president one day


Migogoro ndani ya vyama itapunguwa mfano CDM Kabwe atatupwa Zanzibar, Slaa Bara na Mbowe Muungano. Mrejesheni 'msaliti' wenu, sasa kiini cha ugomvi kishapata suluhu!
 
Huwezi kuwaridhisha wazanzibari ni watu wenye kupenda malumbano. Zenj kuunganika na nchi kubwa ya tanganyika, si lazima tanzania ionekane kama ndio iliyokua tanganyika? ndio maana waasisi wakaona lazima zanzibar iendelee kua na utambulisho wake kwa kua na serikali yake ambayo hakika ina strong autonomy. Mfumo wa serikali tatu hakika hauna maslahi kwa zanzibar ila unatimilisha hatua muhimi kwa wale wanzibari wenye nia ya kuvunja muungano.

Hivyo bwanamkubwa unadai kutaka kuridhisha mtu kwa kitu chake mwenyewe? Ama kweli watu wengine hamueleweki, kwani mtu kutaka chake uungwana si kumpa tu.
Kwani Wazanzibar wanadai kitu gani kutoka Tanganyika? wanachodai mamlaka ya Zanzibar na Watanganyika hiyari yao na nchi yao.
 
Ndugu yangu Nguruvi3 uko wapi? Unaonaje maneno ya Jaji Warioba?
 
Nitaraji kuona kuinuliwa kiuchumi zaid. Sasa madaraka zaidi. Elimu Afya hakuna kitu. Mawaziri na Wabunge mishahara kwao na idadi yao ni wangapi. Mishahara Walimu na Waganga. Mapinduzi ya Joachim ni bora kuliko hayo madaraka lukuki eti serikali 1+1=3? Mh sielewi
 
Hizi hassle zote za nini?. Kwani nani amesema wananchi wanataka muungano?.

kwa mazingira yalivyo kwa sasa nchini, serikali tatu ni njia ya kuelekea katika uvunjifu wa Muungano wakati huo huo serikali mbili kwa sasa wala hazina hata mandate ya Watanzania wengi.

Kwa nini kama nchi mbili tunapita njia ndefu yenye gharama kubwa za kisiasa na kiuchumi wakati kuna njia fupi isiyo na gharama kubwa kama hizo!.

Kura ya maoni kuhusu kuwepo muungano au hapana ni mwarobaini kisiasa na bila hivyo, ni kuwalazimisha wananchi wakubali au kukataa serikali tatu huku wameziba options zingine za serikali moja, mbili, etc.

Itakuwaje wananchi au bunge likikataa hii Rasimu ya Katiba hasa kipengele cha aina ya serikali?.

Ndiyo maana tume ya Jaji Warioba inataka iendelee kuwepo hata wakati wa mchakato wa bunge la Katiba na kura ya maoni kwa sababu ulaji bado uko mezani kwa maana kuwa, wanafahamu kuna uwezekano mkubwa baadhi ya vipengele vya Rasimu ya Katiba (serikali tatu) vikakataliwa na wabunge wengi hasa ikichukuliwa kuwa sera ya CCM ni serikali mbili.

Tutaona na kusikia mengi!.

Lakini nimemsikia mh Rais, akisema wadau watakaoteuliwa kwny Bunge la Katiba wakae kama team, waweke maslahi ya Taifa mbele,ushindani wa kivyama wauweke pembeni ili kulivusha Taifa letu. Ametumia maneno ya hekima na kwa hakika nilimuona anaongea kwa mwenekano akiwa na hisia kuonyesha anachoongea anamaanisha nia yake ya dhati kutupatia katiba, Legacy muhimu na kubwa ndani ya utawala wake.
 
Back
Top Bottom