Wasabato kaeni macho na hii kwaya

Wasabato kaeni macho na hii kwaya

Status
Not open for further replies.
Nilikuwa msabato na bado naipenda sana Sabato mpaka leo hii, ila kwa sasa nimeshakuwa Mlokole! Tatizo kubwa sana nililonalo sasa hivi ni kwamba najua yote yaliyoko kwenye usabato na baadhi tu ya yaliyoko kwenye ulokole, na hilo ndiyo tatizo pekee linalonifanya niendelee kuwa mlokole! Nadhani siku nikishayajua yote yaliyoko kwenye ulokole, naweza nikarudi tena Sabato. Tatizo lililopo ni kuwa itikadi ya walokole imejikita kwa Roho Mtakatifu aliyeshuka siku ya Pentekoste, wiki kadhaa baada ya Yesu kuwa amepaa mbinguni. Sasa huyu Roho Mtakatifu ni FACT kuwa hana mwanzo na wala mwisho, ila tofauti na mimi, mwanzo ninao japo nami mwisho sina.. Sasa najiuliza ni lini yaliyoko kwenye ulokole nitakuja kuyajua yote, ili angalua nipate tena nafasi ya kuhamia kwingine? Msaada tafadhali katika hili, kama upo!
tulia miguuni kwa Yesu acha kutanga tanga
 
Kwahiyo mkeo ni mtoto? Akitongozwa analiwa? Weweeee acha dharau kwa mkeo. Ukiendekeza wivu wa kindezi ataliwa kweli shauri zako, au labda ashaliwa tayari

Shida ya watu mliozoea Facebook ndio hii
 
Na wewe ndio Waziri mwenyewe, watu wanajaribu kukuchafua.... jitafakari huenda kuna wachache wananajisi kazi yako.

Kabisa ni kweli, alikuwa nmb and now amefukuzwa hayo yote ni sawa the ishu is ngono zinavyofanyika pale ni hatari, fanya uchunguzi uwez kuamini
 
Nilikuwa msabato na bado naipenda sana Sabato mpaka leo hii, ila kwa sasa nimeshakuwa Mlokole! Tatizo kubwa sana nililonalo sasa hivi ni kwamba najua yote yaliyoko kwenye usabato na baadhi tu ya yaliyoko kwenye ulokole, na hilo ndiyo tatizo pekee linalonifanya niendelee kuwa mlokole! Nadhani siku nikishayajua yote yaliyoko kwenye ulokole, naweza nikarudi tena Sabato. Tatizo lililopo ni kuwa itikadi ya walokole imejikita kwa Roho Mtakatifu aliyeshuka siku ya Pentekoste, wiki kadhaa baada ya Yesu kuwa amepaa mbinguni. Sasa huyu Roho Mtakatifu ni FACT kuwa hana mwanzo na wala mwisho, ila tofauti na mimi, mwanzo ninao japo nami mwisho sina.. Sasa najiuliza ni lini yaliyoko kwenye ulokole nitakuja kuyajua yote, ili angalua nipate tena nafasi ya kuhamia kwingine? Msaada tafadhali katika hili, kama upo!
Usipende kuhamahama kwenye haya madhehebu, utachanganyikiwa bure. Stick to God , au baki kama mimi tu. Uwepo wa Mungu ni maneno tu ya watu na hayana msingi wowote.
 
Halafu ikatokea unaishi na mwanaume bila ndoa watakavyokunyanyapaa hutapewa hata kazi ya kupanga viti kanisani. Kumbe wameficha midhambi Yao kwenye kujifanya waimbaji na kutoa mimba.
Ukweli mnaaibisha kanisa la Mungu. Kama Lekundayo na wenzako hamtakemea haya na kuifunga hiyo kwaya Kama mlivyofanya kwa kwaya ya muungano basi nitajua Hali imekuwa tete. Simamieni maadili km mnavyosimamia na kusisitiza makusanyo ya zaka na sadaka
Well said madam, hakuna kwaya hiliokua inanibariki kama Muungano kama hii kwaya maovu yapo na yanajulikana inabidi isimamishwe najua Hilo linawezekana.

Kama unakumbuka lile tamasha la IMBA KWA AKILI lilifungiwa kutokana na kutofata misingi ya kanisa
so ni jukumu la uongozi wa kanisa kuliangalia hili.


Opondo ja shirati
 
Usipende kuhamahama kwenye haya madhehebu, utachanganyikiwa bure. Stick to God , au baki kama mimi tu. Uwepo wa Mungu ni maneno tu ya watu na hayana msingi wowote.
ila ni bora kufia madhabahuni kuliko kwenye kichaka damu ya Yesu yatakasa tulia miguuni mwake
 
Mimi nimeolewa RC..Lakini nimeshindwa kbs kusali kule .najiona kbs najidanganya!...bora urudi usabatoni mkuu!
Umepotoka kiasi ndugu yangu, hujautendea haki ukweli ulivyo.

Ninavyojua mimi, kwa hapa kwetu Tanzania na baadhi ya nchi zingine Barani Afrika na pengine hata Ulaya, (hasa Ulaya Mashariki), Watu wengi walioko kwenye Ulokole wanaweza kuwa wamechachanganya damu na madhehebu kadha kubwa lao likiwa ni RC, kiasi kwamba kama yasingekuwa madhehebu hayo, pengine leo wasingekuwa huko waliko, wangekuwa wamepotea nje ya Yesu. Kwa mantiki hiyo ni kwamba RC ndiyo inao mtego mkubwa kabisa wa kuvulia samaki wote waliomo baharini, yaani kondoo kwa ajili ya Yesu.

Huwa ikivua na kuwakamata, inaanza kuwasambazia sasa na wengine. Isingekuwepo RC, haya madhehebu mengine yasingekuwa na waumini wengi kwa idadi waliyonayo sasa, wangekuwa nao ila si kwa uwingi huu walionao sasa. Ukienda kwa mfano kijijini kwetu Shinyanga ng"wanalumango, hata babu wa miaka 90 anajua kuwa dini ipo moja inaitwa Roman Catholic. Kwa hiyo the chances kwamba mtu kama huyu kwa bahati nzuri unaweza ukamkuta yuko dhehebu jingine tofauti na RC, ni baada ya kuwa amemsikia Yesu kupitia RC kwa sababu RC ipo kila mahali mithili ya hewa!
 
ila ni bora kufia madhabahuni kuliko kwenye kichaka damu ya Yesu yatakasa tulia miguuni mwake
Hayo ni maneno tu, yanachagizwa na woga alionao mwanadamu juu ya maisha ya sasa na baada ya kifo chake. Tungekuwa na assurance ya kuishi bila kufa wala usingeona mtu anahangaika na hizi dini/Imani.
 
Hayo ni maneno tu, yanachagizwa na woga alionao mwanadamu juu ya maisha ya sasa na baada ya kifo chake. Tungekuwa na assurance ya kuishi bila kufa wala usingeona mtu anahangaika na hizi dini/Imani.

😂 😂 Absolutely
 
Sasa unataka apate ngoma au
Sikiliza. Mke hachungwi. Utakufa kwa presha.
Kwa hiyo sasa unaamini hatongozwi?
Unaweza kukuta hadi mdogo wako alishamtongoza, lakini kwa kutunza heshima ya familia mkeo amekausha hajasema. Hata babako mzazi anaweza kumtongoza mkeo. Wanawake wanakutana na vituko vingi hawasemi.
Ukimchunguza bata hutomla.
 
Mimi nimeolewa RC..Lakini nimeshindwa kbs kusali kule .najiona kbs najidanganya!...bora urudi usabatoni mkuu!
Utajichanganya tu. Labda kama huna watoto itakuwa rahisi wewe na mumeo kila mmoja kusali kivyake. Halafu kama huko ibadani mmehubiriwa mambo yanayokinzana ukirudi nyumbani kila mmoja anakula kivyake na kulala kivyake. Yatakayofuata sihitaji kukuambia, utaona mwenyewe.
 
Usipende kuhamahama kwenye haya madhehebu, utachanganyikiwa bure. Stick to God , au baki kama mimi tu. Uwepo wa Mungu ni maneno tu ya watu na hayana msingi wowote.
Hii debate tulishaimaliza mimi na Kiranga na tumeshakubaliana kuwa . Mungu yupo, japo si kwa kukiri kwa maneno ila kwa BODY LANGUAGE!, Tatizo lako wewe naona liko kwenye ufahamu. Nashauri umsikilize mtumishi wa Mungu Padre Dr. Faustine Kamugisha Upendo TV kila siku jioni na asubuhi wiki hii, aongeze ukarbati kwenye kichwa chako. Ukishakosa ufahamu sahihi, halafu ukawa hujui kuwa umekosa ufahamu sahihi, ni matatizo. Lakini sasa Padre Dr. kamugisha anasema kuwa MATATIZO SIYO TATIZO. Huyu mtumishi naamini anaweza aawa wa msaada wa pekee sana kwako!
 
Utajichanganya tu. Labda kama huna watoto itakuwa rahisi wewe na mumeo kila mmoja kusali kivyake. Halafu kama huko ibadani mmehubiriwa mambo yanayokinzana ukirudi nyumbani kila mmoja anakula kivyake na kulala kivyake. Yatakayofuata sihitaji kukuambia, utaona mwenyewe.


Hapana..haina shida kwangu...!
 
Ralph Tyler,

Unatoa watu nje ya reli I think ww ni kijana mdogo sana, point ya mtoa mada ni vitendo vya ngono vinavyoendelea kwenye hiyo kwaya yenu vinavyofanywa na huyo Mwalimu wenu kwa mwamvuli wa Kumwimbia Mungu, haijalishi ni mke wangu au ni mke wako au ni mke wa mtu yeyote
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom