Tunaishi kipindi baada ya unabii. Mambo yaliyotabiriwa kumhusu Yesu Kristo yalishatokea. Msione Kitabu cha Ufunuo kimewekwa cha mwisho katika mpangilio wa vitabu vya Biblia mnafikiri hayo ni mambo ya baadaye. Ni kama unabii wa Isaya au manabii wengine ulishatokea.
Maono ya Yohana juu ya dunia mpya na mbingu mpya yalishatokea tangu ukombozi wa Kristo ulipotufikia. Tunaishi siku za ukamilifu wa nyakati na Yesu Kristo ndiye utimilifu wa unabii wote na nyakati zote.
Maono ya Yohana juu ya dunia mpya na mbingu mpya yalishatokea tangu ukombozi wa Kristo ulipotufikia. Tunaishi siku za ukamilifu wa nyakati na Yesu Kristo ndiye utimilifu wa unabii wote na nyakati zote.