Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Jina lako linamaanisha Nini?,,,,nimeikumbuka bendi flani Toka Congo ilikuwa inaitwa Lanouvvele generation wakiwa na mtindo wap Zipompapompa-Motorola.
 
Housegal ashukuru kaambulia cheni binafsi ningekufilisi.Ndugu upande wa mume jifunzeni kupunguza ujuaji ndugu yenu anawatambulisha mchepuko basi mnashupaza shingo mnasahau kuwa ana mke.Audacity ya kupanga mazishi bila mke wa marehemu mnaitoa wapi kama sio kiherehere?Next stop mke kusanya mali za mme wako fungia kabatini kila mtu alie na shida zake
 
Kuna mmoja alifanya hivi mkoa fulani kilichomkuta hakuamini,siku ya mazishi yeye na watoto wake waliishia kulia barabarani na maiti waliaga kabla haijaoshwa tena kwa kuongea na watu wa mochwari.Binti elewa unachokifanya usipende kupoteza muda utakuja kulia mbeleni
 
Ila siyo takwa la kisheria. Sasa waambie ukoo ukae kikao wamteue mtu, halafu mke bila kikao aombe usimamizi.
Halafu tuone nani atashinda.
 
...Na Wanaume tupunguze Ujinga. Mtu.ni Milionea unaweza Kupata Mwanamke yoyote unayetaka, Bado unamgeuza mfanyakazi wako wa Ndani Mchepuko ? Sijui na Akili au Matope ??? [emoji848]
 

Pole kwa msiba,
Umeonekana kumpondda sana mkewe, ila Kumbuka hata kama alimtoa barabarani alikuwa ni Mke wake wa ndoa. Maneno mengi umeandika humu, sifikiri kama Marehemu alipokuwa hai uliwafikiria watoto na kumshauri. Ninyi mlifanya kosa mkijua mke yupo wa ndoa hata kama yukoje na kuamua kwenda ku side na michepuko yake. Mwisho wa siku mke ni mkewe. Mwisho wa siku wa ndoa wanajua wao na Marehemu hayupo tena kujisemea ukweli wa upande wake. Mnamuona mjinga ila anaweza kuwashangaza. Kama anapenda Mali sawa si za mumewe na yeye ndoa ilikuwa bado ipo. Na ndugu lolote alivyo mkewe hamkupaswa kumdharau, mngemjali Marehemu mngemshauri aweke mambo sawa kabla kama talaka etc yeye ndio anajua why hakumuacha na alimpenda na akamuoa yeye huyo huyo Barmaid unayempondea humu.

Kiashiria cha Mali za marehemu kutaka na ndugu zake ipo kubwa sana.
 
Shida ilianzia mtoto wa 4 jamaa alijua kapigwa akamfumania na bodaboda akakoswa risasi 2 mtaa mzima unajua hilo...mama alikua mpiganaji nguli marehemu aliingia cha kike yani alikua barmaid wa songambele bar mirerani
Kwakweli usihukumu kabla ya kusikiliza pande 2 duuh kumbe show iko hivi?
 
Saa nyingine ukisikiliza upande mmoja unaweza hukumu kimakosa. Sidhani kama hao ndugu walifanya tu hivyo kumuonea mwanamke.
Kuna mfanyakazi mwenzetu alifiwa na kaka yake wiki 2 zimepita. Alikuwa na mke mwanajeshi lakini yule mke aliomba talaka na mahakama ikatengua ile ndoa.
Walizaa na jamaa mtoto mmoja. Yule jamaa hakuoa tena ila alizaa watoto wengine wa 2
Jamaa akapata ajali akafa. Siku ya mazishi wanaona gari ya jeshi inakuja msibani na yule mwanamke ,eti kaja kumzika mumewe. Na jeshini kule wamemchangia hela ya mazishi na kusindikizwa kabisa.
Alivyokuwa hana aibu, kaenda kumuambia mdogo wa marehemu kwenye wasifu wa marehemu aongeze kipengele kwamba marehemu ameacha mke mmoja.
Ndugu wa marehemu wakakataa, yule mdogo mtu kwa kumkomesha, akasoma wosia na kuongeza marehemu alishawahi kuoa ila waliachana kwa talaka mahakamani.
Kumbe nia yake ilikuwa ni kupata mafao ya NSSF na ya life insurance huyo marehemu
Aliumbuka pakubwa sana.
 
Hivyo vya kusema mke kaza nje ni visingizio tu Ili kujustfy hoja yake ya kuishi na mwanamke mwingine huko nje... Kosa la mke kuzaa nje ni kosa kubwa sana sana Sasa mbona hakumpa talaka?? Hao watoto wengine ambao ndugu wanasema wamefika 12 ni WA wapi? Mbona mke hawajui?? Hao ndugu wanataka kumdhulimu mke mkubwa na inawezekana hawakupenda ndugu Yao alivyomuoa...Sasa wawe makini MAANA itakula kwao
 
Kwakweli usihukumu kabla ya kusikiliza pande 2 duuh kumbe show iko hivi?
Mke alizaa watoto wawili nje lazima apigwe talaka... We hujiulizi kwanini hakuachwa?? Na mume alikuwa anazaa huko nje anamletea watoto alee. Ndugu wa marehemu walikuwa hawampendi kabisa huyu mke na wakamletea wifi Yao housegirl ndo akaja akageuka kuwa mke. Kwahiyo usisikilize sana maneno ya ndugu. Na walikoswa sana walipokuwa wanamweka kando na kudai eti wanasimamia Mali..kwani marehemu SI anao watoto na watakuwa??
 
Kuhusu documents kuwa kwa mwanasheria sio tatizo. Kama zipo kwa jina la marehemu itafanyika searching tu na Mali zote zitajulikana. Hata zikibadikishwa majina itaonekana zilibadilishwa lini... Yule mke atasaidiwa na wanasheria tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…