Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Shida ilianzia kwa mke mdg kutaka kujiweka mbele angekuwa mpole haya yasingemkuta.

Sema wapambe wake wanamwendesha na kumshauri hovyo wakiwa na lengo apate mali zote wazitumbue.

Iran na Israel wachapane tu tujue moyo sio kukaa na hisia za kibwege bwege za nani atapigwa.
Jina lako linamaanisha Nini?,,,,nimeikumbuka bendi flani Toka Congo ilikuwa inaitwa Lanouvvele generation wakiwa na mtindo wap Zipompapompa-Motorola.
 
Housegal ashukuru kaambulia cheni binafsi ningekufilisi.Ndugu upande wa mume jifunzeni kupunguza ujuaji ndugu yenu anawatambulisha mchepuko basi mnashupaza shingo mnasahau kuwa ana mke.Audacity ya kupanga mazishi bila mke wa marehemu mnaitoa wapi kama sio kiherehere?Next stop mke kusanya mali za mme wako fungia kabatini kila mtu alie na shida zake
 
Kuna mmoja alifanya hivi mkoa fulani kilichomkuta hakuamini,siku ya mazishi yeye na watoto wake waliishia kulia barabarani na maiti waliaga kabla haijaoshwa tena kwa kuongea na watu wa mochwari.Binti elewa unachokifanya usipende kupoteza muda utakuja kulia mbeleni
 
Kwani wwe ndiyo ndugu wa marehemu peke yako ikiwa marehemu ana ndugu wengine, hadi watoto wa marehemu hawakujui!? Kikao cha familia ni muhimu sana ili upate baraka za familia, na hakuna mirathi inafunguliwa tu na mtu mmoja akiwa na Muheshimiwa peke yake! Kwenye nakala ya hukumu itaandikwaje!!??
Ila siyo takwa la kisheria. Sasa waambie ukoo ukae kikao wamteue mtu, halafu mke bila kikao aombe usimamizi.
Halafu tuone nani atashinda.
 
Arusha Mfanyabiashara tajiri wa mawe ndugu Temu amefariki dunia na kuacha kizaazaa nyuma. Bwana huyo ana migodi, magari sita, mashamba, majumba na mahoteli na maviwanja.
Alioa mke aitwae Yasinta ndoa ya kanisani.

Akazaa nae watoto 5 Kama kawa huko chuga hawa mabilionea hua wanapenda chovyachovya.

Baba akazaa nje mtoto wa kwanza akaleta home mke alee, akanogewa akazaa mwingine tena akapeleka nyumbani mkewe alee. Mke akawa hana namna. Kiroho safi analea.
Mke nae amezaa watoto watano tena mmoja mchanga, ukijumlisha wawili wa baba wanakuwa saba.

Mama akaleta housegirl, baba alivyo na tamaa akaanza kutembea na housegirl mpaka akapata mimba. Baba akamfanya mke mdogo, akamjengea na akazaa naye watoto wawili. Yule housegirl ndo akawa na nguvu, mke mkubwa akawa anadharauliwa.

Mke kikawa kinamuuma lakini sasa ndo ashazaa watoto watano akaamua avumilie.

Mara paaap, tajiri kaumwa. Kapelekwa Muhimbili, kwa mapenzi ya Mungu akatwaliwa. Picha ndo ilianzia hapo, mke mkubwa akafika Muhimbili akashangaa anaambiwa na binamu wa mume eti kaa pembeni tutasimamia Mali za watoto na haki zao, akashangaa kiajee Sasa? Lakini kwavile yeye ndo mwenye cheti Cha ndoa akakabidhiwa mwili na cheti cha kifo.

Soma Pia: Arusha: Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauwaji watuma meseji

Ndugu na jamaa na marafiki wakaleta mwili Arusha mochwari ya Mt meru. Mke mkubwa akaelekeza mume azikwe wapi.

Sasa ndugu, marafiki na mke mdogo wakapanga pa kuzika na wakamweka kando bi mkubwa.

Siku ya kuzika bi mkubwa akaingia mahakamani kwa hati ya dharura kuomba zuio na akafanikiwa, issue ilikuwa serious kaburi lishachimbwa, mapadre ikabidi wakafanye Dua pale ya kufunga kaburi tupu na Ile pilau ya msiba wadudu waliifakamia sana.

Sasa leo amri imetolewa na mahakama mke halali amzike mume wake... Housegirl na wale ndugu hawaamini kilichotokea. Eti ndugu na marafiki wanapanga kususia maziko.

Na mke mkubwa amesema mume wangu ni mkristu na ana mke mmoja tu. Akimaliza kuzika anakusanya mali za mumewe baada ya kufungua mirathi.

Housegirl ataambulia simu na cheni za marehemu na nguo..ambazo hata hivyo bi mkubwa anaulizia vipo wapi. Housegirl amegeuka suria..ila wanae watapata mgao wa mali

Wadada wa kazi mnapoenda kufanya kazi kwenye nyumba za watu acheni tamaa kwani hamjui baba na mama wameanzia wapi na wamesotaje kupata mali. Pia ndugu na marafiki acheni upumbavu wa kuingilia mali za marehemu ikiwa ana mke na watoto
...Na Wanaume tupunguze Ujinga. Mtu.ni Milionea unaweza Kupata Mwanamke yoyote unayetaka, Bado unamgeuza mfanyakazi wako wa Ndani Mchepuko ? Sijui na Akili au Matope ??? [emoji848]
 
Hapo ndio atajua hajui marehemu docs zote ziko kwa mwanasheria wake nyumbani hakuna lolote...kaacha watoto 12 pia kaka zake wako vizuri kiuchumi watagawanya mali kwa watoto

mke alikua mlevi anapigwa miti mpka kuzaa watoto wawili na mabodanoda...jamaa amehama kwake mwaka mzima hajafika mpka mauti yamemkuta,mke anamtoto mchanga wa mwezi mmoja kazaa na bodaboda

Pole kwa msiba,
Umeonekana kumpondda sana mkewe, ila Kumbuka hata kama alimtoa barabarani alikuwa ni Mke wake wa ndoa. Maneno mengi umeandika humu, sifikiri kama Marehemu alipokuwa hai uliwafikiria watoto na kumshauri. Ninyi mlifanya kosa mkijua mke yupo wa ndoa hata kama yukoje na kuamua kwenda ku side na michepuko yake. Mwisho wa siku mke ni mkewe. Mwisho wa siku wa ndoa wanajua wao na Marehemu hayupo tena kujisemea ukweli wa upande wake. Mnamuona mjinga ila anaweza kuwashangaza. Kama anapenda Mali sawa si za mumewe na yeye ndoa ilikuwa bado ipo. Na ndugu lolote alivyo mkewe hamkupaswa kumdharau, mngemjali Marehemu mngemshauri aweke mambo sawa kabla kama talaka etc yeye ndio anajua why hakumuacha na alimpenda na akamuoa yeye huyo huyo Barmaid unayempondea humu.

Kiashiria cha Mali za marehemu kutaka na ndugu zake ipo kubwa sana.
 
Shida ilianzia mtoto wa 4 jamaa alijua kapigwa akamfumania na bodaboda akakoswa risasi 2 mtaa mzima unajua hilo...mama alikua mpiganaji nguli marehemu aliingia cha kike yani alikua barmaid wa songambele bar mirerani
Kwakweli usihukumu kabla ya kusikiliza pande 2 duuh kumbe show iko hivi?
 
Saa nyingine ukisikiliza upande mmoja unaweza hukumu kimakosa. Sidhani kama hao ndugu walifanya tu hivyo kumuonea mwanamke.
Kuna mfanyakazi mwenzetu alifiwa na kaka yake wiki 2 zimepita. Alikuwa na mke mwanajeshi lakini yule mke aliomba talaka na mahakama ikatengua ile ndoa.
Walizaa na jamaa mtoto mmoja. Yule jamaa hakuoa tena ila alizaa watoto wengine wa 2
Jamaa akapata ajali akafa. Siku ya mazishi wanaona gari ya jeshi inakuja msibani na yule mwanamke ,eti kaja kumzika mumewe. Na jeshini kule wamemchangia hela ya mazishi na kusindikizwa kabisa.
Alivyokuwa hana aibu, kaenda kumuambia mdogo wa marehemu kwenye wasifu wa marehemu aongeze kipengele kwamba marehemu ameacha mke mmoja.
Ndugu wa marehemu wakakataa, yule mdogo mtu kwa kumkomesha, akasoma wosia na kuongeza marehemu alishawahi kuoa ila waliachana kwa talaka mahakamani.
Kumbe nia yake ilikuwa ni kupata mafao ya NSSF na ya life insurance huyo marehemu
Aliumbuka pakubwa sana.
 
For as long as hao watoto 12 wana mama zaidi ya mmoja nae ni malaya tu kama mkewe....
So Malaya wawili walikutana, hana usafi wowote huyo marehemu mpuuzi.
Na angekuwa wa maana wala asingekimbia, angemtaliki huyo mwanamke na kuendelea huko alikoenda. So ni kenge tu kama kenge zingine kafa kaacha heka heka zisizo na msingi
Hivyo vya kusema mke kaza nje ni visingizio tu Ili kujustfy hoja yake ya kuishi na mwanamke mwingine huko nje... Kosa la mke kuzaa nje ni kosa kubwa sana sana Sasa mbona hakumpa talaka?? Hao watoto wengine ambao ndugu wanasema wamefika 12 ni WA wapi? Mbona mke hawajui?? Hao ndugu wanataka kumdhulimu mke mkubwa na inawezekana hawakupenda ndugu Yao alivyomuoa...Sasa wawe makini MAANA itakula kwao
 
Kwakweli usihukumu kabla ya kusikiliza pande 2 duuh kumbe show iko hivi?
Mke alizaa watoto wawili nje lazima apigwe talaka... We hujiulizi kwanini hakuachwa?? Na mume alikuwa anazaa huko nje anamletea watoto alee. Ndugu wa marehemu walikuwa hawampendi kabisa huyu mke na wakamletea wifi Yao housegirl ndo akaja akageuka kuwa mke. Kwahiyo usisikilize sana maneno ya ndugu. Na walikoswa sana walipokuwa wanamweka kando na kudai eti wanasimamia Mali..kwani marehemu SI anao watoto na watakuwa??
 
Hapo ndio atajua hajui marehemu docs zote ziko kwa mwanasheria wake nyumbani hakuna lolote...kaacha watoto 12 pia kaka zake wako vizuri kiuchumi watagawanya mali kwa watoto

mke alikua mlevi anapigwa miti mpka kuzaa watoto wawili na mabodanoda...jamaa amehama kwake mwaka mzima hajafika mpka mauti yamemkuta,mke anamtoto mchanga wa mwezi mmoja kazaa na bodaboda
Kuhusu documents kuwa kwa mwanasheria sio tatizo. Kama zipo kwa jina la marehemu itafanyika searching tu na Mali zote zitajulikana. Hata zikibadikishwa majina itaonekana zilibadilishwa lini... Yule mke atasaidiwa na wanasheria tu
 
Back
Top Bottom