Wasamaria:Fahamu chanzo chao na kwanini walikuwa hawachangamani na Wayahudi!

Wasamaria:Fahamu chanzo chao na kwanini walikuwa hawachangamani na Wayahudi!

Mkuu Al-Watan naona unatoa darasa mujarab

Sent From Ikulu-Magogoni street
Hahaha,
Darasa muhimu.

Eti Mangi umetoka kwenu kuna majesty yote ya Mlima Kilimanjaro watu wanatoka dunia nzima kuja kushangaa barafu iliyo nyuzi 3 kusini ya Ikweta, jambo la ajabu.

Halafu unaambiwa kwenu sikitu, ukiswali shurti uelekee Kibla!

Unaambiwa Jerusalem ndiyo mji mtakatifu.

Haiyumkiniki.



Ikulu Magogoni Street tutachelea kulimia meno mkuu.
 
Wakuu,

Unapofungua Agano Jipya,hasa katika zile Injili Nne,utakutana na uadui kati ya Wayahudi dhidi ya Wasamaria!

Ila ushawahi jiuliza chanzo cha ukinzani huu? Basi twende sote tupate kujua!

Ukirudi nyuma kidogo katika Agano la Kale utakutana na Mfalme Suleiman!

Baada ya kuikinikia hekima aliyoiomba na kupewa na Mungu,Mungu aliamua kuugawa

ufalme katika vipande viwili hasimu:Ufalme wa Yuda upande wa Kusini na Israel upande wa kaskazini!

Kwa kuwa Mungu hakutaka kuutia doa ufalme wa Suleiman ili kutokuvunja agano lake

aliloliweka na Mfalme Daudi,basi kumrundia heshima Daudi,alisubiri Suleiman afe, ndipo auchane pawili ufalme kama adhabu dhidi ya uasi wa Suleimani kwa Mungu kwa kuleta

ibada ya shetani na miungu ya kigeni kupitia mamia ya wake wa kigeni aliyowaoa!

Punde, Suleiman alipovuta pumzi ya mwisho,Israeli ikachanwa katikati! Makabila kumi yakaasi na kujiunga na Jeroboam na akaanzisha ufalme wake,huku makao makuu yakiwa katika mji wa Samaria! Makabila mawili yakajiunga na kutengeneza ufalme wa Yuda yakiongozwa na Rehoboam mtoto mkubwa wa Mfalme Suleiman!


Pia kumbuka,kabila pekee lilikokuwa na mamlaka ya kutoa mfalme lilikuwa la Yuda! Ila cha ajabu,Jeqoboam alikuwa wa kabila la Ephraim! Dharau namba moja! Kama haitoshi Hekalu la Suleiman lilikuwa Yerusalem kule Yuda, kwahyo kila mwaka Wayahudi wa Samaria wafunge safari ya kuja hekaluni! Jambo hili likamkera Mfalme Jeroboam! Naye pasipo kumuomba Mungu ushauri,akaamua kujitengenezea ndama wawili,katika mji wa Betheli ili Wayahudi wa Samaria wasiende Yerusalem! Jambo hili lilimkera Mungu sana! Uadui uliendelea!


Ila ulikua zaidi mwaka 722 Kabla ya Kristo,baada ya ufalme kupinduliwa na maelfu ya

waisraeli wa Samaria kubebwa utumwani na jeshi la Wassyria! Na mfalme aliyeshinda, akaamua kuleta watu wa mataifa mbali kutoka katika makoloni yake toka Ninawi mpaka Babylon ili wautunze mji na kuilima ardhi! Lengo lake ilikuwa ni kuzima jitihada zote za Wayahudi wa Samaria kujitutumua tena ili kupinga utawala wake! Na pia kutoa somo kwa makoloni madogo kuwa yasithubutu kuleta fyokofyoko! Lakini cha ajabu,nchi ya Samaria ikaanza kuvamiwa na Simba wala watu!


Baada ya watu kusosiwa kwa muda mrefu na taarifa kumfikia mfalme wa Assyria,ikabidi kuhani wa Kiyahudi atafutwe! Baada ya upepelezi,ikaonekana Yahweh hajapendezwa na

miungu ya wakazi wapya wa Samaria,hivyo kuhani akatumwa kwenda Samaria ili

kuwafundisha watu amri za Yahweh!


Baada ya hali kutulia,mwaka 586 Kabla ya Kristo ufalme wa kusini nao ukaanguka kwa mkono wa Nebukadneza! Wayahudi wa Samaria hawakuwahi kurudi Samari,na huo ukawa mwisho wa hayo makabila kumi! Ila yale makabila mawili ya kusini,yalirudi chini ya uongozi wa Nehemia na Ezra! Kwahyo mbele ya Wayahudi,hawa wakazi wapya

wa Samaria,na baadaye katika Agano Jipya wakiitwa walikuwa ni Walowezi,nusu watu na wa mataifa! Walikuwa na haki zote za kuwachukia! Japo Kristo aliwatendea vizuri, kama yule mwanamke msamaria pale kisimani,mpaka hekalu linavunjwa mwaka 70

Baada ya Kristo "bifu" liliendelea!
Sawasawa.
Swali kuu: wapo wapi descendants wa makabila yale mengine 10? Maana si sahihi kuwachukulia Jews (ambao ni makabila mawili tu) kama hao tu ndio uzao wote wa Yakobo na babu yake Ibrahim!
 
Utotole mkuu,acha nitafiti zaidi jibu lake utalipata!
Ila hata Biblia yenyewe haisemi chochote kuhusu makabila hayo kumi na wala haisemi lolote kuhusu vizaria vyao tangu watwaliwe utumwani!
 
Utotole mkuu,acha nitafiti zaidi jibu lake utalipata!
Ila hata Biblia yenyewe haisemi chochote kuhusu makabila hayo kumi na wala haisemi lolote kuhusu vizaria vyao tangu watwaliwe utumwani!
Sure. Ukisikiliza wasemaji wengi toka sehemu mbalimbali unakuta tayari mataifa ya ulaya yameshawagawana wana wa Yakobo. Nchi nyingi za ulaya zimeshapewa makabila yaliyopotea ya Israel. Eg. Descendants wa Reuben wanadai Ni Wafaransa, etc. Of course schools of thought ziko nyingi Sana.
 
Unaweza kunisaidia sehemu yoyote ya Torati inayoonesha Wayahudi wasichangamane kabisa na mataifa/makabila mengine yasiyoabudu Mungu wao? Niko interested kujifunza hapa zaidi
unapotaka kujifunza ukikuta thread yoyote pitia kwanza majibu ya mwanzo usisumbie watu kwa kutaka kujiridhisha nafsi yako. swali lako lishajibiwa vizuri kabsa hapo nyuma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanapenda na kujua historia ya Wayahudi na Wasamaria walioishi miaka maelfu na maelfu mbali huko, lakini ukiwauliza historia ya Mwanamalundi, Kinjekitile, Mkwawa au David Kidaha Makwaia walioishi takriban miaka mia moja iliyopita kwetu hawaijui.

Hili ni jambo la aibu.

Ndiyo maana inakuwa rahisi kutuaminisha kwamba sisi si watu kamili.
usipende kufananisha vitu ambavyo haviendani kijana ilimradi ujifurahishe. unawalazimisha watu wafuate akili yako?! ushajua wanachopenda sasa wakishafahamu ya kinjekitile vipi watawapa bunduki badala ya maji mwenyewe umekua umekuta maandiko tu yaloandikwa na wazungu alafu wajitia mjuaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
usipende kufananisha vitu ambavyo haviendani kijana ilimradi ujifurahishe. unawalazimisha watu wafuate akili yako?! ushajua wanachopenda sasa wakishafahamu ya kinjekitile vipi watawapa bunduki badala ya maji mwenyewe umekua umekuta maandiko tu yaloandikwa na wazungu alafu wajitia mjuaji

Sent using Jamii Forums mobile app
Unawezaje kumlazimisha mtu ambaye humjui, humuonina wala huna nguvu yeyote juu yake, kwa kupitia internet?

Huyo anayeweza kulazimishwa hivyo ni mtu au konokono?
 
Nadhani unahitaji kujifunza zaidi kuhusu makabila ya Israel na namna ya Taifa LA Yuda ililivyopatikana, Wasamaria na wayahudi wote ni waisrael Jifunze kwanza ilikuaje Baadhi ya waisrael wawe wayahudi na tabaka jingine waitwe Wasamari?? Ukijua utofauti wa Myahudi na Mwisrael utatoa maana na kwa nini wasichangamane
 
Unaweza kunisaidia sehemu yoyote ya Torati inayoonesha Wayahudi wasichangamane kabisa na mataifa/makabila mengine yasiyoabudu Mungu wao? Niko interested kujifunza hapa zaidi
anyway nilichokielewa mimi nikwamba wengi katika hii hoja hawajui tafsiri ya neno myahudi,msamalia na muisraeli,
Taifa la israeli lilikuwa na makabila 12 ndani yake kwapamoja yanaunda hilo taifa ,baada ya kifo cha mfalme suleimani hili taifa la israeli liligawanyika sehem mbili kabila 10 zilizokuwa zinakaa kaskazini mwa hilo taifa zilikataa kuendelea kutawaliwa na kabila la yuda so wakajitenga wakaweka makao yao makuu kwenye mji wa SAMALIA na taifa lao likawa linaitwa ISRAELI na kabila zingine mbili zilizobaki ilikuwa ni YUDA (JUDAH) na BENJAMINI wao walikuwa wanakaa kusini mwa nchi so wakabaki na taifa lao likawa linaitwa YUDA,na makao yao makuu yakawa Yerusalemu na wakawa wanatawaliwa na watu wa nyumba ya daudi kama Mungu alivyowaagiza,sasa ukianza kusoma 2Wafalme 16 wale waliobakia kusini wakaanza kutambulika kama WAYAHUDI (JEWS) kutokana na jina la taifa lao kuwa YUDA(JUDAH),sasa ukiendelea kusoma mbele zile kabila 10 za kaskazini zilizojitenga na ambazo hazikuwa zinatawaliwa na wazaliwa wa nyumba ya Daudi kama ilivyokuwa desturi badala yake zilitawaliwa na wafalme wasiofuata misingi ya Mungu wa baba zao wakachukuliwa utumwani na Mfalme wa ASSYRIAN wakaenda huko wakaendelea kutawaliwa na kuchangamana na watu wa mataifa wa huko ndio wakaitwa WASAMARIA,sasa kipindi Yesu anakuja alikuta bado huo mgawanyiko upo ule ufalme wa kaskazini (Samaria) na ufalme wa kusini (YUDEA) ambayo ilikuwa chini ya utawala wa WARUMI(ROMAN RULE),so utaona kwanini wayahudi walikuwa hawataki kuchangamana na wenzao tangia awali ,
Yesu na wanafunzi wake waliihubiri injili Judea yote kutafuta kondoo waliopotea kwa muda wa miaka mitatu na nusu then wayahudi wakamkataa Yesu kama Masihi wao wakafanikiwa kuwashawishi waroma kumuua Yesu na wakafanikiwa lakini baada ya siku tatu akafufuka akajionyesha wazi wazi kwa wanafunzi wake kabla ya kupaa kwenda mbinguni kuketi mkono wa kiume wa Mungu mwenye Enzi! ila kabla hajashikwa na kusulubiwa pale msalabani aliwaambia wanafunzi wake kuwa "Adhabu ya Wayahudi kumkaataa (soma kumb la torati 28) Mathayo 21:41,Yerusalemu itatwaliwa kimabavu na hekalu litavunjwa na wayahudi watachukuliwa utumwani kwenye mataifa yoote ya duniani, huu unabii ulitimia mwaka 70 baada ya Yesu ambapo mfalme TITUS aliyafanya hayo aliyoyasema Yesu!
So Waisraeli (zile kabila 10)au wasamalia waliadhibiwa wakatawanywa koote kama adhabu ya kuto kutii maagizo ya Bwana Mungu ,then YUDEA(JUDAH) nao wakatawanywa kama adhabu ya kumkataa masihi Yesu!
kinachofuata baada ya hapa ndio wakristo wengi tunakuja kutofautiana ...............Je hawa waliorudi pale wanaojiita taifa la israeli ndio wale waliotawanywa miaka takribani 2000 iliyopita?? au hawa ni fake na original bado wapo kwenye utumwa,dhiki,mateso na kila aina ya manyanyaso kama neno la Kristo linavyosema?????? kuna thread kama hii niliianzisha unaweza kuisoma pia kupitia hii link
https://www.jamiiforums.com/threads/uhalisia-wa-taifa-la-israeli.
 
anyway nilichokielewa mimi nikwamba wengi katika hii hoja hawajui tafsiri ya neno myahudi,msamalia na muisraeli,
Taifa la israeli lilikuwa na makabila 12 ndani yake kwapamoja yanaunda hilo taifa ,baada ya kifo cha mfalme suleimani hili taifa la israeli liligawanyika sehem mbili kabila 10 zilizokuwa zinakaa kaskazini mwa hilo taifa zilikataa kuendelea kutawaliwa na kabila la yuda so wakajitenga wakaweka makao yao makuu kwenye mji wa SAMALIA na taifa lao likawa linaitwa ISRAELI na kabila zingine mbili zilizobaki ilikuwa ni YUDA (JUDAH) na BENJAMINI wao walikuwa wanakaa kusini mwa nchi so wakabaki na taifa lao likawa linaitwa YUDA,na makao yao makuu yakawa Yerusalemu na wakawa wanatawaliwa na watu wa nyumba ya daudi kama Mungu alivyowaagiza,sasa ukianza kusoma 2Wafalme 16 wale waliobakia kusini wakaanza kutambulika kama WAYAHUDI (JEWS) kutokana na jina la taifa lao kuwa YUDA(JUDAH),sasa ukiendelea kusoma mbele zile kabila 10 za kaskazini zilizojitenga na ambazo hazikuwa zinatawaliwa na wazaliwa wa nyumba ya Daudi kama ilivyokuwa desturi badala yake zilitawaliwa na wafalme wasiofuata misingi ya Mungu wa baba zao wakachukuliwa utumwani na Mfalme wa ASSYRIAN wakaenda huko wakaendelea kutawaliwa na kuchangamana na watu wa mataifa wa huko ndio wakaitwa WASAMARIA,sasa kipindi Yesu anakuja alikuta bado huo mgawanyiko upo ule ufalme wa kaskazini (Samaria) na ufalme wa kusini (YUDEA) ambayo ilikuwa chini ya utawala wa WARUMI(ROMAN RULE),so utaona kwanini wayahudi walikuwa hawataki kuchangamana na wenzao tangia awali ,
Yesu na wanafunzi wake waliihubiri injili Judea yote kutafuta kondoo waliopotea kwa muda wa miaka mitatu na nusu then wayahudi wakamkataa Yesu kama Masihi wao wakafanikiwa kuwashawishi waroma kumuua Yesu na wakafanikiwa lakini baada ya siku tatu akafufuka akajionyesha wazi wazi kwa wanafunzi wake kabla ya kupaa kwenda mbinguni kuketi mkono wa kiume wa Mungu mwenye Enzi! ila kabla hajashikwa na kusulubiwa pale msalabani aliwaambia wanafunzi wake kuwa "Adhabu ya Wayahudi kumkaataa (soma kumb la torati 28) Mathayo 21:41,Yerusalemu itatwaliwa kimabavu na hekalu litavunjwa na wayahudi watachukuliwa utumwani kwenye mataifa yoote ya duniani, huu unabii ulitimia mwaka 70 baada ya Yesu ambapo mfalme TITUS aliyafanya hayo aliyoyasema Yesu!
So Waisraeli (zile kabila 10)au wasamalia waliadhibiwa wakatawanywa koote kama adhabu ya kuto kutii maagizo ya Bwana Mungu ,then YUDEA(JUDAH) nao wakatawanywa kama adhabu ya kumkataa masihi Yesu!
kinachofuata baada ya hapa ndio wakristo wengi tunakuja kutofautiana ...............Je hawa waliorudi pale wanaojiita taifa la israeli ndio wale waliotawanywa miaka takribani 2000 iliyopita?? au hawa ni fake na original bado wapo kwenye utumwa,dhiki,mateso na kila aina ya manyanyaso kama neno la Kristo linavyosema?????? kuna thread kama hii niliianzisha unaweza kuisoma pia kupitia hii link
https://www.jamiiforums.com/threads/uhalisia-wa-taifa-la-israeli.
Maelezo mazuri. Na aya yako ya mwisho ndilo swali kuu. Je hawa wanaoitwa Waisrael ambao kimsingi wanatarajiwa kuwa wale wa YUDA (jews) ndio wale wale kweli ambao walichukuliwa utumwani Babeli na kurudi na kisha tena kutawanywa enzi ya agano jipya? Au ni wengine walijipandikiza hapo? Je wale watokanao na makabila mengine 10 wako wapi hadi sasa?
 
Itakuwaje iandikwe na watu wanne na kila moja ina utofauti na nyengine? Iliyo kuwa sawa ni ipi ?

Post sent using JamiiForums mobile app
Ukisoma kitabu cha Injili ya Luka sura ya kwanza mstari wa kwanza utapata maana halisi ya kwa nini waandishi wa Injili wapo wanne na hata wakiwepo zaidi. Luka 1:1...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tusikuvunje moyo umu ila jitahidi kusoma kwa bidii sana biblia maana unaonekana unapenda kujifunza na kushare na wenzako.

Pili jitahidi pia kujenga hoja wakati unaandika pia kichwa kiendane na main body ili kuleta kitu murua zaid ya hiki.

Napenda sana kusoma mambo kama hayo.

Wayahudi walikuwa watu pekee walioteuliwa na Mungu mwenyewe kuwa kama taifa teule la kumuwakilisha Mungu duniani kwa kutenda na shika kanuni za mbinguni.

Uteuzi huu uliwakilishwa na tohara yaani kila myahudi ni lazma atahiriwe na hii ni baada tu ya mtoto kuzaliwa akifikisha umri flani bas anatimiza agano la kuwa myahudi kwa kutahiriwa.

Kwa dhana hio basi kukawa na hali flani ya wayahudi kujiona wao kuwa ni bora zaidi ya wengine.

Kwahiyo si kwa wasamaria tu bali ilikuwa ni kwa kila ambaye hakuwa myahudi walijiwekea mipaka kuwa hawaruhusiwi kuchangamana nao.

Hili lilikuwa ni tatzo na ndio maana kristo anapokutana na mwanamke msamaria kisimani anamwambia nipe maji ninywe si kama yesu hakujua sheria ya kutochangamana bali alikuwa anaonyesha kuwa hakuna cha myahudi wala myunani wala mpagani bali wote baba yetu ni mmoja Mungu wa mbinguni hivyo alikuja kuvunja huo ukuta ambao wayahudi waliujenga dhidi ya mataifa yasio ya kiyahudi.
Asante mtoa mada.
Isitoshe Yesu Kristo alipokuja duniani alileta sheria ya matendo ya imani, yaani shahidi wa mtu awe ni nafsi yake na si kama hapo mwanzo ilikuwa ni kama tu kutimiza wajibu na si kwa uwazi wa moyo na kwa kupenda. Ndiyo maana ni ngumu sana kupata haki kwa matendo ya sheria. Asante.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sura ziko nyingi sana kaka, we soma Agano la Kale utaelewa:

Mfano

Kumbukumbu la Torati 7
1 Bwana, Mungu wako, atakapokutia katika nchi uendayo kuimiliki, atakapoyang'oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti, na Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe;
2 wakati Bwana, Mungu wako, atakapowatoa mbele yako, nawe utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao;
3 binti yako usimpe mwanawe mume, wala usimtwalie mwanao mume binti yake.
4 Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi.
5 Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga.
6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako; Bwana Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.
7 .....
16 Nawe angamiza mataifa yote atakayokupa Bwana, Mungu wako; jicho lako lisiwahurumie, wala usiitumikie miungu yao; kwani litakuwa ni mtego kwako jambo hilo.

Kumbukumbu la Torati 20

16 Lakini katika miji ya mataifa haya akupayo Bwana, Mungu wako, kuwa urithi, usihifadhi kuwa hai kitu cho chote kipumzikacho;
17 lakini uwaangamize kabisa, Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, kama alivyokuamuru Bwana, Mungu wako;
18 wasije wakawafunza kufanya mfano wa machukizo yao yote, waliyoifanyia miungu yao; hivyo itakuwa ni makosa juu ya Bwana, Mungu wenu.

Hapo umemjibu bila shaka. Pia kulikuwa ugomvi kati ya wasamaria na wayahudi wakati wa kujenga hekalu, wakina Ezra walikutana na upinzani mzito sana kutoka kwa wakazi waliokuwa wameachwa katika mji ule hicho kikawa chanzo kukibwa kabisa cha uadui kati ya wayahudi na wasamaria, lakini wote walikuwa ni taifa moja hapo awali kabla ya uhamisho.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanapenda na kujua historia ya Wayahudi na Wasamaria walioishi miaka maelfu na maelfu mbali huko, lakini ukiwauliza historia ya Mwanamalundi, Kinjekitile, Mkwawa au David Kidaha Makwaia walioishi takriban miaka mia moja iliyopita kwetu hawaijui.

Hili ni jambo la aibu.

Ndiyo maana inakuwa rahisi kutuaminisha kwamba sisi si watu kamili.
Hapa inategemea sana unavutiwa na kitu gani zaidi katika kujifunza. Historia ya Biblia kwa mtu anayesoma kwa kumaanisha haibakii kuwa historia tu bali ni roho kamili inayo huisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utotole mkuu,acha nitafiti zaidi jibu lake utalipata!
Ila hata Biblia yenyewe haisemi chochote kuhusu makabila hayo kumi na wala haisemi lolote kuhusu vizaria vyao tangu watwaliwe utumwani!
biblia haisemi,ila inasema wameshapotea hawatarudi kamwe,

lakini ukweli ni kua baada ya israel kingdom kuanguka,na ikabaki Judah kingdom,
makuhani wa judah walihakikisha wanayapoteza maandiko ya israel kingdom,
kimsingi hizi nchi mbili baada ya kifo cha solomon,zilikua ni nchi adui,
kwahiyo waandishi na makuhani walihakikisha maandiko ya history na imani ya israel yanapotea,
mfano israel waliabudu mungu aitwae El na ndo asili ya neno el kuwa katika jina israel,
tofauti ya yahwew mungu wa wayahudi,

kimsingi baada ya solomon kufa na nchi kugawanyika,yale makabila 10 ndo yalibaki na jina la israel,
wakati utawala wa kusini uliokua umebaki na makabila mawili wakachagua kujiita Judea,
jina hilo ndo baadae wenyeji walijulikana kama wayahudi,na mungu wao ni simba wa yudah kwa maana ya yahwew ama jehova kiswahili,

kwa maana hiyo ni wazi kuwa unaweza kukuta muisrael,lakini asiwe myahudi,kwani uyahudi sio hata kabila bali asili yake ni yule mtoto wa jacobo alieitwa yuda,

maandiko yalichanganywa mno kama husomi critically,huwezi gundua
 
Utotole mkuu,acha nitafiti zaidi jibu lake utalipata!
Ila hata Biblia yenyewe haisemi chochote kuhusu makabila hayo kumi na wala haisemi lolote kuhusu vizaria vyao tangu watwaliwe utumwani!
biblia haisemi,ila inasema wameshapotea hawatarudi kamwe,

lakini ukweli ni kua baada ya israel kingdom kuanguka,na ikabaki Judah kingdom,
makuhani wa judah walihakikisha wanayapoteza maandiko ya israel kingdom,
kimsingi hizi nchi mbili baada ya kifo cha solomon,zilikua ni nchi adui,
kwahiyo waandishi na makuhani walihakikisha maandiko ya history na imani ya israel yanapotea,
mfano israel waliabudu mungu aitwae El na ndo asili ya neno el kuwa katika jina israel,
tofauti ya yahwew mungu wa wayahudi,

kimsingi baada ya solomon kufa na nchi kugawanyika,yale makabila 10 ndo yalibaki na jina la israel,
wakati utawala wa kusini uliokua umebaki na makabila mawili wakachagua kujiita Judea,
jina hilo ndo baadae wenyeji walijulikana kama wayahudi,na mungu wao ni simba wa yudah kwa maana ya yahwew ama jehova kiswahili,

kwa maana hiyo ni wazi kuwa unaweza kukuta muisrael,lakini asiwe myahudi,kwani uyahudi sio hata kabila bali asili yake ni yule mtoto wa jacobo alieitwa yuda,

maandiko yalichanganywa mno kama husomi critically,huwezi gundua
 
Back
Top Bottom