Wasemavyo wadau na club nyingine Afrika na kile Kinachoendelea katika Page ya CAF baada ya Goli la Yanga kukataliwa

Aly Ahly 2 -0 Simba... Huon hata aibu au ndio ile mishipa imechoka😅😅... Yule mme wenu ametema nyongo bondeni .....
Kutoka ni kutoka tu, aibu ya nini sasa? Tukutane mwakani panapo majaaliwa
 
Hapa ni kukata rufaa kupinga upangaji matokeo maana Aziz Ki alishangilia mara tu baada ya kufunga hiyo ilitosha kumshawishi refa kuomba kuona marejeo ya picha ya VAR au kuamua straight liwe goli.

Hapa njia ingine ni kuomba kujitoa kwenye hayo mashindano at least msimu mmoja ili kushinikiza haki iwepo. Tunapaswa wanayanga kuchafua page ya CAF non stop mwaka mzima kupinga dhuluma iliyofanywa na refa wa kati, kibendera na VAR bench.
 
Refa wao, ila washambuliaji butu wa Yanga nalo ni janga.

Sundowns wanaogopwa bure tu ila ni wa kawaida sana.
Kama ambavyo timu za uarabuni tulivyokua tunaziogopa ila zikikaa vibaya zinapelekewa pumzi ya moto mpaka wanaomba mechi iishe.
Ni kweli
 
Achaneni na hayo bana, hayabadili matokeo. Mpira ni mchezo wa makosa. Refa na jopo lake wamekosea mshindani wetu amefaidika. Tukubaliane na matokeo tu. Tujipange kwa yajayo.
Kuna kukosea, na kupanga njama za kukosea kimakusudi. Kwa yale waliyoyafanya wale waamuzi, ni njama za wazi wazi za kujikosesha kimakusudi. Wanastahili kuadhibiwa haraka iwezekanavyo.
 
Utadhani Uto ndio wa kwanza kufanyiwa hivyo
Kama Yanga sio wa kwanza kuonewa vile basi Yanga ndio wawe wa mwisho kuonewa.
Soka la Afrika limekuwa, technology imekuwa, kwanini sasa mambo ya kihuni wazi wazi kama yale ya jana tuendelee kuyaendekeza?
 
kutoka maktaba ya taifa posta🤣🤣🤣
 

Attachments

  • Screenshot_20240405_232604_Gallery.jpg
    75.4 KB · Views: 2
Kama Yanga sio wa kwanza kuonewa vile basi Yanga ndio wawe wa mwisho kuonewa.
Soka la Afrika limekuwa, technology imekuwa, kwanini sasa mambo ya kihuni wazi wazi kama yale ya jana tuendelee kuyaendekeza?
Kipi ulichoonewa?.hakuna technology ya goal line.kwanini uamini kuwa umeonewa?
 
Kipi ulichoonewa?.hakuna technology ya goal line.kwanini uamini kuwa umeonewa?
VAR ina msaada gani katika lile tukio?
Kama video na Picha za kamera zote zilizopo sasa zimetuonyesha mpira wote ulivuka mstari, kwanini lisiwe ni goli?
Kwanini tusiseme Yanga alionewa?
 
VAR ina msaada gani katika lile tukio?
Kama video na Picha za kamera zote zilizopo sasa zimetuonyesha mpira wote ulivuka mstari, kwanini lisiwe ni goli?
Kwanini tusiseme Yanga alionewa?
Tuwekeeni picha ya camera ya goal line.ipo wapi? Mbona hamuweki?msilalamike tu.
 
Hao wanasiasa wanafanya nini? Wakati wo var zao ni kupita bila kupingwa....
Utopolo kapakatwa na ubuntu...
 
Refa wao, ila washambuliaji butu wa Yanga nalo ni janga.

Sundowns wanaogopwa bure tu ila ni wa kawaida sana.
Kama ambavyo timu za uarabuni tulivyokua tunaziogopa ila zikikaa vibaya zinapelekewa pumzi ya moto mpaka wanaomba mechi iishe.
Ndio shida timu zikicheza na Yanga, zinaonekana ni za kawaida. Wazee tukubali kwasasa Yanga ipo hatua ya mbali katika kufanya scouting ya benchi la ufundi. Hao Mamelodi sio timu ya kawaida, waulize Al Ahly anawajua vizuri hao katika michezo mitano ya hivi karibuni Al Ahly kapata tabu sana iwe kwake au ugenini. Mamelodi ni bingwa wa African football league sio timu ya kawaida bali Yanga ndio timu inayoweza kuwa tishio huko mbeleni.
Goli halali wamenyimwa, halafu wameweza kuwadhibiti Mamelodi bila uwepo wa Aucho,Yao na Pacome. Kama wachezaji muhimu na kocha watabakia msimu ujao basi pengine wakawa na msimu mzuri tena
 
Nimeshangaa kuona rafu aliyocheza Lomlisa ilienda kutazamwa na mwamuzi kwenye VAR ya uwanjani ili kujiridhisha kama inastahili kadi nyekundu, au la!!

Halafu kwenye goli lenye utata kama lile, mwamuzi hakuitwa kwenda kujiridhisha kama kweli mpira ulivuka mstari, au la!!
Hakika lile tukio la jana limewadhalilisha waamuzi wa Afrika. Inaonekaa ni wazi wako kwenye payroll ya Motsepe.
 
 
Sasa huyo Kingwagwala wa nini hapo?

Mijizi ya Kura na huyo refa Wana tofauti gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…