Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Hao wenye strong command ya kingereza walilaumiwa kwa mambo mengi tu.

Kikwete kahudhuria sana forums za World bank lakini ni katika uongozi wake makontena yamepita bure bandarini.

Tuna wajinga wengi tu kwenye jamii zetu wanaongea kingereza cha malkia.

Hizo habari za Chato uwanja wa ndege ni siasa nyepesi sana.

Hapa Dar zinajengwa flyover nane na zenyewe ni sehemu ya chato?.

Zinajengwa zahanati, mashule na upanuzi mkubwa wa bandari na vyenyewe vyote ni Chato?.

Acheni siasa nyepesi za mitandaoni.
 
Sasa kama ulisoma kuanzia form one mpaka phd kwa kutumia kiingereza halafu hujui kiingereza wewe nawe ni msomi? Kiri udhaifu- kumbuka ile kauli maarufu: 'msema kweli ni mpenzi wa Mungu'

Wewe mwenye kujua kingereza mbona huna faida yoyote kwa taifa lako zaidi ya kuja za server za jamii forum.
 

Hawa ni madalali wa wazungu kwa ufupi wanaishi na maumivu hivyo kujifariji ni tabia yao.
 
Kingereza sio lugha ya malaika na makosa ya matamshi ni tatizo letu la waafrika kwani tunakuzwa na lugha zetu za asili.
Tatizo sio makosa ya lafudhi mkuu.
Hivi hiyo sentensi mheshimiwa rais alikuwa anataka kusema nini?
Maneno tumeyasikia Ila maana yake ni ipi?
 
Mabeberu wangapi wanapiga broken za kiswahili au lugha nyingine lakini watu wanachukulia poa tu.

Kumbuka usomi haupimwi kwa kujua lugha ya kiingereza
Hawakisomi mashuleni kutoka msingi mpka vyuoni lkni English unasoma kuanzia msingi mpka vyuoni kinachosikitisha he knows nothing. Não sabe nada o seu presidente pedra.
 
Hayo makosa ya sentensi yanaipunguzia nchi anayoiongoza kitu gani cha maana?.
Sasa kwa nini asiongee kiswahili kama alivyoanza hotuba?
Kwani kulikuwa na lazima gani kuongea kiingereza.
Si kwamba labda sisi hatukosei lakini Kuna kiwango Cha makosa kinazua maswali.
Hivi unajua unaweza kupima uwezo wa akili ya mtu kwa namna anavyojieleza?
 
Ila hii ukiongea kwa slang huwezi jua kama kuna tatizo [emoji23][emoji23][emoji23]labda tu kwasababu ya lafuzi ya kisukuma
 
Tatizo la hivyo ni kwa wasomi wengi sana wa Tanzania, hatuna msingi wowote wa maana wa hii lugha kisha tukaichukulia kuwa yeyote anayeiongea basi anaringa au anajifanya msomi.

Hii ndio inatupa jibu sahihi kuwa wasomi wetu wengi ni watu wa kukariri tu ili kupata cheti, halafu mtu anakuja na utetezi wa kijinga kuwa aliyesomea sayansi hapaswi kujua kiingereza, bure kabisa.

Magufuli atumie tu kiswahili kisha mkalimani atatafsiri, kiingereza kimeshamshinda na lafudhi yake ndio kabisa ni ya "Ancient Sukuma".
 

Please would you correct the mistakes he made in that sentence?
 
natamani malaika waifungie mitandao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…