Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Cha muhimu sio kingereza chake ni ufanisi wa yote anayoyaanzisha na yakawa na faida kwa jamii pana ya Tanzania.

Cha muhimu sio kingereza chake ni kutovumilia urasimu wowote wenye harufu ya upigaji ndani yake.

Cha muhimu sio kingereza chake ni ukaribu na wananchi anaowaongoza na uwezo wa kuyapigania maslahi yao.

Cha muhimu sio kingereza chake bali ni kuifungua nchi kw amiundo mbinu wezeshi kwenye sekta mbalimbali za kiuchumi.

Tumeshakuwa na mawaziri wenye kuongea kingereza kama wabunge wa Uingereza na walichofanya cha maana hakuna zaidi ya ufisadi.

Ni akili za kitoto sana kujadili kingereza cha mtu halafu ukaachana na uwezo wake kikazi.
 
Kwa matukio kama hayo ambapo anahtaji kuongea umombo, Binafsi nashauri Mh. angekuwa anasoma speach kama zilivyoandaliwa na waandishi wake! Na kama vipi awe anapewa mapema iwezekanavyo ili kumpa muda wa kuzisoma ili iwe rahisi hata kuzitoa! Lakini hii ndio maana kuna wengine wanaamini Mheshimiwa haendi Ulaya pengine ni kukwepa changamoto ya lugha ya malkia!
 
As far as ---- is concerned.

Anaipenda sana hii, nakumbuka tulikuwa tunaitumia sana kwenye essay form less huko.
 
Watanzania wengi hasa tuliosoma masomo ya sayansi hatuko fluent sana kwenye kiingereza cha maongezi, lakini hilo halituzuii kuwa best candidates kwenye taaluma zetu. Mfano, magu anaweza kuwa mwalimu mzuri sana wa chemistry kutokana na recommendations za wanafunzi anaowafundisha.

Maana yake ni kwamba, anaweza ku-deliver contents za hilo somo ambalo mostly linatumia terminologies na akaeleweka sana na wanafunzi wa chemistry. In the same sence anao uwezo mkubwa tu wa kufanya presentation kwa wanataaluma kwenye field yake wakamwelewa na hata kumuuliza maswali au any clarification, na aka-respond bila shida yoyote. Mfano, nilipowasilisha draft yangu ya thesis kwa masupervisor wangu ambao ni waingereza hawaku-recommend kabisa kuipeleka kwa editors wa lugha kwa sababu ilikuwa super.

Sijigambi kuwa nipo vizuri sana kwenye kimalkia hasa ninapotakiwa nifanye maongezi ya kawaida, lakini nilipokuwa nafanya discussion na supervisors wangu walisema my english is good na wananielewa sana. Kuthibitisha hili nilishapata a number of best presenter awards kwenye international conferences ambazo zinakuwa zimefurika wazungu. Haya sasa na wengine tupeni experience yenu kwenye kimalkia ili twende sawa.
... proper communication skills is an important tool to manage your audience; it is an important tool for you to deliver what you would like your audience to get. That's why "Communication Skills" is a core course taught in almost every university for new entrants.

Tusidanganyane, lugha ni nyenzo muhimu ya kuwaleta watu pamoja; kama kiongozi unahitaji kuwaunganisha watu wako na pia kuwa na mashirikiano na mataifa ya kigeni. Kiongozi unaposimama kuhutubia, iwe wananchi wako, au wageni, nchi isikie fahari kiongozi leo anawakilisha vyema! Of course kiongozi bora anazo qualities nyingi ila tusitake kuifanya lugha ionekane sio lolote, sio chochote miongoni mwa sifa hizo simply baadhi yetu tuna madhaifu ya mawasiliano. Hiyo ndio hoja ya "kipumbavu" inayotaka kujengwa.

Sifa mojawapo kubwa ya Mwl. Nyerere ilikuwa audience management; akisimama kuhutubia UN, mabeberu wote waliokuwa wametoka nje kuvuta sigara wanarudi ndani haraka sana kumsikiliza. Na anasimama anajenga arguments zenye mashiko; zenye akili; unaona kabisa hoja hii ina madini ndani yake. Sijui tulikuja kukosea wapi!
 
Shida ni kwamba. Toka sekondari mpaka ngazi ya PhD unatumia kiingeleza halafu unakuja kuongea broken kiasi hiki
Kufika ngazi ya PhD sio kuielewa lugha kwa ufasaha. Hakuchukua msimbo wa lugha ya kiingereza.

We kwa akili zako unahisi umepungukiwa nini kwa Jpm kutoimahili vyema lugha ambayo ana wakalimani wanaomsaidia.
 
Kwa matukio kama hayo ambapo anahtaji kuongea umombo, Binafsi nashauri Mh. angekuwa anasoma speach kama zilivyoandaliwa na waandishi wake! Na kama vipi awe anapewa mapema iwezekanavyo ili kumpa muda wa kuzisoma ili iwe rahisi hata kuzitoa! Lakini hii ndio maana kuna wengine wanaamini Mheshimiwa haendi Ulaya pengine ni kukwepa changamoto ya lugha ya malkia!
... rehearsal ni muhimu sana!
 
Nukuu:
"We suppose to focus according our direction according our environment that's only way we can help our peoples no body should come and say that his there to save the problems of our peoples we are the one we are leader we suppose to change the direction"
Rais Magufuli anaking'eng'ena kweli Kidhungu. Ubarikiwe Rais wetu.
 
Akitumia kisukuma mnalalamika, akiongea kiswahili mnanuna, akiongea kingereza mnalalama, Ebu mshaurini mgombea wenu awe anachana nywele.
 
Watumwa wa lugha ya kiingereza bado wapo.

Utakuta balozi wa Uingereza au Marekan au nchi yeyote ile anajitahidi kuhutubia au kuongea Kiswahili kibovu na huku anashangiliwa, lkn dhubutu wewe Mtanzania ukosee kiingereza japo neno moja tu, matusi hayooooo!

Nadhani baadhi ya Watanzania bado wanaabudu lugha ya kiingereza kuliko hata lugha ya kiswahili!

Hongera sana JPM kwa kukipa hadhi na heshima Kiswahili lkn bado kazi ya kukipigania inahitajika, miaka mitano ijayo jitahidi kuhakikisha lugha ya kiswahili ndio inayo tumika ktk shughuli zote za serikali maofisi yote yaweke kumbukumbu zake kwa kiswahili sio Kiingereza.
 
... proper communication skills is an important tool to manage your audience; it is an important tool for you to deliver what you would like your audience to get. That's why "Communication Skills" is a core course taught in almost every university for new entrants.

Tusidanganyane, lugha ni nyenzo muhimu ya kuwaleta watu pamoja; kama kiongozi unahitaji kuwaunganisha watu wako na pia kuwa na mashirikiano na mataifa ya kigeni. Kiongozi unaposimama kuhutubia, iwe wananchi wako, au wageni, nchi isikie fahari kiongozi leo anawakilisha vyema! Of course kiongozi bora anazo qualities nyingi ila tusitake kuifanya lugha ionekane sio lolote, sio chochote miongoni mwa sifa hizo simply baadhi yetu tuna madhaifu ya mawasiliano. Hiyo ndio hoja ya "kipumbavu" inayotaka kujengwa.

Sifa mojawapo kubwa ya Mwl. Nyerere ilikuwa audience management; akisimama kuhutubia UN, mabeberu wote waliokuwa wametoka nje kuvuta sigara wanarudi ndani haraka sana kumsikiliza. Na anasimama anajenga arguments zenye mashiko; zenye akili; unaona kabisa hoja hii ina madini ndani yake. Sijui tulikuja kukosea wapi!

hoja zako hazina mashiko kwa mstakabai huo kila kiongozi angeimahili vyema lugha ya kiingereza, lakini sivyo ilivyo.

Hatuchagui kiongozi kwa sababu anauwezo mzuri wa kuongea lugha fulani, tunachagua kiongozi mwenye uwajibikaji na Maono ndani ya jamii.

Hiyo lugha inayojinasibu/tunayojinasibu inatuleteaje maendeleo au inatunufaishaje kwa watanzania asilimia 80% tusio ijua lugha hiyo.

Kumbuka huyu sio rais wa dunia ni rais wa watanzania wanao tumia lugha ya kiswahili katika nyaja zote.

Isitoshe kunawatu wanaoimahili vyema wakalimani watafanya kazi hiyo. Shida ipo?
 
watumwa wa lugha ya kiingereza bado wapo.

utakuta balozi wa uingereza au marekan au nchi yeyote ile anajitahidi kuhutubia au kuongea kiswahili kibovu na huku anashangiliwa, lkn dhubutu wewe mtanzania ukosee kiingereza japo neno moja tu....!! matusi hayooooo!!!
nadhani baadhi ya watanzania bado wanaabudu lugha ya kiingereza kuliko hata lugha ya kiswahili!!

Hongera sana JPM kwa kukipa hadhi na heshima Kiswahili lkn bado kazi ya kukipigania inahitajika.......miaka mitano ijayo jitahidi kuhakikisha lugha ya kiswahili ndio inayo tumika ktk shughuli zote za serikali maofisi yote yaweke kumbukumbu zake kwa kiswahili sio kiiingereza.

Itapendeza sana mkuu..
Nani nashauli katika taasisi zote Zitumie lugha ya kiswahili
 
Umesehau ndugu yangu. Huko kwenye neno direction ameongeza harufu ''s''. Infact yeye kila neno la kiingereza anadhani linaongezewa herufu ''s''. Nafwaaaaaaaaa!
Kama hivi "tells them not to tells us what to do's, we will do ourselves bcoz tanzania is rich, malawi is rich and africa is rich?
 
Nguseroh

We unapata aibu gani. Una haki ya kumpinga lakini sio kwa hoja dhaifu kiasi hicho.

fanya mambo yako ya maendeleo. Muda ukiifika rais unayempenda wewe atakuja lakini sio leo wala kesho.
 
Kwa kiingereza hiki namkumbuka Ben Saanane alivyokuwa anapinga juu PHD ya bwana Jiwe ......kwa kweli Tanzania hatuna cha kujivunia toka kwa Jiwe na ndio maana hataki kukanyanga nje kwa sabu ameshajiona ana udhaifu fulan kwenye lugha.

2015 CCM mlicheza kamari na hili litawagharimu sana mwaka huu

Rest Easy Ben Saanane.
 
watumwa wa lugha ya kiingereza bado wapo.

utakuta balozi wa uingereza au marekan au nchi yeyote ile anajitahidi kuhutubia au kuongea kiswahili kibovu na huku anashangiliwa, lkn dhubutu wewe mtanzania ukosee kiingereza japo neno moja tu....!! matusi hayooooo!!!
nadhani baadhi ya watanzania bado wanaabudu lugha ya kiingereza kuliko hata lugha ya kiswahili!!

Hongera sana JPM kwa kukipa hadhi na heshima Kiswahili lkn bado kazi ya kukipigania inahitajika.......miaka mitano ijayo jitahidi kuhakikisha lugha ya kiswahili ndio inayo tumika ktk shughuli zote za serikali maofisi yote yaweke kumbukumbu zake kwa kiswahili sio kiiingereza.
Lakini hao wazungu kama wana Phd unakuta wametumia lugha yao ya kiingereza kuzisoma lakini cha kushangaza huyu wa kwetu ana Phd aliyosomea kwa kiingereza lakini hajui kuandika sentesi moja ya kiingereza kilichonyooka sasa hapo ndio ufeki wa Phd yake unapojitokeza
 
Ingekua ni Rais wa nchi nyingine ameongea kiswahili kibovu msingemcheka wala kushangaa ila mtampongeza kwa kujitahidi.

Ila kwa sababu za kisiasa mmeamua kumshikia bango JPM, anyway ndio siasa zilivyo.
Sasa Lissu Anajua Kiingereza au anaongea kwa kukariri Lugha za kisheria, hakuna Gramma anayojua
 
Dk. Magufuli is a scientists not some English literature GURU - why pick on him?
 
Hii lugha sijui ikoje, yaani ni bora ukosee kiswahili kuliko kiingeleza, kwanza utajistukia mwenyewe kabla hujastukiwa - then ghafla unakosa confo.

afu hii lugha sijui ina nini, unaweza kukuta jamaa ana Div Four ila ana flow vibaya mno na mwingine ana PHD ila ni kugokoa mwanzo mwisho.
 
Kwa mtazamo wangu, huyu si mtu huru kama unavyosema. Mfano ni ishu hii ya 'kizungu'. Angekuwa huru na mwenye kujiamini asingelazimisha kuongea kiingereza wakati tayari mfumo wa ukalimani/tafsiri ulikuwepo (utaona wageni walikuwa na zile interpretition headsets). Ilikuwa ni katika kujaribu kuwathibitishia wanaomnanga kuhusu 'kizungu' kuwa naye yumo! Hiyo siyo attitude ya mtu aliye huru kifikra.
Fair point. Lakini mara ngapi mimi au wewe tumeongea au kuandika kiingereza ndani ya jamii forums wakati tunajua members wengi kama si wote wanajua kiswahili?

Suala ni kwamba unafanya kile ambacho utashi wako umekutuma kufanya iwe ni kwa kutaka kuwathibitishia au iwe kwa sababu zinginezo. Ndio uhuru wenyewe. Usinipangie nifanye nini, nitumie lugha gani au hata niseme nini. Iwe mimi, wewe au Rais Magufuli.
 
Back
Top Bottom