Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Alafu unaambiwa ana PHD...huu muda wa wanangu kuwasomesha mpaka uko si bora niwqfungulie duka kariakoo.
 
Magufuli ni PCM Pure combination sasa hapa lugha aliyonayo inatosha
Magu hajasoma Advance, walienda kusoma Diploma ya ualimu kwa mpango maalumu,walichukua vijana wa O-level na kwenda kusoma Teaching kwa level ya Diploma na yeye akiwa mmoja wao. Ni kama mpango uliorudishwa majuzi wa kuchukua vijana waliomaliza Olevel na kupelekwa kusoma Ualimu Udom.
 
Sasa kwa nini asiongee kiswahili kama alivyoanza hotuba?
Kwani kulikuwa na lazima gani kuongea kiingereza.
Si kwamba labda sisi hatukosei lakini Kuna kiwango Cha makosa kinazua maswali.
Hivi unajua unaweza kupima uwezo wa akili ya mtu kwa namna anavyojieleza?
Tafuteni ya maana ya kujadili sio huu upuuzi wa kujivunia kujua lugha za wakoloni.

Akili ya Magufuli ni kubwa sana. Tulifunga siku tatu corona ikakimbia leo Kenya wanafanya lile lile tulilofanya miezi iliyopita.

Huyo Lissu mwenye kujivunia kingereza ni dalali tu wa wazungu wachache ambao ni wapumbavu wa kimaadili.
 
Ni Tanzania tu maajabu kama haya hupatikana. Sasa piga mahesabu darasani alikuwa anafundishaje!
Ndio maana karibu 99.5% ya wanao ongea kiingereza hapa kwetu, lugha inawatatiza. Na wengi tuu ambao ninyi wengi mnaofikiri wanaongea sawasawa hawako vizuri ila wanaongea lugha inayoyo fanana na kiingereza.

Hata Lissu ni shida tuu ila afadhali sana. Wengi hawaongei neno sahahi, kwa tukio sahihi, kwa wakati sahihi, vipambio sahihi ili litoe maana sahihi na ikiwezekana liwe na vibwagizo vya lugha sahihi. Wengi wanaongea kiingereza kikavu. ( na kwa mwanasiasa ambae ni tajiri wa phrases of language na zipo nyingi eg noun phrases, verb phrases, gerund phrases,infinitive phrases na prepositional phrases na idiom anapendezesha sana mazungumzo)

Bahati mbaya hata baadhi ya native speakers of english language wana tatizo hilo. Lazima ama wazazi au jumuia unayoishi na kuchanganyika nayo kila siku wawe waongeaji wazuri na fasaha, na kingine uipende lugha fasaha ndio utaogea vizuri sana.
Mfano: George Bush Jr na Obama wote wanaongea kiigereza lakini Obama ana ufasaha zaidi wa lugha kuliko Bush.
 
Baada ya kushindwa hoja ndipo unasema mada ibadirishwe.


Magufuli kanjanja tu yule. Hajui kidhungu 😀 😀
Mada ya kipumbavu, hatukumpigia kura aje atufundishe kingereza, tulimpigia kura aitekeleze ilani ya uchaguzi.

Tarehe 28 October atashinda tena kwa kutimiza kazi ya kutekeleza ilani aliyopewa.

Mwenye akili za kipuuzi za kitoto ndio atajikita kwenye masuala ya kingereza chake.
 
Magu hajasoma Advance, walienda kusoma Diploma ya ualimu kwa mpango maalumu,walichukua vijana wa O-level na kwenda kusoma Teaching kwa level ya Diploma na yeye akiwa mmoja wao. Ni kama mpango uliorudishwa majuzi wa kuchukua vijana waliomaliza Olevel na kupelekwa kusoma Ualimu Udom.
Alisoma Advanced level. Hicho unachosema mpango maalum yalikuwa mafunzo ya ualimu mwaka mmoja badala ya miaka miwili.
 
Nani kasema kuna binadamu mkamilifu? Naomba tusichanganye mapungufu ya kibinadamu ya kawaida na u-kiazi wa darasani! Yaani mtu asome mpaka level ya Phd tena kwa kiingereza, halafu awe mwalimu afundishe kwa kiiingereza na kisha awe waziri kwa muda mrefu tu na bado simple english inamshinda kama mtoto wa darasa la saba? Hapana. Kuna kitu ambacho hakiko sawa kabisa kwenye mfumo wetu wa elimu. Na huyu tumebahatika kujua kwa sababu tu ni kiongozi. This is serious issue ndugu yangu.
ni kweli kabisa, tulio kaa njee kwa muda mrefu sana, suala hili tunaliona ni kubwa sana kuliko hata tunavyo lizungumza hapa, mbona tunaporudi tukikaa miaka miwili nyumbani tuna soma na kuandika kiswahili vizuri ?.

WHATS WRONG?
 
Magufuli ni PCM Pure combination sasa hapa lugha aliyonayo inatosha
Mzumbe Secondary pale Morogoro kuna vijana wanasoma PCM na wengine PCB lakini wanaongea kingereza kizuri kuliko hata HGL wa pale.
Anyway labda watetezi wake mtasema ile ni shule ya vipaji maalumu, ila all in all kilaza ni kilaza tu
 
Magu hajasoma Advance, walienda kusoma Diploma ya ualimu kwa mpango maalumu,walichukua vijana wa O-level na kwenda kusoma Teaching kwa level ya Diploma na yeye akiwa mmoja wao. Ni kama mpango uliorudishwa majuzi wa kuchukua vijana waliomaliza Olevel na kupelekwa kusoma Ualimu Udom.
Ikawaje sasa yeye magufuli akau crush mfumo ambao ulimfikisha hapo alipo au ndio wivu wenyewe ?
 
Alisoma Advanced level. Hicho unachosema mpango maalum yalikuwa mafunzo ya ualimu mwaka mmoja badala ya miaka miwili.
Huo utaratibu ndio unaoendelea sasa,Diploma ya ualimu miaka mitatu,lakini humo humo wanasoma na Advance na wanafanya mitihani ya Advance kwa masomo mawili.
 
Mzumbe Secondary pale Morogoro kuna vijana wanasoma PCM na wengine PCB lakini wanaongea kingereza kizuri kuliko hata HGL wa pale.
Anyway labda watetezi wake mtasema ile ni shule ya vipaji maalumu, ila all in all kilaza ni kilaza tu

Kipangaspecial lugha sio kilaza, hilo tatizo wanao watu wengi mnoo na hata ambao mnafikiri wanaongea kiingereza vizuri. Lugha sio uwezo wa akili yako.
 
Huo utaratibu ndio unaoendelea sasa,Diploma ya ualimu miaka mitatu,lakini humo humo wanasoma na Advance na wanafanya mitihani ya Advance kwa masomo mawili.
Sasa unasemaje hakusoma Advanced level!
 
Ikawaje sasa yeye magufuli akau crush mfumo ambao ulimfikisha hapo alipo au ndio wivu wenyewe ?

Nakupa mfano halisi : kwa sababu wote hawa wawili ni wana siasa, nimeongea na mara nyingi tuu vipindi mbali mbali, hata leo naongea nao pakiwa na uhitaji.

Pole pole VS Lissu :

Mr Pole Pole : kasomea bongo, japo amefanya kazi na kuchanganyika na wazungu wafadhili wake akiwa Excutive Director kwa miaka mingi alipokuwa akienda njee ni tuu kwa safari za kikazi, Ni muongeaji fasaha wa kiingereza kuliko Lissu ambae alisomea nje na amekaa kwa muda.

HAPO SIRI NI NINI--NAFIKIRI KUPENDA LUGHA.
 
Tafuteni ya maana ya kujadili sio huu upuuzi wa kujivunia kujua lugha za wakoloni.

Akili ya Magufuli ni kubwa sana. Tulifunga siku tatu corona ikakimbia leo Kenya wanafanya lile lile tulilofanya miezi iliyopita.

Huyo Lissu mwenye kujivunia kingereza ni dalali tu wa wazungu wachache ambao ni wapumbavu wa kimaadili.
Wewe ndiyo dalali wa phd ya magufuli kumbe tumejua aliyemuuzia vyeti vya phd ndiyo maana umeamua kufagilia kuwa ana Akili kubwa ili asije kukulaumu kwa kumuuzia vyeti feki kisha mkasahau kwenda kusoma kingereza British cancell ili mfiche udhaifu wenu, wewe ni mmojawapo wa madalali wachache wapumbavu waliokosa maadili
 
Nakupa mfano halisi : kwa sababu wote hawa wawili ni wana siasa, nimeongea na mara nyingi tuu vipindi mbali mbali, hata leo naongea nao pakiwa na uhitaji.

Pole pole VS Lissu :

Mr Pole Pole : kasomea bongo, japo amefanya kazi na kuchanganyika na wazungu wafadhili wake akiwa Excutive Director kwa miaka mingi alipokuwa akienda njee ni tuu kwa safari za kikazi, Ni muongeaji fasaha wa kiingereza kuliko Lissu ambae alisomea nje na amekaa kwa muda.

HAPO SIRI NI NINI--NAFIKIRI KUPENDA LUGHA.
Tatizo ni phd Tatizo siyo polepole wala nini Tatizo ni mmiliki wa phd kutojua kingereza maana yake ni nini? aliyemuuzia vyeti alisahau kumfundisha kingereza?
 
Ukiwa na Elimu ya kawaida usipokijua kingereza hakuna wa kushangaa lakini kumiliki phd pasipo kujua kingereza lazima italeta maswali kibao
 
Wewe ndiyo dalali wa phd ya magufuli kumbe tumejua aliyemuuzia vyeti vya phd ndiyo maana umeamua kufagilia kuwa ana Akili kubwa ili asije kukulaumu kwa kumuuzia vyeti feki kisha mkasahau kwenda kusoma kingereza British cancell ili mfiche udhaifu wenu, wewe ni mmojawapo wa madalali wachache wapumbavu waliokosa maadili
Mtaishia kuandika ujinga jamii forum wakati nchi inazidi kupaa. Watu wanazidi kufanya kazi yenye matokeo yenye kuonekana.
 
Back
Top Bottom