Washukiwa wa shambulio la kigaidi la "Crocus" wanasema kwamba walikuwa wakisafiri kwenda Kiev kupokea zawadi waliyoahidiwa

Washukiwa wa shambulio la kigaidi la "Crocus" wanasema kwamba walikuwa wakisafiri kwenda Kiev kupokea zawadi waliyoahidiwa

Uvamizi wa Urusi nchini Ukraine umeiachia Urusi madhaifu mengi kwenye intelijensia yake ikiwemo kutengwa kimataifa katika masuala ya intelijensia.
Madhaifu yapi? Watu wamefanya tukio la ugaidi wamekamatwa ndani ya siku moja na watuhumiwa wanasema yote baada akili kuwarudia wewe upo Maji Matitu unasema Urusi dhaifu daaah.
 
Urusi inafanya "plot twisting" kwenye hii issue ya shambulizi la kigaidi.

Siku chache zilizopita, Putin alirudia yale madai yaliyokuwa yakisambaa awali kabisa kuwa magaidi walikuwa wakikimbilia Ukraine. Akatuachia swali tujiulize kwamba ni kwa nini walitaka kwenda Ukraine.

Saa kadhaa baadaye, mshirika wa karibu wa Putin, rais wa Belarus, Alexander Lukashenko, akadai kwamba magaidi walikuwa wakielekea Belarus kwanza ila walikutana na vizuizi (vituo vya ukaguzi ama checkpoints) ndipo wakabadili njia ili kuelekea Ukraine. Na akasema kuwa atatoa ushirikiano wa kiintelijensia kwa Urusi kuhusiana na hilo.

Hii statement ya Mzee Lukashenko inaonekana kuleta mkanganyiko mkubwa ukilinganisha na kauli za viongozi mbalimbali wa Urusi.

Pia, saa chache baadaye, mkurugenzi wa FSB (hili ni shirika la ujasusi la Urusi), akadai [bila uthibitisho] kuwa Marekani, Uingereza na Ukraine ndio walioratibu na kuwezesha shambulizi la Moscow huku Ukraine ikitajwa kama mhusika wa kutoa mafunzo kwa "magaidi" katika eneo lisilojulikana ndani ya Mashariki ya Kati.

Hiyo statement pekee inaonesha uzembe wa hali ya juu na ingetosha wakati uleule kumfuta kazi huyo mkurugenzi.

Hilo la watuhumiwa kwenda Ukraine "kupokea zawadi" ni jipya katika mtiririko wa matukio na huenda tukasikia mengine mengi zaidi ya haya.

Madai karibu yote kuhusu Ukraine kuhusika yanasemekana yametokana na kauli za wale watuhumiwa wa ugaidi mara baada ya kufanyiwa mahojiano. Tatizo ni kwamba, kauli zinazotokana na watuhumiwa waliopitia mateso wakati wanahojiwa huwa sio za kuaminika kwa namna yoyote ile.
Utawala wa Putin utafanya kila namna Ukraine ibebe hii lawama ili wahalalishe Vita yao.

Ila uzembe wa FSB yao utafichwa.
 
Utawala wa Putin utafanya kila namna Ukraine ibebe hii lawama ili wahalalishe Vita yao.

Ila uzembe wa FSB yao utafichwa.
Hahaha wewe upo Uyole halafu hautaki Ukraine wahusishwe kwa mapenzi yako yaani Putin akusikilize wewe🤣
 
Waongo hao,ila kipondo watachopata watasema tu data zote,na kule hawauliwi ni kiungo kimoja kimoja wanatambaa nacho.
Wasikilize hapa
 
Hivi ushawahi Kujiuliza kwanini walipokuwa wanafanya hilo tukio la Kigaidi walikuwa na confidence kabisa ila walipokamatwa walikua wanatetemeka Mwili mzima?

Kuna mambo mengi sana hatuyajui kuhusu haya mashambulizi ya Kigaidi, inakuwaje mtu anajitoa Mhanga yupo kawaida tu?

Urusi hawa unaowasema hawana kitu kwenye intelijensia wametupa jibu, hao magaidi walipewa dawa maalum ambayo inatoa hofu kabisa, wakati wanafanya tukio ile sio akili yao kabisa, akili imewarudia Walipokamatwa.

Uzuri wa hili tukio kila findings Wanazozipata zinawekwa online, tutajua tu ukweli muda si mrefu.
Bahati mbaya ni kwamba, uwezekano wa hadhara kuujua ukweli ni mdogo sana kuliko uwezekano wa hadhara kujua kile ambacho serikali ya Urusi inataka hadhara ikijue.
 
Madhaifu yapi? Watu wamefanya tukio la ugaidi wamekamatwa ndani ya siku moja na watuhumiwa wanasema yote baada akili kuwarudia wewe upo Maji Matitu unasema Urusi dhaifu daaah.
Hili tukio la ugaidi lisingetokea na kuleta madhara ambayo yameonekana mpaka sasa endapo intelijensia ingekuwa imara.

Kama ni suala la taarifa za kiintelijensia kabla ya ugaidi wenyewe walipewa ila Putin alizipuuza hadharani kwenye media siku 3 kabla ya tukio la ugaidi.

Ingekuwa ni kwenye nchi za magharibi, raia wangekuwa barabarani hivi sasa kumtaka rais ajiuzulu ama bunge limuondoe kwa kura ya kutokuwa na imani naye (impeachment).
 
Hili tukio la ugaidi lisingetokea na kuleta madhara ambayo yameonekana endapo intelijensia ingekuwa imara.

Kama ni suala la taarifa za kiintelijensia kabla ya ugaidi wenyewe walipewa ila Putin alizipuuza hadharani kwenye media siku 3 kabla ya tukio la ugaidi.

Ingekuwa ni kwenye nchi za west, raia wangekuwa barabarani hivi sasa kumtaka rais ajiuzulu ama bunge limuondoe kwa kura ya kutokuwa na imani naye (impeachment).
Unakumbuka tukio la Sept 11 Marekani? Vipi wananchi waliandamana kutaka Rais Bush ajiuzuru? Au bunge lilipiga kura kutokuwa na imani naye?
 
Unakumbuka tukio la Sept 11? Vipi wananchi waliandamana kutaka Bush ajiuzulu? Au bunge lilipiga kura kutokuwa na imani naye?
Bush hakuwahi kupuuza hadharani taarifa muhimu za kiintelijensia zinazohusu usalama wa raia kama ambavyo Putin amefanya.

Kauli ya rais wa nchi ya kupuuza hadharani taarifa muhimu ambazo zingeweza kutumika kuepusha maafa kwa raia ni kauli inayoonesha uzembe mkubwa katika ofisi ya rais.
 
Bush hakuwahi kupuuza hadharani taarifa muhimu za kiintelijensia zinazohusu usalama wa raia kama ambavyo Putin amefanya.

Kauli ya rais wa nchi ya kupuuza hadharani taarifa muhimu ambazo zingeweza kutumika kuepusha maafa kwa raia ni kauli inayoonesha uzembe mkubwa katika ofisi ya rais.
Jibu swali tukio la Sept 11 Marekani Bush alijiulzilu?
Marekani, Ukraine , Uingereza ndiyo wamehusika na tukio la Urusi imeishajulikana kwa mujibu wa uchunguzi wa Urusi.
 
Bahati mbaya ni kwamba, uwezekano wa hadhara kuujua ukweli ni mdogo sana kuliko uwezekano wa hadhara kujua kile ambacho serikali ya Urusi inataka hadhara ikijue.
Wanajeshi wa Urusi wanarecord live, vikosi vingi vya Urusi vipo independent, ama unafikiri ni kauli ya Putin kwamba mkimkamata tu kata sikio? Si Usa si Urusi wenye uwezo wa kuzuia taarifa zisitoke, nchi zote zina watu wenye inside info wanazo leak.
 
Wanajeshi wa Urusi wanarecord live, vikosi vingi vya Urusi vipo independent, ama unafikiri ni kauli ya Putin kwamba mkimkamata tu kata sikio? Si Usa si Urusi wenye uwezo wa kuzuia taarifa zisitoke, nchi zote zina watu wenye inside info wanazo leak.
Kwa kiasi kikubwa taarifa tulizopata mpaka sasa ni kutoka kwa watuhumiwa walioteswa. Hatuwezi kuujua ukweli kamili kwa staili hiyo.

Kuna mwanajeshi yeyote aliyerekodi live huo msafara wa watuhumiwa kuelekea Ukraine na ana ushahidi kwamba walikuwa wanaenda kupewa zawadi? Ama ni kauli tu zilizotolewa na watuhumiwa?
 
Hakuna lolote .......wale jamaa wanateswa na wanaambiwa hili mateso yapungue kira kitu waseme ni Ukraine......maana hata passport zao walisema ni za Ukraine kumbe uongo mijamaa ni kutoka Tajikistan..........yaani kira wakitaka kufanya kitu kina goma ......ila wanahalalisha vita kwa sababu walikuwa kwenye smo iliyoipa urusi gharama kubwa sana tokea taifa lile liundwe sasa hivi mafuta anaagiza Belarusian kwake jamaa wamelipua karibia visima vyote
Hizi taarifa bila shaka umezipata kutoka "RADIO KOMBOLELA"
 
Urusi inafanya "plot twisting" kwenye hii issue ya shambulizi la kigaidi.

Siku chache zilizopita, Putin alirudia yale madai yaliyokuwa yakisambaa awali kabisa kuwa magaidi walikuwa wakikimbilia Ukraine. Akatuachia swali tujiulize kwamba ni kwa nini walitaka kwenda Ukraine.

Saa kadhaa baadaye, mshirika wa karibu wa Putin, rais wa Belarus, Alexander Lukashenko, akadai kwamba magaidi walikuwa wakielekea Belarus kwanza ila walikutana na vizuizi (vituo vya ukaguzi ama checkpoints) ndipo wakabadili njia ili kuelekea Ukraine. Na akasema kuwa atatoa ushirikiano wa kiintelijensia kwa Urusi kuhusiana na hilo.

Hii statement ya Mzee Lukashenko inaonekana kuleta mkanganyiko mkubwa ukilinganisha na kauli za viongozi mbalimbali wa Urusi.

Pia, saa chache baadaye, mkurugenzi wa FSB (hili ni shirika la ujasusi la Urusi), akadai [bila uthibitisho] kuwa Marekani, Uingereza na Ukraine ndio walioratibu na kuwezesha shambulizi la Moscow huku Ukraine ikitajwa kama mhusika wa kutoa mafunzo kwa "magaidi" katika eneo lisilojulikana ndani ya Mashariki ya Kati.

Hiyo statement pekee inaonesha uzembe wa hali ya juu na ingetosha wakati uleule kumfuta kazi huyo mkurugenzi.

Hilo la watuhumiwa kwenda Ukraine "kupokea zawadi" ni jipya katika mtiririko wa matukio na huenda tukasikia mengine mengi zaidi ya haya.

Madai karibu yote kuhusu Ukraine kuhusika yanasemekana yametokana na kauli za wale watuhumiwa wa ugaidi mara baada ya kufanyiwa mahojiano. Tatizo ni kwamba, kauli zinazotokana na watuhumiwa waliopitia mateso wakati wanahojiwa huwa sio za kuaminika kwa namna yoyote ile.
Kwahiyo tuamini za kwako hapo Kimara bonyokwa, kisa unaitwa the great?!!
 
Urusi inafanya "plot twisting" kwenye hii issue ya shambulizi la kigaidi.

Siku chache zilizopita, Putin alirudia yale madai yaliyokuwa yakisambaa awali kabisa kuwa magaidi walikuwa wakikimbilia Ukraine. Akatuachia swali tujiulize kwamba ni kwa nini walitaka kwenda Ukraine.

Saa kadhaa baadaye, mshirika wa karibu wa Putin, rais wa Belarus, Alexander Lukashenko, akadai kwamba magaidi walikuwa wakielekea Belarus kwanza ila walikutana na vizuizi (vituo vya ukaguzi ama checkpoints) ndipo wakabadili njia ili kuelekea Ukraine. Na akasema kuwa atatoa ushirikiano wa kiintelijensia kwa Urusi kuhusiana na hilo.

Hii statement ya Mzee Lukashenko inaonekana kuleta mkanganyiko mkubwa ukilinganisha na kauli za viongozi mbalimbali wa Urusi.

Pia, saa chache baadaye, mkurugenzi wa FSB (hili ni shirika la ujasusi la Urusi), akadai [bila uthibitisho] kuwa Marekani, Uingereza na Ukraine ndio walioratibu na kuwezesha shambulizi la Moscow huku Ukraine ikitajwa kama mhusika wa kutoa mafunzo kwa "magaidi" katika eneo lisilojulikana ndani ya Mashariki ya Kati.

Hiyo statement pekee inaonesha uzembe wa hali ya juu na ingetosha wakati uleule kumfuta kazi huyo mkurugenzi.

Hilo la watuhumiwa kwenda Ukraine "kupokea zawadi" ni jipya katika mtiririko wa matukio na huenda tukasikia mengine mengi zaidi ya haya.

Madai karibu yote kuhusu Ukraine kuhusika yanasemekana yametokana na kauli za wale watuhumiwa wa ugaidi mara baada ya kufanyiwa mahojiano. Tatizo ni kwamba, kauli zinazotokana na watuhumiwa waliopitia mateso wakati wanahojiwa huwa sio za kuaminika kwa namna yoyote ile.
Upo sahihi Sana mkuu. Hao jamaa kutokana kibano walichopewa kwenye interrogation lazima waseme chochote kile ambacho serikali inataka.
 
Back
Top Bottom