BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Mkurugenzi Mkaazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Zlatan Milisic amesema uchunguzi waliofanya umeonesha wasichana watatu kati ya 10 wenye chini ya miaka 18, wapo kwenye ndoa za utotoni.
Zlatan amesema wanaoathirika zaidi ni wasichana wanaoishi vijijini huku akitaja madhara wanayokumbana nayo kiafya kuwa ni pamoja na Kuathirika Kiuchumi, Kijamii, Kisaikolojia na Kuondolewa Utu wao.
Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii pamoja na Kamati ya Sheria na Katiba kupitia Mkutano wa Bunge unaoendelea Dodoma, zinatarajiwa kujadili kwa pamoja ili kufanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa.
Kwa mujibu wa takwimu za UNICEF, inakadiriwa kuwa, wasichana watatu kati ya 10 nchini wanaolewa wakiwa bado watoto, na kuifanya Tanzania kushika nafasi ya 11 kwa ndoa za utotoni duniani.
Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inaweka miaka 18 kuwa umri mdogo ambao wavulana wanaruhusiwa kuoa, lakini imeweka umri wa miaka 15 kwa wasichana kuolewa kwa ridhaa ya wazazi, sheria hiyo wadau wametaka serikali ifanyie marekebisho, kwani inapingana na wakati na haipo wazi, ikishindwa kufafanua mtoto ni nani.
Zlatan amesema wanaoathirika zaidi ni wasichana wanaoishi vijijini huku akitaja madhara wanayokumbana nayo kiafya kuwa ni pamoja na Kuathirika Kiuchumi, Kijamii, Kisaikolojia na Kuondolewa Utu wao.
Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii pamoja na Kamati ya Sheria na Katiba kupitia Mkutano wa Bunge unaoendelea Dodoma, zinatarajiwa kujadili kwa pamoja ili kufanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa.
Kwa mujibu wa takwimu za UNICEF, inakadiriwa kuwa, wasichana watatu kati ya 10 nchini wanaolewa wakiwa bado watoto, na kuifanya Tanzania kushika nafasi ya 11 kwa ndoa za utotoni duniani.
Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inaweka miaka 18 kuwa umri mdogo ambao wavulana wanaruhusiwa kuoa, lakini imeweka umri wa miaka 15 kwa wasichana kuolewa kwa ridhaa ya wazazi, sheria hiyo wadau wametaka serikali ifanyie marekebisho, kwani inapingana na wakati na haipo wazi, ikishindwa kufafanua mtoto ni nani.