Wasichokijua Wengi Kuhusu Marko 10: 25 katika Biblia

Jana wakati naangalia ile muvi ya Yesu, nimekuja kuona Yesu anaisema iyo kauli wakati wakiwa wanapishana na ngamia mnyama. [emoji16][emoji16]

Balaa hili
 
Uyasemayo sidhani kama yanaakisi huwalisia...

Wengi watu wa imani tunautafsiri utajiri ktk Hali hasi...lakini tunasahau kuwa tunaviongozi wengi wa dini tena wanatuongoza ktk nyumba za ibada wanautajiri wa kupindukia.

Embu fikiria Hali ya kiuchumi ya wachungaji wengi barani Africa...afu angalia Hali ya wafuasi wao ( waumini).

Njoo tuwaangalie mapadre Hali zao za kiuchumi...afu tuangalie waumini wao.

Kwa kifupi tukiangalia wachungaji na mapadre wengi ni matajiri...

Swali la kujiuliza,je utajiri wao wa Hali??

Nahitimisha kwa kusema...utajiri si dhambi,wala sio kwamba matajiri hawataiona mbingu...wapo watakaoiona mbingu Ila ni wachache.

Kuichukua dunia haimaanishi kujitenga na utafutaji wa pesa,haimaanishi kutokujipenda kula vzur,kuvaa na kuendesha magari mazuri.

Kuichukia dunia ni kujiepusha na matamanio ambayo yanamchukiza Mungu...na kujisahaulisha kwa starehe fupi za kidunia na kusahau majukumu ya kimungu.
 
Uwe Padri, Askofu, Mchungaji, Unatoa pepo, Maadam wewe ni tajiri, unaangukia kwenye kanuni ile ile ya huwezi kumtumikia Mungu na Mali, either uambatane na Mungu au Uambatane na Mali zako. Mungu ni mwaminifu, maneno yetu mengi ya kupambana labda alimaanishe vingine haimsumbui. Kumbuka tajiri kuingia kwenye Ufalme wa Mungu anatakiwa achukue kanuni ya Yesu Kristo ya "Kujitoa Sadaka Yeye Mwenyewe". Yaani amtumikie Mungu yeye sio mali zake. Hakuna mtu mwenye hela nyingi ata kama ni Askofu anaejitoa sadaka kwa Mungu, wengi wanampa Mungu Sadaka ya pesa zao na mali zao na kujiokoa kutoka kwa Mungu. Matajiri siku zote huziokoa na kuziponya nafsi zao zisizurike kwa maana, wana vyeo na Mali, wanazipenda na wana fedha za kuzirinda, masikini yeye huiangamiza nafsi yake maana haoni samani ya dunia (Yesu alisema haiponyae nafsi yake ataingamiza na haingamizae nafsi yake ataiponya), Put Masikini yeye hujimaliza kwa sababu hana fedha wala dhahabu kwahiyo humpa Mungu vyote roho na mwili. KWA BINADAMU HAIWEZEKANI LAKINI KWA MUNGU YOTE YAWEZEKANA. Tuombeane.
 

Mkuu umaskini sio ndo kipimo cha uchamungu....kama ulikuwa hujui umaskini ni nusu ya ukafiri (kukufuru).

Bado hujajua kusudio sahihi wa ule msemo,na huenda ule msemo umekuja sahihishwa na aya hii ktk Qur'an.

Na si kwamba enzi za mitume hapakuwa na matajiri wakiwaamini mitume...laaa.

Walikuwepo matajiri wengi wakiwaamini mitume na walikuwepo maskini wakiwaamini mitume pia na kinyume chake.

Ondoa dhana hii kichwani kwako...utajiri sio dhambi,utajiri sio chanzo cha maovu...kuwa tajiri haimaanishi hauna sifa ya kuwa mfuasi wa Mungu (mcha Mungu).

Embu ilewe kwanza aya hiyo apo juu ndo utanielewa namaanisha nini.
 
Sawa, unavyoamini wewe. Naeshimu mawazo yako pia.
 
Hapana. Haina maana hiyo. Kule palestina enzi hizo za taifa la Israel kulikuwa na eneo la mlimani ambapo illikuwa ni njia kuelekea malishomomlakoni Ni wanyama wadogo tu hasa kondoo waliweza kupenya katikati ya miamba hiyo iloyokuwa imegusana. Kwenye njia hiyo, ngamia walishindwa kupenya kwa hiyo oakaitwa "tundu la sindano" kwa sababu ya udogo wake. Yesu alipotoa mfano huu was tajiri, alikuwa akimaanisha mahali ambapo ngamia wanashindwa kupenya na sio sindano ya kawaida.
 

Hakika unastahili heshima ya kipekee kuweza kudadavua hiyo hoja ya ama NGAMIA au KAMBA kwenye mfano alioutoa Yesu.

Mchambuzi mwingine anafafanua ifuatavyo:

Je! Katika Marko 10:25 Bwana Yesu alimaanisha ngamia mnyama au kamba katika Injili Takatifu ya Marko:10:25 alipowaambia mitume wake kuwa, ni rahisi ngamia kupenya katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu..

Mwanzilishi wa mjadala amehitimisha tafsiri yake ya aya hiyo kwa kuandika ngamia/camel inayomaanishwa kwenye bible ni kamba.

Baada ya kupitia Biblia Takatifu na baadhi ya nyaraka zenye kutoa ufafanuzi wa aya zenye utata fulani katika Biblia; naomba kutoa mchango wangu zaidi katika mjadala huu kama ifuatavyo:

1. Mafundisho ya Bwana Yesu katika Marko 10:25 yanalingana na Luka 18: 25 na Mathayo 19:24. Katika aya hizi zote, hakubainishwi kama Bwana Yesu alikuwa anaongelea ngamia mnyama au ngamia kamba.

2.THE AFRICAN BIBLE katika ukurasa wa 1766 imelifafanua neno CAMEL kwenye safu ya ufafanuzi ( footnote) kama ifuatavyo: ( tafsiri yangu ya kawaida) " A camel: ngamia kupita kwenye tundu la sindano ni usemi wa mfano kuelezea kile kisichowezekana kibinadamu. Ni Mungu pekee anayeweza kuleta wokovu. Lakini kuacha vyote kwa ajili ya kuingia katika ufalme wa Mungu kuna maana ya kupata zawadi iliyo kuu, sasa na baadaye. Huyo NGAMIA (kwa Kiebrania "GAMAL"), anayeelezwa mara nyingi katika Biblia hutumika kubeba mizigo mizito na kwa usafiri wa watu; na mara nyingi anahusishwa na makabila ya watu wanaohama hama, wa Afrika ya Kaskazini. Huu ni ufafanuzi uliotolewa wa Injili ya Luka 18:25.

Ufafanuzi wa Mathayo 19:24 ni kama ifuatavyo: " Camel": ( Linganisha Marko 10:25; Luka 18:25; Mathayo 23:24). Ngamia ambaye Mafarisayo hummeza wakati wakimchuja mbu(?) . Baadhi ya wadadisi wa maandiko wanatilia shaka kuwa huenda maandiko ya awali yalisomeka kama "KAMILOS" katika lugha ya Kigiriki yakimaanisha KAMBA ( au waya, CABLE). Hata hivyo, sura ya ngamia ( mnyama) kupenya kwenye tundu la sindano, haielezei ugumu, bali kutowezekana". Hapa pameonyeshwa picha ya mnyama ngamia.

Ufafanuzi wa Marko10:25 kwenye footnote: " Camel: "ni kama ifuatavyo: " Jambo muhimu ambalo Bwana Yesu anataka kusema hapa ni kwamba wokovu ni zawadi kutoka kwa Mungu; nayo haipatikani kwa juhudi za kibinadamu pekee".

2. GRUDEN'S COMPLETE CONCORDANCE TO THE OLD AND NEW TESTAMENT katika kufafanua neno "CAMEL", imeonyesha ifuatavyo katika ukurasa wa 74: "CAMEL": ( Ngamia ndio walikuwa wanyama waliotumika kwa usafiri wa binadamu katika nchi za mashariki kwa kuwa ni wanyama wenye nguvu kuliko farasi na wenye kustahimili zaidi magumu. KWA KUWA SEHEMU KUBWA YA ULIMWENGU WA KI-BIBLIA ILIKUWA AMA JANGWA AU NCHI KAVU/ KAME KATIKA VIPINDI FULANI VYA MWAKA, uwezo wa kipekee wa mnyama ngamia wa kuhimili mazingira magumu ya jangwani, ulikuwa ni wa kipekee. Mara nyingi utajiri wa mtu ulipimwa kwa kigezo cha wanyama ngamia. Ngamia walifugwa kwa ajili ya kufanyishwa kazi au kwa ajili ya usafiri wa haraka; na singa zake zilitumika kutengenezea mavazi ( HAPA ZIKANUKULIWA AYA ZA BIBLIA IKIWAMO HIYO INAYOSEMA :
" Ni rahisi kwa ngamia kupenya katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mbinguni, zikaorodheshwa aya Marko 10:25; Mathayo 19: 24; Luka 18:25 na Mathayo 23:24).

3. THE BIBLE READER'S
ENCYCLOPAEDIA AND CONCORDANCE: Imefafanua jina "CAMEL" kama ifuatavyo: "Camel ( Hebrew: " GAMAL". "Kati ya kumbukumbu za kale kabisa za watu wa mashariki, ngamia alichukuliwa kuwa miongoni mwa vianzo muhimu vya utajiri. Ngamia walipotajwa kwa mara ya kwanza kupatikana huko Misri, Arabuni au Kanaani, wanyama hao walipatikana kwa idadi kubwa na walilinganishwa na kondoo, ng'ombe na punda. Ngamia mwenye nundu moja ndiye ngamia anayeongelewa hapa. Haikuruhusiwa kula nyama ya ngamia, ijapokuwa maziwa yake yalikuwa yakitumika kama chakula kwa kiasi kikubwa. Ngamia walifugwa katika idadi kubwa mno". ...hapa pakaorodheshwa aya za Biblia ikiwemo Mathayo19:24 inayohusu somo tunalolijadili hapa.

Kwa upande mwingine, neno kamba, au kwa Kiingereza "CABLE" au "CORD", hakuna mahali katika Biblia Takatifu ambapo limeonyeshwa kuhusishwa na mafundisho ya Bwana Yesu katika Marko 10:25; Luka 18:25; Mathayo 19:24 au Mathayo 23:24 tofauti na maelezo ya mwanzilishi wa mjadala huu. Hata pale tulipoonyeshwa neno la Kigiriki "KAMILOS" katika ufafanuzi wa The African Bible kama ilivyonukuliwa hapo juu, pameoneshwa mashaka katika usahihi wa tafsiri hiyo. Na kwa kuwa enzi hizo Biblia ilipoandikwa, lugha ya Kiswahili ilikuwa bado haijazaliwa, kwa maoni yangu, ni makosa kusema kuwa Bwana Yesu alikuwa anafundisha juu ya ugumu wa kamba kupenya katika tundu la sindano.

Kinyume chake, na kama tulivyoona katika maandiko yenye kuaminika hapo juu; ni wazi kuwa Bwana Yesu alipokuwa anawafundisha mitume wake kwa kutoa mfano wa urahisi kwa ngamia kupenya katika tundu la sindano kuliko kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu kama alivyonukuliwa katika Marko 10:25; Luka 18:25 na Mathayo 19:24, alimaanisha mnyama ngamia na wala siyo "camel" kwa tafsiri ya kamba katika lugha ya Kiswahili.

Kwa hitimisho langu hilo naungana nawe kuwa tundu la sindano lilikuwa ni lango dogo la kuingia mji wa Yerusalem. Yesu hakumaanisha "sindano ya kushonea" kwa kuwa kwa wakati ule na hata wa sasa "sindano" zina ukubwa wa aina tofauti kulingana na ukubwa wa uzi. Na hata hiyo kamba inayotumika kwenye majahazi pia hupitishwa kwenye matundu yenye ukubwa unaostahili.
 
Kuna mtu aliwahi kusema hivi: ngamia iiliyoongelewa hapa na Yesu, ni milango ya majumba makubwa ya zamani yale yaliyokuwa yanayojengwa kwa architecture ya duara kama uwanja wa mpira, halafu mule ndani kunakuwa na uwazi mkubwa, na majumba hayo yanakuwa na nyumba nyingi zimekaa kwenye mduara. Majumba hayo yalikuwa yanakuwa na milango michache mikubwa (kama gates) na pia milango mingine midogo midogo yenye sura kama tundu la sindano, ambayo ngamia mnyama, alikuwa hawezi kupita kwenye milango hii isipokuwa binadamu peke yake. Ngamia wenyewe walikuwa na uwezo wa kupita kwa kutumia yale mageti yale makubwa tu. Milango hii iliyofanana na matundu ya sindano, ilikuwa inaitwa tundu la sindano. Ukweli ni kuwa tafsri uliyoitoa wewe hapa ndiyo ina uwezekano mkubwa wa kuwa sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…