Wasifu mfupi wa Mkurugenzi Mpya TISS, Ali Idi Siwa

Wasifu mfupi wa Mkurugenzi Mpya TISS, Ali Idi Siwa

Joined
Feb 18, 2019
Posts
53
Reaction score
539
Amb_Ali_Idi_Siwa.jpg
Balozi mstaafu Ali Siwa amekuwa katika utumishi wa umma tangu mwaka 1977 na kuweza kushika nafasi mbalimbali za uongozi.

Kati ya mwaka 2001 mpaka 2014, Balozi Mstaafu Ndugu Siwa alikuwa Afisa Mambo ya Nje, Mkuu katika ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Abu Dhabi iliyoko nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates); Moscow, nchini Urusi na baadaye Berlin, nchini Ujerumani.

Mwaka 2014, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, alimteua Ndugu Ali Idi siwa kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kigali, nchini Rwanda, nafasi aliyoihudumu mpaka mwaka 2018.​

Siwa.jpg

September 2018, aliteuliwa na Hayati Rais John Pombe Magufuli kuwa mwenyekiti wa bodi ya wadhamini NSSF, nafasi ambayo alikuwa anaitumikia mpaka mwaka huu.
Siwaa.jpg
 
Rais Paul Kagame alichelewesha kupitishwa kwa uteuzi wa Siwa toka August 2014 hadi Mei 2015 ambapo hatimaye aliruhusiwa kuwasilisha kitambulisho chake, na hivyo kumaliza tetesi za vyombo vya habari kwamba Kagame amekataa chaguo la Kikwete la kuwa mjumbe mpya wa Tanzania mjini Kigali.


Mwamba kama mwamba..
 
Utumishi wa miaka 46 serikalini. Kama alianza kazi mwaka 1977 akiwa kijana wa umri miaka 20 basi mwaka huu 2023 hakosi upungufu wa miaka 65 kwa umri.

Katiba ya nchi inatamka nini kuhusu ajira ya mtu wa miaka 65 ambaye ameshastaafu kazi miaka kadhaa kwa heshima na utumishi uliotukuka serikalini anayepata pensheni, Na swali kuu je anaweza kuteuliwa kurudi kwa ngazi ya Mkuu wa Usalama wa Taifa?

Toka maktaba 13 July 2023
NSSF INA UWEZO wa KULIPA MAFAO ZAIDI ya MIAKA 40 IJAYO, THAMANI YAKE ni KUBWA'' - BALOZI ALI IDI SIWA


View: https://m.youtube.com/watch?v=CcIR3esWuV8&
...Mwenyekiti wa Bodi ya Waadhamini ya NSSF, Balozi Ali Idi Siwa amewahakikishiwa wanachama wa NSSF kuwa Mfuko upo imara na kwamba una uwezo wa kuendelea kuwalipa Mafao mbalimbali kwa zaidi ya miaka 40 ijayo
 
Utumishi wa miaka 46 serikalini. Kama alianza kazi mwaka 1977 akiwa kijana wa umri miaka 20 basi mwaka huu 2023 hakosi upungufu wa miaka 65 kwa umri.

Katiba ya nchi inatamka nini kuhusu ajira ya mtu wa miaka 65 ambaye ameshastaafu kazi miaka kadhaa kwa heshima na utumishi uliotukuka serikali na kwa ngazi ya Mkuu wa Usalama wa Taifa.
Ndio na hapo anaweza akagonga mpaka 2030 ndio wakamchomoa
 
Back
Top Bottom