Wasifu wa Godbless Jonathan Lema


Diploma inatosha kuongoza, ila nimependa zaidi publication zake. Nilikuwa namchukulia poa ila sasa nampa heshima kwa hizo kazi zake.
 
Umejuaje kama ni chuo? hapa JF unavyowajua wenzio nawao wanakujua hivyo...Pole sana dogo hata kukanusha hujui, by the way upo kwenye ignore list yangu, waweza endelea tu< eti sikijua chuo, umejuaje Butimba ni chuo

Teh teh teh, umeniweka kwenye Ignore list yako halafu bado unahangaika kunisoma na kufuata thread zangu.
 
Mkuu Samaritan,

Unapinga halafu hapo hapo unaniambia nilete orodha, hata kama ni distance learning hawawezi kujua wanafunzi waliopata diploma 2008?

Nnachomaanisha ni kwamba, hawana huo utaratibu unaoutegemea wa formal kwamba wanafunzi kadhaaa wamemaliza kipindi flan.

Ndio maana nikasema kama unalist ya wahitumu wote wa diploma wa mwaka 2008 isiyo na jina la Lema utakua sahihi kwamba amedanganya. Ikumbukwe kwamba amejiunga 2008 na akamaliza 2010, list yako lazima iwe ni ya wahitimu wa 2010.

Na hata hivyo sijajua lengo lako kwamba hakusoma huko au ana elimu ndogo. Thanks mkuu Ritz
 
Kamanda Godbless Jonathan Lema kiboko ya magamba ndiyo habari ya mujini. Ametoka kuwapiga 4 o'clock na sasa amejielekeza mikoa ya kusini kuwazindua watanzania walioko usingizini. Katika hali kama hiyo ni lazima buku saba fc waanzishe threads kumi kwa siku zinazomhusu Lema.

Bahati nzuri sasahivi watanzania wengin hawaangalii uzuri au ubaya wa cv ya mtu kwenye makaratasi bali wanaangalia utendaji wake zaidi. Na katika hilo kamanda Lema amethibitisha kuwa yeye ni mtendaji wa uhakika na ndio maana amekubalika kwa wananchi.

Kamanda Godbless Lema atosha, ccm wanahaha wakimsikia anapita mtaani kwao.
 

Mkuu Lema hajawahi kusoma Uingereza.
 
Ofisi ya Bunge, wabunge wote wanapeleka CV zao ofisi ya bunge.

...for that case issue ipo kwa aliyeingiza data na sio aliye peleka vyeti, so ofisi ya bunge lazima iseme kwanza kwamba hawajakosea ndipo utaweza kumlaumu lema,vinginevyo itabaki kuwa technical error...
 
Mkuu Lema hajawahi kusoma Uingereza.

Yaani nimecheka kweli kiongozi, mbona mimi nimesoma hicho chuo japo sijafika Uingereza? Any way mwisho wa siku tunaangalia anawatumikiaje wananchi au jamii. Siku njema
 
sasa kama ana CV ya Uongo na bado anawahenyesha ccm basi huyu JAMAA ni genius ! kama hajaenda shule ya kutosha alimmwaga DR Batilda na elimu yake yote basi jua huyu mtu ana karama nani kiongozi wa watu, kama Kundi zima la wapiga kelele la ccm lilimshindwa hivi juzi kule Arusha akiwa na elimu yake ndogo basi jua huyu ni mti maalumu.
Kama Lema mwenye elimu ndogo anawabwaga ccm hata mahakamani basi jua ccm ni chama cha watu wasio na weledi wakutosha.

kama Lema mwenye elimu ndogo anaweza kuwakosesha usingizi ccm wote basi HUYU MTU ANABARAKA ZA MUNGU.
 
A CV is just a piece of paper like any other e.g a serviette paper; and who cares about the contents of that piece of paper?!
We the people of Arusha and particularly members; followers nad fans of CHADEMA tuliomchagua na kumtuma GJL mjengoni hatuna haja ya kujua kilichoandikwa ndani ya CV yake, tunachojali zaidi ni kama anakidhi mahitaji na matakwa yetu.

If you are a who is who in Tanzania; tafadhali weka VC yako hapa for comparison na hii ya GJL, But if you are a none entity then achana nayo kwa sababu hatuna jinsi ya kui-authenticate.

So the magical question here is: Is GJL performing and meeting Arusha peoples expectations? the answer is YES INDEED; and gallantly so. kama hutaki kuamini tafadhali make time mtafute Savimbi Mwigulu Nchemba (May he rot in hell!) atakwambia GJL: ni nani Nji hii.

Bravo GJL; stay focused on your noble cause. A new Tanzania; The Tanzania we want; free of Che_Che_Mea a.k.a CCM psycophants, embezellers and the corrupt.
 
Ishu sii elimu...ishu ni unaitumiaje elimu uliyoipata!..Mbona kuna yule jamaa yenu wa Harvard alionekana akimwaga ndumba bungeni?Huyo nae elimu imemsaidiaje?au mzee wa"nasema wapigwe tu"naye si mwanasheria?mbona aliongea pumba hizo na vilio juu tena mjengoni?Lema ni mchapa kazi full stop.
 
Katika siasa mtaji ni watu na sio cv,,,ubunge,,uwaziri na urasi sio taaruma bali ni cheo,,,mfano aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani masha na mbunge wa nyamagana ameleta maendeleo gani katika jimbo,,,yeye ana cv nzuri lakini hana mtaji wa siasa,,ndio maana hata msahau wenje maisha yake,,,,,
lema- anaanza na mungu na anamaliza na mungu,
-mtaji wake ni watu na sio cv,,,,, siri ya ccm anaijua lema....anasema ccm ni waogaaaaaa
 
Mkuu Lema hajawahi kusoma Uingereza.
Ritz...Cambridge International Collage sio Cambridge University...hivi ni vitu viwili tofauti kabisa.Cambridge International Collage(CIC) ni chuo kinachotoa mafunzo kwa distance learning.Mbona watu kibao tu wamepata diploma zao kupita chuo hiki?Unaposema Lema hajasoma Uingereza ni kweli kabisa lakini hilo maaninishi kwamba hiyo diploma hana.
 
Yeye (Mh. Lema) anasema "dhambi kubwa kuliko zote ni uoga", nyie endeleeni kusema "dhambu kubwa ni kuishia Form IV" alafu msubirie 4 - 0 nyingine.
 
Yaani nimecheka kweli kiongozi, mbona mimi nimesoma hicho chuo japo sijafika Uingereza? Any way mwisho wa siku tunaangalia anawatumikiaje wananchi au jamii. Siku njema

Kama umesoma online sawa kwa hiyo mmesoma wote na Lema online?
 

Yote unayosema ninayafahamu vizuri tu wala sijachanganya vyuo angalia juu ya CV ya Lema nimeweka link ya chuo gani.
 
Ritz katoa CV tu jamani mbona anashambuliwa?
Mkuu wangu hawa makamanda wana mapenzi mabaya sana Chadema imewapa upofu.

Lema kachekama vibaya kwenye CV wanasema wao wanaangalia mtu hawana haja na CV teh teh teh.

Angekuwa mtu mwingine wangemuita majina mengi mara kilaza, pimbi, lakini Lema wote kimya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…