Wasifu wa Godbless Jonathan Lema

Wasifu wa Godbless Jonathan Lema

Jamani jaribuni kumuelewa Masando anasema nini?mbona mnaingiza mada nyingine sasa mnakuwa kama sio great thinkers,mambo ya waarabu ya nini hapa tuongelee yetu,Approach ya Lema ndio inayotakiwa kudai haki kutokana na watawala wa Tanzania walivyoziba masikio yao kwa pamba,wamenogewa mpaka wanaona ni dhambi kuachia madaraka,ni dhambi kwao kuwa wakweli,ni dhambi kwao kuacha kuiba mali ya umma na hata kura,ni dhambi kwao kuona CDM inashika dola,ni dhambi kwao kuona CUF inashika dola,ni dhambi kwao kuona NCCR kushika dola,ni dhambi kwa CDM kuwa chama rasmi bungeni kwa tafsiri walioifuta, sasa ukiangalia vyote hivi mimi ninakubaliana na Msando kuwa iko haja ya kubadili approach ya kudai haki,kwani haki haiombwi.Ukichunguza vizuri kuna mambo ambayo sasa yamelegezwa baada ya CDM kufanya,naomba niwambieni kuna vitu viwili vimefanyika baada ya maandamano ya tarehe 05.01.2011 Arusha,uchaguzi wa meya Mwanza ilibidi ufanyike na mshindi halali kupatikana,maana huko nako CCM walikuwa wanaleta kasheshe wakitaka wao ndio wawe na meya,maandamano sasa hivi yanafanyika baada ya watawala kuona sasa wao ndio wavunja katiba,wangekuwa na uwezo leo wangebadilisha na kuondoa kabisa kipengele kinacho sema ruksa maandamano baada ya kutoa taarifa,na hili alilofanya Lema kwa mtoto wa mkulima nalo ni fundisho kwa watawala na hawatarudia tena kuwa bias na kudhulumu haki ya watanzania.Bado inabidi tuwasaidie wale wote walioamua kujitoa muanga kwa ajili ya taifa letu na vizazi vyetu.Tusiporekebisha mfumo wa utawala leo ndio tutaingia katika machafuko yasio ya lazima,hao wanao hubiri amani amani je tuwaulize kwanini wanafinyanga haki zetu za kuchagua,kuchaguliwa,Elimu, afya na nyinginezo,watawala wa Tanzania sasa hivi ndio wamekuwa mabilionea je wamezipata wapi fedha hizi kama sio kudhulumu haki za watanzania.Wakati umefika sasa kila mtu awe askari wa mwenzake tuwamulike wote mabaladhuli wanoipa umasikini Tanzania yenye kila kitu, maji,chakula,madini,gesi,aridhi,misitu,mbuga za wanyama na watu wa kutosha wenye nguvu ya kuzalisha wanokandamizwa na kudhoofishwa kiafya kwa lazima na watawala wetu ili waneemeke wao na famila zao.Nchi hii inaliwa na viongozi kwa mambo ya hovyo hovyo nani aliwaleta au walijuaje tunataka mashine za kufua umeme au kuendesha shirika letu la Reli,ni viongozi hao ndio waliowaleta Dowans,IPTL,RITES,RICHMOND na wengine wote wanao dhulumu haki yetu hakuna mwingine ni viongozi wetu fuatilieni sana hivi vitu vinavyoitwa ziara ziara za viongozi ndio haya mambo yanakotokea,tusubiri hao wafanyabiashara wa India tulioambiwa watakuja kuwekeza kwetu kuna madudu humo ndani yatakuwapo tu ninavyo hisi,ndio yalikotokea IPTL,kuna mradi ulikuwa uje wa kusafisha maji ya bahari ili kutumiwa na binadamu kwa kunwa huo mradi nilikuwa nasubiri nione watanzani ambavyo tungekamuliwa mpaka tukauke damu na mradi mingine mingine,maana viongozi wetu wamekuwa wepesi wanarubuniwa na wao wanakubali kwa kupewa au Pesa au ubia wa hayo makampuni
Hima sasa tuongeze nguvu tulinde mali zetu na utajili tulio nao kwa manufaa ya Tanzania.
 
Du hapo kwa Lema kweli anaonewa, maana ya Dowans lisizungumzike kwani lipo Mahakamani, la Arusha leta ushahidi wakati kesi inaendelea hivi BUNGE ni MAHAKAMA? Spika kweli anaelewa mihimili mitatu? jana kanichanganya tena Dada Matiku wa Viti maalum CDM Mara kachakachuliwa asubuhi kweupe na Stela Manyanya (nafasi ya UDSM)
Mwacheni mmachame apandishe munkari (kapa kyandu kikifinjika utalipa) amesema risasi bora
 
Lema anaelewa kilichompeleka kule, hajaenda kusinzia, wala kuunga mkono hoja zisizo za msingi, pia hajaenda kuuza sura ameenda kufanya kazi so nawashangaa wanaomuona mkorofi, big up Lema kaza buti kuna jeshi kubwa sana nyuma yako!
 
Lema, Mbowe, Ndesa, Slaa, na wengine wanajua wakiwa na madaraka katika nchi biashara zao ziko salama zaidi. Usitegemee kupata msaada kutoka kwao. Watatutumia kwa manufaa yao tu. Tunisia wamemtoa rais bado wanasema shida zipo palepale. African we are finished. Why western countries are supporting opposition parties? Kuna kitu wanakikosa kwa watawala wa zamani. They want new system to rule Africa politicaly, economicaly and mind.

we ndg umepotoka:-
Kwa taarifa yako hata wewe kuingia humu jamvini unajua biashara zako zitakuwa salama. Na maanisha kwamba kila mtu anaingia au kufanya jambo fulani ili biashara yake iwe salama. Biashara ni pamoja na kuona mawazo yake yananufaisha watu wengine, kuona unakumbukwa kwa mema uliyofanya, kuona unakumbukwa kwa mabaya uliyofanya na mengine mengi yanayofanana na biashara hizo. Mfano Mkapa alitaka kukumbukwa kwa kukuza uchumi wa nchi; Mwinyi alitaka kukumbukwa kwa kutoa ruhusu kwa kila mtanzania afanye atakalo; Nyerere alitaka kukumbukwa kwa kujenga umoja wa watanzania na waafrika kwa ujumla wake n.k. hao wote biashara zao ndizo hizo na walitaka ziwe salama hata kama kwa kuumiza wengine. ndiyo sababu mkapa liiingiza uongozi mpya tanesco kwa bunduki, ndiyo sababu mwinyi aliruhusu waislam wavunje bucha za nguruwe huku akiruhusu watu wale nguruwe, ndiyo sababu nyerere aliwafanya akina Babu wakimbie nchi, n.k.
KWA MIFANO HIYO HAPO JUU; Bado akina Slaa, Mbowe na Ndesa wana kila sababu ya kuchukua nchi ili biahsara zao ziwe salama maana walishaziainisha kwamba ni kuondoa umaskini uliokithri katika nchi hii. Na wameenda mbali zaidi kwa kuonyesha mamna gani wataondoa huo umaskini!!! wangesema tu bila kutueleza namna watakavyoondoa, basi ningesema biashara zao hazna maslahi kwa watanzania na HAWAKUBALIKO!!!!
 
Ni kweli kaka, binafsi sikupata kumjua Lema before, ila nilimsikiliza vizuri sana wakati wa kampeni zake na kwenye midahalo na vikao mbalimbali. Huyu jamaa inawezekana akawa hana elimu kubwa ila reasoning capacity yake ni kikubwa sana na ana uwezo wa kufanya mambo mengi makubwa kama msomi tena msomi kweli kweli. Mimi naamini leaders are born so Lema was born to be the Leader. Let us support him coz atatusaidia sana kusukuma hili gurudumu la maenedeleo

Kama vipi ikifika 2015 tumsimamishe yule mzanzibari aliyekuwa mgombea mwenza kwa nafasi ya urais na Lema awe mgombea mwenza maana hawa wasio na elimu ndio mtaji mkubwa wa CDM na wanauelewa wa hali ya juu na tunu za uongozi zisizo na kasoro
 
Lema, Mbowe, Ndesa, Slaa, na wengine wanajua wakiwa na madaraka katika nchi biashara zao ziko salama zaidi. Usitegemee kupata msaada kutoka kwao. Watatutumia kwa manufaa yao tu. Tunisia wamemtoa rais bado wanasema shida zipo palepale. African we are finished. Why western countries are supporting opposition parties? Kuna kitu wanakikosa kwa watawala wa zamani. They want new system to rule Africa politicaly, economicaly and mind.

Mkuu naona kama una mawazo ya mwaka 47 ya zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa chama!!!! Usiogope mabadiliko. Lazima tuthubutu kujaribu mabadiliko na tutakaowapa wakishindwa tunawanyanganya tunawapa wengine mpaka tutakapopata wanaotufaa. Mbona Rwanda wanaweza?
 
..hana lugha ya kubembeleza.

..hana nidhamu ya woga.

..CCM inaogopa sana watu wenye tabia kama za Godbless Lema.

NB:

..sijui kama mliona facial reaction ya Mzee Msekwa siku alipoambiwa na Lema kwamba watanzania wanadai katiba mpya hawaombi katiba mpya. Msekwa looked shocked inawezekana ktk utumishi wake wa muda mrefu amezoea kukutana na watu wanaoomba haki badala ya wanaodai haki.
 
Lema hana lolote. He is just a former criminal.

kishongo bwana tushakuzoea kwa pumba zako... Ebu tupe ushahidi mmojawapo wa moja ya crimes alizowahi kutenda lema,... Manake lema ni jirani yangu, na ni siku nyingi sana tunaishi karibu maeneo ya njiro arusha, sijawahi kupata kusikia lolote baya alilowahi kutenda, ebu tujuze ndugu kishongo...
 
hivi Rage aliwahi kufungwa? Kingereza anakuwa 'former criminal' au 'convicted person'. Na Mramba ni nani? Chenge je?
 
Tunamheshim, Tunamkubari, Tunampenda lakini ikua MP bado hajakomaa vyakutosha inapaswa azidi kujijenga labda kufikia 2025 atakua ameiva kiasi chakua mtulivu na asie kulupuka.
 
wanasiasa wanaonifurahisha sana ni pamoja na huyu mh Lema.
 
Zomea zomea jana iliwakuta baadhi ya wajumbe wa halmashauri ya ccm wakiwa katika mabasi mawili ya abood wakitokea dodoma na bendera zao katika eneo la ubungo stendi kuu; wananchi waliokuwepo walisikika wakitaamka kwa nguvu;- mafisaadi hao! Wala hatudanganyiki.

Kwa kweli akina mukama wana kazi kubwa kurudisha imani kwa wananchi; sie wana ccm mzigo tunao
 
Eti wana mpango wa kuenda kujisafisha mikoani. Hawa jamaa hawajui huku mitaani kwetu tunawaonaje .
 
Hiyo nayo mijinga ilikuwa inafata ninin pale wakati hilo jimbo la CDM? Wangeipiga ingelalamika? CDM msiwaruhusu hawa ambao hawajavua magamba kuingia katika majimbo yenu!
 
hata watumie jik kamwe hawasafishiki, nyoka ni nyoka tu hata akijivua gamba hawez kuwa tumbili, wasipoteze muda wajiachie tu, kwa sasa wananchi wanajjua kila kinachoendelea, HATUDANGANYIKI TENAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA! what is CCM bana!
 
hata watumie jik kamwe hawasafishiki, nyoka ni nyoka tu hata akijivua gamba hawez kuwa tumbili, wasipoteze muda wajiachie tu, kwa sasa wananchi wanajjua kila kinachoendelea, HATUDANGANYIKI TENAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA! what is CCM bana!
werawera weraaaaaaa. Nimeipenda hii mkuu
 
Back
Top Bottom