Wasifu wa Rais Samia Suluhu Hassan

Wasifu wa Rais Samia Suluhu Hassan

Nchi imefika mahali, tunaweza kuwekewa pandikizi toka popote na akawa ndiye kiongozi wanchi.
Kama hali hiyo siyo ya kutisha, tuiite ni hali ya namna gani hiyo?

Sijasema popote kuwa aliyepo sasa ni pandikizi, lakini inawezekana, kwa sababu hatujui alitokea wapi hadi akafika alipo sasa.
Kama pandikizi la Burundi!
 
Kuna yule mzee aliwai onyewshawa kwa TV akisema aliwai soma na samia na kucheza nae utotoni huyo ataweza tusaidia
 
Wasifu wa sasa🐒🐒🐒
 
Tanzania anastahiki kumpata rais anayekubalika na kuwafanyia kazi waTanzania, siyo mataifa ya huko unayoyatafuta wewe.
Samia hana uwezo. Hadi 2025 Tanzania itakuwa ni jalala la uchafu wa hao unaowaita watu wa nje wanaomkubali yeye.

Na zaidi ya yote, na pengine ndiyo chanzo cha ubovu wa uongozi wake, Samia hana maslahi ya nchi hii moyoni mwake.
.
 
Bi Samia Suluhu alizaliwa Januari 27, 1960 visiwani Zanzibar. Alisomea shule za msingi za Chawaka (Unguja), Ziwani (Pemba) na Mahonda (Unguja) na kati ya 1966 na 1972 na kisha akasomea masomo ya upili Ngambo, Unguja (1973-1975) na Lumumba, Unguja (1976).

Alisomea kozi mbalimbali hadi akafikia kupata shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Southern New Hampshire nchini Marekani.

Kazi
Aliajiriwa kama mchapishaji katika serikali ya Zanzibar mwaka 1977 na akapanda ngazi hadi kuwa afisa wa mipango serikalini kati ya 1987 na 1988.

Alihudumu pia kama meneja wa mradi wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) Zanzibar kati ya 1985 na 1997, na pia kama meneja mkurugenzi wa Mwamvuli wa NGO 1998 hadi 1999.

Bi Samia anasema kuwa njia yake ya ufanisi haijakuwa rahisi kama inavyodhaniwa.

''Safari yangu katika siasa imekuwa njia ndefu na yenye tija.''

Kimsingi ufanisi wangu katika siasa za Tanzania umetokana na uweledi na umakini katika kila jambo ninalolifanya.''

''Sio rahisi kuwajibikia familia yako wakati huohuo ukiendelea na maisha ya siasa elimu na majukumu mengine ya kikazi," anasema Bi Samia.

Familia
Aliolewa mwaka wa 1978, kwa Bw Hafidh Ameir, ambaye wakati huo alikuwa afisa wa Kilimo .

Walijaliwa watoto wanne.

Mmoja kati ya wanawe Wanu Hafidh Ameir (1982), ni mwakilishi maalum katika bunge la Zanzibar

Siasa
Alijiunga na siasa mwaka wa 2000.

Wakati huo alijiunga na bunge la wawakilishi la Zanzibar kama mjumbe maalum.

Haikuchukua muda mrefu nyota yake ikaanza kung'aa na akateuliwa kuwa waziri na rais Amani Karume, akipewa wadhifa wa Waziri wa Leba, Jinsia na Watoto.

Alitumikia taifa hadi mwaka wa 2005 alipochaguliwa tena na kuteuliwa upya kama waziri, wakati huu akipewa wizara ya Utalii, Biashara na Uwekezaji katika serikali ya visiwani.

Mwaka wa 2010 alichaguliwa kuwa mwakilishi wa jimbo la Makunduchi.

Punde tu akateuliwa na rais Jakaya Kikwete kuwa waziri wa maswala ya muungano katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akihudumu chini ya Makamu wa Rais Mohamed Gharib Bilal.

Machi mwaka 2014, aliwania na kuchaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba nmjini Dodoma. Bi Hassan alichaguliwa kwa kura 390 sawa na asilimia 74.6 na kumshinda mpinzani wake Amina Abdalla Amour ambaye alipata kura 126 sawa na 24%.

Julai mwaka 2015, Dkt John Magufuli alimteua kuwa mgombea mwenza.
===
First Name: Samia
Middle Name: Hassan
Last Name: Suluhu
Member Type: Elected Member
Political Party: Chama Cha Mapinduzi
Office Location: P.O. Box 3021, Dar Es Salaam
Office Phone: +255 774 010 203/+255 784 717 712 Office Fax:
Date of Birth 27 January 1960

EDUCATION
  • School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
  • Ziwani Primary School, Pemba CPEE 1970 - 1971 Primary School
  • Mahonda Primary School, Unguja CPEE 1972 - 1972 Primary School
  • Chwaka Primary School, Unguja CPEE 1966 - 1968 Primary School
  • Ngambo SecondarySchool, Unguja CSEE 1973 1975 Secondary School
  • Lumumba Secondary School, Unguja CSEE 1976 1976 Secondary School
  • National Institute of Public Administration, Lahore Pakistan Course 1989 1989 Certificate
  • Institute of Management for Leaders, Hyderabad, India Management Course 1991 1991 Certificate
  • Zanzibar Institute of Financial Administration, ZIFA Statistics 1983 1983 Certificate
  • Institute of Development Management, IDM, Mzumbe (Morogoro) Advanced Diploma 1983 1986 Advanced Diploma
  • Manchester University, London Postgraduate 1992 1994 Postgraduate Diploma
  • Open University Southern New Hampshire, USA M.A 2004 2005 Masters Degree

EMPLOYMENT HISTORY
  • Company Name Position From To
  • The Parliament of Tanzania Member - Makunduchi Constituency 2010 2015
  • Ministry of Tourism, Trade and Investment, Zanzibar Minister 2005 2010
  • Ministry of Labour, Gender Development and Children Minister 2000 2005
  • Mwamvuli wa NGO Managing Director 1998 1999
  • Revolutionary Government of Zanzibar Planning Officer 1987 1988
  • World Food Programme, WFP - Zanzibar Project Manager 1985 1997
  • Revolutionary Government of Zanzibar Typists (Typing Pool) 1977 1986

POLITICAL EXPERIENCE
  • Ministry/Political Party/Location Position From To
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Guardian (Warden) - North Unguja Region 2009 Todate
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Guardian (Warden) - North Pemba Region 2004 2007
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Member - National Executive Committee (NEC) 2002 Todate
Dah umenistua wasifu wa nini tena?
 
7. Mwanamke akilala na mwanaume huyu leo, na mwanaume huyu kesho, halafu akapata ovulation on the 3 day... hawezi kujua for sure ni ujauzito wa yupi mpaka mtoto azaliwe!......

9. Anayejua for surely who is baba halisi wa mtoto, ni mama!
Huoni kwamba unaji contradict ? Tushike lipi tuache lipi?

Bullet point yako namba 7, Mama mtu hawezi jua Baba ni nani iwapo amelala na watu wawili ndani ya siku kadhaa za ovulation, ndio sayansi. Sentensi yako namba tisa, "anaemjua baba ni mama" ni total garbage, msemo wa Waswahili tu, Nakusoma nielewe umekuja na sayansi ya kuni support au kunipinga nione nimekosea wapi, nakuta humo humo unaji contradict we mwenyewe, mbona unakurukupa kurupuka tu Mayalla ?
 
Haya mambo haya yakiendelea kufichwa fichwa iko siku moto utalipuka

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
Kuna wapuuzi humu wanatuambia Eti baada ya huyu anakuja aliyepo zenji nw aje kutawala huku 2025,

Nchi hii tupate KATIBA mpya na Tume huru kabla ya Uchaguzi wowote.

Nchi imevimba,

Wakilazimisha, mbeleni Si kuzuri.

Tusubiri.
 
Baba yake ni marehemu Mzee Suluhu Hassan.

Kaka yake ni Rashid Suluhu Hassan.

Dada yake ni Mgeni Suluhu Hassan.

Kwa mujibu wa makala hii ya BBC.

'Rais Samia alipenda kusoma, baba yetu alimhimiza afaulu’. Familia yake yaeleza​

  • Halima Nyanza
  • BBC Swahili
20 Aprili 2021
---

Akiwa mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya urais nchini Tanzania, Watanzania wamekuwa na hisia na mitazamo mbalimbali juu yake.

Lakini familia yake na watu wake wa karibu wanamfahamu vizuri kuliko ilivyo kwa watu wengine .

Rashid Suluhu Hassan ni kaka wa Rais Samia anasema jitihada anazozionesha hii leo , alianza tangu akiwa mdogo.

''Alikuwa mtu ambaye ana ari ya kusoma, bidii ya kusoma, alikuwa anapenda kuambiwa soma uwe kama mtu fulani, unamuona kaka yako hapa kwasababu Baba yetu alikuwa mwalimu, hivyo openness alikuwa nayo tangu zamani sana kwa hiyo watoto wake alikuwa akiwaachia nafasi''. Alisema Bw. Rashid.

Kaka yake anasema hakuna yeyote kwenye familia aliyewahi kuwa na ndoto kuwa siku moja atakuwa kiongozi...

''Hakuna mtu alijua.. kama ingewezekana kumfufua marehemu Mzee Suluhu sasa hivi akaamka ukamwambia leo Samia ni rais atakushangaa sana''. Alisema Bw. Rashid

Mgeni Suluhu Hassan ni dada wa Rais Samia anasema hakutarajia mdogo wake kushika nafasi ya juu kabisa ya uongozi nchini Tanzania.

Lakini pia hakushangazwa pia kutokana na rekodi yake ya kushika nafasi mbalimbali akipanda hatua kwa hatua.

''Kapita kwenye nyanja nyingi akianza tangu chini kabisa, mpaka akawa mbunge, kaliongoza bunge la katiba pia, anaweza na anajitahidi kuweza na ataweza''.

Tumsaidie na kumshauri vizuri.'' alisema Bi.Mgeni

Chanzo cha picha, Ikulu Tanzania

Chanzo: BBC

Kwamba baba yake ni Marehemu Suluhu Hassan?

Lipo wapi kaburi Hilo?
 
Wewe inaonekana bado ni mtoto mdogo sana!!! Samia kafahamika mwaka 2015!!!!! Tafuta nyadhifa mbalimbali alizowahi kushika kabla huko Zanzibar na kwenye URT kabla hujaandika huu utumbo!!!
Nani anafuatilia viongozi wa Zanzibar wee kima!! Huyo alikuwa nobody hata huko Zanzibar.Labda nyie Maccm ndiyo mna interest ya kufuatilia nyadhifa za Maccm wenzenu hadi level ya mtendaji wa mtaa.
 
Aliyepewa Gari Mpya aina ya Benz iliyo chini sana miaka kadhaa iliyopita ili asipate shida Kuipanda kutokana na sasa kuwa ni Mzee mno huku akikosa hata Kumbukumbu za Kuwajua Wanawe baadhi wenye Vyeo kama alivyokuwa navyo Yeye kati ya mwaka 1985 hadi 1995.
Kumekuchaaaaaaa!!!! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom