Wasikilizaji wa Radio Imani: Ole wake atakayewalisha watoto wetu mchele wa msaada wenye virutubisho

Wasikilizaji wa Radio Imani: Ole wake atakayewalisha watoto wetu mchele wa msaada wenye virutubisho

Sakata la mchele wenye virutubisho kutoka Marekani limeendelea kuchukua sura mpya baada ya waislamu kuukataa bila kumumunya maneno. Wakiongea kupitia redio ya kiislamu ya Imaan FM inayounguruma kutokea mkoa wa Morogoro, wamesema hawautaki mchele huo na wametoa tahadhari kwa mtu yeyote atakayewalisha watoto wao. Wamesema chakula wanacho cha kutosha hapa nchini na kushauri waletewe vitu wasivyokuwa navyo kama vile ndege, magari na ambulance.

Ili kuonyesha kuwa hawatanii katika hili, hata watangazaji waliokuwa wakiendesha kipindi walionekana kushabikia kitendo hicho. Mtu yeyote aliyepiga simu kwenye kipindi akionyesha kwenda kinyume na msimamo wao, walimkatia simu mara moja. Hebu wasikilize wewe mwenyewe kupitia klipu hiyo hapo chini.

MAONI YANGU
Huu mchele sasa naona umeanza kutugawa kiitikadi. Wakristo nao wakitoka hadharani na kuweka msimamo wao, hapatatosha. Ifike mahali ubaguzi wa kijinga kama huu ukemewe kwani unaweza kuligawa taifa na kuhatarisha umoja na mshikamano tulio nao hapa nchini. Tusiruhusu kikundi kidogo cha watu kitugawe kwa sababu yoyote ile.

Nawasilisha.
ujinga ni tatizo kubwa sana nchini kwetu..!
 
ujinga ni tatizo kubwa sana nchini kwetu..!
Sana. Majitu yanajifanya kukataa msaada wa mchele huku yakikubali kupokea misaada ya fedha, scholarships, dawa na vitu vingine. Kama ina jeuri ya kutosha, basi ikatae kila kitu. Pambaf!
 
Wewe wa wapi ,kwamba hata kwenye familia yako ukiletewa msaada bila kujali unatweza utu wako na familia yako unapokea tu.

Mfano waje watu TASAFU, wakuletee msaada kwako kama kaya masikini na wewe haupo kwenye mlengo huo we unapokea tu, aisee we no noma,
Zawadi ni zawadi (kumbuka wimbo wa Twanga Pepeta). Usijitoe ufahamu. Ukiletewa zawadi hata iwe ndogo, usiibeze. Kuwa na utu na kujitambua.
 
Sana. Majitu yanajifanya kukataa msaada wa mchele huku yakikubali kupokea misaada ya fedha, scholarships, dawa na vitu vingine. Kama ina jeuri ya kutosha, basi ikatae kila kitu. Pambaf!
hao wenzetu wameleta huo mchele sababu ya data zetu utapia mlo ni mkubwa maana yake hatuli chakula cha kutosha au chakula chenye virutubisho vya kutosha!
 
Zawadi ni zawadi (kumbuka wimbo w Twanga Pepeta). Usijitoe ufahamu. Ukiletewa zawadi hata iwe ndogo, usiibeze. Kuwa na utu na kujitambua.
Hivi kuna tofauti kati ya zawadi na msaada ? Kama ipo soma tena ulichoandika
 
Kama ilivyo aibu kuletewa vyakula, hata hayo magari, ndege iwe aibu kuomba na kupewa kama msaada huku tuna kila rasilimali ya kununua hivyo.
Kuomba chochote ni aibu kubwa sanaaa
 
Wewe, mafundisho ya kishetani kupitia dini yamekufanya kuwa kiumbe mwanana cha shetani kilichojaa chuki dhidi wanadamu wengine. Umeishia kuwa punguani. Ujue kuwa upunguani na ujinga ulio nao, siyo sehemu ya utakatifu.

Nchi za kiarabu zimejaa wanaume wachafu wanaowaingilia wanawake kinyume cha maumbile. Je, walibarikiwa na Papa?

Kwa akili yako, ukienda Mbeya na Zanzibat au Tanga kuwatafuta wenye tabia hizo chafu, wapi utawakuta wengi zaidi?
Hata ukasirike nitaendelea kupinga ushoga, yani unanikasikia kisa napinga ushoga?
 
Wewe utakuwa umechanganyikiwa. Ni lini Papa alisema mashoga waende wakapewe baraka makanisani?

Mnaokoteza maneno ya mitaani, na kwa sababu za chuki zenu, mnatengeneza tafsiri zenu kuziridhisha nafsi zenu.

Unatakiwa kuelewa misingi ya imani za dini na tofauti zake:

Uislam ni dini inayoruhusu kisasi kwa aliyekukosea, na kukutaka kujiweka mbali na mwovu.

Ukristo unasisitiza upendo, tena hata kwa adui yako. Tena Yesu anasema ukimpenda rafiki yako na kumchukia adui zako, huna tofauti na watu wasiomjua Mungu, maana nao hufanya hivyo hivyo. Halikadhalika Yesu anasema kuwa tabibu hayupo kwaajili ya walio wazima bali wagonjwa. Kwa hiyo yeye hakuja kwaajili ya watakatifu bali kwaajili ya wenye dhambi ili awatoe katika dhambi. Na ili umtoe katika dhambi, ni lazima kwanza umwoneshe upendo wa Mungu. Ndiyo maana Papa akasisitiza kuwa mashoga kama walivyo majambazi, wazinzi, wevi, na wengineo, wasitengwe. Na akasisitiza kuwa ushoga ni dhambi, na hata siku moja Mungu hawezi kubariki dhambi. Kwenye ukristo, hata jambazi akienda kwa kasisi na kusema kuwa anaomba baraka, kasisi atambariki na kumwusia umuhimu wa kuyabadili maisha yake, na kinachobarikiwa siyo ule ujambazi wake au kumtaka aendelee na ujambazi wake, bali kupokea baraka ya Mungu ili aweze kuyatafakari maisha yake na kumgeukia Mungu.
Mr OKW BOBAN SUNZU, you have to see this comment.

Binafsi niliona uzito kukujibu maana nachukia mijadala ya dini kwa sababu inajaa emotions badala ya logic. Na mbaya zaidi mtu anaamua kuchagua upande Fulani na kupotosha upande wa pili kwa makusudi ili mradi kutimiza haja ya moyo wake. Mijadala ya kidini ni kama ushabiki wa Simba na yanga,once you are Simba,hutakiwi kukubali chochote cha yanga hata kiwe kizuri na kinyume chake ndiyo hivyo hivyo.

Asante mkuu Bams kwa huu ujumbe,usichoke kutoa elimu kuhusu hii mijadala ya ushoga hasa inapohusishwa na dini ya kikristo(hasa ukatoliki).

Wewe ni Moja kati ya wakatoliki Bora humu ndani.
 
1. Mtoto mdhaifu ki-Afya, hata homa ya kawaida kabisa inatosha kumuua. 2. Mtoto mdhaifu hata darasani yupo-yupo tuu hata mwalimu afundisheje hatoelewa vizuri kile kinachofundishwa kwani ana njaa anawaza chakula.
3. Mtoto mwenye njaa aghalabu hujiongeza kwa kutoroka kwenda kujitafutia matunda porini, kuwinda ndege ili apate kumchoma na kula au kitoweo, kutoroka kwenda kuiba matunda kwa majirani au kuiba mboga iliyotunwa nyumbani kwa matumizi ya baadaye n.k.
4. Mtoto mwenye njaa mara nyingi anagombana na wenzake i.e. ana hasira muda wote.
Inafaa uzione athari za njaa kwa mtoto wa shule kwa mapana yake kuliko kung'ang'ania Udini.
5. Vipo vifo vingi vya wanafunzi lakini ni Indirectly related to severe malnutrition.
Mwisho: Kwa kweli kwa hapa Tz; mmmh! kazi ipo tena sio kidogo. Nawapa pole sana viongozi wa serikali wa Nchi hii - Kazi wanayo.
Hata kama unaweza kuwa umeandika vizuri , je wizara ya Elim hawajui? Kama wanajua kwanini isipangwe bajet kutoka kwenye tozo nakupeleka vyakula mashuleni mpaka subili letewa mchele wa virutubisho toka Ulaya?

Kwamba sasa mpaka NGO kwa kushirikiana na mataifa ya nje ndo waje na vyakula vya kusaidia wanafunzi ,serikali , wizara husika kazi yake nini?

Ipo misaada ya kupewa ila sio mchele, maharage au aina nyingine ya nafaka
 
Hawa huwa ni wapuuzi wapuuzi tu
Hawana jeuri ya kukataa ubwabwa hao
Nawashangaa sana. Hawa jamaa ni wabaguzi hatari. Mbona hawakatai misaada ya nyama ya ngamia kutoka uarabuni? Mbona magaidi ya DP World yaliwapa misaada hawakuIkataa?

Wanakataa mchele kwa kuwa umetolewa na wagalatia kutoka Marekani. Wapuuzi na wabaguzi wakubwa!
 
1. Mbona chanjo na dawa za wazungu unatumia mkuu? Je, wakitaka kukunyoosha kupitia kwenye dawa na chanjo utasalimika?
2. Hicho chakula unachosema kimajaa Tanzania kimefichwa wapi watoto wanashinda njaa shuleni na kuteswa na utapiamlo?
3. Uliwahi kujitolea hata kilo 1 ya mchele ukapeleka shuleni watoto wapikiwe?
Punguza unafiq wako mkuu.
Hivi kweli unadhani Ataweza kuyajibu maswali yako? Ingekuwa ni mtihani hapo utarajie div.o
 
Mpuuzi kweli wewe maneno mengi alafu pumba tupu nani asiejua Papa Francis anaunga mkono ushoga? anavaa hadi msalaba wa rainbow au ulikua kaburini umefufuka leo?
Mkuu nilitaka nipite kimya kimya baada ya kusoma comment yako,coz sipendagi kujadiliana mambo ya dini.

Ila uliopoleta hoja ya msalaba wa papa kwenye quote ya Bams ,ndiyo nimeamua kukujibu maana umemjibu kwa dharau na kejeli badala ya kutaka kuelimishwa kuhusu msalaba wa papa na zile rangi.

Kwa kukusaidia ingia google mwenyewe ukajifunze kuhusu zile rangi maana humu ndani zimejadiliwa sana. Kiufupi hazina uhusiano na rangi za ushoga 🌈. Ziko tofauti sana na zinaelezea maana yake.

Tuache kukashifiana kuhusu dini wakuu.
 
R.I.P Magufuli

Sasa tunaletewa vitu vya kijinga badala ya kuletewa vitu vya maendeleo kwa nchi yetu.

Ni wamarekani hawahawa kwa kumtumia mamluki Tundu Lisu wanayemsomeshea watoto wake walipinga ujenzi wa bwawa la umeme alafu wanajifanya wanatupenda sana kutuletea mchele!!
Project za kulisha watoto mashuleni zipo Tangu enzi za Magufuri, Jk na Samia, acha ujinga
 
Una ujuaji mwingi wa kipuuzi.
Kipindi chake aliwezaje kutatua tatizo la umeme bila hilo bwawa??
Kipindi hiki na chake ni kipi umeme ulikua na ufanisi??
Unaongea hisia zako ambazo ni baseless nonfactual.
Pole sana
Ata Sasa hivi mbona Kuna tatizo la umeme? We acha kumshabikia yule shetwain. Hana maana yoyote yule. Kalazimisha mitambo iendelee mpaka imechoka, angekuwepo nchi ingekuwa gizani, na ukiongea unatekwa. Afie zake huko.
 
Back
Top Bottom