Wasomaji wa Biblia Kwanini shetani hakumgusa mke wa Ayubu

Wasomaji wa Biblia Kwanini shetani hakumgusa mke wa Ayubu

Alimtumia kwa kumwambia amtukane Mungu ili afe!
Kwani Ayoub Hakumtukana Mungu??
Ukisoma Kitabu cha Ayoub Utagundua sehemu za Kusifia Mungu Ziliongelewa na wale madaktari watatu marafiki.zake waliokuja Kumsalimia..

Ila Ayoub wa Kwenye Biblia Kamnenea Mbovu sana Mungu
 
Kwani Ayoub Hakumtukana Mungu??
Ukisoma Kitabu cha Ayoub Utagundua sehemu za Kusifia Mungu Ziliongelewa na wale madaktari watatu marafiki.zake waliokuja Kumsalimia..

Ila Ayoub wa Kwenye Biblia Kamnenea Mbovu sana Mungu
Kasemaje mkuu!Nikumbushe.
 
Kasemaje mkuu!Nikumbushe.
Umesoma Kitabu cha Ayoub?

Nitajie sehemu ayoub alipomsifia Mungu?
Au kunena Mema juu Yake..
Ukiacha Zile sehemu za Rafiki zake..
Ambao ni Elifazi mtemani, Bildadi Mshuhi na Sofari mnaamathi ..

Hawa ndo walikuwa Wanamsihi asitoe maneno ya Kashfa kwa Mungu..

Nataka Tuende sawa!
Ili unielewe
 
Wanatheolojia wa jf, baada ya kupitia kitabu cha Ayubu kilicho andikwa mambo mengi ambayo shetani alimtendea Ayubu kama majaribu.
Kama ilivyo andikwa shetani alirdhuru mifugo,wajakazi,utajiri,watoto na zaidi afya ya Ayubu mwenyewe ,ila mke wake yeye tu alikua safe, wanasema Kila kitu na sababu hapo imekaaje wajuzi.
Hakuwa mlengwa
 
Shetani anafanya kazi yake kwa malengo na mikakati. Anajua nani amfanyie nini na kwa namna gani ili amwangushe.

Si ajabu alimwendea Kristu jangwani akiwa amefunga siku 40 mchana na usiku, lakini akashindwa pia.

Tageti hapa ilikuwa ni Ayubu kwa sababu ndiye alikuwa mwakilishi wa Mungu kiroho na kitabia, tofauti na mkewe ambaye alikuwa mguu pande, mguu sawa.

Ingekuwa rahisi zaidi kummaliza Ayubu kupitia mtu wake wa karibu zaidi - mkewe. Japo pia akashindwa! Mungu atukuzwe milele amina!

Maana jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lile lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili. (1Kor 10:13).
Mkuu hili andiko la 1Kor ni kweli kila jaribu lana mlango wakutokea? maana kwangu naona milango yote imejifunga
 
Ay
Umesoma Kitabu cha Ayoub?

Nitajie sehemu ayoub alipomsifia Mungu?
Au kunena Mema juu Yake..
Ukiacha Zile sehemu za Rafiki zake..
Ambao ni Elifazi mtemani, Bildadi Mshuhi na Sofari mnaamathi ..

Hawa ndo walikuwa Wanamsihi asitoe maneno ya Kashfa kwa Mungu..

Nataka Tuende sawa!
Ili unielewe
Ayubu2:9mkewe Ayubu anamshutumu Ayubu kwamba Bado anashikamana na Mungu,amkufuru afe!2:10,Ayubu anamjibu mkewe kwamba anafanana na wanawake wapumbavu,! Itaendelea kusema Ayubu hakunena Dhambi kwa mdomo wake Hao hawakuwa madaktari mkuu ni jamaa zake tuu.
 
Ay

Ayubu2:9mkewe Ayubu anamshutumu Ayubu kwamba Bado anashikamana na Mungu,amkufuru afe!2:10,Ayubu anamjibu mkewe kwamba anafanana na wanawake wapumbavu,! Itaendelea kusema Ayubu hakunena Dhambi kwa mdomo wake Hao hawakuwa madaktari mkuu ni jamaa zake tuu.
Una uhakika hawakuwa Madaktari (Physician) ??
Maana Ayoub mwenyewe anatuambia Kuwa walikuwa madaktari...
Ayoub/Job 13:4..

Ayubu 13:4
"Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo,
Ninyi nyote ni matabibu Msiofaa."

Au Kwa Lugha ya Malkia..

Job 13:4..

"But you, forgers of lies, you are all worthless physicians."

Mimi nataka USIELEZE Maneno ya Muandishi wa Kitabu cha Ayoub nataka Nukuu za Ayoub akiongea Halafu niambie hata Moja..
 
Na pia kupitia mke wa Ayubu kuna kitu cha kujifunza

Ni muhimu sana unapokuwa na mwenza Imani zenu ziambatane pamoja yaani wote kama mnamtumikia Mungu basi mumtumikie Mungu kiuwaminifu haswa hata linapotokea. Jaribu kwa pamoja mnaweza kusolve

Hapa inaonesha mke wa Ayubu hakuwa vizuri na Mungu yaani alikuwa mjanja janja mlokole jina😀 na usikute jamaa hakustukia mpaka pale mke alivyomwambia amkufuru Mungu wake ndipo jamaa akaona sura halisi ya mkewe ni wa aina gani.
Na vitatu vinaruhusiwa kumwacha mke.

1. Kifo.

2. Uzinzi

3. Akiasi Imani.
 
Shetani Na Mungu Ni Washikaji Kinoma
Na ni afadhali uadhibiwe na shetani kuliko Mungu,

Maana ukishambuliwa sana na shetani, Mungu aweza ingilia kati akakuokoa,

Lakini Ukiadhibiwa na Mungu, ukikumbana na hasira yake, hayupo wa kukusaidia.
 
Wanatheolojia wa jf, baada ya kupitia kitabu cha Ayubu kilicho andikwa mambo mengi ambayo shetani alimtendea Ayubu kama majaribu.

Kama ilivyo andikwa shetani alirdhuru mifugo,wajakazi,utajiri,watoto na zaidi afya ya Ayubu mwenyewe ,ila mke wake yeye tu alikua safe, wanasema Kila kitu na sababu hapo imekaaje wajuzi.
Kuna sababu kadhaa zinazoweza kufanya aonekane kutojumuishwa kwenye jaribu la Ayubu alilofanyiwa na shetani kwa ruhusa ya Mungu.

Mke wa Ayubu Naye Alitumika Kama Chombo cha Jaribu
Katika Ayubu 2:9, mke wa Ayubu anamwambia: "Bado unashikilia uadilifu wako? Mwisho wa yote, mlaani Mungu ufe!"
Hii inaonesha kwamba mke wake alitumika kama sehemu ya jaribu la Shetani. Badala ya kumwondoa kabisa, Shetani alitumia uwepo wake kujaribu kumshawishi Ayubu apoteze imani yake kwa Mungu.
Kwa mtazamo huu, Shetani hakumgusa kwa sababu aliona kuwa mke wa Ayubu angeweza kuwa chombo cha kumvunja moyo na kumtenga na Mungu.

Mke Alikuwa Kama Kipimo cha Uvumilivu wa Ayubu
Katika jaribu la Ayubu, ni muhimu kuzingatia kwamba majaribu yake yalihusisha vipengele vya kihisia na kiroho.
Kuwa na mke ambaye hakuwa msaada wa kiroho au kihisia katika kipindi hicho cha mateso kuliongeza uzito wa jaribu lake. Shetani alihitaji kuweka mazingira magumu zaidi kwa Ayubu ili kujaribu imani yake kwa Mungu.

Ulinzi wa Mungu Juu ya Mke wa Ayubu
Shetani alipomwomba Mungu ruhusa ya kumjaribu Ayubu, Mungu alimwekea mipaka. Katika Ayubu 1:12, Mungu alimwambia Shetani: "Tazama, yote aliyonao yako mikononi mwako, lakini juu yake mwenyewe usinyoshe mkono wako."
Hii inaonesha kuwa Shetani alikuwa na mipaka kuhusu kile alichoweza kufanya. Inawezekana mke wa Ayubu alibaki hai kwa sababu ya uamuzi wa Mungu, ili aendelee kushuhudia ushindi wa Ayubu katika majaribu.

Mke wa Ayubu Kama Mwakilishi wa Maisha
Wengine wanaamini kuwa mke wa Ayubu alibakizwa hai kama sehemu ya mpango wa Mungu wa kurejesha maisha ya Ayubu baada ya majaribu kumalizika.
Mwisho wa hadithi, Ayubu alibarikiwa tena na watoto wengine (Ayubu 42:13), na uwepo wa mke wake ulikuwa wa muhimu katika urejesho huu.

Ova
 
Hakupewa ruhusa na Mungu ya kumgusa!
Mlengwa alikuwa Ayubu! Nadhani Mkewe asingeweza kustahamili majaribu.
 
Shetani alifanikiwa kumuangusha mwanaume kwa kupitia mwanamke; Adams, Samson na Daudi akaona ili niweze kumuangusha Ayubu nimtumie tena mwanamke. Wanawake wako strategically to destroy men. Ndio maana tunaambiwa tuishi nao kwa akili na siyo kutanguliza hisia.
 
Wanatheolojia wa jf, baada ya kupitia kitabu cha Ayubu kilicho andikwa mambo mengi ambayo shetani alimtendea Ayubu kama majaribu.

Kama ilivyo andikwa shetani alirdhuru mifugo,wajakazi,utajiri,watoto na zaidi afya ya Ayubu mwenyewe ,ila mke wake yeye tu alikua safe, wanasema Kila kitu na sababu hapo imekaaje wajuzi.
Duuuu
 
Mkuu hili andiko la 1Kor ni kweli kila jaribu lana mlango wakutokea? maana kwangu naona milango yote imejifunga
Huo mstari ni miongoni mwa mistari ya kumpa matumaini mtu anayepitia matatizo.

Mlango unautafuta wewe binafsi na siyo kumsubiri Mungu aliye mbinguni aje akutafutie mlango.

Nimeongea kilayman perse.
 
Wanatheolojia wa jf, baada ya kupitia kitabu cha Ayubu kilicho andikwa mambo mengi ambayo shetani alimtendea Ayubu kama majaribu.

Kama ilivyo andikwa shetani alirdhuru mifugo,wajakazi,utajiri,watoto na zaidi afya ya Ayubu mwenyewe ,ila mke wake yeye tu alikua safe, wanasema Kila kitu na sababu hapo imekaaje wajuzi.
Tumia akili alimgusa ...sijui watanzania mna matatizo gani ya mtindio wa ubongo ama nini ! hadi mnakuwa wagumu kuelewa mambo ...kuna mtu alianzisha uzi wa watakatifu ambao awakufa kabisa bali walitwaliwa na katika huo uzi alimtaja nabii Eliya mimi nikamwambia kuwa Eliya alikufa tena kwa kuchinjwa yeye wala hqkuelewa hakabisha.....ndiyo kama wewe
 
Back
Top Bottom