Wasomi UDOM waandamana kumuunga mkono JK kuwa mgombea pekee CCM, akerwa na Zitto!

Wasomi UDOM waandamana kumuunga mkono JK kuwa mgombea pekee CCM, akerwa na Zitto!

Bramo,
Mkuu usinifanye mimi mtoto mdogo, I can read between the lines. Unakokwenda ndiko niliamkia mwenzako.. lol! Unakusudi kuandika habari hii na haihusiani na swala lolote zaidi chuki binafsi.. Sina haja ya kutumia neno Udini isipokuwa hizi zinaitwa chuki binafsi kutokana na utumwa wa akili..Sasa kama wewe unajua kwamba hizi fedha hawakuzitoa wao mfukoni zimepandikizwa kwa nini unawaulamu wanafunzi hawa na sio wale waliopandikiza?..Inaingia akilini hii!

Licha ya yote watu wote nchini wanayo haki ya kuchagua mchango wao unakwenda wapi, Ukinyimwa mkopo benki haina maana kesho utaenda kufunga account yako..na wala mtu akikuona una deposit fedha zako haina maana wewe ni cheap. Hizi ndio politics za bongo. wanacheza watu wote wengine tunao humu humu JF ni makada wa CCM piga uwa..

Naelewa kwa Uhakika huko kwenu UDSM wapo wanafunzi wamechangia mfuko wa CCM tena kwa simu zao na hamsemi kitu wala kukusanya data zao ila inapofikia hao wengine mnaowachukia swala liakuwa kubwa. Asilimia 80 ya viongozi wa vijana CCM wamepitia UDSM na hakuna mtu anayezungumza..rais wenu katokea UDSM na pengine nusu ya viongozi wote (kama sii zaidi ya hapo) wa CCM walipitia UDSM mbona sioni mtu akichukia chuo hiki na kuwaita cheap!

Pimeni kwanza malalamiko yenu na sii kuongozwa na chuki binafsi!
Hii post imeku touch sana Mkandara...any way...lazima kutakuwa na jambo...tu
 
M.M. Nkunya siku alipojiunga wengi tulisisimka na binafsi niliamua kumuuliza kama ni M.M.Nkunya tunayemjua (huenda wewe humjui ila alikuwa Chief Academic Officer wa UDSM kwa muda mrefu, baada ya hapo (mpaka sasa nadhani) ni CEO wa Tanzania Commission of Universities. Kutokana na madaraka yake huyu ni mtu muhimu ktk jamii. Jamaa kaona lugha iliyotumika haiwezi kutumiwa na Prof. M.M.Nkunya.

Labda kama tatizo ni hilo jina la mwisho 'Nkunya' (ingawa huyo wa tcu naamini hana hati miliki!) lakini kwa maana ya jina kamili huyo wa TCU anaitwa "Prof Mayunga H. H. Nkunya" (http://www.tcu.go.tz/about.html) na huyu wa JF yeye anajiita "M.M. Nkunya". Binafsi sijaona tatizo bado, labda ufafanue zaidi.
 
Dodoma hakuna chuo kikuu ni mambo ya ovyo ovyo, udom ni porojo na unqualified teaching staff tu , cbe ni mambo ya ngono na ovyo ovyo , st. John no teachers sasa kazi ya wanafunzi wa hapa ni kushabikia ccm tu.
 
Bongo protein intake kuwa ndogo, hususan kwenye formative years, kunaweza kuchangia watu kuwa na fikra mgando miaka nenda miaka rudi.

What else can I say? Inabidi tuanze ku entertain factors fulani zinazoweza kuonekana kichaa lakini ziko universal. How else can you explain the general complacency, Kikwete and his ilk?
 
Nawachukia sana hawa wanafunzi wanaoongozwa na njaa zao kwa kushabikia wasichokielewa, mikopo yao inachelewa badala ya kumuweka JK kitimoto wao wanaomba kumpigia kampeni, mianafunzi ya namna hii ovyo kabisa creating no future kwa watanzania masikini.

Further more kiwango cha elimu inayotolewa UDOM ni kidogo sana walimu wengi pale ni undergraduates na hivyo tunategemea hata products zao ni pumba tupu, natoa heko kwa best universities za tanzania ambazo ni Mzumbe, UDSM, MUHIMBILI, SUA NA IFM na kuwaomba graduates wa vyuo hivyo wasijiingize kwenye siasa za CCM

Infact hata mimi nilipoona zile picha roho yangu iliumia sana. Yaani hawa ndio wasomi ambao wanajuwa kila kitu namna ambavyo mkwere na serikali yake wamechemsha jumla kila eneo lakini still kwa njaa zao wanashabikia upuuzi huu jamani. To be honest hata jk mwenyewe kama akiamua kuwa mkweli toka moyoni anajuwa kabisa kwamba kazi imemshinda ila tu mambo ya siasa asingependa awe rais wa kwanza Tanzania kuongoza kipindi kimoja. Najiuliza tutarajie nini toka kwa wale maskini kule Namtumbo na Mpanda? Unajuwa inasikitisha sana hivi Tanzania mtu ufanye nini ili uonekane umeshindwa kazi?

Rais gani huyu anazungumzia internet kabla ya vyumba vya madarasa, madawati, walimu (mbayuwayu) na mengineyo very basic? Hivi hao wataalam anaosema wamekuja tayari kufanya utafiti si watakuwa wametudharau wote jamani? Ni uwendawazimu huu kuzungumzia kukimbia kabla hata ya kutambaa.
 
Naona kuna watu wamekerwa sana kuona wanafunzi wa vyuo vikuu kumuunga mkoni Kikwete!
 
Naona kuna watu wamekerwa sana kuona wanafunzi wa vyuo vikuu kumuunga mkoni Kikwete

Ukitizama heading ya thread na maelezo ya mto mada, hoja ni huo 'ugombea pekee' ambao kwa maoni ya M.M Nkunya unafinyanga demokrasia. Kwani JK ili ashinde anahitaji kuwa peke yake katika kinyang'anyiro?

Mimi nitapenda kama 'kuwatumia/kuwahusisha' wanafunzi wa vyuo vikuu kwa namna hizi za kisiasa sisiwe kwa JK na CCM tu. Hata vyama vingine vitakapotaka 'kuwatumia/kuwahusisha' wasomi hawa visiwekewe mizengwe!
 
WADANGANYIKA bwana, si unaona wameanza kusahau.....?

Juzi juzi tu hapa walikuwa wanasema Kikwe hafai, leo wameanza eti maandamano ya kumuunga mkono kuchukua fomu.

Ubongo wa Taifa hili umeoza. Hivi wasomi wa nchi hii, na ninyi wanafunzi mlio vyuoni. Tafakarini mkaelewe, ni lini mtakubali KUACHA kutumiwa ili kufanikisha ajenda za watu fulani kisiasa? Si ni ninyi mlikuwa mnalia ukata wa Mikopo ya Elimu ya juu? Si ni ninyi mlikuwa mnalia mishahara ya wahadhiri haitoshi? Si ni ninyi mlikuwa mnalia na kulalama kuwa elimu ya siku hizi ni majengo tu, ubora haupo ( shule kibaaaao za kata zimejengwa lakini hazina huduma muhimu kama maabara, maktaba, vitabu, waalimu wakutosha n.k). Jamani tutafika kwa mwendo huu?

Ama kwakuwa mnategemea kupata chochote kwa takrima ndo mnaanza kusahau majanga na majonzi yaliwasibu kwa miaka mitano inayokamilika mwaka huu?

Mimi nasema, historia, umaskini wowote uliosababishwa na utawala huu wa awamu wa nne, vifo, majonzi, vilio, masikitiko, mashaka VIWE JUU YA VICHWA VYENU NA NYUMBA ZENU! Kama mmeshiriki kwa namna yoyote ile, na iwe LAANA juu yenu!

Ninyi kama wasomi mmeshindwa kulisaidia taifa lenu, na kwa mantiki hiyo, jamii hii haiwahitaji na inajuta kujinyima ili kuwasomesha, inasikitishwa, inafedheheshwa kwa kupoteza lengo kwenu, tazama sasa mwazigeukia faraja na za kitambo kidogo tu wakati wa uchaguzi: Pesa, pombe, ahadi za nafasi nzuri n.k na kusahahu machungu na huzuni nyingi mlizozivumilia katika miaka mitano iliyopita na sasa mpo tayari kufanya makosa yale yale!

Jamani, tunazungumzia maisha ya watu na kesho yao na vizazi vijavyo! Mbona mnaanza kuchukulia rahisi rahisi tu? Kama hatuna upendo kwa watanzania wenzetu, basi tuwe japo na UTU wa kutambua kuwa japo keki hii ya Taifa ni ndogo, tuigawane kwa usawa na haki!
 
......... natoa heko kwa best universities za tanzania ambazo ni Mzumbe, UDSM, MUHIMBILI, SUA NA IFM.....

Umesahau Tumaini University, Iringa College. Bonge la Chuo with competent graduates!
 
Maskini wasomi wetu bado njaa inawafanya wasahau umuhimu wao..
Na wachange... subirini baada ya kupata hizo kura zenu..
Juzi hapa Chuo cha St Joseph waliaandamana sikumbuki kama Mh Dk JK aliliongelea..
Tulizivaa hizo tshirt,tukaenda Diamond na posho juu(2005)....
Jifunzeni tokana na makosa yetu...
TUMIENI KICHWA KUAMUA SIO TUMBO
 
Nawachukia sana hawa wanafunzi wanaoongozwa na njaa zao kwa kushabikia wasichokielewa, mikopo yao inachelewa badala ya kumuweka JK kitimoto wao wanaomba kumpigia kampeni, mianafunzi ya namna hii ovyo kabisa creating no future kwa watanzania masikini.

Further more kiwango cha elimu inayotolewa UDOM ni kidogo sana walimu wengi pale ni undergraduates na hivyo tunategemea hata products zao ni pumba tupu, natoa heko kwa best universities za tanzania ambazo ni Mzumbe, UDSM, MUHIMBILI, SUA NA IFM na kuwaomba graduates wa vyuo hivyo wasijiingize kwenye siasa za CCM
Wakikua wataacha. Watajifunza kutokubali kuwa migongo ya watu kupanda ili waende wanakokutaka.
 
Binafsi singashangai. By the time nilipokuwa versity ilikuwa ni buku 5, kwenda kwenye mikutani au maandamano ya CCM (unalipwa). Kwa sasa sina hakika ni ngapi lakini nadhani ni zaidi ya hapo. Hali ya kifedha kwa wanafunzi (na watz wengi) ni mbaya... Buku 10 mtu anaandamana tu ingawa najua moyoni mwao sio wanamuunga mkono....


...Mkuu, kama wasomi wa CHUO KIKUU ambao tunaamini should know better wanauza UTU wao kwa shilingi Alfu 10 tu watakuwa na jeuri gani kesho na keshokutwa kuwalaumu wazazi wao wanapouza UTU wao kwa Pilau, Kanga na Kofia ya Kijani na Njano????? Yes, This is a TRAGEDY in Capital Letters.
 
Wasomi wa Tanzania tumelogwa na nini?

Tutajikomboaje kutokana na ugando huu wa mawazo?

Sishangai serikali itawadharau wanapotoa ya msingi leo wakiwa wanafunzi, na kesho wakiwa wafanyakazi!

Si wana mawazo ya ndumilakuwili? Leo anafikiri hivi na kuamini hivi, kesho anafikiri vingine na kuamini vingine, kisa kapewa takrima!
\Yaani ni kioja, msomi wa tanzania mpe chochote, atacha kufikiri kwa kichwa chake ( and neglect his cause ) na kuanza kufikiri kwa tumbo lake!

What a courrupt society? Kweli watu hawa wakifika kwenye system tutegeeme mabadiliko? Tutampata wapi Daktari asiyeomba rushwa ili atibu? Tutampata wapi hakimu, mwanasheria asiyeomba chochote ili atende haki. Tutampata wapi mwalimu asiyeomba chochote ili afundishe vizuri kama inavyompasa? Tutampata wapi afisa ardhi ambaye hayuko tayari kupokea chochote ili kupanga na kusimamia matumizi ya ardhi ki-usahihi na kwa haki? Tutampata wapi mthamini (valuer) asiyeomba chochote ilikufanya uthamini wake kwa haki bila kumpunja mwananchi ama kushiriki katika kuuibia umma? Tutampata wapi Consultant wa majenzi amabaye haitaji kuomba chochote ili kumpatia mjenzi (contractor) zabuni ?

Kwa mwendo huu, itafika pahala tutaenda kununua wasomi hawa nje ya nchi! Si tumezoea kununua kila kitu nje ya nchi? hapa kwetu si hakuna? Ama kama wapo si wapenda chochote?

Jamani jamani jamani, tuwe makini wasomi wa nchi hii!
 
Wametoa na 1.2M kabisa ya boom lao.

Ni watoto hawahawa ambao wanalalamika kuwa mikopo haitoshi kwa matumizi yao leo wanajikamua shs zote hizi kumpa mtu ambaye ana kiachi hicho mara dufu. Hapa ndio unaanza kuhisi kuwa kuna hitilafu kubwa vichwani mwa watoto wetu.

Akitoka hapo anakuja nyumbani na hadithi ndefu ambayo mwishoni ni suggestive of the fact that hana hela, therefore mpe hela ili kesho akamsaidie mbunge wake akachukue fomu.

Tanzania, Tanzania, where are we going?
 
...Mkuu, kama wasomi wa CHUO KIKUU ambao tunaamini should know better wanauza UTU wao kwa shilingi Alfu 10 tu watakuwa na jeuri gani kesho na keshokutwa kuwalaumu wazazi wao wanapouza UTU wao kwa Pilau, Kanga na Kofia ya Kijani na Njano????? Yes, This is a TRAGEDY in Capital Letters.

BABA DESI, Nilidhania tunauza utu wetu kwenye tiketi za brazil tu, kumbe kila mahali tunauza utu wetu. I hope desi was not amongst them, na kama alikuwepo chalaza viboko na unamfungia chumbani mwezi mmoja ( solitary confinement) halafu akiwa ndani unampa vitabu vya Marx, lenin, Ngugi wa thiongo, Franzt Fanon, Ibsen, Peter Abraham, sauti ya dhiki among others ili ajijue yeye ni nani.
 
Kweli siasa ni njema sana. Imekuwaje hao majamaa wa UDOM kwenda kumwangukia JK? au wanadhani watapata mikopo kwa uchee???? walie tu na kiherehere chao. Mbona hawasomi nyakati? Au ni Vilaza sana? inkuwaje wanadnganywa mchana kweupe naoo wanameza maskini!!!! Wakavishwa nguo za kijani kibichi wakaflenishwa na kwenda mumsujudia JK!! Hivi hao ni miomgoni mwa wanaoitwa wasomi wa nchi hii??? Hata mstakabali wa o hawaujui. Hizo copmputer tu hawana still wanaanmini kuwa kila mtoto atatmia video conferencing katika masomo nao wanameza!! Bless!!! Hata mzee Matonya anawashinda kwa kuanisha mantiki ya uoingozi!!!!! Sham sham sham sham
 
Bila kumtaja jina, Rais Kikwete alimjibu Zitto ambaye alitoa kijembe hicho wakati akichangia bajeti ya serikali ya 2010/2011kuwa licha ya ujenzi wa UDOM kutokuwa ndani ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), chuo hicho kimejengwa na serikali ya chama hicho.

Jibu la kitoto sana hili kwa swali la Zitto. Mbunge alisema kuwan CCM haikutekeleza ahadi zake, ilizotumia kwenye Ilani yake kuomba kura za wanachi. UDOM haikuwamo kwenye Ilani. Rais anatakiwa aseme ujenzi wa UDOM umeingiaje kwenye Ilani. Sana sana ninalofahamu hapa ni kuwa kuna tajiri mmoja alijitolea pesa zake binafsi kujenga chuo kikuu cha IT Tanzania, hivyo akaiapproacha serikali yetu na offer hiyo, na hivyo offer ikaenda kwa Kikwete ambaye ndiye Rais. As Kikwet au mwenyekitiu wa CCM hakuwa na plan yoyote ya kujenga UDOM, vinginveyio wasingeshindwa kuiweka kwenye Ilani hasa kwa vile ni mradi uliotumia hela nyingi sana.

Rais ajifunze ustaarabu unaoendana na madaraka yake; aache kuwa anajibizana moja kwa moja na watu wanaomkosoa. Hilo ni mojawapo ya makosa makubwa yaliyokuwa yakifanywa na Lowasa hadi akafikia kututangazia kuwa eti amenunua Boeing 787 kwa uchumi wa Tanzania ilhali tunajua kuwa nchi haina hata mpango wa kununua 737.

Miaka kadhaa Kikwete huyu huyu alijibizana na watu waliokuwa wanahoji elimu ya mbunge mmjawapo wa CCM, baadaye watu wake wakaja kutoa kauli za kujitetea kuwa Mzee hakuwa anatetea elimu ya mbunge huyo; jambo ambalo lilikuwa ni embarrasment kwake kama rais wa nchi.
 
• Ni kwa kuikejeli CCM kwa ujenzi wa UDOM



“Nasikia kuna mtu mmoja, (Zitto) eti anasema mpango wa ujenzi wa Chuo Kikuu Dodoma hauko kwenye Ilani ya CCM, hiyo ni kweli hatukuandika hivyo, lakini ilani yetu inazungumzia upanuzi wa elimu kwa ujumla kuanzia ngazi ya msingi hadi vyuo vikuu.”

Mkwere huyu kwa vijembe bana!!! Eti kuna mtu mmoja!! Huo upanuzi wa elimu kwa ujumla wake ndo shule za kata?!!! na walimu VODA fasta!!! Umeona wapi walimu wanatoka kwa form 6 kupigwa crasg program ya less than a year!!

Huyu mkwere hajui hata analoongea sasa; anatapa tu...aarrg...
 
“Kuna watu wanasema ninapokuwa ziarani nje naenda kutembea, hapana, nimekutana na wamiliki wa kampuni kubwa za teknolijia ya mawasiliano (IT), wataalam wao wameshakuja nchini kufanya utafiti ili kutuunganisha Tanzania na barabara ya mawasiliano ya IT duniani na itafika mahali watoto wetu watakuwa wanasoma kwa kutumia kompyuta tu, tena wakiwa mbali na mwalimu wao,” JK alisema jana.

26366.jpg



Juakali-Chunya.jpg


SchoolClassroom.jpg


Imefikia wakati ambapo badala ya kumbeza rais wangu inabidi nianze kumsikitikia kwa kuwa ana safari ndefu, urais ni kazi ngumu kuna wakati Obama alisema inafikia wakati unasema chochote angalau upate makofi ya waliopo kwenye kikao.

Tunapozungumzia masuala ya kuunganisha mawasiliano ya IT mashuleni bila kwanza kuangalia mambo ya msingi ni hatari kwa mradi kufanywa kitapeli, je madarasa yameandaliwa, je umewaandaa walimu wa IT, umeme wa uhakika upo? je vitendea kazi text/reference books zipo? uendeshaji wake ukoje au ni kutegemea mikopo ya wahisani.

Wakati shule zetu za kata zimetushinda watoto bado wanakaa chini hatuna walimu hata meza ya mwalimu sasa hiyo komputa utaiweka wapi, overhead projector utazitundika wapi. Tuimarishe kwanza vitu vya msingi (fundamental basics of Education) kama uhakika wa walimu, madarasa, vitabu nk, kabla ya kukimbilia a complex project ambayo ninauhakika kwa sasa ni kiini macho tu.

Inawezekana alikuwa anatania tena.
 
Back
Top Bottom