Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Habari Wakuu!
Ukifuatilia kwa umakini uchaguzi huu. Utagundua Wasomi wengi na watu wanaopenda elimu wengi wao wanamuunga Mkono Tundu Antipas Lisu kuwa Mwenyekiti.
Hii ni tofauti na upande wa pili ambao wengi wao hata Elimu yao ni yamashaka, Elimu ya kuungaunga, huku wengine wakiwa wamekimbia shule na hawaamini katika shule.
CHADEMA zamani kidogo walikuwa wanasifika kwa kuwa na vijana wengi na Wasomi wengi.
Kwa kupenda Elimu, ndio wakaleta Ile Sera ya Elimu bure kuanzia shule ya msingi Mpaka Chuo kikuu ambayo baadaye CCM waliichukua wakafanya Elimu bure shule ya msingi Mpaka shule ya sekondari.
Sio ajabu wanachama wengi wa CHADEMA waliohamia kwenda CCM iwe Kwa kupenda kwao au kushinikizwa Elimu Zao zilikuwa za uhakika. CCM walifanya usajili muhimu kuchukua vijana wa CHADEMA na kuwatumia katika shughuli zao za kiserikali.
Mwenyekiti Mbowe ikiwa atashinda itampasa ajitafakari, ajitathmini kwa nini vijana Wasomi haswa, yaani vipanga na wenye fikra kubwa hawamsapoti yeye na badala yake walimsapoti Tundu Lisu
Huwezi kuzungukwa na Watu wenye upeo WA Kati au UPEO mdogo alafu wakati huohuo wenzako CCM wanavijana maelfu kwa maelfu ya Wasomi WA uhakika ambao wapo kuwatumia na kuwalinda kivyovyote.
CHADEMA ili iende mbele inahitaji watu. Lakini katika Safu ya juu lazima wawepo watu wenye akili kubwa na elimu ya kidunia isiyotia mashaka, au Elimu ya kudunduliza au kuungaunga.
Kisha inahitaji watu wenye misimamo mikali, wazalendo, Jasiri na ambao wapo kwaajili ya mabadiliko ya kweli.
Ukifuatilia hata huku mitandaoni, Wanaomuunga Mkono Lisu wanauwezo Mkubwa wa kiakili, kujenga hoja, na elimu zao sio za kuungaunga. Na wanapenda Elimu na mabadiliko chanya
Moja ya dalili ya mtu mwenye AKILI, UPEO na ELIMU ni kukubali mabadiliko chanya.
Karibuni kwa mjadala
Ukifuatilia kwa umakini uchaguzi huu. Utagundua Wasomi wengi na watu wanaopenda elimu wengi wao wanamuunga Mkono Tundu Antipas Lisu kuwa Mwenyekiti.
Hii ni tofauti na upande wa pili ambao wengi wao hata Elimu yao ni yamashaka, Elimu ya kuungaunga, huku wengine wakiwa wamekimbia shule na hawaamini katika shule.
CHADEMA zamani kidogo walikuwa wanasifika kwa kuwa na vijana wengi na Wasomi wengi.
Kwa kupenda Elimu, ndio wakaleta Ile Sera ya Elimu bure kuanzia shule ya msingi Mpaka Chuo kikuu ambayo baadaye CCM waliichukua wakafanya Elimu bure shule ya msingi Mpaka shule ya sekondari.
Sio ajabu wanachama wengi wa CHADEMA waliohamia kwenda CCM iwe Kwa kupenda kwao au kushinikizwa Elimu Zao zilikuwa za uhakika. CCM walifanya usajili muhimu kuchukua vijana wa CHADEMA na kuwatumia katika shughuli zao za kiserikali.
Mwenyekiti Mbowe ikiwa atashinda itampasa ajitafakari, ajitathmini kwa nini vijana Wasomi haswa, yaani vipanga na wenye fikra kubwa hawamsapoti yeye na badala yake walimsapoti Tundu Lisu
Huwezi kuzungukwa na Watu wenye upeo WA Kati au UPEO mdogo alafu wakati huohuo wenzako CCM wanavijana maelfu kwa maelfu ya Wasomi WA uhakika ambao wapo kuwatumia na kuwalinda kivyovyote.
CHADEMA ili iende mbele inahitaji watu. Lakini katika Safu ya juu lazima wawepo watu wenye akili kubwa na elimu ya kidunia isiyotia mashaka, au Elimu ya kudunduliza au kuungaunga.
Kisha inahitaji watu wenye misimamo mikali, wazalendo, Jasiri na ambao wapo kwaajili ya mabadiliko ya kweli.
Ukifuatilia hata huku mitandaoni, Wanaomuunga Mkono Lisu wanauwezo Mkubwa wa kiakili, kujenga hoja, na elimu zao sio za kuungaunga. Na wanapenda Elimu na mabadiliko chanya
Moja ya dalili ya mtu mwenye AKILI, UPEO na ELIMU ni kukubali mabadiliko chanya.
Karibuni kwa mjadala