Wastaafu wawe wanaandaliwa kisaikojia kabla ya kukabidhiwa mafao

Unamlazimishaje mtu na hela yake. Ni marufuku kupangia matumizi pesa, nyumba au gari la mtu mwingine.
 
Wee!inategemea na mzazi wako wengi wakipata hizo pesa hawataki kabisa watoto wawaingilie ktk matumizi yao wanakua watata balaa!wanatafuta watu wengine wa kuwaamini mwisho wa siku wanavuna mabua
Km umepata mzazi wa hivyo wa kukusilikiza shukuru sana Mungu.
 
Unamlazimishaje mtu na hela yake. Ni marufuku kupangia matumizi pesa, nyumba au gari la mtu mwingine.
Unaweza kumpangia hasa kama pesa aliyonayo ikiisha atageuka tegemezi kwako. Hata akiwa mbishi ni lazima umshauri ili siku pesa ikimuishia akuogope
 
Uzuri wangu Maza mwenyewe ameshaona mifano ya wenzie wengi tuu waliomtangulia na ameapa kutokufanya makosa.

Na mimi kila nikipata muda wa kupiga nae stori huwa napenda kumseminisha ili asijiingize katika mtego wa kutapeliwa au matumizi mabaya na kuishia kua masikini[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Unamlazimishaje mtu na hela yake. Ni marufuku kupangia matumizi pesa, nyumba au gari la mtu mwingine.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Acha wivu mkuu[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Acha wivu mkuu[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Wivu! Siyo wewe unayefuatilia pesa za watu ndiyo mwenye wivu? Ndiyo nyie vinara wa kugombania mirathi.
 
Wahanga wa matukio haya ni wengi sana. Unamkuta mfanyakazi alikua anapokea laki nne na nusu kwa mwezi ghafla anamiliki milioni 60 benki.
Huwa sielewi kabisa hesabu za mafao zinapigwa vipi. Kwa kanuni ambazo mifuko inatutangazia haiwezekani kipato cha laki nne unusu kikazaa milioni 60 hata ungefanya kazi miaka 50!
 
Kweli kabisa mkuu! Ila ile hela huwa nyingi mno huwa inawachanganya akili! Fikria mzee wa miaka 60 ghafla anapigwa milioni 250! Hapo unategemea nini? Sijui labda wangekuwa wanawafungulia akaunti zenye limit ya kutoa hela (lakini hii iwe kulingana na pesa aliyonayo) ili angalau iwatoe mpaka miaka 10 mingine!
 
Kumbukeni mzee Malegesi (sijui kama ndiyo jina lake) alifia kwenye kinena cha binti mbichiiii, juzi hapa akiwa hotelini! Hela ya ustaafu ni hatari sana maana unaweza kufunua vyupi hata vya akina Uwoya na miaka yako hiyo 60+
 
Hesabu nyingine ya uongo hiyo

45,000/= kwa mwezi ( hata ingekuwa kwa wiki) haiwezi kuzaa 200 milion ya mafao!

hapa wamejaa vijana ambao hawajui wazee wao wanapewa kiasi gani cha mafao.
 
Kikubwa hela imeingia kwenye mzunguko
 
hesabu nyingine ya uongo hiyo!

45,000/= kwa mwezi haiwezi kuzaa 200 million kwenye mafao!

thread imejaa uongo wa vijana ambao hawajui wazee wao wanapokea kiasi gani cha mafao
Hukusoma vizuri hiyo nilitoka mfano wa take home baada ya makato ya serikali pamoja na makato ya mikopo! Hivi unawajua watumishi wa serikali huko halmashauri maisha wanayoishi wewe? Nilikuwa huko nikawatupia makaratasi yao ujinga mtupu! Asilimia kubwa huwa wana mikopo benki na kwenye hivi vi microfinance! Kwa hiyo mwisho wa siku anabaki na salary slip inayosoma hivyo! Cheza wewe!
 
Okay, take home 45,000/= kwa mwezi...
tuseme amekatwa 90% ya mshahara wake...
Yani hiyo take home zidisha mara kumi ndio mshahara wake...

450,000/= kwa mwezi

Bado haifiki milioni 200 za mafao!

Haifiki hata robo!
 
Wanaandaliwa, Acha uzushi
 
Tatizo wasitaafu walio wengi niwa bishi sana kisikiliza mtu yoyote, na pia hawajazoea pesa nyingi lazima zipotee kwanza ndo watafute zingine za biashara huo ndo mfumo wao.

Kweli mkuu mimi ni Hr mahali fulani mtu akikaribia kustaafu tunawakalisha chini kuwafundisha matumizi mazuri pindi wapatapo pesa lakini wengi hawasikilizi,kuna mmoja alipata pesa tena ana nyumba mjini mbili mjini hapa akasema akipata pesa anataka akajenge kijijini sisi tukamwambia kwanini kijijini kwani una mpango wa kwenda kukaa huko? Akasema hapana nataka tu heshima baada ya kustaafu kamuachia mtu hela amjengee hela zimeisha na pesa zimeisha yani kaishia kupata stroke.
 
Kwel kabis na wastafuu wengi wanataka kuishi kama vijana wanapend vibinti vidogovidogo ndo vinawakomba pensheni zao ndan ya mwaka wanabaki ombaomba!
 
Kwel kabis na wastafuu wengi wanataka kuishi kama vijana wanapend vibinti vidogovidogo ndo vinawakomba pensheni zao ndan ya mwaka wanabaki ombaomba!
 
Hili somo kweli lipewe kipaumbele.
Kitaa kuna mzee mmoja mjeda alipata milioni 200 plus kama mafao yake. Huyu mjeda ana mke na watoto 4. Alipopata mafao akavuta mchepuko "mtoto mweupee"... Aisee kilichomkuta mjedaaa hatosahau maisha yake yote. Ile pension yote imeliwa, na mchepuko akamwacha baada ya kufulia. Mjeda saiv anakopa unga wa ugali kwa mangi! Inasikitisha
 
Okay, take home 45,000/= kwa mwezi...
tuseme amekatwa 90% ya mshahara wake...
Yani hiyo take home zidisha mara kumi ndio mshahara wake...

450,000/= kwa mwezi

Bado haifiki milioni 200 za mafao!

Haifiki hata robo!
Asante nimekuelewa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…