warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,218
- 18,440
Jamani wambea wenzangu wa humu jamii forum na bloggers, hii tabia nimeona inakua sana siku hizi , unakuta msanii au mtu yeyote maarufu kapiga picha na gari Kali na kutundika mitandaoni, unakuta wengine hawaandiki chochote kama wamenunua au wanayamiliki hayo magari, Sisi sasa tunavyowashwa kusambaza umbea kwenye ma blog na humu Jamii forum "Mkoko mpya wa msanii flani","huyu ndo msanii anayemiliki mkoko mkali kuliko wote apa Tz." Najua kila mtu anatamani awe wa kwanza kusambaza umbea kwenye ma blogs au mitandao mingine, ila tuwe wavumilivu ,hawa wasanii wetu ni wasanii sana wanatumia psychology Ku catch attention zetu, ki ukweli nimeona wasanii wengi wakipiga picha na magari ya watu na kusambaza mitandaoni , Ajabu kila siku tunapishana nao kwenye mabasi ya mbagala au wengine unakuta hawaendeshi magari wanayosambaza kwenye Mitandao.
Mfano halisi juzi kati msanii wa hip hop Young Dee alitundika picha ya Nyumba kwenye Mtandao wa Instagram. Wambea wenzangu sasa wasivyotaka kupitwa fasta kusambaza mitandaoni, flani kanunua mjengo wa million 800 , duh nilichoka nilivyokuja kusikia habari halisi ya hiyo nyumba aliyopiga picha young Dee yani vitu viwili Tofauti. Ukiona msanii kama masanja kapost picha na kusema " AHsante mungu kwa hii gari" apo ujue basi kweli msanii huyu hii gari kainunua, ukiona msanii kapiga picha na Ndinga kubwa halafu hasemi kit, we chukua jembe kalime. Na nyie mashabiki muache vihele hele mtu akipost picha na gari Mnaanza oooh hongera sana umetisha, hakuna kama wewe TZ , sifa kibao , halafu unakuta msanii husika hajibu chochote hakubali kuwa gari sio lake au kusema chochote.
Nirudi kwa wastara, pita pita yangu Leo IG nikaikuta hii picha imetundikwa na msanii wa bongo movie wastara. Nimeona pongezi kibao wakati mwenyewe ajaongelea chochote kuhusu hiyo picha. Bado haijajulikana kama kanunua au anaringisha kapanda hummer.
Nilikuwepo warumi.
Mfano halisi juzi kati msanii wa hip hop Young Dee alitundika picha ya Nyumba kwenye Mtandao wa Instagram. Wambea wenzangu sasa wasivyotaka kupitwa fasta kusambaza mitandaoni, flani kanunua mjengo wa million 800 , duh nilichoka nilivyokuja kusikia habari halisi ya hiyo nyumba aliyopiga picha young Dee yani vitu viwili Tofauti. Ukiona msanii kama masanja kapost picha na kusema " AHsante mungu kwa hii gari" apo ujue basi kweli msanii huyu hii gari kainunua, ukiona msanii kapiga picha na Ndinga kubwa halafu hasemi kit, we chukua jembe kalime. Na nyie mashabiki muache vihele hele mtu akipost picha na gari Mnaanza oooh hongera sana umetisha, hakuna kama wewe TZ , sifa kibao , halafu unakuta msanii husika hajibu chochote hakubali kuwa gari sio lake au kusema chochote.
Nirudi kwa wastara, pita pita yangu Leo IG nikaikuta hii picha imetundikwa na msanii wa bongo movie wastara. Nimeona pongezi kibao wakati mwenyewe ajaongelea chochote kuhusu hiyo picha. Bado haijajulikana kama kanunua au anaringisha kapanda hummer.
Nilikuwepo warumi.