Wastara Juma aomba Watanzania tumuombee, Nyumba zake 2 zawekwa x

Wastara Juma aomba Watanzania tumuombee, Nyumba zake 2 zawekwa x

Hahahahaaa CCM ni ileile ooh ni ileileeeeee.
Tumejipangaaa,mwaka huu wataisomaaa.
Nimekamiss sana haka kawimbo jamani!
Walikuwa wanajiita team mama ongea na mwanao. Wacha magufuli awanyooshe.
 
Mi simjui na wala siangaliagi hizi bonge movie lakini pole yake. Kubomolewa nyumba mbili lazima presha ipande mpaka Kilimanjaro
 
Kuna watu sometimes wanatia sana hasira.Mfano huyu msanii wa bongo movie ambaye alikuwa msatari wa mbele kwenye kampeni za CCM na alikuwa hodari wa kukata viuno ulipopigwa ule wimbo wa kuisoma #Namba.

Leo namba kaanza kuisoma yeye,Analalamika kwenye mitandao ya kijamii"Eti nyumba zake mbili zinavunjwa.Nani wa kumsaidia?
Si aende Lumumba kulalama?

Bulembo si yupo,akamweleze na si kuipigia jamii kelele.Wakati akikata mauno alidhani nini kitafuata?

Wanaomuonea huruma acha wamwonee tu.Ila mimi nasema acha aisome #Namba vizuri next time na wengine wawe na adabu.Hovyo kabisa"

Lakini mkuu kosa la huyu dada ni lipi?
Wote tulikuwa tunataka serikali inayowajibika na kufuata sheria zilizowekwa, serikali ya awamu hii inajitahidi kufanya hivyo tena bila kufuata itikadi. Labda tujiulize je, Wastara amewekewa X kwa sababu za itikadi yake? kama jibu ni hapana basi ana haki ya kuelezea machungu yake kama raia mwingine yoyote.

Swali la kizushi, Je kama upinzani ungechukua nchi wangefanya tofauti na haya? Na kama wengefanya haya haya, kilio cha huyu kingetafsiriwa je?
 
Kuna watu sometimes wanatia sana hasira.Mfano huyu msaniwake, bulembo walahi hahusiki... bongo movie ambaye alikuwa msatari wa mbele kwenye kampeni za CCM na alikuwa hodari wa kukata viuno ulipopigwa ule wimbo wa kuisoma #Namba.

Leo namba kaanza kuisoma yeye,Analalamika kwenye mitandao ya kijamii"Eti nyumba zake mbili zinavunjwa.Nani wa kumsaidia?
Si aende Lumumba kulalama?

Bulembo si yupo,akamweleze na si kuipigia jamii kelele.Wakati akikata mauno alidhani nini kitafuata?

Wanaomuonea huruma acha wamwonee tu.Ila mimi nasema acha aisome #Namba vizuri next time na wengine wawe na adabu.Hovyo kabisa"
bulembo amsaidie mini? kila show alikuwa analipwa stahiki zake, kama anadai kitu aseme...hayo ni uzembe wake bulembo wala ccm hayawahusu..
 
Msanii wa bongo movie ameomba watanzania tumuombee, kwani ameanza mwaka vibaya baada ya nyumba zake mbili kuwekwa x na kuwa hatarini kubomolewa.View attachment 315200View attachment 315201View attachment 315202
#Hapa kazi tu
#Hatunywi sumu wala hatunyongi
#Mtaisoma namba
#CCM mbele kwa mbele.

Mimi nilikuwa nikiwaona wote hao wakikata mauno na sare zao za ccm wakiimba ni ile ile,mtaisoma namba wakawa wanajisahaulisha jambo moja kuwa hata Magufuli mwenyewe kwenye kampeni zake hakujinadi kwa kuitumia ccm ingawa ndiyo iliyomteua. Mara zote alikuwa anasema mchagueni Magufuli na sio ccm kwani aliwaelewa hawana usafi wowote. Wananchi waelewe Magufuli hakuchaguliwa kulea upuuzi wa chama kulea mafisadi kwa kupokea michango mikubwa toka kwao na kufilisi nchi. Mwezi June mwaka huu huu Magufuli atakabidhiwa uenyekiti ccm taifa uone atakavyonyoosha mambo. Muda wa kukabidhiwa uenyekiti umefupishwa kumpa nafasi ya kunyoosha mambo ya nchi hii. Sasa waliokuwa wakikata mauno na kuimba ngonjera wakidhani watavunja sheria waachwe tu kwa kuwa zipo clips zinazoonyesha michango yao kwa chama waanze kuisoma namba wao na wabadili nyimbo zao ziwe HAPA NI KAZI TU.
 
Kuna jamaa kamuombea dua wastara eti "Mungu usimchukue huyu mtu kabla hajaona tingatinga likibomoa vibanda vyake" ha ha ha watu wamevurugwa

Sisiem au fisiem? Kumbe masikio yangu yana matatizo enh??
 

Attachments

  • IMG-20160107-WA0006.jpg
    IMG-20160107-WA0006.jpg
    103.2 KB · Views: 26
Kuna jamaa kamuombea dua wastara eti "Mungu usimchukue huku mtu kabla hajaona tingatinga likibomoa vibanda vyake" ha ha ha watu wamevurugwa
Hahahahaha... watu wamepinda balaa.... Ombea Wastara wetu... aishi muda mrefu.... ili atapobomolewa... ajionee kwa macho.....
 
Anapenda sana kulalamika....yaani yeye nikujitilisha huruma tu kila Mara.Kwani nyumba kavunjiwa peke yake mpaka tumuombee yeye?ya kwetu yanayotukuta anatuombeaga?Anazidi sasa.
 
Kuna jamaa kamuombea dua wastara eti "Mungu usimchukue huyu mtu kabla hajaona tingatinga likibomoa vibanda vyake" ha ha ha watu wamevurugwa
Sasa akisoma maneno kama haya si ndo atazima kabisa hahahaa
 
Back
Top Bottom