Wasudan wajiuliza kuhamishwa raia wa nje kuachwa wao wapigane kuna hekima gani

Wasudan wajiuliza kuhamishwa raia wa nje kuachwa wao wapigane kuna hekima gani

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mataifa karibu yote duniani yenye raia zao Sudan wanashindana kuwakimbiza nchini humo. Imekuwa kama ni siasa kuwahi kuwaondoa raia hao kwa mbinu tofauti. Nchi inayochelewa kufanya hivyo kama kwamba inahofia kuingia matatani kwa wananchi wake huko nyumbani.

Katika kuondoka huko kila nchi imekuwa ikifanya mbwembwe zake ili ionekane ni hodari zaidi katika kukimbia eneo lenye vita. Upande wa Marekani awali walisema wana mpanga wa kuwahamisha raia wake haraka. Kumbe wakati wakisema hivyo helikopta za Chinook zilikuwa tayari zipo Khartoum kuchukua maafisa wa ubalozi tu na familia zao wanaofikia 100.Wale raia wengine pacha wafikao 16000 kila mmoja ametakiwa aangalie usalama wake.

Uiengereza, Ufaransa, Ujerumani, Italy, Spain na nchi nyingi zimeshafanya zoezi hilo. Kwa upande wa Urusi imesema raia wake wote wameshajikushanya ndani ya Ubalozi wa nchi hiyo Khartoum na wanaangalia muda muafaka ili kuwaondoa.Hali ni hiyo hata kwa vinchi vidogo kama Kenya na Misri nao eti wanafanya mipango kuondoa raia zao huo ambao huenda wala hawajui namna walivyoingia na wala idadi yao.

Majenerali wanaopigana nchini humo kila mmoja anajaribu kutoa picha kwamba ndiye aliyepanga mipango ya kusaidia kuondoka raia wa nchi moja baada ya nyengine. Kama wana madai ya kweli katika kuanzisha vita hivi basi badala ya kusaidia kuondoka raia hao wangewashikilia mateka mpaka usalama urudi nchini humo.Wangewaambia hawawezi kuwahakikishia usalalma wao.

Upande wa wananchi matukio hayo ya kukimbizwa kwa raia wa nje kumewakatisha tamaa sana.Alsadig Alfatih amesema kuwaona watu hao wakihamishwa na kuachwa wao wapigane kumemkatisha tamaa sana kwani alitaraji wao ndio wangesaidia kuleta amani.
6d24f0c0-e272-11ed-bffb-d0e242b79dbb.cf.webp
 
Kwan nchi si yao, kama wanaona vita ni sahihi kwao, basi wao ndo wakwanza kutokuwa na busara, waafrika tunapenda mteremko sana, tujifunze kwa Ukraine ilivyosimama kiume dhidi ya Urusi, sasa kama nyinyi pia mnataka muiache nchi yenu mnabusara kweli?
 
kwan nchi si yao , kama wanaona vita ni sahihi kwao , basi wao ndo wakwanza kutokuwa na busara , waafrika tunapenda mteremko sana , tujifunze kwa Ukraine ilivyosimama kiume dhidi ya Urusi , sasa kama nyinyi pia mnataka muiache nchi yenu mnabusara kweli ?
Hao washenzi kutoka nje ndio chanzo cha chokochoko.Muda kama huu kama hao majenerali wanajua wanachopigania basi wangewashikilia mateka.Wakawaambia mutakufa pamoja nasi hapa.Mukileta ushoga na kuiba mali zetu mnataka uhuru lakini mambo yakiharibika munajali usalama wenu.
 
Hao washenzi kutoka nje ndio chanzo cha chokochoko.Muda kama huu kama hao majenerali wanajua wanachopigania basi wangewashikilia mateka.Wakawaambia mutakufa pamoja nasi hapa.Mukileta ushoga na kuiba mali zetu mnataka uhuru lakini mambo yakiharibika munajali usalama wenu.
Wanaweza kuwashikilia mateka nyie Waafrika mnaofanana nao akili ila hawawezi kushikilia mateka raia wa Marekani au Ulaya.
 
Wanaweza kuwashikilia mateka nyie Waafrika mnaofanana nao akili ila hawawezi kushikilia mateka raia wa Marekani au Ulaya.
Ndipo ujinga wao ulipo hapo.Yaani kila mmoja anajipendekeza aonekane ndiye aliyesaidia kufanikisha kuwakimbiza.Marekani iliwasiliana na Hemedti mwanzo kabla ya kuleta chinook na wakati huo zikawasiliana na Burhan.

Baada ya kuhadaiwa kila mmoja akajitangaza atafanya juhudi kuhakikisha wanaondoka kwa usalama na kweli walisitisha mizinga zilipokuwa zinapakia raia wao. Kule Marekani Biden anasifu ushujaa wa vikosi vyake vilivyowaokoa maofisa wake wa ubalozi.
 
Hao washenzi kutoka nje ndio chanzo cha chokochoko.Muda kama huu kama hao majenerali wanajua wanachopigania basi wangewashikilia mateka.Wakawaambia mutakufa pamoja nasi hapa.Mukileta ushoga na kuiba mali zetu mnataka uhuru lakini mambo yakiharibika munajali usalama wenu.
Haya ni mawazo ya kigaidi.
 
AU ipo Kimyaaa kama hili swala linatokea Asia

West wao wanaandaa mpango wokovu, nchi zinaandaa wanajeshi kibao ili waende saidia wokozi na ikitokea lakutokea Sudani ivamiwe kwa lazima na ndio maana Marekani kaingia hajarushiwa hata risasi
 
Hao washenzi kutoka nje ndio chanzo cha chokochoko.Muda kama huu kama hao majenerali wanajua wanachopigania basi wangewashikilia mateka.Wakawaambia mutakufa pamoja nasi hapa.Mukileta ushoga na kuiba mali zetu mnataka uhuru lakini mambo yakiharibika munajali usalama wenu.
ila nyiny ndo mnashika silaha , au unataka sema hamjui madhara ya hizo sIlaha , media zipo hao wazalishaj wa silaha mbona wao hawauani ? mbona viongoz wana heshimu katiba zao ? nyiny mnasubir mzungu ndo awaambie musiuane?
 
Mwana kulitafuta , mwana kulipata
Janjaweed ambao ndio RSF waliundwa, walifadhiliwa na kulindwa na serikali ya Sudani ili wawauwe Wasudani weusi huko Darfur.

Warussi ndio walinzi wa migodi ya dhahabu huko MALI na SUDAN

HEMELTI mkuu wa RSF amezuru Russia karibuni
 
Back
Top Bottom