DocJayGroup
JF-Expert Member
- Jan 17, 2020
- 1,654
- 3,346
Ukishajua kwamba matofali yanaingia mangapi.. nondo ngapi.. mifuko ya cement mingapi.. bati ngapi.. mbao kiasi gani.. tiles ngapi.. gypsum boards ngapi.. nk.. ndio utapata makisio kwa kwenda kuulizia bei ya hivyo vitu hardware nk. Lakini lazima mtu ajue vipimo. Mfano sakafu ya chumba cha futi 10 kwa futi 10 inaingia tiles 100 zile za 30cm×30cm. Wanauza kwa boksi lenye tiles 17 na kuendelea.. manake maboksi 6 kwa hichi chumba. Pia kuna cement ya kuzishikiza nk. Japo kwa ujenzi.. tiles ni za mwisho kabisa.. ila ukitaka quotation halisi lazima uzijumlishe..
Kama alivyosema mwingine.. hapa kuna wataalamu tungekuasaidia ushauri wa bure.. vipimo ni muhimu sana.. sababu Kwa Mfano.. kama ukuta una upana wa futi 10 (inch 120) na juu kina unaenda futi 9 (inch 108).. manake hapo kwa matofali ya block ya inch 9 kwa inch 6.. itatumia matofali 12 kila laini (jointi ni inch 1) mara laini 15 (kila laini ni inch 7 kina sababu joint pia ni inch 1).. jumla ni matofali 12x15= na matofali180 ya block ya inch 9x inch 6 kwa huo ukuta .. cement.. mifuko mitatu hadi mitano ya jointi. (Kutegemea na ratio uta-mix).. lenta kwa huu ukuta mmoja ni vipande vinne vya nondo kila kimoja inch 10 (sawa na futi 40 au nondo nzima).. cement ya lenta.. ya plasta.. ya zege sakafu nk. dirisha fremu na shata zake... nk.. unafanya mahesabu namna hiyo kila ukuta.. kisha mahesabu ya bati.. mbao za makench.. mbao za draft.. jipsam boards.. milango fremu.. milango shata... plumbing.. wiring... rangi.. tiles za sakafu.. nk.. Bado ww unajifunza mambo ya ujenzi.. NGOJA UPIGWE KWANZA NDIO UTAJIFUNZA.. All in all we wish you the best. Ujenzi raha sana.