Watakatifu ni wazungu waliokufa zamani. Waafrika waliokufa zamani eti ni mizimu

Vipi kuhusu Africa chini ya jangwa la Sahara(Sub Saharan Africa)
Utakuwa huna taarifa sahihi! Afrika Kaskazini kuna watakatifu wengi tu. Mt. Augustino hakuwa Mzungu!
 
Tatizo lako ni kuchukulia neno mzimu kwenye negativity Bujibuji Simba Nyanaume.
 
Wanawajua
mt kizito
Mt karol lwanga
Mt mathias Mulumba Kalemba
Mt agustino.
To mention a few
- usipende kujadili vitu ambavyo vipo nje ya uwezo ewe @gilesi
 
Wanawajua
mt kizito
Mt karol lwanga
Mt mathias Mulumba Kalemba
Mt agustino.
To mention a few
- usipende kujadili vitu ambavyo vipo nje ya uwezo ewe @gilesi
Hao ni watakatifu wa dini ya wazungu. Hawa ni wasaliti wa imani walizoachiwa na babu zao.
 
Mkuu, Kuitwa Mtakatifu ni ka-utaratibu tuu ka-kibinadamu kuweka maandishi/Kumbukumbu ili itumike kama Reference au utoaji wa aina ya Tuzo lakini UKWELI ni kwamba watakatifu wapo na ni WENGI mno sana ila hawajarasimishwa na hako ka-Utaratibu.

Kwa mfano: Ni ukweli usiopingika kwamba hiyo takwimu imetengenezwa na kuhaririwa na Binadamu -Sio ya kutoka kwa Mungu aliyewaumba Binadamu. Inawezekana kabisa hata baadhi ya Jamaa na Ndg. zako/zetu ni watakatifu kwa kigezo kwamba wapo Mbinguni.

Ni kweli kwamba Upatikanaji wa Taarifa sahihi ni shida Lakini hilo haliondoi Ukweli wa Watu wetu kuwa ni miongoni mwa Watakatifu ila hawajaorodheshwa au kutajwa. Naunga mkono Hoja yako 100%.
 
Shindwa na ulegee. Ujinga wake umesababisha vifo vingi sana vya watu . Tena usimtaje kabisaa, utawala wake ulijaa damu za watanzania kibao.
 
Kweli kabisa unayosema ila kwa sasa tunaye MTAKATIFU MAGUFULI NA NYERERE TUTAKUWA TUNAKWENDA KUHIJI WALIKO ZIKWA
 
Vipi kuhusu Africa chini ya jangwa la Sahara(Sub Saharan Africa)
Wapo Karoli Lwanga na wenzake. Kwa ujumla wao wanaitwa Mashahidi wa Uganda. Anwarithe Nangepeta huyu bado Mwenyeheri. Yupo pia Mtanzania yuko mbioni kutangazwa Mwenyeheri. Sr. Benardetta Mbawalla.
 
Kitu kitakachowafungua Akili ni Hiki.

Yesu alipopanda Mlimani kusali alitokewa na Musa na Elia. Tunajua Musa na Elia si malaika wale ila Walikuwa ni Binadamu kama Sisi. Walipokufa ndio Yesu akaenda Kuongea nao na kulingana na Biblia inasema Walikuwa wanaongea kuhusu kifo chake

Sasa Inakuwaje Hawa wanaokesha Kuhubiri Wawatukane watu wanaoenda Kuongea na Mababu zao na Wanasema Mababu zao ni Mizimu.
 
Wanaowatusi wazee wao waluotangulia mbele ya haki, nipo Massanza Kona hapa kwa Mzee Lufungulo Kapongo Manota MUGWATA nawajengea wazee wangu makaburi.

Waendelee kupumzika kwa amani
 
Hii hoja yako bwn Kenzy haina mashiko. Kwani hao tunaolazimishwa tuwaombe tukiwa na shida hawajafa...
 
Ww bila Shaka akili yako ndio inaokutuma hivi unavyoviongea bila shaka.haya twende kihoja.kwanini ww mweusi na wale weupe ilikuakuaje hadi ikawa hivo??? Unamana gani kwakusema watakatifu wao?

Watakatifu hao kina nani. Unaudhibitisho/wao wanaudhibitisho gani kua hao watakatifu walikua weupe na sio weusi ?

Nakushauri uwe mwenye kufanya uchunguzi kabla ya kukubali kila ulisikialo Mana mengi hayana ukweli
 
St. Francis alikuwa ni Mmatumbi? Vipi kuhusu St. Andrews?

Ifike wakati na sisi tuwathamini watu wetu, kwani kuna ubaya gani Mrisho Mpoto naye akawa mtakatifu?
 
Usidanganye watu. Msimamo wa Magufuli kuhusu covid-19 kuwa haipo ulipelekea wengi kutochukua tahadhari. Mikusanyiko ya watu iliongeza vizalia vya ugonjwa. Matokeo ni vifo ambayo ilizuiwa visitangazwe. Kwa idadi ya watu waliopotezwa na kuteseka wakati wa utawala wake, naamini kama ipo mbingu utakatifu wake utakuwa wa motoni.
 
Maalim umeongea kwa ukali sana.Nimekuelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…