Watanganyika ajira za TRA 1574 Wazanzibar wametengewa 21%

Watanganyika ajira za TRA 1574 Wazanzibar wametengewa 21%

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Heshima sana wanajamvi.

TRA wametangaza ajira mpya 1,574.

Hili ni jamba zuri sana vijana wetu watapata ajira za uhakika zenye mishahara mizuri na nafasi kubwa ya kutengeneza kipata cha ziada kupitia urefu wa kamba zao.

Kitu wasichakijua WATANGANYIKA katika ajira hizo WAZANZIBAR wametengewa nafasi 331 huku WATANGANYIKA MACHOGO wakitengewa 1243 tu.

Idadi ya watu TANGANYIKA ni zaidi ya 64 Million idadi ya watu ZANZIBAR ni 836,000.
Hizi hesabu nimejaribu kuzipiga,kugawanya,kuzidisha nimetoka kapa.

Huu upuuzi uliletwa na Mchengerwa katika bunge hili linalomaliza muda wake WABUNGE wetu hawakuhoji,hawakudadisi,hawakuuliza waligonga meza kama kawaida yao.

Wakati LISSU akishangaa idadi ya wabunge wa ZANZIBAR kuchanguliwa na wastani wa watu 11,000 tu wakati wabunge wa TANGANYIKA wanachaguliwa na idadi ya watu 300,000 na kuendelea angejiuliza na kudadi inakuwaje WAZANZIBAR wanatengewa nafasi 331 katika taasisi moja tu.Siku BOT wakitangaza ajira utaratibu ni huo huo.

Lissu badala ya kutazama nafasi za kisiasa pekee yake angetazama pia suala zima la ajira katika hii JMT.



Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano

Sheria ya Utumishi wa Umma Na.8 ya mwaka 2002 na kanuni zake za mwaka 2003 zimeweka utaratibu wa wazi wa ajira katika Utumishi wa Umma na kuondoa dosari zilizokuwepo. Serikali ya Jamhuri ya Muungano imekuwa ikitoa fursa sawa za ajira kwaWananchi wote wa Tanzania ambao wanaomba na kuwa na vigezo kama Elimu, Uzoefu na Sifa husika. Kuhusu nafasi za watumishi wa kawaida kwenye taasisi za Muungano, utaratibu wa muda wa mgao wa ajira uliokubalika kutumika ni asilimia 79 kwa Tanzania Bara na asilimia 21 kwa Tanzania Zanzibar. Utaratibu huu unatekelezwa kwa mujibu wa Waraka wa Serikali wa tarehe 10 Mei, 2013.
 
Yana mwisho hayo
Hayawezi kuwa na mwisho iwapo wahusika wakuu (wanafunzi wa vyuo vikuu) wapo kimya.

Enzi zetu yangeshafanyika maandamano makubwa sana ya wanafunzi wote wa elimu ya juu.Fikiria wakati huo vyuo vikuu au taasisi za elimu ya juu zilikuwa chache sana.

Leo vyuo vikuu vipo bwerere wamekaa kimya wanangoja malaika wa kuwasemea.
 
Ubia ni 50/50,yaani hapo bado mmewaonea sana, mara nne? No hii haikubaliki, muungano ni inchi kwa inchi so mgao ni nusu kwa nusu


Siku mkiiachia Zanzibar na mambo yao ndio siku mtamaliza mzizi wa fitina,

Ila kwa sasa endeleeni kuumia tu, si mliyataka wenyewe?

Rejesha akili kidogo.

ZANZIBAR wana Zanzibar Revenue Authority yao ambayo MTANGANYIKA hatii pua.
 
sio Kwa ubaya ila viongozi wetu wengi ni vichwa nazi.

hawa idara ya usalama hawa kupaswa kukaa kimya, eti Wana mwachia kiranja mkuu aji amulie anavyo taka.

Inge pendeza wange kamata au kuwa lazimishwa waji uzuru wafanya maamuzi mabovu.

Sema usalama yenyewe ni Kama mlevi, full kusukumwa tu.
 
Mzanzibar wa Kizimkazi ndo kashika usukani ulitegemea nn
Heshima sana wanajamvi.

TRA wametangaza ajira mpya 1,574.

Hili ni jamba zuri sana vijana wetu watapata ajira za uhakika zenye mishahara mizuri na nafasi kubwa ya kutengeneza kipata cha ziada kupitia urefu wa kamba zao.

Kitu wasichakijua WATANGANYIKA katika ajira hizo WAZANZIBAR wametengewa nafasi 331 huku WATANGANYIKA MACHOGO wakitengewa 1243 tu.

Idadi ya watu TANGANYIKA ni zaidi ya 64 Million idadi ya watu ZANZIBAR ni 836,000.
Hizi hesabu nimejaribu kuzipiga,kugawanya,kuzidisha nimetoka kapa.

Huu upuuzi uliletwa na Mchengerwa katika bunge hili linalomaliza muda wake WABUNGE wetu hawakuhoji,hawakudadisi,hawakuuliza waligonga meza kama kawaida yao.

Wakati LISSU akishangaa idadi ya wabunge wa ZANZIBAR kuchanguliwa na wastani wa watu 11,000 tu wakati wabunge wa TANGANYIKA wanachaguliwa na idadi ya watu 300,000 na kuendelea angejiuliza na kudadi inakuwaje WAZANZIBAR wanatengewa nafasi 331 katika taasisi moja tu.Siku BOT wakitangaza ajira utaratibu ni huo huo.

Lissu badala ya kutazama nafasi za kisiasa pekee yake angetazama pia suala zima la ajira katika hii JMT.
 
Nyie waKAVIRONDO wajinga kweli ile pesa yetu munayoikusanya huku ya TRA mukaletewa nyie kwani sisi hatuumii mulishazoea kutunyonya kwa mali zetu Sasa Leo viajira hivo tu vinakutoweni utu, katika mkataba wa Muungano kuna 4% ya Wazanzibari na hamutupi yote mumeiiba, Shenzi Waheed nyie
 
Back
Top Bottom