Watangazaji wa kizazi hiki wanakera mpaka basi. Hivi wanaokotwa wapi hawa viumbe?

Watangazaji wa kizazi hiki wanakera mpaka basi. Hivi wanaokotwa wapi hawa viumbe?

Tanzania haijawahi kuwa na waandishi wa habari bali ni makanjanja na wababaishaji,wavivu wa kufikiri na kutafiti.
Mwandishi wa habari anatakiwa awe mtafiti na mfuatiliaji wa Mambo kiujumla,ili awe anaibua na kuufahamisha umma usioyafahamu na sio umma ndiyo umfahamishe!
Kuna vituko vingi vimejiri kiasi Cha kujiuliza hawa waandishi huwa wanajipa muda wa kujiridhisha kabla ya kuandika habari ?
Nakumbuka 2003 walimuandika Ammy Ninje anacheza ligi daraja la pili Uingereza nilikuwa nikiangalia sky nacheka Sana!
 
Hii nchi hivi Sasa ni ya maigizo tu kila idara, ndo maana inakata kona Mpaka twasikia kizungu zungu, hawajiheshimu waongo, wajuaji Lakin I awajui kitu
Basi tu tuwaachie nchi Yao vijana
 
Unakuwa na mtangazaji Mauldi Kitenge, Eddo Kumwembe hawa hawana shule ya Uandishi wa habari ni ujanja wao na kulaghai watu. Baraka Mpenja kaenda shule ila mropokaji na wala sio mtangazaji. Fuatilia goli la Dube alivyotangaza kuna maneno aliropoka kuhusu Dube. Ama fuatilia goli la Aziz Ki alilofunga dhidi ya Simba alivyoropa maneno ya kijinga. Anaropoka baada ya kutangaza maneno ya kiswahili fasaha. Pia wamiliki wa hivi vyombo hawalipi vyema wafanyakazi wao. Mfano pale Azam media pana njaa ya kufa mtu. Na media zingine nyingi tu zina malipo hafifu kwa wafanyakazi wao.
Salum mwalim alipokuwa dtv ndiyo
Alimuingizaga eddo kumwembe
Alikuwa wanamuita anachambua ligi ya uingereza,wanamdakisha 40000-50000,Edd9 akajiongeza kdg
Ndiyo hivyo

Ova
 
Salum mwalim alipokuwa dtv ndiyo
Alimuingizaga eddo kumwembe
Alikuwa wanamuita anachambua ligi ya uingereza,wanamdakisha 40000-50000,Edd9 akajiongeza kdg
Ndiyo hivyo

Ova
Shule hakuna pale ujanja mwingi tu. Yeye na Kitenge hakuna kitu. Mpe script ya kiingereza Kitenge akusomee ndio utajua ujinga wake.
 
Kwa matumizi ya r na l ni tatizo la watanzania wengi na linaanzia shuleni pale anayefundisha(mwalimu)naye hajui kutofautisha r na l.Lakini kupungua kwa wasikilizaji wa radio inatokana na urahisi wa kupata taarifa kupitia simu janja
 
Kwa matumizi ya r na l ni tatizo la watanzania wengi na linaanzia shuleni pale anayefundisha(mwalimu)naye hajui kutofautisha r na l.Lakini kupungua kwa wasikilizaji wa radio inatokana na urahisi wa kupata taarifa kupitia simu janja
Mother Tongue...., Ingawa Kiswahili ni lugha ya Taifa lakini bado Makabali yana-affect matamshi..., Kama vile mzungu akiongea Kiswahili anachapia au mchina akiongeza kingereza n.k.

Ingawa kama kitendea kazi chako ni kuongea basi kama una kigugumizi, kithembe sauti ya kukera n.k. inabidi utafute kazi nyingine..., Ila kama una sauti ya kubembeleza na kumtoa nyoka pangoni kazi tutakupa tu..., hayo mambo mengine ya ujuzi na ufahamu na kufanya research kuna watu wapo watakufanyia (Presenter uta-present tu)...
 
Tanzania haijawahi kuwa na waandishi wa habari bali ni makanjanja na wababaishaji,wavivu wa kufikiri na kutafiti.
Mwandishi wa habari anatakiwa awe mtafiti na mfuatiliaji wa Mambo kiujumla,ili awe anaibua na kuufahamisha umma usioyafahamu na sio umma ndiyo umfahamishe!
Kuna vituko vingi vimejiri kiasi Cha kujiuliza hawa waandishi huwa wanajipa muda wa kujiridhisha kabla ya kuandika habari ?
Nakumbuka 2003 walimuandika Ammy Ninje anacheza ligi daraja la pili Uingereza nilikuwa nikiangalia sky nacheka Sana!
Kweli kabisa. Ndio maana comrade Mkapa alikuwa hapendi kuhojiwa na hawa vilaza.
 
Kutana na watangazi nguli wa RTD ambao kila mmoja alifurahia kuwasikiliza wakitangaza. Zamani tulikuwa na watangazaji weledi sana.

 
Juma lokole&Co ltd mtangazaji hapo unategemea nini?

Ova
 
Habari wanaJF?

Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha na maneno mengi. Kwa mujibu wa utafiti binafsi nilioufanya hivi karibuni, usikilizaji wa redio na utazamaji wa TV umepungua sana miongoni mwa wafuatiliaji wa habari. Hili halijatokea kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu ya kupungua usahihi wa taarifa na ubora wa watangazaji. Sote ni mashahidi jinsi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Voice of Kenya (VoK) zilivyokuwa na watangazaji nguli ambao huchoki kuwasikiliza.

Watangazaji wengi wa redio na TV zinazochipukia kama uyoga hapa nchini wanakera mno kwa utangazaji wa ovyo na unaokosa weledi. Ukisikiliza redio na kutazama TV, hasa hizi zinazoitwa Redio/TV za Kijamii, utahisi kichefuchefu na huwezi kuendelea kusikiliza kwa zaidi ya dakika 5! Wanachotangaza ni zaidi ya utumbo. Na kibaya zaidi, hawa makanjanja hawakupitia kabisa kwenye vyuo vya uandishi wa habari. Inasikitisha mtangazaji kutoongea Kiswahili fasaha unabaki unajiuliza: hivi huyu mtu alienda shule kweli au ameokotwa jalalani? Na kama alienda shule, je, huko alienda kujifunza ujinga au maarifa? (FaizaFoxy, 2015). Yaani hawa viumbe hawawezi kabisa kujieleza kwa Kiswahili na Kingereza fasaha.

Zamani haikuwa rahisi mtu yeyote kujipenyeza kwenye utangazaji ikiwa hajui Kiswahili na Kiingereza fasaha. Na si hilo tu, mtangazaji anatakiwa kuwa na uhakika wa jambo analolitangaza. Juzi nilipata hasira sana niliposikia mtangazaji wa mpira akiutangazia umma kuwa mmiliki wa sasa wa Klabu ya Chelsea ni Roman Abramovich. Wanajiropokea tu ilmradi tonge liingie kinywani.

Utakuta mtu ana lafudhi mbovu na uelewa mdogo kama mbegu ya hardali lakini bado anang’ang’ania kuwa mtangazaji. Ni aibu kubwa. Yaani pale inapotaikiwa kuweka “r”, yeye anapachika “l”, kwa mfano mpira anatamka mpila. Ni aibu iliyoje! Na pia ni wazuri sana kwenye upotoshaji kwa mfano neno wimbo, hutamka nyimbo……..mfano: Leo nawachezea nyimbo moja ya Diamond inayoitwa Kantangaze. Ovyo kabisa!

Kwa ujumla, nchi hii ina watangazaji wenye uelewa finyu na upeo mdogo wa utangazaji. Natoa wito kwa serikali na vyombo vinavyohusika kudhibiti maudhui ya vyombo vya habari kufanya kazi yao kikamilifu ili kuzuia upotoshaji huu unaofanywa na baadhi ya watangazi makanjanja. Aidha, kiwango cha elimu na weledi wa mtu anayefaa kuwa mtangazaji kipitiwe upya. Watangazaji wasiokidhi vigezo wachujwe na kutupwa nje ya ulingo wa utangazaji. Tumechoshwa na upotoshaji.

View attachment 2628193
We mtu kazaliwa 2010 leo anapewa kipindi amfanyie mtu interview wakati hajuwi anasema nini au kuuliza nini, unafikiri nini kitakachojiri?
 
Juma lokole&Co ltd mtangazaji hapo unategemea nini?

Ova
Ila hawa wamiliki wa redio sijui wanatuonaje aisee. Eti akina Mwijaku nao ni watangazaji! Wanachekesha sana 😀 😀 😀
 
Back
Top Bottom