Watangazaji wa kizazi hiki wanakera mpaka basi. Hivi wanaokotwa wapi hawa viumbe?

Watangazaji wa kizazi hiki wanakera mpaka basi. Hivi wanaokotwa wapi hawa viumbe?

Nadhani mngejua kutofautisha kwenye ukemeaji wenu kati ya maudhui na mtindo wa ufikishaji wa sanaa.
Mnapokemea maudhui kama ushoga, ngono,ulevi,umbea, uongo, uzembe katika uwasilishwaji wa sanaa kama habari, muziki, nk. Hapo ni sawa.

Lakini sasa mnapoenda mbali/kuchanganya na kuanza kukemea mtindo wa sanaa inavyowasilishwa kama matumizi ya Lugha, mandhari, mahadhi, nk. Hapo mnakosea.
Mtindo huwa unabadilika kuendana na muda.

Mfano kwenye lugha hapo, mngetakiwa kutambua sifa ya Lugha mojawapo ni kukua, lugha sio gereza kwamba lazima ujifunge kwenye kanuni na sheria za kisarufi, misamiati nk. Zilizowekwa na wataalamu kule maofisini. Kumbuka sanaa ni kioo cha jamii. Sasa kama jamii inaongea "kwendaga" basi haina budi sanaa iakisi lugha inayotumiwa na jamii.
Hata kiingereza cha leo hakikuwa hivyo miaka 500 iliyopita. Wangeng'ang'ania na wao kisibadilike ingekuwaje?
Hata lugha za matusi pia ni mojawapo wa mtindo wa ufikishwaji wa sanaa. Haya matusi yana maana na yangekuwa mabaya sana basi jamii isingeyatunga na kuyaweka kwenye kamusi.

Mfano mwingine kwenye mziki, kuna watu wanalalamika mtindo wa kisasa wa mziki haufai, unakuta mtu kama Scars anapinga mziki wa leo kwasababu mabiti ni ya Trap, yeye anataka mabiti yaleyale ya bum bap ya miaka ya 90 mpaka leo watu waimbie.
Au unakuta mzee analalamika kuwa sikuizi mnaiga wanaijeria hamna uhalisi wa kitanzania. Well, No shit Sherlock..Have you ever heard the term 'globalization'?
Hapana mzee uli catch vibaya kusudio langu

Katika mziki kwanza huwa nafurahishwa na mambo makuu mawili ambayo ni ubunifu na content. Beat kwangu sio kipaumbele thats why hata kwenye ngoma za Joyner Lucas nilizozikubali zilizingatia contents.

Wakina Young Lunya wanapita kwenye trap beats lakini ukiangalia katika jicho la kisanaa utaona kuna makosa mengi ukiachana na contents lakini pia hata vina utaona havipo au ni vile vya magumashi

Vina vya magumashi mfano wake ni kama ile Dear God ya Kalla Jeremiah, mle hamna vina ila kwa wasiojua mziki hawawezi kuelewa. Na ndio maana nilipenda kuona hawa wagawaji tuzo wawe ni watu wanaojua mziki na sio kutoa tuzo kwaababu ya trend.

Kama wanataka kutuweka kwenye mfumo huo basi wazitafutie kipengele chao ili tuwe tunawaelewa kuliko kusema wimbo bora wakati lyrically ni zero

Ubunifu bongo umepungua au umeisha kabisa, hususani kwenye Bongo Fleva

Mfano leo hii katika kizazi cha Bongo Fleva tunao wasanii wakubwa kina Diamond nk. Hawa wasanii to be honestly they lack some creativity wameanza kufanya remake kwenye nyimbo za zamani

Na hata wakifanya nyimbo mpya walizotunga wao bado utaona wana pwaya kwenye content though wanabebwa na fame plus fan base waliyo nayo na ndio maana hata wakitoa nyimbo ya dakika 3 afu humo wawe wanajikoholesha tu bado ita trend tu.

Sasa hiyo inatengeneza mwendelezo mbovu kwa hawa chipukizi ambao wanataka kufikia malengo makubwa kupitia mziki.

Kwasababu watakuwa wanajenga dhana kichwani kuwa ili uweze kufikia level za juu za kimafanikio basi unapaswa kuimba style kama ile ile wanayoimba hawa wakubwa.
 
Mkuu nakuelewa sana unaposema kwamba lugha yoyote hukua. Lakini sikubaliani nawe unapotetea kwamba lugha sanifu ambayo tayari ipo kwenye matumizi iharibiwe eti huko ndiko kukua kwa lugha. Big NO!

Kukua kwa lugha huhusisha kuongeza misamiati mipya sio kupindisha misamiati ambayo tayari ipo na inaeleweka kwa wazungumzaji wa lugha husika. Kwa mfano huwezi kutetea kwamba mtu akitamka "kwendaga" badala ya "kwenda" au "sintokubali" badala ya sitakuballi". Hii haimaanishi kukuwa kwa lugha bali huo ni upotoshaji wa lugha unaopaswa kukemewa kwa nguvu zote.
Mkuu, tuanze na general meaning ya kitu kuharibiwa.
Kitu tunasema kimeharibika kama pale ambapo kimeshindwa kufanya lile dhumuni la uwepo wake. Yani kama mkanda haukazi tena suruali kiunoni basi hapo tunasema mkanda umeharibika.

Lugha huharibiwa pale inaposhindwa kufanya kazi yake ambayo ni kufikisha ujumbe.
Sasa kama mtu ametumia neno 'Kwendaga' halafu watu wasimuelewe hapo ameharibu lugha. ila kama hadhira imeelewa basi hajaharibu lugha, ameikuza.
Kwani neno 'kwenda' lina kitu gani special zaidi ya 'kwendaga'?

Tena by the way, kwendaga ni bora kuliko kwenda kwasababu linaonesha mazoea. Kuliko kusema 'huwa unaenda' mtu anasema 'unaendaga' so hapo tayari amefupisha maneno na ameongeza efficiency ya lugha.
Lugha hukua kwa style nyingi tofauti tofauti, sio lazima ikue kwa style unayotaka wewe ya kuongeza misamiati migeni kabisa kwenye kamusi.
Inaweza kukua pia kupitia kubadili misamiati iliyopo.

Ngoja nikupe mfano kwenye kimalkia.
Kulikuwa na neno Awe:-likimaanisha mshangao (wonder) au hofu juu ya kitu kikubwa chenye nguvu sana kama Mungu, mfalme nk.
Sentesi: After realizing what God had done to save my wife, I was in awe.

Sasa kile kitu kinacholeta hisia za Awe kilikuwa kinaitwa Awful..yani kitu kinachomfanya mtu ashangae ukuu wake (Awful:-Full of awe)
Sentesi: God is awful.

Lakini muda ulivyoenda watu wakaanza kulibadilisha hilo awful badala ya full wakaanza kuweka some, wakazaa neno 'awesome' lenye hiyohiyo maana....na walipofanya hivyo wakabadili matumizi ya hili neno awful mpaka sasa limekuwa kinyume chake kabisa.
Sasaivi ukisema Awful unamaanisha kitu kibaya, kisichofurahisha, kisichopendeza.

Sasa hapo huoni msamiati ambao tayari ulikuwa unaeleweka umebadilishwa muundo na maana na kuzaa misamiati mipya?
 
Watangazaji makanjanja wanapomhoji mtu, hasa mwanasiasa, huwa wanamuacha atiririke tu bila kuhoji wala kuomba ufafanuzi wa majibu. Katika mahojiano na mwandishi wa habari, mtu anayehojiwa anaweza kuulizwa swali linalohusu nutrition akatoa majibu ya astronomy lakini mtangazaji akabaki amemtumbulia macho tu bila kumuongoza. Ovyo sana.

Hivi ndugu zetu waandishi akina Pascal Mayalla ndivyo mnavyofundishwa huko SJMC au mnaamua tu kutuburuza kwa makusudi? 😀 😀 😀
Unamfahamu mtu anaitwa Tundu Lissu, makamu mwenyekiti wa CHADEMA ambaye kwa sasa anaishi uhamishoni Ubelgiji...?

Huyu jamaa waandishi wa habari na watangazaji wengi makanjanja humgwaya kumfanyia mahojiano kwa sababu mwandishi au mtangazaji habari husika asipokuwa makini yeye ndiye anaweza kugeuzwa kuwa mhojiwa badala ya mtangazaji au mwandishi wa habari kwa kumfundishwa mtangazaji au mwandishi wa habari yampasayo kufanya kama mwandishi/mtangazaji...!

Na wakati mwingine haoni haya kumwambia, "wewe unajua unachokifanya kweli hapa..?"

Sasa mwandishi/mtangazaji ikifikia hatua ya mhojiwa wako anakuambia hivi mbele ya TV Cameras, uelewe kabisa wewe mwandishi au mtangazaji umekosa weledi....you are a complete failure...!!
 
Again, inategemeana na hadhira. Kama hadhira ni waingereza wanaojali past tense, verb noun hapo atakuwa anakosea.
ila kama hadhira ni watu kama mwajuma wa mwabepande ambaye yeye kila siku anasema 'ofkozi mimi ni beuty' na jamii husika ndio inaelewa hivyo. Basi hata watangazaji wakisema hivyo sioni shida.

Kumbukeni jamani hizi lugha ni nothing but tools tu za kufikisha ujumbe.
Lugha zipo kwa ajili ya watumiaji na sio vice versa.

Kama wewe ukitumia kiswahili sanifu/fasaha kwa misamiati migumu na kuifanya majority ya jamii isikuelewe na mwingine akatumia kiswahili hiki kinachoongewa mtaani chenye mbwembwe na vikolombwezo 'shazi' halafu watu wakamuelewa. Aliyefikisha ujumbe zaidi ni yupi?

Angalieni kwanza hadhira inayokusudiwa ni ipi. Kama hadhira ni ya kimataifa kama BBC, basi wakifanya hivyo wanakosea.
Lakini kama kipindi husika kinaitwa XXL kwaajili ya vijana wa mtaani wanaondika sasa 'Xaxa'..inabidi mtindo uendane na vijana walengwa.
Uko sawa kabisa
 
Again, inategemeana na hadhira. Kama hadhira ni waingereza wanaojali past tense, verb noun hapo atakuwa anakosea.
ila kama hadhira ni watu kama mwajuma wa mwabepande ambaye yeye kila siku anasema 'ofkozi mimi ni beuty' na jamii husika ndio inaelewa hivyo. Basi hata watangazaji wakisema hivyo sioni shida.

Kumbukeni jamani hizi lugha ni nothing but tools tu za kufikisha ujumbe.
Lugha zipo kwa ajili ya watumiaji na sio vice versa.

Kama wewe ukitumia kiswahili sanifu/fasaha kwa misamiati migumu na kuifanya majority ya jamii isikuelewe na mwingine akatumia kiswahili hiki kinachoongewa mtaani chenye mbwembwe na vikolombwezo 'shazi' halafu watu wakamuelewa. Aliyefikisha ujumbe zaidi ni yupi?

Angalieni kwanza hadhira inayokusudiwa ni ipi. Kama hadhira ni ya kimataifa kama BBC, basi wakifanya hivyo wanakosea.
Lakini kama kipindi husika kinaitwa XXL kwaajili ya vijana wa mtaani wanaondika sasa 'Xaxa'..inabidi mtindo uendane na vijana walengwa.
Mkuu kila nikijaribu kukuelewa nashindwa. Kama ni hivi basi hakuna haja ya kuwa na fasihi ya lugha. Kwa maoni yako, kila kitu kitakachosemwa au kuandikwa kipo sahihi. Hebu angalia mifano ifuatayo labda utanielewa. Sasa itabidi nirudi darasani. Hapa naandika maneno ambayo watangazaji hupotosha lakini wewe unawatetea unasema eti wanakuza lugha:
Neno sahihi Neno wanalotamka watangazaji makanjanjaMfano katika matumizi yasiyo sahihi
SaaMasaa/LisaaNimekaa hapa kwa masaa matatu/Nitakuja baada ya lisaa limoja
MadhumuniDhumuniDhumuni la barua hii ni kukualika mkutano
Sina budiNi budiNi budi kila mtu kujali afya yake
MakontenaKontenaGari imebeba kontena tano.
WimboNyimboNyimbo hii ni nzuri sana
MadaftariDaftariDaftrari zako ziko wapi?
JumaLijumaNitakuwa nje ya ofisi kwa muda wa lijuma limoja
Ndugu yangu hivi upotoshaji wa lugha kama huu utasema ni kukua kwa lugha kweli? Upo serious kabisa au unachokoza mada tu?
 
Habari wanaJF?

Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha na maneno mengi. Kwa mujibu wa utafiti binafsi nilioufanya hivi karibuni, usikilizaji wa redio na utazamaji wa TV umepungua sana miongoni mwa wafuatiliaji wa habari. Hili halijatokea kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu ya kupungua usahihi wa taarifa na ubora wa watangazaji. Sote ni mashahidi jinsi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Voice of Kenya (VoK) zilivyokuwa na watangazaji nguli ambao huchoki kuwasikiliza.

Watangazaji wengi wa redio na TV zinazochipukia kama uyoga hapa nchini wanakera mno kwa utangazaji wa ovyo na unaokosa weledi. Ukisikiliza redio na kutazama TV, hasa hizi zinazoitwa Redio/TV za Kijamii, utahisi kichefuchefu na huwezi kuendelea kusikiliza kwa zaidi ya dakika 5! Wanachotangaza ni zaidi ya utumbo. Na kibaya zaidi, hawa makanjanja hawakupitia kabisa kwenye vyuo vya uandishi wa habari. Inasikitisha mtangazaji kutoongea Kiswahili fasaha unabaki unajiuliza: hivi huyu mtu alienda shule kweli au ameokotwa jalalani? Na kama alienda shule, je, huko alienda kujifunza ujinga au maarifa? (FaizaFoxy, 2015). Yaani hawa viumbe hawawezi kabisa kujieleza kwa Kiswahili na Kiingereza fasaha.

Zamani haikuwa rahisi mtu yeyote kujipenyeza kwenye utangazaji ikiwa hajui Kiswahili na Kiingereza fasaha. Na si hilo tu, mtangazaji anatakiwa kuwa na uhakika wa jambo analolitangaza. Juzi nilipata hasira sana niliposikia mtangazaji wa mpira akiutangazia umma kuwa mmiliki wa sasa wa Klabu ya Chelsea ni Roman Abramovich. Wanajiropokea tu ilmradi tonge liingie kinywani.

Utakuta mtu ana lafudhi mbovu na uelewa mdogo kama mbegu ya hardali lakini bado anang’ang’ania kuwa mtangazaji. Ni aibu kubwa. Yaani pale inapotaikiwa kuweka “r”, yeye anapachika “l”, kwa mfano mpira anatamka mpila. Ni aibu iliyoje! Na pia ni wazuri sana kwenye upotoshaji kwa mfano neno wimbo, hutamka nyimbo……..mfano: Leo nawachezea nyimbo moja ya Diamond inayoitwa Kantangaze. Ovyo kabisa!

Kwa ujumla, nchi hii ina watangazaji wenye uelewa finyu na upeo mdogo wa utangazaji. Natoa wito kwa serikali na vyombo vinavyohusika kudhibiti maudhui ya vyombo vya habari kufanya kazi yao kikamilifu ili kuzuia upotoshaji huu unaofanywa na baadhi ya watangazi makanjanja. Aidha, kiwango cha elimu na weledi wa mtu anayefaa kuwa mtangazaji kipitiwe upya. Watangazaji wasiokidhi vigezo wachujwe na kutupwa nje ya ulingo wa utangazaji. Tumechoshwa na upotoshaji.
Pascal Mayalla tuambie taaluma yenu imekumbwa na nini?
 
Habari wanaJF?

Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha na maneno mengi. Kwa mujibu wa utafiti binafsi nilioufanya hivi karibuni, usikilizaji wa redio na utazamaji wa TV umepungua sana miongoni mwa wafuatiliaji wa habari. Hili halijatokea kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu ya kupungua usahihi wa taarifa na ubora wa watangazaji. Sote ni mashahidi jinsi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Voice of Kenya (VoK) zilivyokuwa na watangazaji nguli ambao huchoki kuwasikiliza.

Watangazaji wengi wa redio na TV zinazochipukia kama uyoga hapa nchini wanakera mno kwa utangazaji wa ovyo na unaokosa weledi. Ukisikiliza redio na kutazama TV, hasa hizi zinazoitwa Redio/TV za Kijamii, utahisi kichefuchefu na huwezi kuendelea kusikiliza kwa zaidi ya dakika 5! Wanachotangaza ni zaidi ya utumbo. Na kibaya zaidi, hawa makanjanja hawakupitia kabisa kwenye vyuo vya uandishi wa habari. Inasikitisha mtangazaji kutoongea Kiswahili fasaha unabaki unajiuliza: hivi huyu mtu alienda shule kweli au ameokotwa jalalani? Na kama alienda shule, je, huko alienda kujifunza ujinga au maarifa? (FaizaFoxy, 2015). Yaani hawa viumbe hawawezi kabisa kujieleza kwa Kiswahili na Kiingereza fasaha.

Zamani haikuwa rahisi mtu yeyote kujipenyeza kwenye utangazaji ikiwa hajui Kiswahili na Kiingereza fasaha. Na si hilo tu, mtangazaji anatakiwa kuwa na uhakika wa jambo analolitangaza. Juzi nilipata hasira sana niliposikia mtangazaji wa mpira akiutangazia umma kuwa mmiliki wa sasa wa Klabu ya Chelsea ni Roman Abramovich. Wanajiropokea tu ilmradi tonge liingie kinywani.

Utakuta mtu ana lafudhi mbovu na uelewa mdogo kama mbegu ya hardali lakini bado anang’ang’ania kuwa mtangazaji. Ni aibu kubwa. Yaani pale inapotaikiwa kuweka “r”, yeye anapachika “l”, kwa mfano mpira anatamka mpila. Ni aibu iliyoje! Na pia ni wazuri sana kwenye upotoshaji kwa mfano neno wimbo, hutamka nyimbo……..mfano: Leo nawachezea nyimbo moja ya Diamond inayoitwa Kantangaze. Ovyo kabisa!

Kwa ujumla, nchi hii ina watangazaji wenye uelewa finyu na upeo mdogo wa utangazaji. Natoa wito kwa serikali na vyombo vinavyohusika kudhibiti maudhui ya vyombo vya habari kufanya kazi yao kikamilifu ili kuzuia upotoshaji huu unaofanywa na baadhi ya watangazi makanjanja. Aidha, kiwango cha elimu na weledi wa mtu anayefaa kuwa mtangazaji kipitiwe upya. Watangazaji wasiokidhi vigezo wachujwe na kutupwa nje ya ulingo wa utangazaji. Tumechoshwa na upotoshaji.
Hao ni ma prizenta.
 
Niliacha kusikiliza redio punde tuu nilipogundua wimbo mmoja unaitwa 'nyimbo moja'..
 
Mkuu hili jambo nimelifanyia utafiti kwa kusikiliza redio na TV mabalimbali na kwa kuwahoji wasikilizaji. Ni kweli wengi wamechelea kufuatilia taarifa za redio na TV za jamii kwa sababu ya upotoshaji na utangazaji wa ovyo.
Exactly
 
Ingawa unayosema yana ukweli lakini inabidi tu- Call a Spade a Spade...., Hii industry ipo katika transition, business models inabidi zibadilike, Competition imekuwa kubwa na consumption / concentration span ya mlaji imekuwa fupi.., sekunde mbili hauja-mshika mlaji tayari kabonyeza remote kwenda pengine..., kwenye Video on demand ndio watu wapo...

Pia Big Network News zimekuwa propaganda machines, badala ya kuangalia habari / news unapewa opinions za a given network kulingana na mlengo wao... (and this is world over) kwahio mlaji inabidi ufanye mwenyewe upembuzi yakinifu
Na wewe nawe ni kama vile hujui vizuri Kiswahili. Yaani unabaki kudokoa dokoa vijimaneno ya Kiingereza alimradi tu uonekane unajua Kiingereza. Unakera kweli kweli na huo ulimbukeni wako.
 
Na wewe nawe ni kama vile hujui vizuri Kiswahili. Yaani unabaki kudokoa dokoa vijimaneno ya Kiingereza alimradi tu uonekane unajua Kiingereza. Unakera kweli kweli na huo ulimbukeni wako.
Kwahio kujua Kiswahili ni moja ya requierments za kujiunga JF ?

Ukitaka definition ya Ulimbukeni ni hicho ulichoweka hapo juu.....
 
Back
Top Bottom