Watangazaji wa kizazi hiki wanakera mpaka basi. Hivi wanaokotwa wapi hawa viumbe?

Watangazaji wa kizazi hiki wanakera mpaka basi. Hivi wanaokotwa wapi hawa viumbe?

Both are correct.
Ni sawa na kwenye mziki mnavyolalamikaga mziki wa sikuizi this and that.
Free advice for you;
Fanyeni kuwa mnasikiliza miziki yenu ya zamani tu muache kusikiliza ya sasaivi.
Kwenye news, angalieni zile recorded za miaka 20 iliyopita youtube.
Au muende hospitali kutibiwa kwasababu Nostalgia is one hell of a disease.

Because frankly speaking, hata mlalamikeje hamuwezi kubadilisha kitu.
Law of demand and supply, ukiona kitu kipo supplied kwa wingi basi ujue demand ndio inataka hiko kitu.
And it's a free market.
Maybe anzisheni stesheni yenu ya wazee afu muone how that'll go.
Muda ni ukuta, Huwezi kupambana nao.
Cool down kijana; kumbuka hakuna kijiji kisichokuwa na wazee. Heshaima kwa wazee ni kitu bora. Hatuwezi kuona jamii inakengeuka na kuharibika tukakaa kimya. Kwa mfano, zamani hakukuwa na vitendo vya ushoga na usagaji lakini sasa hivi haya mambo yanafanyika hadharani. Tukiuliza kwanini haya mambo yanakuwa hivi mnasema wazee hatuendi na wakati. Hili sawa?

Tatizo wazee tukikemea upumbavu huu mnaona tunawaingilia mambo yenu. Kumbuka ujinga unaotangazwa na watangazaji hawa unaathiri jamii nzima; mwisho wa siku hata mtoto wako au ndugu yako ataiga mambo ya kishoga halafu utaanza kumtafuta mchawi wakati mchawi ni wewe mwenyewe unayeshabikia ukengeufu.

Tukirejea kwenye muziki ndio mnaimba upumbavu kabisa. Wanamuziki wa zamani waliimba nyimbo za mapenzi ambazo baba unaweza kusikiliza na familia yako bila wasiwasi. Siku hizi vijana wanaimba nyimbo za NGONO ambazo zikiimbwa inabidi baba na mama waondoke kwa kuwa zimejaa matusi makubwa. Hata video za muziki zinazotolewa na vijana wa siku hizi hazina maadili hata kidogo......watu wanacheza wakiwa uchi eti mnatuambia huu ndio usasa! Mmerogwa nyie sio bure.

Huwa napata taabu sana wakati ninaposafiri kwenye basi la abiria hizi nyimbo na video zinachezwa tangu mwanzo hadi mwisho wa safari. Mtu huwezi hata kusafiri na mkweo au watoto wako kwenye basi moja kwa kuwa video na nyimbo zinazoimbwa mle zimejaa matusi yenye mwelekeo wa ngono. Inasikitisha sana.

Leo nimesikitika kuna wanaume wawili wanatangaza kule Wasafi FM kwenye kipindi cha mipasho wanaongea mambo ya kimbeya kama wanawake mashangingi. Nadhani hawa wanapaswa kupimwa tuone kama kweli ni wanaume au la. Mwanaume mzima utaongeaje mambo ya umbeya na mipasho kama mwanamke? So sad!
 
Aisee wapuuzi San wakat mwingine mm nasima radio siwez kuja kumsikiliza Bab level ,zembwela ,mpoki ,doki , yaani Ni balaa siwezi kuwasikilizaa hao watu Bora Nile rege tu
Kuna wanaume wawili kule Wasafi FM wanaitwa Idriss Kitaa na Juma Lokole wanaongea umbeya kama wanaume aisee! Leo wakati nafanya utafiti wangu nime-tune Wasafi FM nimeshangaa sana jinsi wanavyoongea kishoga. Hawa wanapaswa kupimwa ili tuwatambue kama ni wanaume au la. Isije ikawa sensa inaonesha wanaume ni wengi kumbe wapo wachache. Ni shida aisee!
 
Kuna wanaume wawili kule Wasafi FM wanaitwa Idriss Kitaa na Juma Lokole wanaongea umbeya kama wanaume aisee! Leo wakati nafanya utafiti wangu nime-tune Wasafi FM nimeshangaa sana jinsi wanavyoongea kishoga. Hawa wanapaswa kupimwa ili tuwatambue kama ni wanaume au la. Isije ikawa sensa inaonesha wanaume ni wengi kumbe wapo wachache. Ni shida aisee!
Wanaume wa dar hao
 
Kweli kabisa. Kiswahili kinachotumika pia ni kibovu.
Mfano:
1. Napendaga kula mihogo.
2. Alikwendaga Ujerumani kusoma
Au utasikia mtangazaji anatangaza kwa kujiamini anatamka upumbavu ufuatao:
1. Zimekasoro dakika mbili ifike saa 3.
2. Nitaendesha kipindi kwa muda wa masaa mawili.
3. Sintokubali kuondoka bila kukuchezea muziki.
4. Yamebaki mawiki kadhaa kuelekea kombe la Dunia.
5. Ni budi kufikiri kabla ya kuongea.
6. Leo nimeokota funguo ya gari iliyopotozwa na dereva wa gari iliyokuwa imebeba kontena mbili.
7. Nimemnunulia mwanangu daftari tatu.

Yaani fani ya utangazaji kwa sasa hivi imevamiwa na kenge kutoka kila kona; wanajiropokea tu kama walevi, mateja au wehu. Inasikitisha mno. Bila serikali kuingilia kati, muda mfupi ujao tutakuwa na kizazi cha ovyo sana.
 
Sasa ulitegemea nin unakuta mtot wa kiume anaandika sms""kaandika xmx,,,,xio,xaxaivi,,,,,,,yaani unakaa unawaza unasema huyu kapote au
Nawaza ifikapo 2050 nchi hii itakuwa imejaa mateja, mashoga, wasagaji na wehu tupu. Serikali inapaswa iingilie kati.
 
Upuuzi uko kwenye fani ya habari kwa ujumla. Mfano audience ya Kenya inakubali makanjanja kama sisi?

Fananisha ushiriki wa wa Tz na wakenya kwenye Twitter na social media nyingine uone tofauti. Tatizo ni kubwa na linahusu hadhira na jamii kwa ujumla.
Ndio maana kule BBC Swahili kuna wakenya wengi kuliko watanzania kwa sababu watanzania hawako makini, mbali na ukweli kwamba tanzania ndiko Kiswahili kilikozaliwa.
 
Afadhali wewe umeliona na kilianzishia mada ili tujadili...

Ni kweli kabisa. Kwa mfano pale ITV pana watangazaji fulani wawili mmoja anaitwa JUMA KAPALATU mwingine nimemsahau jina...

Lakini hawa ndio mara kwa mara huongoza kipindi kile cha kila Alhamisi kuanzia saa 3 - 5 usiku kinachoenda kwa jina la "MALUMBANO YA HOJA"..

Hawa jamaa hawana professionalism kabisa ya kuongoza na kusimamia mijadala huru...

Kwa wanaoweza kufuatilia, wafanye hivyo kesho tarehe 10/11/2022 Alhamisi watagundua makosa mengi sana ya watangazaji kiasi cha kuondoa radha ya kipindi na mjadala wote kwa ujumla...

Ni waongo na kilicho kibaya zaidi wao wenyewe kama waendesha mjadala huwa hawana taarifa za kutosha juu ya "issues" wanazoziibua ili watu wajadili...

Hili ni tatizo la waandishi na watangazaji wengi kwa zaidi ya 70%...

Tena ukienda kwenye Online Media/TV huko ndo kuna uchafu mtupu wa wanaojiita waandishi/watangaji...

Kuna watangazaji huko ambao kama ulivyosema kule kusoma taarifa kwa ufasaha tena kwa lugha yao ya kiswahili ni shida...

Mtangazaji anasoma taarifa huku anakata kata kama vile redio iliyo na betri zilizoisha nguvu yake ya kuiendesha...!
Watangazaji makanjanja wanapomhoji mtu, hasa mwanasiasa, huwa wanamuacha atiririke tu bila kuhoji wala kuomba ufafanuzi wa majibu. Katika mahojiano na mwandishi wa habari, mtu anayehojiwa anaweza kuulizwa swali linalohusu nutrition akatoa majibu ya astronomy lakini mtangazaji akabaki amemtumbulia macho tu bila kumuongoza. Ovyo sana.

Hivi ndugu zetu waandishi akina Pascal Mayalla ndivyo mnavyofundishwa huko SJMC au mnaamua tu kutuburuza kwa makusudi? 😀 😀 😀
 
Kuna mwingine nilishangaa hajuwi hata majiji tuliyonayo hapa Tanzania, akasema eti morogoro ni Jiji, Yupo siriasi kabisa redioni kusema kuwa morogoro Ni jiji, waandishi wa siku hizi Ni wajuaji Sana na hawafanyi utafiti wa yale wanayozungumza ,pia nahisi hata hawajiandai kabla ya kuingia ofisini ndio sababu unakuta wanajiropokea tu na kufanya upotoshaji mkubwa Sana bila kujuwa kuwa wanasikilizwa na watu wengi Hadi watoto wa shule ambao wanaweza wakakalili uongo kisa tu wamesikia Redioni,

Nakala kwa: Pascal Mayalla
Masikini, inasikitisha sana! Huyu mpuuzi aliwapotosha wanafunzi waliokuwa wakimsikiliza maana wanafunzi wanaamini kuwa watangazaji wanaongea ukweli daima. So sad!
 
Bro pole sana. Hilo ni janga la kitaifa. Hali ni mbaya kuliko tunavyodhani. Kuna siku tumejadiri hili kwenye uzi aliouanzisha pascal Mayala kuhusu umahili wa waandishi wa habari. Kwa ujumla ni changamoto, na kikubwa katika ugumu huo ni kwamba hawa watangazaji wanaongea kwa kujiamini sana, huku wakiongea vitu visivyokuwa na uthibitishoau vyenye makosa. Lalafu, kubwa kuliko, wanasikilizwa sana na vijana wa kizazi kipya.
Kufupisha mambo, ushauri ni kuboresha udhibiti wa sifa za watu wanaojiunga na fani ya uandishi. Waongeze minimum requirement au grades za kuingilia kwenye fani.

Lingine wawe na board ya kuwa regulate. Wawe wanasajiliwa ili waweze ku practice kama wahasibu, wagavi n.k.
Asante sana mkuu. Naomba huo uzi wa Pascal Mayalla ukiupata unitag, sikuwahi kuusoma. Najua atakuwa amedadavua vizuri hii mada.
 
Nawaza ifikapo 2050 nchi hii itakuwa imejaa mateja, mashoga, wasagaji na wehu tupu. Serikali inapaswa iingilie kati.
Unajua ujinga wa ushoga unaanza na vitu vidogo vidogo mtoto wakiume unafanya vitu vyakike kike mwisho was siku unashindwa kujitofautisha wew na wanawake unaanza kufanya usodoma
 
Habari wanaJF?

Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha na maneno mengi. Kwa mujibu wa utafiti binafsi nilioufanya hivi karibuni, usikilizaji wa redio na utazamaji wa TV umepungua sana miongoni mwa wafuatiliaji wa habari. Hili halijatokea kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu ya kupungua usahihi wa taarifa na ubora wa watangazaji. Sote ni mashahidi jinsi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Voice of Kenya (VoK) zilivyokuwa na watangazaji nguli ambao huchoki kuwasikiliza.

Watangazaji wengi wa redio na TV zinazochipukia kama uyoga hapa nchini wanakera mno kwa utangazaji wa ovyo na unaokosa weledi. Ukisikiliza redio na kutazama TV, hasa hizi zinazoitwa Redio/TV za Kijamii, utahisi kichefuchefu na huwezi kuendelea kusikiliza kwa zaidi ya dakika 5! Wanachotangaza ni zaidi ya utumbo. Na kibaya zaidi, hawa makanjanja hawakupitia kabisa kwenye vyuo vya uandishi wa habari. Inasikitisha mtangazaji kutoongea Kiswahili fasaha unabaki unajiuliza: hivi huyu mtu alienda shule kweli au ameokotwa jalalani? Na kama alienda shule, je, huko alienda kujifunza ujinga au maarifa? (FaizaFoxy, 2015). Yaani hawa viumbe hawawezi kabisa kujieleza kwa Kiswahili na Kiingereza fasaha.

Zamani haikuwa rahisi mtu yeyote kujipenyeza kwenye utangazaji ikiwa hajui Kiswahili na Kiingereza fasaha. Na si hilo tu, mtangazaji anatakiwa kuwa na uhakika wa jambo analolitangaza. Juzi nilipata hasira sana niliposikia mtangazaji wa mpira akiutangazia umma kuwa mmiliki wa sasa wa Klabu ya Chelsea ni Roman Abramovich. Wanajiropokea tu ilmradi tonge liingie kinywani.

Utakuta mtu ana lafudhi mbovu na uelewa mdogo kama mbegu ya hardali lakini bado anang’ang’ania kuwa mtangazaji. Ni aibu kubwa. Yaani pale inapotaikiwa kuweka “r”, yeye anapachika “l”, kwa mfano mpira anatamka mpila. Ni aibu iliyoje! Na pia ni wazuri sana kwenye upotoshaji kwa mfano neno wimbo, hutamka nyimbo……..mfano: Leo nawachezea nyimbo moja ya Diamond inayoitwa Kantangaze. Ovyo kabisa!

Kwa ujumla, nchi hii ina watangazaji wenye uelewa finyu na upeo mdogo wa utangazaji. Natoa wito kwa serikali na vyombo vinavyohusika kudhibiti maudhui ya vyombo vya habari kufanya kazi yao kikamilifu ili kuzuia upotoshaji huu unaofanywa na baadhi ya watangazi makanjanja. Aidha, kiwango cha elimu na weledi wa mtu anayefaa kuwa mtangazaji kipitiwe upya. Watangazaji wasiokidhi vigezo wachujwe na kutupwa nje ya ulingo wa utangazaji. Tumechoshwa na upotoshaji.
Na wahariri ama waliowaajiri nao unaweka kundi gani?
 
Cool down kijana; kumbuka hakuna kijiji kisichokuwa na wazee. Heshaima kwa wazee ni kitu bora. Hatuwezi kuona jamii inakengeuka na kuharibika tukakaa kimya. Kwa mfano, zamani hakukuwa na vitendo vya ushoga na usagaji lakini sasa hivi haya mambo yanafanyika hadharani. Tukiuliza kwanini haya mambo yanakuwa hivi mnasema wazee hatuendi na wakati. Hili sawa?

Tatizo wazee tukikemea upumbavu huu mnaona tunawaingilia mambo yenu. Kumbuka ujinga unaotangazwa na watangazaji hawa unaathiri jamii nzima; mwisho wa siku hata mtoto wako au ndugu yako ataiga mambo ya kishoga halafu utaanza kumtafuta mchawi wakati mchawi ni wewe mwenyewe unayeshabikia ukengeufu.

Tukirejea kwenye muziki ndio mnaimba upumbavu kabisa. Wanamuziki wa zamani waliimba nyimbo za mapenzi ambazo baba unaweza kusikiliza na familia yako bila wasiwasi. Siku hizi vijana wanaimba nyimbo za NGONO ambazo zikiimbwa inabidi baba na mama waondoke kwa kuwa zimejaa matusi makubwa. Hata video za muziki zinazotolewa na vijana wa siku hizi hazina maadili hata kidogo......watu wanacheza wakiwa uchi eti mnatuambia huu ndio usasa! Mmerogwa nyie sio bure.

Huwa napata taabu sana wakati ninaposafiri kwenye basi la abiria hizi nyimbo na video zinachezwa tangu mwanzo hadi mwisho wa safari. Mtu huwezi hata kusafiri na mkweo au watoto wako kwenye basi moja kwa kuwa video na nyimbo zinazoimbwa mle zimejaa matusi yenye mwelekeo wa ngono. Inasikitisha sana.

Leo nimesikitika kuna wanaume wawili wanatangaza kule Wasafi FM kwenye kipindi cha mipasho wanaongea mambo ya kimbeya kama wanawake mashangingi. Nadhani hawa wanapaswa kupimwa tuone kama kweli ni wanaume au la. Mwanaume mzima utaongeaje mambo ya umbeya na mipasho kama mwanamke? So sad!
Nadhani mngejua kutofautisha kwenye ukemeaji wenu kati ya maudhui na mtindo wa ufikishaji wa sanaa.
Mnapokemea maudhui kama ushoga, ngono,ulevi,umbea, uongo, uzembe katika uwasilishwaji wa sanaa kama habari, muziki, nk. Hapo ni sawa.

Lakini sasa mnapoenda mbali/kuchanganya na kuanza kukemea mtindo wa sanaa inavyowasilishwa kama matumizi ya Lugha, mandhari, mahadhi, nk. Hapo mnakosea.
Mtindo huwa unabadilika kuendana na muda.

Mfano kwenye lugha hapo, mngetakiwa kutambua sifa ya Lugha mojawapo ni kukua, lugha sio gereza kwamba lazima ujifunge kwenye kanuni na sheria za kisarufi, misamiati nk. Zilizowekwa na wataalamu kule maofisini. Kumbuka sanaa ni kioo cha jamii. Sasa kama jamii inaongea "kwendaga" basi haina budi sanaa iakisi lugha inayotumiwa na jamii.
Hata kiingereza cha leo hakikuwa hivyo miaka 500 iliyopita. Wangeng'ang'ania na wao kisibadilike ingekuwaje?
Hata lugha za matusi pia ni mojawapo wa mtindo wa ufikishwaji wa sanaa. Haya matusi yana maana na yangekuwa mabaya sana basi jamii isingeyatunga na kuyaweka kwenye kamusi.

Mfano mwingine kwenye mziki, kuna watu wanalalamika mtindo wa kisasa wa mziki haufai, unakuta mtu kama Scars anapinga mziki wa leo kwasababu mabiti ni ya Trap, yeye anataka mabiti yaleyale ya bum bap ya miaka ya 90 mpaka leo watu waimbie.
Au unakuta mzee analalamika kuwa sikuizi mnaiga wanaijeria hamna uhalisi wa kitanzania. Well, No shit Sherlock..Have you ever heard the term 'globalization'?
 
Mfano kwenye lugha hapo, mngetakiwa kutambua sifa ya Lugha mojawapo ni kukua, lugha sio gereza kwamba lazima ujifunge kwenye kanuni na sheria za kisarufi, misamiati nk. Zilizowekwa na wataalamu kule maofisini. Kumbuka sanaa ni kioo cha jamii. Sasa kama jamii inaongea "kwendaga" basi haina budi sanaa iakisi lugha inayotumiwa na jamii.
Hata kiingereza cha leo hakikuwa hivyo miaka 500 iliyopita.
Ni sawa wangeongea tu basi kiswahili. Shida wanajifanya na kiingereza wanajua ila kila wanalochomekea wanakosea!!!! Past tense, noun, verb, adverb havibadiliki hata miaka 500!!! Lugha za watu zina misingi yake mkuu kama huwezi hata basics ni kuachana nazo tu!!!
 
Nadhani mngejua kutofautisha kwenye ukemeaji wenu kati ya maudhui na mtindo wa ufikishaji wa sanaa.
Mnapokemea maudhui kama ushoga, ngono,ulevi,umbea, uongo, uzembe katika uwasilishwaji wa sanaa kama habari, muziki, nk. Hapo ni sawa.

Lakini sasa mnapoenda mbali/kuchanganya na kuanza kukemea mtindo wa sanaa inavyowasilishwa kama matumizi ya Lugha, mandhari, mahadhi, nk. Hapo mnakosea.
Mtindo huwa unabadilika kuendana na muda.

Mfano kwenye lugha hapo, mngetakiwa kutambua sifa ya Lugha mojawapo ni kukua, lugha sio gereza kwamba lazima ujifunge kwenye kanuni na sheria za kisarufi, misamiati nk. Zilizowekwa na wataalamu kule maofisini. Kumbuka sanaa ni kioo cha jamii. Sasa kama jamii inaongea "kwendaga" basi haina budi sanaa iakisi lugha inayotumiwa na jamii.
Hata kiingereza cha leo hakikuwa hivyo miaka 500 iliyopita. Wangeng'ang'ania na wao kisibadilike ingekuwaje?
Hata lugha za matusi pia ni mojawapo wa mtindo wa ufikishwaji wa sanaa. Haya matusi yana maana na yangekuwa mabaya sana basi jamii isingeyatunga na kuyaweka kwenye kamusi.

Mfano mwingine kwenye mziki, kuna watu wanalalamika mtindo wa kisasa wa mziki haufai, unakuta mtu kama Scars anapinga mziki wa leo kwasababu mabiti ni ya Trap, yeye anataka mabiti yaleyale ya bum bap ya miaka ya 90 mpaka leo watu waimbie.
Au unakuta mzee analalamika kuwa sikuizi mnaiga wanaijeria hamna uhalisi wa kitanzania. Well, No shit Sherlock..Have you ever heard the term 'globalization'?
Mkuu nakuelewa sana unaposema kwamba lugha yoyote hukua. Lakini sikubaliani nawe unapotetea kwamba lugha sanifu ambayo tayari ipo kwenye matumizi iharibiwe eti huko ndiko kukua kwa lugha. Big NO!

Kukua kwa lugha huhusisha kuongeza misamiati mipya sio kupindisha misamiati ambayo tayari ipo na inaeleweka kwa wazungumzaji wa lugha husika. Kwa mfano huwezi kutetea kwamba mtu akitamka "kwendaga" badala ya "kwenda" au "sintokubali" badala ya sitakuballi". Hii haimaanishi kukuwa kwa lugha bali huo ni upotoshaji wa lugha unaopaswa kukemewa kwa nguvu zote.
 
Ni sawa wangeongea tu basi kiswahili. Shida wanajifanya na kiingereza wanajua ila kila wanalochomekea wanakosea!!!! Past tense, noun, verb, adverb havibadiliki hata miaka 500!!! Lugha za watu zina misingi yake mkuu kama huwezi hata basics ni kuachana nazo tu!!!
Again, inategemeana na hadhira. Kama hadhira ni waingereza wanaojali past tense, verb noun hapo atakuwa anakosea.
ila kama hadhira ni watu kama mwajuma wa mwabepande ambaye yeye kila siku anasema 'ofkozi mimi ni beuty' na jamii husika ndio inaelewa hivyo. Basi hata watangazaji wakisema hivyo sioni shida.

Kumbukeni jamani hizi lugha ni nothing but tools tu za kufikisha ujumbe.
Lugha zipo kwa ajili ya watumiaji na sio vice versa.

Kama wewe ukitumia kiswahili sanifu/fasaha kwa misamiati migumu na kuifanya majority ya jamii isikuelewe na mwingine akatumia kiswahili hiki kinachoongewa mtaani chenye mbwembwe na vikolombwezo 'shazi' halafu watu wakamuelewa. Aliyefikisha ujumbe zaidi ni yupi?

Angalieni kwanza hadhira inayokusudiwa ni ipi. Kama hadhira ni ya kimataifa kama BBC, basi wakifanya hivyo wanakosea.
Lakini kama kipindi husika kinaitwa XXL kwaajili ya vijana wa mtaani wanaondika sasa 'Xaxa'..inabidi mtindo uendane na vijana walengwa.
 
Mwijaku naye mtangazaji
Juma Lokole naye mtangazaji
Baba Levo
Orodha ni ndefu.

Hali ni shaghalabaghala
Kwakweli. Halafu kariba watangazaji wote kuna kamsemo kao wanakapenda. Utasika "Ee bana eeh" kila mtangazaji akianza kutangaza lazima aanze na neno "Ee bana eeh". Sijui ndio wanafundishwaga huko vyuoni kwao, au wanaigana. Sikapendi hako kamsemo basi tu.
 
Back
Top Bottom