Mwamuzi wa Tanzania
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 15,486
- 45,256
Habari!
Nilileta Uzi hapa kuonesha matumizi mabaya ya serikali, au niite matumizi yasiyo na msingi.
Semina ya sensa wiki tatu ilikuwa haina ulazima. Siku 3 tu zingetosha. Sasa ngoja nitoe mfano mmoja tu ili mjue kuwa serikali hii haina huruma na mwananchi.
Mwaka huu serikali ilikuwa na zoezi la post codes (anuani za makazi). Mabilioni yalitumika katika zoezi hili. Na sasa kuna zoezi la sensa nalo limetafuna mabilioni ya pesa.
Cha ajabu katika zoezi la sensa nalo kuna zoezi la kuhesabu makazi. Sasa kwanini zoezi la kuhesabu makazi lisingejumuishwa pamoja na zoezi la sensa?
Au kwanini zoezi la sensa libebe na bajeti ya kuhesabu makazi ilhali ndani ya mwaka huu huu tumetupa mabilioni mengine kwenye zoezi la kuhesabu makazi?
Ni dhahiri serikali hii imejaa watu wenye mawazo finyu na kutokujali.
Nilileta Uzi hapa kuonesha matumizi mabaya ya serikali, au niite matumizi yasiyo na msingi.
Semina ya sensa wiki tatu ilikuwa haina ulazima. Siku 3 tu zingetosha. Sasa ngoja nitoe mfano mmoja tu ili mjue kuwa serikali hii haina huruma na mwananchi.
Mwaka huu serikali ilikuwa na zoezi la post codes (anuani za makazi). Mabilioni yalitumika katika zoezi hili. Na sasa kuna zoezi la sensa nalo limetafuna mabilioni ya pesa.
Cha ajabu katika zoezi la sensa nalo kuna zoezi la kuhesabu makazi. Sasa kwanini zoezi la kuhesabu makazi lisingejumuishwa pamoja na zoezi la sensa?
Au kwanini zoezi la sensa libebe na bajeti ya kuhesabu makazi ilhali ndani ya mwaka huu huu tumetupa mabilioni mengine kwenye zoezi la kuhesabu makazi?
Ni dhahiri serikali hii imejaa watu wenye mawazo finyu na kutokujali.