Watanzania hatujachelewa; tuwekeze kwenye Cryptocurrencies!

Daaah uliiwahi mkuu! Tuendelee kupambana! Mimi plan yangu kwa sasa ni kutafuta coin zenye future nzuri niwekeze zaidi!!
 
Je wachina ni wajinga kukataa hizo coins na kuzipiga marufuku??

Je Mama Samia ni mjinga kuiambia benki kuu ya Tanzania ianze kujiandaa?


Je nchi kama Elsavado ambayo sio tu imeruhusu bali imeanza kutumia bitcoin kama legal tender nao wajinga?

Alafu tumalizie na hii...

Je gavana wa federal reserve (benki kuu ya USA) alipo sema hawana mpango wa kuzuia cryptoes nao wajinga??

Embu tufikirie pamoja mkuu!
 
Hizo coins zinazalisha nini hasa mpaka thamani yake inapanda hivyo?

Angalia hii...


Hii ni coin inaitwa Cardano, moja ya coin kongwe katika ulimwengu wa cryptoes!

Hapa waziri wa elimu nchini Ethiopia anaelezea jinsi walivyo toa tenda kwa coin ya cardano ili watengenezewe mfumo wa kumanage sekta ya elimu nchini mwao!!

Nami nimalizie na swali ulilo uliza...

Je Ethiopia nao ni wajinga kutumia cryptoes katika sekta ya elimu (moja ya sekta nyeti) katika nchi yao?

Embu tuendelee kuwaza pamoja...
 
Cryptocurrency Haina utapeli kama FOREX. Kwa hiyo Kama hujui tulia hivyo hivyo.

Afu uache kuandika maherufi makubwa.
hapa umejibu vizur sana! watu wanaijua forex tu ambayo vijana wengi wameangukia pua wakidhani watatoboa kumbe wanapigwa na kuishia kulia lia!! hawana elimu ya cryptocurrencies..cryptocurrencies sio utapeli hata kidogo na haina chembe hizo
 
Mkuu Upepo wa Pesa vipi naomba nipate mawazo yako kuhusu hii coin ya kuitwa pïcoin vipi una idea nayo?

Vipi unaonaje mtazamo WAKO future yake ni promising Au vipi?
 

Pia kuna coin kama SHIBA INU na dogecoin. Hizi ni nzuri lakini risky yake ni kubwa ila kama unaweza si vibaya pia ukaziangalia..
meme coins
 
Kusema kweli bado sijashawishika kuwekeza katika crypto business kwa kuwa security yake ni ndogo na pia Amna regulatory authority inayocontrol kwaio kuwekeza katika crypto ni lazma ujiridhishe juu ya usalama na udhibiti wake maana isije kuwa Kama miaka ya nyuma wale wazee wa dot-com
 
Kama unaamni katka crypto, af huamin forex akat zote ni financial markets na zina same strategies of trading them, unashangaza ndugu, hujui kitu, kifupi tu strategies ninazotumia kutrade forex I can use them to trade any financial markets
endelea na forex yako!! kuna jamaa zangu wanajuta!! najua kuwa cryptos zinatumika katika trading lakin cryptos ni nzuri kuliko hiyo forex yako ambao vijana wanaota utajili wa siku moja!! Hakunaga formula ya utajiri wa siku moja
 
Kama unaamni katka crypto, af huamin forex akat zote ni financial markets na zina same strategies of trading them, unashangaza ndugu, hujui kitu, kifupi tu strategies ninazotumia kutrade forex I can use them to trade any financial markets
Utofauti upo mkubwa tu usiwe too general!! Eti forex na Cryptos zina same trading strategies? Watu wanaunguza hela huko forex mtu anaweka ka milion kake kanaungua kote na kumwacha na madeni...Tafuta uzi humu jamaa analalamika jinsi forex ilivomuingiza kwenye mikopo..full madeni!! Alafu crptos zipo nyingi na watu wanakuja na projects zao e.g Pi coins, e.t.c
 
Mkuu Upepo wa Pesa vipi naomba nipate mawazo yako kuhusu hii coin ya kuitwa pïcoin vipi una idea nayo?

Vipi unaonaje mtazamo WAKO future yake ni promising Au vipi?

Kwa kweli sijawahi ichunguza ila nimeiangalia kwenye site ya coinmarketcap sioni data yoyote ya msingi kuhusu hii coin.

So sina cha kusema!
 
Duuh utakua wewe ni milionea mkubwa bila shaka aiseeh inaonekana unazijua vizur sana hizi mambo..una dollar za kutosha au maskini tu kama mimi unayejitahidi kujitutumua
 
huyu nadhani ni mkongwe kuliko wewe👇
 
Hizo coin zinajihusisha na shughuli gani ya uzalishaji mpaka nyie mpate hela??

Yaani inakuwaje uweke million alafu baada ya muda upate faida ya million nyingine labda? Naomba mnijulishe nifanye maamuzi
Mkuu hizi coin unapata faida pindi thamani inapopanda ...

Mfano Bitcoin 1 mwaka 2010 ilikuwa sawa na $230, lakini Sasa hivi Bitcoin moja ni sawa na $57,000 kwa hiyo Basi Kama uliweza kununu Bitcoin enzi hizo ukahold kwa Sasa wewe ni millionea mzuri tu ,huo ni mfano .....

Kuna coin zina project nzuri tu ,yaani hizo coin Kama Shiba Inu,Tron ,Solana,umi ,....na coin nyingine mbalimbali zinategemewa kuja kupanda Bei ,kufika mwaka 2030 mtu aliyenunua hizo coin atakuwa mbali Sana ,kwani Bei yake ya Sasa haitakuwa sawa na ya mwaka 2030 kabisa ...

Mfano
kwa Sasa 1shiba inu=$0.0000345. Huu ni mwaka 2021

Kufika 2030 ,kutokana na project ya shiba inu ,inaweza kuwa 1 Shiba = $1.3

Aise mtu aliyenunua shiba 3000 akauza 2030 kwa hio Bei hapo juu hampo nae Tena meza moja ,...

Note usifikili 2030 ni mbali ,.........





Coin zinapanda vipi ...demand and supply of coin ndio inasababisha coin kupanda na kushuka ....

Coin inaweza kupanda mwezi huu ,mwezi ujao ikashuka ,ikapanda tana ,ila baada ya miaka 7 hio coin lazima itakuwa mbali kutokana na project za mafounder na developers wa hio coin ..,


Hivyo Basi coin zenye project kila mwaka lazima dhamani itapanda ,hii haijarishi watu wanafanya exchange kidogo au kwa wingi ....

Ukitaka kufanya hii biashara ,Soma kwanza ,kuwa na uelewa ,usikurupuke kutanguliza hela ,Soma ,elewa ,changanua Mambo ,usiwe na tamaa ,hii biashara haiitaji tamaa ni project ya muda mrefu ,yaani unajiaandalia kuwa millionea miaka 10 ijayo ,hapa ndipo watu wanafeli Kwan wanataka vitu vya fasta ........


Note ,kutrade crypto currency ndio unaweza kupoteza pesa lakin kuhold coin. Hautakuja kupoteza hela ,ni sawa na kununua mahindi kuweka ndani huku unasubili Bei ipande uuze ( ndio maana ya kuhold coin ),narudia Tena mtu ambaya ana trade crypto ndio mwenye possibility kubwa ya kupoteza kiasi kikubwa cha pesa ......
 
shukrani, Admitted, hopefully I will go through it!
 
Umeeleza vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…