Kama Gadaffi alifanya ujinga kama huo haipaswi kuiga, sasa nini maana ya mawasiliano kama hamuelewani, wewe nikuulize maswali unijibu kwa lugha ambayo sina uelewa nayo na hakuna mkalimani, tutaonekana sote majuha. Labda ingeeleweka kama hao waandishi wangekuja kukuhoji kwenye nchi yako, hapo wao ndio waje na wakalimani maana uko kwako, wewe umekwenda kwenye nchi yao na haujui kutumia ipasavyo lugha wanayotumia, umewafuata wewe na huna mkalimani....
Hili mtajaribu kulikwepa kwa kuweka twist twist za kuponda kingereza eti cha mkoloni lakini mwisho wa siku ukweli uko pale pale, inafahamika mumeogopa kwenda Ulaya kwa kusingizia mnabana matumizi, ila tatizo linajulikana wazi kuwa lugha imewagomea, muajiri mkalimani hapo ikulu, kuna Watanzania japo wachache huwa wanaongea Kingereza kizuri tu, hivyo muwape ajira ili kuondoa aibu ndogo ndogo.