Elections 2010 Watanzania kwa nini tunakuwa wepesi kuamini uongo wa CCM?

Elections 2010 Watanzania kwa nini tunakuwa wepesi kuamini uongo wa CCM?

kwa nchi ambayo huduma sasa ziko katika hali mbaya mno, ni bora kukusanya malipo (japo kidogo) kwa wanaojiweza ili kuboresha huduma hizo hasa ikiwa nchi bado haijajipanga uzuri katika ukusanyaji wa mapato.

elimu bila ya malipo, huduma za fya bila ya malipo zitaendeshwa kwa mapato gani ikiwa bado nchi haijaweza kukusanya hata kodi kwa ufanisi?
 
Kiranga, Mkuu wangu hata sielewi unazungumza vitu gani. Hapa canada tuna mfumo huo na unafanya kazi vizuri sana kiasi kwamba tupo ranked juu tk Elimu, In fact nchi zenye kutoa elimu bure ndizo ziko ranked juu ya nchi nyinginezo ktk Elimu na hata Huma development index..
Wewe bado huoni kama mfumo huu ndio tutauhitaji kwa sasa kwa sababu umeweza kufanya kazi na matunda yakle yanaonekana?

Mkandara mkuu ninachosema ni kwamba Tanzania uchumi wetu mdogo na tuna kazi nyingi za kufanya kwa kila shilingi au dola yetu. Na hatuwezi kuwaiga wa Canada kwa sababu hatuna uchumi kama wao.

Canada inaweza kuwa na lofty all inclusive social programs kwa sababu imesha fika katika kiwango cha uchumi cha juu sana, Tanzania hatuwezi kusema tajiri na maskini wote tuwalipie kwa sababu uchumi wetu mdogo.

Mkuu usitake kuiga tembo mashonde utapasuka msamba.

Mimi nataka watu kama kina Mengi, Rostam Aziz na wengine wote wenye uwezo wa kujilipia wajilipie, maana wasipojilipia ndio wanachukua nafasi za wakulima ambao hawana option nyingine. Hao wengine wasiojiweza wapetesheni tu, nchi yetu ina masikini wengi bado. Is that too much to ask for ?
 
Mimi kamwe sikubaliani au kupingana na mtu, nakubaliana au kupingana na jambo, dhana, kwa kuangalia mantiki.

Ndiyo maana mambo mengine nakubaliana na CHADEMA, mengine napingana nao. Na Mwalimu naye ni hivyo hivyo, kuna mengine nakubaliana naye, mengine sikubaliani naye. Wasioelewa hili hawawezi kunielewa.

Ukiona watu wanakubaliana kila kitu ujue kuna wengine wanaburuzwa hapo.

Haya mkuu, hapa nimekubaliana nawewe (oopppsss na jambo ulilosema). Nachelea hii itatutoa kwenye topic at hand.

Naona Bob kakupa issues za Canada hapo.
 
Mkandara mkuu ninachosema ni kwamba Tanzania uchumi wetu mdogo na tuna kazi nyingi za kufanya kwa kila shilingi au dola yetu. Na hatuwezi kuwaiga wa Canada kwa sababu hatuna uchumi kama wao.

Canada inaweza kuwa na lofty all inclusive social programs kwa sababu imesha fika katika kiwango cha uchumi cha juu sana, Tanzania hatuwezi kusema tajiri na maskini wote tuwalipie kwa sababu uchumi wetu mdogo.

Mkuu usitake kuiga tembo mashonde utapasuka msamba.

Mimi nataka watu kama kina Mengi, Rostam Aziz na wengine wote wenye uwezo wa kujilipia wajilipie, maana wasipojilipia ndio wanachukua nafasi za wakulima ambao hawana option nyingine. Is that too much to ask for ?

Mbona hutaki kuaddress issue ya Kenya, Namibia, na mifano mingine iliyotolewa hapo juu?
 
kwa nchi ambayo huduma sasa ziko katika hali mbaya mno, ni bora kukusanya malipo (japo kidogo) kwa wanaojiweza ili kuboresha huduma hizo hasa ikiwa nchi bado haijajipanga uzuri katika ukusanyaji wa mapato.

elimu bila ya malipo, huduma za fya bila ya malipo zitaendeshwa kwa mapato gani ikiwa bado nchi haijaweza kukusanya hata kodi kwa ufanisi?

Nchi ambayo ina mashangini elfu moja na ushee, ndege ya raisi (mbili to be correct), inanunua rada kwa mabilioni. Je sh bilioni mia moja kwa mwaka (this is still alot for a mere estimation) ni pesa nyingi kiasi hicho?

Let's be serious guys.... kwa nini tushindwe, just tell me why we cant afford this. Give just one reason
 
Mbona hutaki kuaddress issue ya Kenya, Namibia, na mifano mingine iliyotolewa hapo juu?

Just because anybody is doing it it does not mean it is right.

Ukiangalia nafasi za elimu ya umma kama ziko limited, ukawaangalia masikini kama watu wasio na option zaidi ya nafasi hizi za elimu ya umma, na ukawaangalia matajiri / wenye uwezo wa kujilipia kama watu walio na option ya kwenda kwenye private institutions au kujilipia, huwezi kupinga wazo la kuwalipisha wenye uwezo wa kulipa.
 
hebu tutizame kwa upana kidogo .........

mapato kwanza mie nayapa kipa umbele yende kwenye afya ( na grants za elimu kwa wasiojiweza)

tukitizama afya kuna sehemu hakuna hata zahanati achilia mbali hospitali. Hospitali za rufaa nazo ziko taabani.....kuna na suala la dawa pia.

sasa hapo kwanza tujiulize mashangingi hayo elfu kadhaa na ndege mbili za raisi zinatosha walau kufanya hali ikawa bora?
 
Just because anybody is doing it it does not mean it is right.

Ukiangalia nafasi za elimu ya umma kama ziko limited, ukawaangalia masikini kama watu wasio na option zaidi ya nafasi hizi za elimu ya umma, na ukawaangalia matajiri / wenye uwezo wa kujilipia kama watu walio na option ya kwenda kwenye private institutions au kujilipia, huwezi kupinga wazo la kuwalipisha wenye uwezo wa kulipa.

It is not about anybody doing it, it is about somebody doing it successfully.

Kama hii ingekuwa case, nchi kama kenya zilizoanzisha elimu ya bure, watoto wa matajiri wangejaa kwenye shule za serikali na kuwanyima masikini nafasi. That has not been the case so far. Kwa nini tuongelee mifano ambayo haipo?
 
It is not about anybody doing it, it is about somebody doing it successfully.

Kama hii ingekuwa case, nchi kama kenya zilizoanzisha elimu ya bure, watoto wa matajiri wangejaa kwenye shule za serikali na kuwanyima masikini nafasi. That has not been the case so far. Kwa nini tuongelee mifano ambayo haipo?

And who with our type/ size of economy is doing it successfully ?

Kwa nini uruhusu system ambayo hata watoto wachache wa matajiri wasiotaka kutumia pesa zao kwenye private institutions waweze kuchukua nafasi zinazoweza kwenda kwa watoto wasio na uwezo ?

Sababu inayofanya matajiri wasitake kuweka watoto zao kwenye hizi public institutions ni efficiency. Zikianza kuwa na efficiency sawa/ kuzidi private institutions (which should be the goal from day one) matajiri wengi watakosa incentive ya kuwapeleka watoto wao kwenye private institutions.

So basically ukisema utengeneze system ya elimu bora kwa wote bila kujali need ukitegemea matajiri hawatakuja unachosema ni kwamba unatengeneza system ambayo itakuwa mediocre. Anything worth doing is worth doing well. Kwa nini mnataka kuwa shortchange wasio na uwezo.
 
hebu tutizame kwa upana kidogo .........

mapato kwanza mie nayapa kipa umbele yende kwenye afya ( na grants za elimu kwa wasiojiweza)

tukitizama afya kuna sehemu hakuna hata zahanati achilia mbali hospitali. Hospitali za rufaa nazo ziko taabani.....kuna na suala la dawa pia.

sasa hapo kwanza tujiulize mashangingi hayo elfu kadhaa na ndege mbili za raisi zinatosha walau kufanya hali ikawa bora?

Gaijin,

Twende kwa numbers if we may, elimu bure itagharimu kiasi gani. Kuna mtu hapo juu kaonesha kuwa ni kama bilioni 52. Mimi naweka namba hiyo katika bilioni 100. Bado Tanzania yaweza kufanya hili na pia ikajenga zahanati na vingine.

kwa nini msisitizo uko kwenye shule katika hii mada? Kwa sababu kila mtoto anategemewa kwenda shule. Shule ni kati ya mahitaji muhimu ya binadamu wa leo. Ingawa sio kila mtu anategemea kuugua, watoto wote wanategemewa kusoma.

Twaweza fanya vyote, kwa nini hii negativity kuwa hatuwezi?
 
And who with our type/ size of economy is doing it successfully ?

R U serious about this? Now you want to compare "things" with the people of your size? What about higher standards you always stand for in this forum?

You keep saying that CHADEMA should do better than ccm (means when compared with ccm, they should be better than ccm) and yet you want to compare Tanzania with some country of her size?!
 
R U serious about this? Now you want to compare "things" with the people of your size? What about higher standards you always stand for in this forum?

You keep saying that CHADEMA should do better than ccm (means when compared with ccm, they should be better than ccm) and yet you want to compare Tanzania with some country of her size?!

Kuna vitu fulani havigharimu dola au shilingi, hivi unaweza kusema nataka Tanzania iwe sawa na Marekani. Freedom of expression haigharimu resources, kwa hiyo nikilinganisha Tanzania na Marekani sawa.

Hizi habari za elimu bure kwa wote zinagharimu resources, resources ambazo zinatakiwa sehemu nyingine.Kwa hiyo huwezi kulinganisha ambition za welfare system ya nchi masikini na nchi tajiri, hapa ndipo naongelea swala la political populism vs applied economics.

CHADEMA doing better than CCM should include a better management and allocation of our limited resources.

From this issue alone, it seems kwamba CCM wanakuwa progressives kwa maana ya kwamba wanaonekana kukubali kwamba zama za elimu bure kwa wote zimeisha, tunaingia katika dunia mpya ambayo kama anavyosema Nyerere hapo juu ina mamilionea wa Kitanzania, wajilipie. Sikatai kuwalipia wasiojiweza, lakini na hawa mamilionea nao? Na watu wengine wanaoweza kujilipia je ?

CHADEMA inaonekana kuturudisha kwenye siasa za Ujamaa, siasa za serikali kukulipia kila kitu, whether unahitaji kulipiwa au huhitaji. Siasa hizi, hususan kwa nchi masikini, invariably huwa zinaleta a "tragedy of the commons" effect. Tragedy hii inatupeleka kwenye catch-22 ya kwamba, tukiwa na mfumo mzuri wa elimu ya umma, kuna masikini wataukosa kwa sababu wenye uwezo wameingia, sababu itakayofanya wenye uwezo waukimbie mfumo huu ni kama utatoa elimu mbovu, kwa hiyo hata wenye uwezo wakiwa wachache, masikini hawatafaidika kwa sababu elimu yenyewe itakuwa mbovu.


Kwa hiyo CHADEMA haionyeshi kuishinda CCM katika kutoa uongozi unaoendana na challenges za dunia ya leo, kwa sababu inaonekana either haielewi issues au inaelewa inataka kuendekeza populism.

Uchumi wetu unataka serikali itakayojua kusimamia matumizi ya pesa zetu chache vizuri zaidi, siyo serikali itakayotoa freebies kwa wote bila kujali kama walengwa wanahitaji hizi freebies au la.
 
Kwa nini uruhusu system ambayo hata watoto wachache wa matajiri wasiotaka kutumia pesa zao kwenye private institutions waweze kuchukua nafasi zinazoweza kwenda kwa watoto wasio na uwezo ?

Kwa sababu nchi zote zilizoruhusu hii system, matajiri wengi hawakwenda kwenye hizo shule za bure. Walibaki kwenye shule zao za kitajiri (za kulipia)

Sababu inayofanya matajiri wasitake kuweka watoto zao kwenye hizi public institutions ni efficiency. Zikianza kuwa na efficiency sawa/ kuzidi private institutions (which should be the goal from day one) matajiri wengi watakosa incentive ya kuwapeleka watoto wao kwenye private institutions.

Umeanza kubadili theme ya debate ....ukitaka kujadili efficiency, sema tu na nitajiunga kwenye new debate. Hiki nacho kitatokea Tanzania, matajiri wa Tanzania, kama matajiri wengine wote duniani, wataendelea na shule zao za private bila kujali kuwa public schools ni bure.

So basically ukisema utengeneze system ya elimu bora kwa wote bila kujali need ukitegemea matajiri hawatakuja unachosema ni kwamba unatengeneza system ambayo itakuwa mediocre. Anything worth doing is worth doing well. Kwa nini mnataka kuwa shortchange wasio na uwezo.

Hizi ni bangeeeee... na kama kawaida yangu sibishaniii bangeee.
Soma post ya mkandara kuhusu elimu ya Canada na sio kuweka vitu visivyo na evidences yoyote ile.
 
CHADEMA doing better than CCM should include a better management and allocation of our limited resources.

Unaanza kubishania hadi mifano

From this issue alone, it seems kwamba CCM wanakuwa progressives kwa maana ya kwamba wanaonekana kukubali kwamba zama za elimu bure kwa wote zimeisha, tunaingia katika dunia mpya ambayo kama anavyosema Nyerere hapo juu ina mamilionea wa Kitanzania, wajilipie. Sikatai kuwalipia wasiojiweza, lakini na hawa mamilionea nao? Na watu wengine wanaoweza kujilipia je ?

Hili swali la mamilionea umelijibu mwenyewe hapo juu

CHADEMA inaonekana kuturudisha kwenye siasa za Ujamaa, siasa za serikali kukulipia kila kitu, whether unahitaji kulipiwa au huhitaji.

Kwa hiyo CHADEMA haionyeshi kuishinda CCM katika kutoa uongozi unaoendana na challenges za dunia ya leo, kwa sababu inaonekana either haielewi issues au inaelewa inataka kuendekeza populism.

Kama ujamaa huo umefanikiwa Canada, Marekani, Ulaya na kwingineko, I am for that na ninawapongeza chadema kwa kufuata mafanikio ya wajamaa wa ulaya magharibi na america

Uchumi wetu unataka serikali itakayojua kusimamia matumizi ya pesa zetu chache vizuri zaidi, siyo serikali itakayotoa freebies kwa wote bila kujali kama walengwa wanahitaji hizi freebies au la.

Hii sio freebies Kiranga, an educated population is the best resource you can have in a country .. dont forget that fact
 
BTW -- Gaijin hapo juu anaongelea health system inayogharimiwa na serikali. What's your take on that?
 
BTW -- Gaijin hapo juu anaongelea health system inayogharimiwa na serikali. What's your take on that?

Kabla ya kuongelea health/ education system ya serikali, inabidi uwe na serikali. Sie hatuna serikali.

Kabla ya serikali, inabidi uwe na vyama, sie hatuna vyama, upinzani wala CCM.

Kabla ya vyama vya siasa, inabidi uwe na ideologies, sie hatuna hata ideologies. Ideology ya CCM ni contradiction. Huko upinzani ndiko kabisaa hata hawaeleweki wanasimamia nini. Leo watakwambia mrengo wa kulia kesho wanataka free education for all.

You gotta miss Kolimba.
 
Kabla ya kuongelea health/ education system ya serikali, inabidi uwe na serikali. Sie hatuna serikali.

Kabla ya serikali, inabidi uwe na vyama, sie hatuna vyama, upinzani wala CCM.

Kabla ya vyama vya siasa, inabidi uwe na ideologies, sie hatuna hata ideologies. Ideology ya CCM ni contradiction. Huko upinzani ndiko kabisaa hata hawaeleweki wanasimamia nini. Leo watakwambia mrengo wa kulia kesho wanataka free education for all.

You gotta miss Kolimba.

I gotta mrs Kolimba,

Mirengo ya kulia katika nchi za kibepari imeishi na free education for all kwa miaka karibu 50 sasa. Na kwa jinsi nilivyomfuatilia PM Brown wa UK wakati wa debate na baada ya kukamata uongozi, torries hawaonekani kama wataachana na free education (achilia mbali health system) in the near future.

Unachokiadvocate hapa, hakijatokea nchi yoyote iliyoendelea. Nchi zilizoendelea zimegundua umuhimu wa an educated population na wanafanya kila wanachoweza kuelimisha kila mtu.
 
Mkandara mkuu ninachosema ni kwamba Tanzania uchumi wetu mdogo na tuna kazi nyingi za kufanya kwa kila shilingi au dola yetu. Na hatuwezi kuwaiga wa Canada kwa sababu hatuna uchumi kama wao.

Canada inaweza kuwa na lofty all inclusive social programs kwa sababu imesha fika katika kiwango cha uchumi cha juu sana, Tanzania hatuwezi kusema tajiri na maskini wote tuwalipie kwa sababu uchumi wetu mdogo.

Mkuu usitake kuiga tembo mashonde utapasuka msamba.

Mimi nataka watu kama kina Mengi, Rostam Aziz na wengine wote wenye uwezo wa kujilipia wajilipie, maana wasipojilipia ndio wanachukua nafasi za wakulima ambao hawana option nyingine. Hao wengine wasiojiweza wapetesheni tu, nchi yetu ina masikini wengi bado. Is that too much to ask for ?
Mkuu wangu labda unajichanganya.. hakuna mahala popote Dr.Slaa na Chadema wamesema watazifunga shule za Private wala hakuna nchi inayotoa elimu bure wamefunga shule za Private ikiwa ni pamnoja na Canada. Na hata kiuchumi, nchi za Kikomunist hazikukataza mtu kuwa na biashara binafsi kabisaaa, au mtu kuwa na kitu Private kwa sababu ati Ukomunist unasema uchumi wa nchi hizo utakuwa controlled na Government..

Sii kweli hata huko zilikuwepo biashara za watu binafsi iwe elimu au Hospital na hata wakati wa Nyerere zilikuwepo shule Private nyingi zikiendesha education kama biashara lakini walilazimika kufanya vizuri zaidi ili kuwavuta wananchi toka shule za Serikali (bure). Hospitali vile vile Hindu Mandal haikuanza jana.. na ndivyo ilivyo hata hapa Canada, UK, US au nchi za Nordic zipo shule za Private isipokuwa zinakuwa na ushindani mkubwa toka shule za serikali hivyo bar ya elimu bora inakuwa raised kila ushindani unapozidi toka upande wa bure.

Ndivyo walivyoweza kufadanikiwa wenzetu na sio swala la Utajiri au nini tena wao ndio naweza kusema Elimu kwao ni Unachukua sehemu ndogo sana ya Bajeti kuliko mipango ya wizara nyinginezo ambapo Exploration au case study pekee inaweza chukua mabillioni ya fedha..Kwa hiyo Elimu kwao ni bure sio kwa sababu ni matajiri laa hasha kwa sababu Elimu ni RIGHT ya kila mwananchi (necessity) ktk maendeleo ya binadamu kwani ndio chanzo cha maendeleo ya nchi. Na wengine wameweka kwamba elimu ni privilege hivyo sii lazima kuwa na za bure kwa sababu wananchi wake walio wengi wanajiweza.

Leo wewe una taifa lenye wananchi wenye kipato cha average ya dollar moja kwa siku, wanashindwa hata kuweka mkate mezani unakuja watoza fedha ukifikiria kwamba unajenga?..Mkapa mbona alishindwa na elimu ya msingi tu.. au mmesahau matokeo ya elimu wakati wake..Na how come toka tumefanya hivyo miaka 20 iliyopita mbona Elimu nchini ndio inazidi kuporomoka..Au kipimo cha Mtanzania ni hicho kiingereza? maanake siku hizi wazazi Bongo akimsifia mwanaye kuwa ana akili sana ni kwa sababu anazungumza kiingereza!.. Elimu Bongo imekuwa lugha ya kiingereza ambacho Ukija huku Canada au USA utachekwa na hizo chicken 'n Chips, I shall - should, Petrol, Spanner, Trouser na kadhalika..


Mkuu wangu, historia ya Elimu duniani nchi nyingi kama sii zote zimeanza na mfumo huu wa Elimu bure kisha baada yake ndio wameanza kuingia ktk hatua ya kulipa kwa hatua na kama sikosei hata Marekani wenyewe shule bado nyingi sana ni bure. Naweza kusema kuna shule nyingi za bure sawa au zaidi ya za kulipa (To highschool) na wamegundua kwamba hata mfumo wao wa Elimu ni mbaya sana kiasi kwamba wanashuka rank pamoja na kuwa na shule nyingi na nzuri kuliko sehemu yoyote duniani.

Hapa nikiwa na maana hata hizo nchi zilizoendelea wanazo shule za bure kwa sababu hakuna taifa lolote ambalo tayari limeondoa tabaka za wananchi wake..Elimu sio swala la matabaka ila ni RIGHT ya kila mwananchi hivyo uwe tajiri au maskini haijalishi kipato kama kwenda choo vile. Huwezi poasuka msamba kushusha kipudu kama Rostam sana sana yeye anakula pilipili zaidi..

Mkuu wangu it's only less than 10% ndio matajiri wanao control uchumi wa nchi zetu iwe hiyo Marekani, Uingereza, Japan na kokote uendako utakuwa matajiri hawajai mkononi.. na Utajiri wa hawa watu unategemea Uzalishaji na Consumers power ambao wote wanahitaji elimu kuwawezesha..Kumbuka tu kwamba human development inaanza na elimu, hata dini zetu zimetusisitiza hivyo laa sivyo tungekuwa bado tunaamini Mitunga..

Mkuu wangu Tanzania Matajitri hawafiki hata asilimia 1 ya population na hiyo middle class ni chini ya asilimia 10 wakati una maskini wasikipungua asilimia 80. Rais wako mwenyewe amnakataa kuongeza mshahara kufikia Tsh 315,000 kwa mwaka ambazo ni sawa na Dollar 300 (less than), leo unategemea mtu anayepokea Mshahara wa Tsh 120, 000 kwa mwaka kulipia ada ya mtoto au watoto wake inayodzidi Tsh. 50,000? Hii akili kweli mkuu wangu.

Haya ni kiasi gani basdi tunachozungumzia? Ikiwa leo serikali inamtoza mtoto mmoja Tsh 50,000 hadi 100,000 hizi zinaleta tofauti gani ktk uwezo wa serikali ambayo tunaambiwa inakusanya kodi toka kwa wateja wasiozidi millioni 2!.

Wewee mwenyewe unaona misamaha ya kodi mahotel yanajengwa na kila baada ya miaka mitano ownership inabadilishwa kwa kuwezeshwa na serikali iliyopo. Tender ya bomba la mafuta toka Dar hadi Mwanza wanachukua wao hapa utategemea kodi gani kukusanywa! Haya majuzi tu umeona mkataba wa Umeme toka Millenium unarudi kupewa shirika la kwao badala ya Tanesco, halafu mtakuja sema hata Tanesco haiwezekani.Wala sintashangaa kama ile mitambo ya Dowans inafanya kazi leo na kulipwa mabillioni ya fedha.. Tazama mikataba feki mkuu wangu bado unaweza sema ati sisi ni maskini wakati tunaweza kujenga banki Kuu kwa gharama inayozidi Usd 500, millioni.. twintower zisizozidi ghorofa 20 each. hatufahamu mishahara wala posho za viongozi ni siri kweli hii nchi mkuu wangu... aaah niache miye nisije fika kusikotakiwa...
 
Mkandara,

Kiranga anasema kuwa, kwa vile hatuna serikali, vyama na ideology kwa standard yake, basi tuachane kabisaaa na investment kwenye human resource. Kwa maoni yake, ni upotevu wa pesa za serikali kutoa elimu ya msingi kwa raia wa nchi yako.

ohhhh then... I give up
 
Mkuu wangu labda unajichanganya.. hakuna mahala popote Dr.Slaa na Chadema wamesema watazifunga shule za Private wala hakuna nchi inayotoa elimu bure wamefunga shule za Private ikiwa ni pamnoja na Canada. Na hata kiuchumi, nchi za Kikomunist hazikukataza mtu kuwa na biashara binafsi kabisaaa, au mtu kuwa na kitu Private kwa sababu ati Ukomunist unasema uchumi wa nchi hizo utakuwa controlled na Government..

Mkuu kabisa Bob Mkandara, naona kama kujichanganya unajichanganya wewe, naomba unielimishe kuna sehemu gani nimesema CHADEMA watafunga shule za private, hii dhana unaipata wapi?

Sii kweli hata huko zilikuwepo biashara za watu binafsi iwe elimu au Hospital na hata wakati wa Nyerere zilikuwepo shule Private nyingi zikiendesha education kama biashara lakini walilazimika kufanya vizuri zaidi ili kuwavuta wananchi toka shule za Serikali (bure). Hospitali vile vile Hindu Mandal haikuanza jana.. na ndivyo ilivyo hata hapa Canada, UK, US au nchi za Nordic zipo shule za Private isipokuwa zinakuwa na ushindani mkubwa toka shule za serikali hivyo bar ya elimu bora inakuwa raised kila ushindani unapozidi toka upande wa bure.

Elimu ya umma inaweza kutoa ushindani kwa private institutions bila kumpa nafasi milionea asome bure, tuna wasioweza kujilipia wengi tu wa kujaza system ya elimu ya umma.

Ndivyo walivyoweza kufadanikiwa wenzetu na sioo swala la Utajiri au nini tena wao ndio naweza kusema Elimu kwao ni Unachukua sehemu ndogo sana ya Bajeti kuliko mipango ya wizara nyinginezo ambapo Exploration au case study pekee inaweza chukua mabillioni ya fedha..Kwa hiyo Elimu kwao ni bure sio kwa sababu ni matajiri laa hasha kwa sababu Elimu ni RIGHT ya kila mwananchi (necessity) ktk maendeleo ya binadamu kwani ndio chanzo cha maendeleo ya nchi. Na wengine wameweka kwamba elimu ni privilege hivyo sii lazima kuwa na za bure kwa sababu wananchi wake walio wengi wanajiweza.

Nimeeleza hapo juu kuhusu rights zenye gharama na zisizo gharama. Free speech as a right is not the same as education as a right.Moja haihitaji resources, nyingine inahitaji.Tukishakuwa na kitu kinahitaji resources tu inabidi tuingie katika budget and maximum allocation of resources, hii hairuhusu kuwapa wawezao kujilipa free ride.

Leo wewe una taifa lenye wananchi wenye kipato cha average ya dollar moja kwa siku, wanashindwa hata kuweka mkate mezani unakuja watoza fedha ikifikiria kwamba unajenga?.. Na how come toka tumefanya hivyo miaka 20 iliyopitya mbona Elimu nchini ndio inazidi kuporomoka..Au kipimo cha Mtanzania ni hicho kiingereza? maanake siku hizi wazazi Bongo akimsifia mwanaye kuwa ana akili sana ni kwa sababu anazungumza kiingereza!.. Elimu Bongo imekuwa lugha ya kiingereza ambacho Ukija huku Canada au USA utachekwa na hizo chicken 'n Chips, I shall, Petrol, Spanner, Trouser na kadhalika..

Hapa ndipo Bob unajionyesha kabisa hujanifuatilia wala kunisoma kabisa, nimerudia mara elfu moja na moja humu kwamba wasiojiweza wasaidiwe, sina tatizo na hilo, ila tatizo langu kuwalipia watu wanaojiweza. Nime argue kwamba elimu bora kwa wote itawapendelea wanaojiweza at the expense of wasiojiweza, kwa sababu wanaojiweza wana option, wasiojiweza hawana option, sasa kwa nini uachie kiti cha bure kiende kwa mtu mwenye option wakati kuna mtu hana option?

Ni sawa na uwe kwenye msiba, mnaenda mazikoni, kuna watu kibao, wengine wana magari yao binafsi na wengine hawana magari yao binafsi. Halafu kunatolewa usafiri wa bure wa mabasi kuwafikisha watu makaburini, halafu atokee mtu kusema ni sawa tu kwa watu wote kupanda basi la bure, bila kujali kama wana uwezo wa kutumia magari yao binafsi au la. Hii system haitumii resources vilivyo kwani wenye magari yao binafsi ambao hawana huruma wanaweza kusema ngoja tupande gari la bure, halafu wengine ambao hawana magari binafsi wakakosa usafiri pekee uliokuwapo kwao. Hii ndiyo beef yangu, nataka hawa wenye uwezo watumie uwezo wao, wasipewe free ride tu.

Mkuu wangu, historia ya Elimu duniani nchi nyingi kama sii zote zimeanza na mfumo huu wa Elimu bure kisha baada yake ndio wameanza kuingia ktk hatua ya kulipa kwa hatua na kama sikosei hata Marekani wenyewe shule bado nyingi sana ni bure. Naweza kusema kuna shule nyingi za bure sawa au zaidi ya za kulipa (To highschool) na wamegundua kwamba hata mfumo wao wa Elimu ni mbaya sana kiasi kwamba wanashuka rank pamoja na kuwa na shule nyingi na nzuri kuliko sehemu yoyote duniani.

Na sisi tulipitia huko kwenye elimu bure, tukaona UPE ya limited resources na na demand kubwa ilivyotupa madarasa ya watu 120, mchizi anasoma mwaka mzima mwalimu wake wa darasa hamjui hata jina. Matatizo yetu ya kielimu ya sasa yamerithi mengi kutoka mfumo huu, kwa nini tunataka kudekeza mambo yaliyopitwa na wakati ? Hususan kama tuna njia ya kupunguza makali ya pressure ya demand kwenye hii system ?

Hapa nikiwa na maana hata hizo nchi zilizoendelea wanazo shule za bure kwa sababu hakuna taifa lolote ambalo tayari limeondoa tabaka za wananchi wake..Elimu sio swala la matabaka ila ni RIGHT ya kila mwananchi hivyo uwe tajiri au maskini haijalishi kipato kama kwenda choo vile. Mkuu wangu it's only less than 10% ndio matajiri wanao control uchumi wa nchi zetu iwe hiyo Marekani, Uingereza, Japan na kokote uendako utakuwa wanao control uchumi hawajai mkononi na Utajiri wa hawa watu unategemea Uzalishaji na Consumers ambao wote wanahitaji elimu kuwezesha..Kumbuka tu kwamba human development inaanza na elimu, hata dini zetu zimetusisitiza hivyo laa sivyo tungekuwa bado tunaamini Mitunga..

Tangu juu umeonekana hukunielewa, sina tatizo na shule za bure, tatizo langu ni eligibility ya kukubalika katika shule hizi. Sikubali mtu mwenye uwezo aende kusoma shule ya bure. Kama elimu ni right, jua pia kwamba inalipiwa na ujue namna bora kabisa ya kuilipia.

Mkuu wangu Tanzania Matajitri hawafiki hata asilimia 1 ya population na hiyo middle class ni chini ya asilimia 10 wakati una maskini wasikipungua asilimia 80. Rais wako mwenyewe amnakataa kuongeza mshahara kufikia Tsh 315,000 kwa mwaka ambazo ni sawa na Dollar 300 (less than), leo unategemea mtu anayepokea Mshahara wa Tsh 120, 000 kwa mwaka kulipia ada ya mtoto au watoto wake inayodzidi Tsh. 50,000? Hii akili kweli mkuu wangu.

Hata kama angekuwa tajiri mmoja tu, jifikirie wewe ndiye maskini ambaye unakosa kusoma kwa sababu tajiri mmoja kachukua nafasi yako, utaona sawa hilo ?

Haya ni kiasi gani basdi tunachozungumzia? Ikiwa leo serikali inamtoza mtoto mmoja Tsh 50,000 hadi 100,000 hizi zinaleta tofauti gani ktk uwezo wa serikali ambayo tunaambiwa inakusanya kodi toka kwa wateja wasiozidi millioni 2!.

Inabidi tujenge utamaduni wa matumizi mazuri ya fedha hata kama ni shilingi moja tu, haba na haba hujaza kibaba waswahili walisema.

Wewee mwenyewe unaona misamaha ya kodi mahotel yanajengwa na kila baada ya miaka mitano ownership inabadilishwa kwa kuwezeshwa na serikali iliyopo. Tender ya bomba la mafuta toka Dar hadi Mwanza wanachukua wao hapa utategemea kodi gani kukusanywa! Haya majuzi tu umeona mkataba wa Umeme toka Millenium unarudi kupewa shirika la kwao badala ya Tanesco, halafu mtakuja sema hata Tanesco haiwezekani.Wala sintashangaa kama ile mitambo ya Dowans inafanya kazi leo na kulipwa mabillioni ya fedha.. Tazama mikataba feki mkuu wangu bado unaweza sema ati sisi ni maskini wakati tunaweza kujenga banki Kuu kwa gharama inayozidi Usd 500, millioni.. twintower zisizozidi ghorofa 20 each. hatufahamu mishahara wala posho za viongozi ni siri kweli hii nchi mkuu wangu... aaah niache miye nisije fika kusikotakiwa...

Two wrongs do not make a right, misamaha ya kodi holela ni mibaya, tuipinge, tusitake kuihalalisha zaidi kwa kuleta mfumo usio na mahesabu ya kiuchumi, tutakuwa tunaongeza tatizo, sio kutatua tatizo
 
Back
Top Bottom