Watanzania kwa pamoja tuzilinde rasilimali zetu za nchi kwa pamoja na kwa wivu mkubwa sana

Watanzania kwa pamoja tuzilinde rasilimali zetu za nchi kwa pamoja na kwa wivu mkubwa sana

Wtz inabidi tuchukue hatua ya kiwazuia hawa viongozi majangili.tufanya maandamano yasiyo na kikomo kupinga matendo mabaya yanayofanywa na hawa majangili.kwanza hatujawachagua.sudani wameweza,congo wanapambana kwa nini sisi tusiweze?matumizi mabayavya rasilimali sasa basi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Lazima tuweke miguu chini tuwaambie hapana si lazima kuandamana ila hata kwa kuoaza sauti hivi naamini wanatusikia. Ki ukweli hii awamu inahitaji uangalizi wetu sote watanzania .hiki ni kitu kizito kwetu
 
Afrika ni bara vulnerable sana linapokuja suala la rasilimali zake. Sababu ni kutokana na viongozi wasiokuwa na uadirifu na kutokuwa na uzarendo.
Leo nimekutana na waraka wa serikali unaoruhusu uuzwaji wa wanyamapori. kwa u vulnerable ule ule ni lazima hii iwe work up call kwani serikali ni serikali hii hii ilifanya zuio hilo. Tulishawahi kupigwa kwa kuwasafirisha Twiga wetu bila kujua wanaenda wapi.
Si ajabu kila mmoja anajua kuwa kwa sasa tushaanza kuwa Darling wa mataifa ambayo hatuna record nzuri tangu enzi za chief Mangungo mpaka leo juu ya rasilimali. No wonder huo u sweetheart na udarling ukatupofusha pakubwa.
Naomba kwa pamoja hili Tangazo la kuuza hawa viumbe wetu aliotujalia mola iwe work up call kuhakikisha kwa pamoja na kwa wivu mkubwa tusifikie kale ka hatua ka kupeleka Twiga kusikojulikana.
Ni kama mwezi tangu jabari la vito linalodhaniwa kutoka Tanzania lilionekana Dubai japo hatujapata mrejesho ulio clear kuwa linatuhusu ama la.
Kwa kuwa prevention is better than cure ,watanzania tufungue mboni zetu maana hii yaweza kuwa loop hole ya kupigwa kivingine .
Acha upotoshaji Mzee,kama ni twiga wapo Dunia nzima kama tuu kwa aina nyingine nyingi za wanyama..

Pili kama ni biashara ya wanyama hai iko Dunia nzima wala haijaanza Tanzania ndio maana kuna vitalu vya uwindaji na mabucha rasmi ya nyama pori..

Biashara hii ilikuwepo kitambo na ilipigwa marufuku mwaka 2015 kutokana na kukiukwa kwa masharti na uhuni wa kusafirisha Wanyamapori wasioruhusiwa..

Ikumbukwe kwamba miaka hiyo hakukuwa na mbinu thabiti za udhibiti na ulinzi kama ilivyo sasa,mfano jeshi usu ni full combat kwa ajili ya ulinzi wa maliasili..

Kwa sasa ikitokea uhuni kama ule ujue ni mbinu rasmi..Hata hivyo naona serikali imeruhusu Kwa miezi 6 tena Kwa wanyama ambayo waliathirika baada ya ile marufuku Kwa sababu waliooewa vibali walikuwa wamelipia kabisa.
 
Back
Top Bottom