Watanzania msibabaishwe na maisha ya Marekani. Wamarekani wengi ni choka mbaya, hawana uwezo wa kumiliki nyumba kama ninyi, wanaishi kwenye kota

Na maisha utapata na nyumba utajenga nina uhakika ndugu yangu, hapa Tz utatoboa
Labda utoboe katiba na sheria ndiyo utatoka kimaisha, kinyume na hapo sahau. Hata wewe kama ni kweli uliishi ulaya au US basi tambua kilichokufanya utusue siyo kuishi bongo bali ni exposure na capital uliyoipata nje ya bongo.

Ushauri wangu ni kwamba, hizi siyo zama za kuzubaisha akili za watu, waacheni waende popoye wanapoweza kutafuta kihalali wakatafute.

Hata wewe ulipoamua kwenda bongo bado haukwenda Kijijini kwa mababu zako.
 
Asee tuwe serious Chris Brown anadaiwa mkopo naona ndo utamuua, ile nchi isikie kwenye Tv gusa unase. Mm nayosema hapa sio kichaa nimeishi pale muda mrefu na nimeondoka baada ya kugundua kwa Mwaka ile nchi inanichukulia 30M, pale nmeishi kwenye single room lakini kumbuka kwa mwaka 30M zilikatika sana natoka pale narudi Bongo nimejenga na usafiri nikapata wenzangu waliobakia pale bado wanazidi kumfanyia Biden kazi, kumbuka ile nchi imetengeneza mfumo wa mwananchi kuwa mtumwa wa Serikali ndio maana uchumi wao unashikiliwa na Serikali sio wananchi, huwezi kufanikiwa ukiwa kwenye mikono ya Serikali ya Marekani kumbuka wale ni wakoloni tangu zamani, sasa hivi wanafanya ukoloni kwa akili mfano kumnyima mwananchi kumiliki assets ili aishi kama mbumbumbu
 
Huduma za afya utapewa lakini kumbuka hela utakayolipia bima hapa bongo utapata boda nne ambazo ukiwapa vijana umetoka

Ukiwa na akili kama hizi utakufa na umasikini yaani 30M ndio hela ya kuongelea humu Kodi ya mwaka mzee kumbe ulivamia jiji kwahiyo ulitaka ulipe Kodi kama unayolipa huko tandale kwenye panya sio
 
Ukiwa na akili kama hizi utakufa na umasikini yaani 30M ndio hela ya kuongelea humu Kodi ya mwaka mzee kumbe ulivamia jiji kwahiyo ulitaka ulipe Kodi kama unayolipa huko tandale kwenye Mendes na panya sio
30M bado sijaweka mazagazaga asee tuwe serious. Nakupa mfano mmoja Raisi mstaafu Kikwete ana pesa mingi sio kwamba hawezi kuishi Los Angeles amesomea uchumi na maraisi wengi wa wamesomea uchumi na wanafahamu maana ya neno pesa ndio maana wakistaafu wanaendelea kuishi hapa wanafahamu kuishi kwenye nchi ambayo gharama za maisha ni kubwa sana ni ujinga vinginevyo tungewaona wanakimbilia kuishi kule. Mtu anayekimbilia kuishi Marekani hajasomea uchumi aliyesomea uchumi anaishi Tanzania
 
Huyo uliemtolea mfano ushasema raisi mstaafu kuendelea kwake kubaki hapo tanzania ni muendelezo wa kuiibia serikali unataka aje huku ataiba wapi acha habari zako halafu 30M marekani ni pesa ndogo sana ambayo mafukara wanaipata Kwa mda mfupi sana kama unafanya kazi Sasa nakushangaa unalalamika aisee ulivamia jiji wewe usilazimishe furaha marekani na tanzania ni mbingu na ardhi
 
$100usd haitoshi kitu pale ukweli ndo huo bill ya maji na umeme sio sh mbili internet sio sh mbili bei ya kucharge gari pale unaijua kweli? Je bei ya parking kila siku, asee
Wakati huo unaingiza kiasi gani? Au ulitaka ufanye kazi ya $15 kwa saa (nimeshatoa makato) kwa masaa nane halafu urudi zako ghetto ukalale? Upo serious kweli?
Maana kuna wengine mnafanya kazi only masaa 8 na kwa siku 3 au 4 hizi nyingine mle bata.
Tenga masaa yako 8 ya ku commute na kulala 16 yote piga kazi, halafu tenga a day or two kwa ajili ya kupumzika uene kama utakuja mitandaoni kulilia na kudekea watu.
 
Mbona unaandika kama upo Yombo vituka
 
Mtoa mada we kweli ni kiazi na hauna hoja za msingi tofaufi na kutaka kuaminisha watu ujinga, uzuri kila mtu na maisha yake na formula ya maisha hazifanani wewe Marekani imekushinda ila wengine ndio imewatengenezea pesa na kuwapa maisha ambayo hawakuyapa Tanzania au Afrika.
 
Kwani kumiliki nyumba ndio nini?
Ukimiliki nyumba huku unalala njaa inakuwaje hapo.hapo.
 
Ukiwa na akili kama hizi utakufa na umasikini yaani 30M ndio hela ya kuongelea humu Kodi ya mwaka mzee kumbe ulivamia jiji kwahiyo ulitaka ulipe Kodi kama unayolipa huko tandale kwenye panya sio
Yaani jamaa analia kulipa kodi ya 950 kwa mwezi? Hisia zangu kuhusu ufanyaji kazi wake na anachoingiza kumbe nilikuwa sahihi.
Huyu kwa hela hiyo nadhani alikuwa halipii kodi bali anachangia kodi.
US ukiishi kichwakichwa utaishia kulipia bill kila unachoungiza. Kabla ya kuishi US unatakiwa kwanza uwe na akili za kimikakati.
Anaweza akawa na hela zote atakazo and yet akaishia ku run bankrupt
 
Hoja ni kwamba Marekani kuna homeless au hakuna?
Hufanyi kazi, huna kipato, au umeshaharibu na kupoteza uaminifu kiasi kwamba kila unapoomba ajira waki run background check wanakuta una rekodi mbaya, kwanini usilale mitaani kwa kukosa ajira?
Marekani mtu kujikuta homeless ni dakika tu. So ukiyajua maisha ya US wala hilo la homeless siyo story
 
Kwa hiyo homeless wapo au hawapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…